Kibajaji amvaa vikali Zitto Kabwe kumsema Magufuli, amuita muoga kwani wakati yupo hakusema?

Kibajaji amvaa vikali Zitto Kabwe kumsema Magufuli, amuita muoga kwani wakati yupo hakusema?

Je ulifanikiwa au umeshindwa??? Na bado Zitto anayo nafasi ya kuja kuwa Rais na ukampigia magoti.
Labda awe rais wa wachawi na mizimu, zitto serikali imeisha mtumia kama agent wao,hawawezi kumpa nchi,sana sana viwalisha vya kuunganisha upinzani au kuuwa mpinzani mwenye nguvu
 
Acha kufananisha waasisi na huyo taahira.

Magufuli alikuwa Rais katili kuliko wote. Watu wanapata tetemeko hawapi msaada, eti sio yeye alileta tetemeko. Pesa akzipiga zote kwenye begi.
Kwa sababu ya uelewa au umri wako unafikiria UASISI badala ya matokeo.
Kama hujui watu waliokufa chini ya Mwalim ni wengi zaidi
Wakimbizi wa kisiasa wengi zaidi
Detentions without trials nyingi sana kuliko unavofikiria
Hakosoleki haambiliki
Jamii ilijaa hofu tukaamini kila raia ni jasusi uchumi ulikufa watu wakava katambuga kamanyola wakifulia magwanji mikalya na mipapai


So ukiwa muasisi ndio uuwe
Watu wakimbie nchi yao?
 
Zito alifukuzwa kwa kuwa ni idealistic mzuri sana!! huyo ni kawaida kwa sisi watu wenye akili mingi, hata ukiwa na akili saana drsn wanafunzi wajinga wana kuchukia hiyo ni kawaida....ni suala la muhusika kujisifu tu!! na kujiona

si unaona Nyerere kambona alimchukia tu bila sababu!....Mama yake km alikuwa mchawi basi alikuwa mchawi mzuri wenye manufaa!! tena unapaswa umuige kwa sababu mtoto wake anaishi kwa mafanikio chanya!

km kuna mtu alimsema vibaya Mama wa hivi ni kwa ajili ya wivu wa maendeleo ya watoto wake ....kwani mara ngapi walisema kifimbo cha nyerere ni uchawi?? kwa kuwa walimjaribu waka shindwa! alitawala mpaka akachoka ni kawaida ya maskini kuropoka hovyo!
Kuna mchawi mzuri bongo? Wote kazi yao ni kuroga watu, sasa kuna uzuri kwenye kuroga watu? Na huyo Zitto kutwa kujisifu ushirikina si ajabu karithishwa. Zitto ni mpigaji tu kapiga sana hela kipindi cha Kikwete ila alivyokuja Jiwe akaminya mirija na hapo ndipo Zitto alipocharuka hadi wanamwita mdini ila hana udini wowote ni mshirikina tu.

Sasa hivi Zitto kimya hakosoi huu utawala yeye anamkosoa mtu aliyekufa, ndio maana haaminiki anatambulika kama msaliti na chama chake cha mchongo.

Nyerere huwa hasemwi si uliona watu walivyomjua juu Lissu alivyokuwa anamchambua Nyerere makosa yake? Ila tukiwa huru kumchambua Baba wa taifa makosa yake kwenye utawala wake basi itakuwa balaa.
 
Ndugu, narudia. Usihalalishe ubaya kiss umefanywa Mara nyingi. Magufuli alimpoteza Been saanane na Azory mpaka leo. Huoni dosari kubwa.
Hizo ni tuhuma mnashindwa kuelewa hapo tu, na tuhuma kama hizo mbona zipo hata kwenye awamu ya Kikwete ila mbona hamkumuona ni katili?
 
Sasa cdm uliingiza ya nini kama ni Vita vya Zito na yule dhalimu?
Nilikuwa namuelezea Zitto na CDM ni sehemu ya mapito ya Zitto kwamba waliwahi kumtimua Chadema na hadi leo Zitto haaminiki hujulikana kuwa ni msaliti. Na chama chake hakijawahi kuwa chama cha upinzani.
 
