Kibu Denis alipopewa uraia kwa njia ya mlango wa nyuma ilikuwa sawa ila ni kosa kwa Singida Black Stars kufanya kwa wachezaji wake

Hapo unazidi kuonyesha uwezo wako mdogo wa kiakili, nitakujibu Mara ya mwisho usipoelewa ni juu yako. Kibu alivyocheza Geita na Mbeya City alicheza Kama mtanzania au mgeni? Kama alicheza Kama mgeni kwanini alichaguliwa timu ya taifa inaelekea mwalimu wako akipata shida Sana wakati anakufundisha.
 
Wakati Kibu anaitwa kuichezea timu ya Taifa Kwa mara ya kwanza alikuwa mchezaji Simba?
 
Tatizo la uelewa tu sheria zetu ni nyepesi sana kwa raia wa kigeni kupata uraia Tanzania ...Sheria zetu ni ngumu kwa Watanzania kuwa na uraia wa nchi mbili...Watu wengi wamechukua uraia kimya kimya uko mitaani tatizo ya hawa ni wacheza mpira....Tatizo kwa watu wa chini ni Fee yake kidogo ni kubwa kwa mtu wa chini dola 1500 na vigezo vingine ni rahisi sana ..lugha yenyewe wameandika Swhili OR English
 
Alicheza kama mgeni mambo ya uraia wa kibu yaliibuliwa alipokuwa anasajiliwa kutoka mbeya kwenda simba

Wewe ndo unauwezo mdogo sababu ulipinga wazi wazi video ikionyesha mashabiki wa simba wakivunja viti kwa hiyo na hili lazima ulipinge
 
Kwahiyo nyie ndio mpo nyuma ya huu uhuni wa singida black star?
 
Mimi Yanga ila kwenye hili Simba hawajakosea kwa Kibu, kwani alikua anajulikana ni raia wa Tanzania toka akiwa Geita. Pia ameingia nchini akiwa na umri wa miaka sita.
Na simba imeomba uraia wa nwachezaji wake 9 waje watueleze tena
 
Ndiyo maana wanaitwa mbumbumbu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…