Kiboko ya mtoto anayelia lia hovyo kama zezeta au kulilia vitu vya watu

Kiboko ya mtoto anayelia lia hovyo kama zezeta au kulilia vitu vya watu

Kulupango

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2020
Posts
288
Reaction score
535
Hawa ni wale watoto ambao hawana competition na watoto wenzao, ukiona mtoto wako analia kila mara au kulilia vitu vya watu kila wakati, jitahidi utafute mtoto mwenzake wa rika lake uishi nao pamoja utaona atavyo badilika na kuwa mtoto mzuri.

Njia nyingine nzuri ya kumkanya huyu mtoto, siku akiumwa na akalazimika kuchomwa sindano na akalia kwa maumivu ya sindano, basi wewe kama mzazi unaweza ukanunua bomba la sindano ukae nalo nyumba, chomoa sindano uitupe baki na lile bomba la kuvutia dawa, akianza kulia tu wewe lichukue hilo bomba fanya kama unalinyanyua juu na kulivuta kama unaingiza dawa vile. Atahofiia maumivu ya sindano na atapunguza tabia ya kulia lia.

Hawa ni wale watoto kuanzia umri wa miaka miwili na nusu kupanda juu, ambao wanakuwa tayari wameanza kuongea na kuchanganua taarifa mbalimbali za kijamii lakini wanakuwa na tabia ya kulia lia kila wakati bila sababu ya msingi.

1652096229284.png
 
True hii dawa kabisa, ngoja niwahi pharmacy kabla hawajafunga.
 
Ukiona mtoto wako anatabia kama hizo ujue tatizo ni wewe.
Pia mtoto adhibitiwi, bali mtoto hulelewa, hufundishwa na kukanywa.
 
Si umtandike fimbo ili alie kweli ss,
Why unahangaika na mibomba ya sindano kama nesi
 
Back
Top Bottom