Kuna mchawi mzuri bongo? Wote kazi yao ni kuroga watu, sasa kuna uzuri kwenye kuroga watu? Na huyo Zitto kutwa kujisifu ushirikina si ajabu karithishwa. Zitto ni mpigaji tu kapiga sana hela kipindi cha Kikwete ila alivyokuja Jiwe akaminya mirija na hapo ndipo Zitto alipocharuka hadi wanamwita mdini ila hana udini wowote ni mshirikina tu.

Sasa hivi Zitto kimya hakosoi huu utawala yeye anamkosoa mtu aliyekufa, ndio maana haaminiki anatambulika kama msaliti na chama chake cha mchongo.

Nyerere huwa hasemwi si uliona watu walivyomjua juu Lissu alivyokuwa anamchambua Nyerere makosa yake? Ila tukiwa huru kumchambua Baba wa taifa makosa yake kwenye utawala wake basi itakuwa balaa.
Sasa kma mtu ame- fanya uchawi ili akapige pesa ndefu!!! hizo hizo hela hazijatoroshwa nje bali
analipa kodi!
ameweka mjengo wa maana, wanawe wataishi milele , mafundi wakalipwa vizuri wakala na watoto wao!
zitto huyohuyo akamnunulia mkewe na watoto nguo
akawapeleka shule humuhumu bongo akalipa ada zao vizurii shuleni!!
anakanunua gari!!

ambalo gari hilo analilipia ushuru kila mwaka
ana nunua mafuta kwa watanzania na wao
wanasomesha watoto wao
wana kula!! kifupi hela alizopiga kazisambaza humu humu kwa watanzania !! ni wewe ukitaka ufanye kazi kwake uzipate pia mfano kamuoshee hilo gari atakulipa! kawe mlinzi kwake atakulipa, kifupi amaajili umati !!

Sasa Mtu km huyu kosa lake ni nini?? Jiwe alipiga hela ndefu akazipeleka kulipa wazungu (kwa kununua midege cash) maadui zetu wazidi kutu nyonya!! akaagiza vifaa na lami ya kujenga chato air port cash! .....

Km mtu huyu Zito kabwe ni mchawi /mwizi wa hivi huyu basi uchawi wake ni mzuri sana!! tena wenye manufaa mengi sana aongezewe!! ndo wachawi wa hivi tunao wataka! sisi watanzania!! angekuwa Moshi anaongezewa na mke bure kabisa!

ila sasa nyie watu wa majitombweganii mnamchukia mtu km huyu!
 
Tatizo la watanzania wa Sasa NI watu wa kuhemuka kuliko kutafuta ukweli tumsamehe Zitto kwa kauli zake wakati NI ukuta tusubiri hukumu ya wakati tumuache Magufuli apumzike kwa amani nasi tupambane na vitabu vyetu maana bado tunaviandika tuache kusikiliza ya wadau. Tuandike vyetu Magufuli ameandika chake kimeisha. Maisha yetu ya Sasa NI msalaba mzito bado tupo hapa tunamjadili aliyepumzika akiwa amemaliza kazi yake.
 
Leo bungeni mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde amemvaa vikali kiongozi mkuu wa ACT, Zitto Kabwe kwa kumsema Hayati Magufuli. Kibajaji amemuita Zitto muoga kupitiliza kwani wakati Magufuli yupo hai hakusema mpaka ameondoka.

Pia Kibajaji amesema wote wanaomsema Magufuli ni wanafki na hata Samia akiondoka nae watamsema vilvile. Amemsifu Nyalandu kwa kusema kwa vitendo hawezi kufanya kazi na Magufuli wakati yupo hai na kuachia nafasi yake ya ubunge.

