Kichuguu si Mlima CAG: Chuki Dhidi ya Magufuli imewatoa ufahamu sasa?

Kichuguu si Mlima CAG: Chuki Dhidi ya Magufuli imewatoa ufahamu sasa?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Watu wanaendekeza siasa mno kuhusu suala la CAG. Rais halazimiki kumteua CAG yule yule kila baada ya miaka mitano. Katiba na Sheria viko wazi kwa yeyote kuona. Kwa vile marais waliopita walimteua mtu yule yule kwa vipindi zaidi ya kimoja haina maana Rais ajaye analazima kurudia kumteua.

Kilichowazi ni kuwa pindi akishateuliwa na kuapishwa CAG hawezi kuondolewa kirahisi hadi muda wake wa miaka mitano upite au yatokee yale yaliyoanishwa kwenye Katiba kuweza kumuondoa. Ina maana Rais hawezi kuamka na kumtumbua au kumuondoa ofisini kiholela - ndio maana Ndugai pamoja na majaribu yote hakuweza kumuondoa.

Sasa kipindi cha miaka mitano kikiisha CAG anaweza (eligible) kuteuliwa tena; lakini hawezi kulazimisha kuteuliwa tena kwa vile tu alikuwa CAG miaka mitano iliyopita. Huku ni kutokusoma na kuelewa kwa usahihi Katiba na sheria.
Swali ambalo linaweza kuulizwa na labda la muhimu kisheria ni hili:

Kwa vile CAG inadaiwa hajafikisha miaka 60 ya kustaafu kwa lazima na kwa vile hajateuliwa kushika tena nafasi hiyo je bado anaendelea kuwa mtumishi wa umma au la? Kama ni ndiyo basi ni wazi atapangiwa kazi nyingine hadi atakapofikisha miaka 60 ya kustaafu (Ubalozi??). Lakini kama siyo, ni wazi atalipwa mastahili yake yote kwa muda wote aliokuwa CAG na kurudi uraiani.

Tusitengeneze mlima toka kichuguu.
 
Naona kama tulikuwa tunawaza sawa kiaina.

Nimetoka kuanzisha uzi muda huu huu...

 
Wewe mtu hujui maana ya katiba na muongozo wa kanuni za taasisi ya umma. Umeandika hovyo hovyo mawazo ya kijinga ili yule mtu akuone. Mumeshaujua udhaifu wake imebaki kazi kwenu kujito ufahamu na kuweka akili pembeni. Kabla hujaandika madudu humu uwe unajiridhisha kwanza!

Sasa nakueleza. Magufuli kwa kuteua CAN mpya kavunja katiba ya nchi mchana kweupeee. Na hata tafsiri sahihi ya maneno yaliyopo kwenye kanuni zinazoongoza ofisi ya CAG hajaielewa achilia mbali kama tutajielekeza kwenye kanuni na kuitupa katiba kama yeye alivyofanya.
 
Nimekuelewa lakini hapa lengo ni kutengeneza mazingira ya "plunder with impunity"

Huyu Jiwe ana operate na oligarchy yake iliyo royal kwake. Tukubali tulikosea kumpa nchi atawale, tusubiri the worst to come from him hadi aje atoke ofisini.
 
Sawa sawa.
Si lazima pia kwa Yohana kutawala mara ya pili.
Apigwe nduli iddi aminiiiiii......
Hilo naona nalo watu hawaliangalii na ndio maana Membe kuonyesha dalili za kuchukuwa fomu 2020 kesha onekana kama mhaini.

Kama ilivyo kwa CAG, hata Rais sio lazima wananchi wampe kipindi kingine cha miaka mitano. Hakuna mahali panalazimisha hivyo.

Kichuguu (Rais) hakiwezi kuwa mlima (wananchi).
 
Magufuli amejionyesha kuwa ni fisadi papa yaani kwa hili la Assad ataficha wapi uso wake Dotto James a ajiandae kufungwa kwa uhujumu uchumi na utakatishaji pesa madudu ni mengi mengi ha ha jamaa jizi kweli
 
Mkuki mtamu kwa nguruwe mchungu kwa binadamu. Lakini amesahau kuwa usimfanyie mtu kitu ambacho hupendi kufanyiwa, sasa na yeye aruhusu watu wachukue form za uraisi 2020
Hilo naona nalo watu hawaliangalii na ndio maana Membe kuonyesha dalili za kuchukuwa fomu 2020 kesha onekana kama mhaini.
Kama ilivyo kwa CAG, hata Rais sio lazima wananchi wampe kipindi kingine cha miaka mitano. Hakuna mahali panalazimisha hivyo.
Kichuguu (Rais) hakiwezi kuwa mlima (wananchi).
 
Nimekuelewa lakini hapa lengo ni kutengeneza mazingira ya "plunder with impunity"

Huyu Jiwe ana operate na oligarchy yake iliyo royal kwake. Tukubali tulikosea kumpa nchi atawale, tusubiri the worst to come from him hadi aje atoke ofcn.
Haitakuwa leo wala 2025 hatoki, uchaguzi unaokuja watu wake sasa wanakimbia ofisi. CAG hakutakiwa tangu mwanzo kwa sababu msema kweli, katka kipindi hiki msema kweli hastahili kuishi.
 
Siku ambayo tutakaa na kuona umuhimu wa kikatiba wa kufanyia "vetting" teuzi zote zinazofanywa kupitia taasisi ya Rais kwa maslahi mapana ya taifa, hapo ndipo ambapo manung'uniko na kelele juu ya teuzi husika zitapungua. Watu wanasukumwa na mashaka ya "intimidation & blackmailing" ili kuwa na "undue political advantages" kwa baadhi ya teuzi.
 
Back
Top Bottom