Kifo cha Asimwe Novath (Albino); Baba mzazi na Paroko msaidizi washikiliwa kwa tuhuma za mauaji

Kifo cha Asimwe Novath (Albino); Baba mzazi na Paroko msaidizi washikiliwa kwa tuhuma za mauaji

Oldmantz

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2023
Posts
704
Reaction score
1,457
mama-pic.jpg
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amesema kuwa tayari Jeshi la Polisi limewakamata watu wanaodaiwa kuhusika na mauaji ya mtoto mwenye ualbino Asimwe Novath (2).

Mei 30, 2024 Asimwe anadaiwa alichukuliwa na watu wasiojulikana nyumbani kwao Muleba mkoani Kagera na juhudi za kumtafuta hazikuxzaa matunda hadi hapo Juni 17, 2024 mwili wake ulipopatikana ukiwa katika mfuko wa sandarusi huku baadhi ya viungo vikiwa vimenyofolewa.

Waziri Masauni amesema watuhumiwa hao wamekamatwawakiwa na vithibiti vya kutendea kosa hilo na kufafanua kuwa hawajabahatisha katika kuwakamaa watu hao.

“Hakuna hata mmoja ambaye amehusika na mauaji ya binti huyu malaika wa Mungu atakayrepona, tumefikia pazuri na kitakachofanyika itakuwa fundisho kwa wahalifu wengine, tupo vizuri katika kukabiliana na uhalifu na ndiyo maana hakuna mtu atakayefanya uhfifu asipatikane,” amesema Masauni

Credit: Bongo 5

___
Kupitia taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi David Misime imewataja watuhumiwa waliokamatwa ambao walieleza jinsi walivyoshiriki katika tukio hilo ni pamoja Baba mzazi wa mtoto huyo aitwaye Novart Venant, Desideli Evarist ambaye ni mganga wa jadi mkazi wa Nyakahama, Elipidius Rwegoshora Paroko Maidizi wa Parokia ya Bugandika ambaye anadaiwa kumfuata na kumshawishi Baba mzazi wa mtoto ili wafanye biashara ya viungo vya binadamu.

Paroko huyo pia anatuhumiwa kuwa ndiye allyemtafuta mganga wa jadi na kulipia gharama zote za uganga.

Watuhumiwa wengine ni Dastan Kaiza mkazi wa Bushagara, Faswiru Athuman mkazi wa Nyakahama, Gozibert Alkadi mkazi wa Nyakahama Kamachumu, Rwenyagira Burkadi mkazi wa Nyakahama Kamachumu, Ramadhani Selestine mkazi wa Kamachumu na Nurduni Hamada mkazi wa Kamachumu.

Pia soma:
Update
- Kagera: Watuhumiwa tisa wa mauaji ya Asimwe Novart wafikishwa mahakamani na kusomewa shtaka la kuua kwa kukusudia
 
Kuwakamata hao wahalifu ilikuwa ni kazi nyepesi sana kwa polisi.

Watu wanaoamini ushirikina huwa ni wajinga hawanaga akili ya kupanga tukio bila kuacha trace.

Nina uhakika kipindi wanamuiba mtoto walikuwa na simu zao mfukoni. Na hata kipindi wanamuua mtoto simu zilikuwepo.

Polisi hawajatumia hata nguvu ya kuwajua na hata kuwatafuta. Wamecheza na simu zao tu
 
Back
Top Bottom