========

Kibajaji: Nchi yetu imeweka vizuri sana masuala ya utawala bora kisheria lakini kuna baadhi ya vyama kwa mfano pale Zanzibar, ACT tunashirikiana nacho kwenye utawala bora, sisi tuna Rais, tuna Serikali wao wana makamu wa kwanza wa Rais lakini mmesikia kiongozi mkuu wa ACT Wazalendo, Zitto anamnanga mheshimiwa Magufuli kana kwamba Zitto hashiriki kwenye Serikali.

Magufuli aheshimiwe, Zitto aelewe kwamba suala la kufiwa ni suala kubwa. Haiwezekani kwenye utawala bora tuache suala la Magufuli kuzungumzwa vibaya na mimi sitaacha.

Leo nnapoongea Waislamu mmefunga, dini inawakataza kuwasema vibaya marehemu, Zitto ni muislamu anajua.

Mheshimiwa Zitto anatutaka tunaompenda mheshimiwa Magufuli tukazikwe nae. Zitto amewahi kufiwa na mama yake, mimi sitaki kufika huko, mama wa Zitto ni mama yangu mimi. Mimi nimewahi kufiwa na baba yangu lakini ACT wamewahi kufiwa na makamu wa kwanza wa Rais, Zitto anatulazimisha sisi tuanze kumsema vibaya Maalim Seif, hatuwezi.

Inakuwaje watu mnakuwa waoga, viongozi wakiwepo hamsemi wakiondoka ndio mnasema, huu ni uoga uliopitiliza. Mtu mmoja tu alisema kwa vitendo kwamba yeye hawezi kufanya kazi na Magufuli, Nyalandu.

Aliachia ubunge akaondoka lakini watu tuliobaki hapa ni watu wa Magufuli na tumefanya nae kazi na tulikuwa tunamsifu.

Hawa watu ambao sasa wanamsema Magufuli ni wanafiki wakubwa, Samia akiondoka watamsema vibaya hivyohivyo, ni bora mimi Lusinde ambae niko wazi na siwezi kuacha.

Pia, soma => Zitto: Wanaompenda Magufuli wakazikwe naye Chato, alikuwa Rais fisadi zaidi kuwahi kutokea Tanzania
Kibajaji ni mtaalamu wa matusi na mipasho
 
Ni kweli kabisa
Simple minds discuss people.
Kila siku kibajaji kinaongelea watu tu, hakijawahi kuleta hoja yenye mashiko.
Utamsikia Kinana hivi, Mbowe vile, Magufuli hivi, Deceiver vile.....
Najiulizaga, miaka yote hii jimboni kwake hakuna hata form six mmoja agombee kuondoka hii aibu?
 
Tunapomsema mwendazake vibaya ndiyo tunapata tofauti ya uongozi wa Nyerere na Magufuli.
 
Leo bungeni mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde amemvaa vikali kiongozi mkuu wa ACT, Zitto Kabwe kwa kumsema Hayati Magufuli. Kibajaji amemuita Zitto muoga kupitiliza kwani wakati Magufuli yupo hai hakusema mpaka ameondoka.

Pia Kibajaji amesema wote wanaomsema Magufuli ni wanafki na hata Samia akiondoka nae watamsema vilvile. Amemsifu Nyalandu kwa kusema kwa vitendo hawezi kufanya kazi na Magufuli wakati yupo hai na kuachia nafasi yake ya ubunge.

========

Kibajaji: Nchi yetu imeweka vizuri sana masuala ya utawala bora kisheria lakini kuna baadhi ya vyama kwa mfano pale Zanzibar, ACT tunashirikiana nacho kwenye utawala bora, sisi tuna Rais, tuna Serikali wao wana makamu wa kwanza wa Rais lakini mmesikia kiongozi mkuu wa ACT Wazalendo, Zitto anamnanga mheshimiwa Magufuli kana kwamba Zitto hashiriki kwenye Serikali.

Magufuli aheshimiwe, Zitto aelewe kwamba suala la kufiwa ni suala kubwa. Haiwezekani kwenye utawala bora tuache suala la Magufuli kuzungumzwa vibaya na mimi sitaacha.

