Kibu Denis amemzidi nini Ditram Nchimbi?

Kibu Denis amemzidi nini Ditram Nchimbi?

demigod

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2015
Posts
8,292
Reaction score
15,250
Leo sikuwa na ratiba ya kutazama mechi ya Taifa Stars dhidi ya Benin. Ila baada ya kusikia watu wakiwa na hamu na shauku ya kumuona Kibu Denis, nikaona nayo ni fursa ya kuweza kumtazama.

Lengo pia ni kutazama ni kipi ambacho Taifa kama Taifa tumekiona kwa Kibu Denis hata tukafikia hatua ya Kugawa Uraia kwake. Ni kheri tungempa uraia Steven Sey (Namungo FC)

Baada ya kufanyika mabadiliko na Mwl Kim Poulsen nikaja kugundua kuwa tumepoteza nafasi ya Uraia kwa mtu asiye na cha ajabu sana katika uchezaji wake wa Mpira.

Hata ukijaribu kuchambua uchezaji wake na takwimu zake kiujumla huoni tofauti kati yake yeye na Ditram Nchimbi.

Nilicho kuja gundua kingine ni kuwa mshawasha uliopo machoni pa watanzani kuhusu Kibu Denis unatokana na uhalisia kuwa watanzania wengi hawajawahi kushuhudia jitu lenye miraba saba likiichezea timu yao ya Taifa, hivyo wakadhani wamejiokotea Lukaku Wao.

Kiuhalisia uwepo wa Kibu Denis kwenye Timu ya Taifa ya Tanzania kunapunguza hamasa na ladha ya Ushindi. Maana mara nyingi anaonekana akikosa basic skills kama vile Kupokea Mipira, Anticipation, Ball Control, Tactical Decisions.

Nadhani kama tusinge muingiza Kibu Denis kwenye mechi ya leo basi Taifa Stars tungepata Ushindi.

Sioni Taifa Stars ikipata matokeo ya Ushindi endapo Kibu Denis anahusika kwenye mechi.
 
Kiufupi mchezo ulikuwa mzuri sana, tumepata nafasi nyingi tumezitumia vibaya.

all in all naamini gem ya marudiano tunashinda kwa goli 3.

kibu Dee anaanza first eleven.
 
Kilichofanya aonekane hivyo ni nafasi aliyowekwa yule ni striker wa kati au atokee pembeni lakini Leo aliwekwa namba 10 ambayo ilikuwa inamfanya asicheze vizuri.

Hata Mimi nimeona kwa alivyocheza Leo imekuwa kama nchimbi tu
 
Hahaha ......vitu vingine ushabiki unazidi Sana ......tuwe tunaangalia mpira basi walau. tatizo tukiwa vibanda umiza tuna"focus" kubishana Sana kuliko hata kuangalia TV mbele kule.
Wewe mchezaji hajui hata Kupiga Kichwa Mpira....Sisi tumemuona anafaa kwa sababu ana misuli mikubwa mguuni kushinda wakina Iddi Nado.
 
Wewe mchezaji hajui hata Kupiga Kichwa Mpira....Sisi tumemuona anafaa kwa sababu ana misuli mikubwa mguuni kushinda wakina Iddi Nado.
Maneno kuntu kama haya huwa yanawakera kweli wale jamaa waliompa ule uraia wake tata.
 
Kilichofanya aonekane hivyo ni nafasi aliyowekwa yule ni striker wa kati au atokee pembeni lakini Leo aliwekwa namba 10 ambayo ilikuwa inamfanya asicheze vizuri.

Hata Mimi nimeona kwa alivyocheza Leo imekuwa kama nchimbi tu
😂 😂
 
Ujinga upi ,takwimu za Nchimbi yanga ana magoli mangapi msimu mzima na Kibu ana magoli mangapi na mbeya city ?
Mbeya City akienda hata Yohana Mkomola ni lazima amalize ligi akiwa na magoli mengi kuliko Mugalu.
 
Jamaa aache papala ndio zinazomuharibia, pia kama ananguvu sio kila sehemu anahitaji kutumia nguvu, pathetic performance ilikuwa wa nahodha wao, anafanya upuuzipuuzi tu

Sent from my Infinix X652 using JamiiForums mobile app
 
Tanzania bado hajatokea mchezaji ambae anaweza kuharibu ratiba za watu ili wamuangalie yeye akicheza
 
Kibu ni overrated

Bado anapapara sana, ball control take ni ndogo sana bado anahitaji mda sana kufikia katika kiwango ambacho wengi walitarajia awe nacho.
 
Back
Top Bottom