Leo nnapoongea Waislamu mmefunga, dini inawakataza kuwasema vibaya marehemu, Zitto ni muislamu anajua.

Mheshimiwa Zitto anatutaka tunaompenda mheshimiwa Magufuli tukazikwe nae. Zitto amewahi kufiwa na mama yake, mimi sitaki kufika huko, mama wa Zitto ni mama yangu mimi. Mimi nimewahi kufiwa na baba yangu lakini ACT wamewahi kufiwa na makamu wa kwanza wa Rais, Zitto anatulazimisha sisi tuanze kumsema vibaya Maalim Seif, hatuwezi.

Inakuwaje watu mnakuwa waoga, viongozi wakiwepo hamsemi wakiondoka ndio mnasema, huu ni uoga uliopitiliza. Mtu mmoja tu alisema kwa vitendo kwamba yeye hawezi kufanya kazi na Magufuli, Nyalandu.

Aliachia ubunge akaondoka lakini watu tuliobaki hapa ni watu wa Magufuli na tumefanya nae kazi na tulikuwa tunamsifu.

Hawa watu ambao sasa wanamsema Magufuli ni wanafiki wakubwa, Samia akiondoka watamsema vibaya hivyohivyo, ni bora mimi Lusinde ambae niko wazi na siwezi kuacha.

Pia, soma => Zitto: Wanaompenda Magufuli wakazikwe naye Chato, alikuwa Rais fisadi zaidi kuwahi kutokea Tanzania
Yeye mbona hamsemi Kinana sasa hivi, kuna wakati mtu unalazimika kukaa kimya ili kulinda uhai kwa watalaam wa mapigano wanakwambia unapokuwa mateka jaribu kuhakikisha unailinda kila dakika kwa sababu huwezi kujua huwenda ikatokea muda wa kuokolewa. Kifupi ukiwa mateka usiwe mbishi, watanzania tulikuwa mateka hivo hatukuwa na nafasi ya kufanya uchaguzi.
 
Sasa kma mtu ame- fanya uchawi ili akapige pesa ndefu!!! hizo hizo hela hazijatoroshwa nje bali
analipa kodi!
ameweka mjengo wa maana, wanawe wataishi milele , mafundi wakalipwa vizuri wakala na watoto wao!
zitto huyohuyo akamnunulia mkewe na watoto nguo
akawapeleka shule humuhumu bongo akalipa ada zao vizurii shuleni!!
anakanunua gari!!

ambalo gari hilo analilipia ushuru kila mwaka
ana nunua mafuta kwa watanzania na wao
wanasomesha watoto wao
wana kula!! kifupi hela alizopiga kazisambaza humu humu kwa watanzania !! ni wewe ukitaka ufanye kazi kwake uzipate pia mfano kamuoshee hilo gari atakulipa! kawe mlinzi kwake atakulipa, kifupi amaajili umati !!

Sasa Mtu km huyu kosa lake ni nini?? Jiwe alipiga hela ndefu akazipeleka kulipa wazungu (kwa kununua midege cash) maadui zetu wazidi kutu nyonya!! akaagiza vifaa na lami ya kujenga chato air port cash! .....

Km mtu huyu Zito kabwe ni mchawi /mwizi wa hivi huyu basi uchawi wake ni mzuri sana!! tena wenye manufaa mengi sana aongezewe!! ndo wachawi wa hivi tunao wataka! sisi watanzania!! angekuwa Moshi anaongezewa na mke bure kabisa!

ila sasa nyie watu wa majitombweganii mnamchukia mtu km huyu!
Wewe toka uzaliwe ushawahi kumuona mtu anayehesiwa mchawi/mwanga ambaye ni tajiri? Nimekwambia wachawi bongo ni wa kurogana tu kurudisha watu nyuma kimaendeleo na kutoa watu kafara, huyo Zitto kutwa kutiwa watu mikwara na huo uchawi wake kwamba atawaroga na kujisifu yeye harogeki sasa hapo kuna uchawi wa faida? Huyo Zitto angekuwa arabuni angeshanyongwa kwa huo uchawi wake halafu nashangaa watu wanamwita mdini mtu anayejisifu kwa uchawi waziwazi.
 
Sasa hata akimsema JPM sasa atamsikia? .Hizo ni dalili za upunguani ni sawa kuongea na mawe ukidhani yanakusikia.lazima aliye sanaa aliporwa hela alizopata kiharamu alipokuwa PAC
Abasemwa yeye ili wafuasi wake wlio hai, aliokuwa anashirikiana nao kutenda udhalimu, wasikie wsiebdelee, waonyeke.
Angalia wanavyo re act sasa.
Hii ni nzuri ili wajue kuwa wtu waliumia na wanawajua, na wapo tayari kurudisha kisasi kwa hawa wanufaika nae walio hai.
 
Wewe toka uzaliwe ushawahi kumuona mtu anayehesiwa mchawi/mwanga ambaye ni tajiri? Nimekwambia wachawi bongo ni wa kurogana tu kurudisha watu nyuma kimaendeleo na kutoa watu kafara, huyo Zitto kutwa kutiwa watu mikwara na huo uchawi wake kwamba atawaroga na kujisifu yeye harogeki sasa hapo kuna uchawi wa faida? Huyo Zitto angekuwa arabuni angeshanyongwa kwa huo uchawi wake halafu nashangaa watu wanamwita mdini mtu anayejisifu kwa uchawi waziwazi.
ushawahi kumuona mtu anayehesiwa mchawi/mwanga ambaye ni tajiri?
Wa kwanza Zitto Kabwe umemtaja mwenyewe!!
AZAM
Kugis
Tanganyika Bus!
Jawal Nehru!nk!
wachawi bongo ni wa kurogana tu kurudisha watu nyuma kimaendeleo na kutoa watu kafara,
Uchawini unachagua aina ya uchawi unaotaka kuufanya!! km ukiona ni maskini yeye ametaka ivo!
Zitto kutwa kutiwa watu mikwara na huo uchawi wake kwamba atawaroga na kujisifu yeye harogeki sasa hapo kuna uchawi wa faida?
Jamani sasa kama wanamtisha kuwa watamroga kwa nini asiwajibu jamani? hee!! km ni mchawi ina maana wamemjaribu kumuua km Amina chifupa Walivo mfanya lkn huyu wamemshindwa!.....sasa km ni mchawi amejaribiwa na wachawi pia! wewe km si mchawi hana shida yule! kwani hujui dawa ya moto ni moto??
hapo kuna uchawi wa faida?
Jibu ni ndiyo!! faida kubwa ipo kwa sababu huo uchawi wake umemuweka hai mpaka leo lkn wabaya wake wamepukutika!! hivo analinda afya za mashabiki wake na wale anao wawakilisha, zaidi familia yake mke na wanae!! zitto yuko sahihi!
Zitto angekuwa arabuni angeshanyongwa kwa huo uchawi wake
Wangekufa wao kabla hawaja mgusa! uarabuni si mbali hata hao wanao taka kumuua waende wakachukue hizo dawa za uarabuni wakamuue waone nyota saba!
nashangaa watu wanamwita mdini mtu anayejisifu kwa uchawi waziwazi.
Watu wakimwita mdini ni wao wameamua huwezi wazuia!! kwanza Dini zipi izo za Yesu mzungu?? au Muarabu!! Zito kasoma yule anajua kayesu kazungu hakaji ng'oo! mtasubiri sana!
 
Labda awe rais wa wachawi na mizimu, zitto serikali imeisha mtumia kama agent wao,hawawezi kumpa nchi,sana sana viwalisha vya kuunganisha upinzani au kuuwa mpinzani mwenye nguvu
Hayo ni maoni yako soma Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 Ibara12 na 13
 
Back
Top Bottom