Kifo cha kampuni ya mabasi SCANDINAVIA EXPRESS

Kifo cha kampuni ya mabasi SCANDINAVIA EXPRESS

Binafsi nilipenda sana mabasi na huduma za hii kampuni, hususan miaka ya 2003/2006. Mabasi mazuri, huduma za ndani lukuki! Ilikuwa hata watoto wadogo wanasafirisha bila shida yoyote, na coverage yao ilikuwa nzuri hadi nje ya nchi. Nadhani zilikuwa miongoni mwa marcopolo za mwanzo hapa tz, na miongoni mwa luxury za hali ya juu. Sasa miaka ya hivi karibuni ~ 2008 ndipo mizengwe ikaanza. Nikaja kusikia ni kampuni ya wakubwa wa serikali kipindi kile, mara ya wahindi mara ya fulani. Hadi sasa sijajua kwa nini kampuni ile imekufa, na nini kilikuwa nyuma ya pazia? Kama kuna mtu mwenye taarifa juu ya hili namuomba atujuze jamani

outright theft, kaulize mabenki mangapi yameachiwa kilio na scandanavia, the guy just shifted the capital to other business and melted....
 
Na mengine yalikua yanaitwa HEKIMA ROYAL CLASS,siyaoni, yalikua njia ya Dar-Tunduma
 
Mimi nilikua nashangaa basi linatoka Dar kwenda Arusha na abiria 14?
 
wana kesi mahakama kuu ya biashara miaka nenda rudi haiishi
 
Pia kuna ile iliyokuwa inaitwa Zainabs! Sijui yalipotea vipi haya mabasi!
Zainabus yalikuwa ya familia ya mzee Hasunu wa kasulu. Baada ya mwanae kufariki na magari yote yakamfuata. Hadi sasa mzee hasunu kapinda hana lolote kaisha
 
outright theft, kaulize mabenki mangapi yameachiwa kilio na scandanavia, the guy just shifted the capital to other business and melted....
kweli mkuu kifo cha Scandinavia kilisababishwa na madeni makubwa waliyokuwa wanadaiwa. Mmiliki wake anaitwa Mohamed Abdullah(aliwahi kuwa m/kiti wa Taboa). Pia alikuwa anadivert mikopo kwenda kwenye biashara zingine hususan tankeers na kiwanja cha ngano
 
bado sumry na yeye kupotea kabisa cjui kabakisha gari 4 za bukoba na kigoma ambazo nazo zimechoka
 
Dah umenikumbusha Dar-K'la long time. Nakumbuka enzi hizo mademu wa kiganda ukimwambia utamleta bongo na atapanda Scandinavia unang'oa kilaini.
 
mengne yalibadilishwa jina, ndio haya Green Star yanayofanya safari za Dar - Mwanza

hee mkuu sidhan kama yalibadirishwa jina na kuitwa green star sababu enzi zile hakukua na yutong sasa ukisema mengne yalubadirishwa jina ni uongo. labda useme wamilik wa scandinavi ndio wamilk wa greenstar ya sasa.
 
hee mkuu sidhan kama yalibadirishwa jina na kuitwa green star sababu enzi zile hakukua na yutong sasa ukisema mengne yalubadirishwa jina ni uongo. labda useme wamilik wa scandinavi ndio wamilk wa greenstar ya sasa.

Na Scandinavia hayakuwa ya mmiliki m1.
 
SADIQ LINE " rafiki wa wote" sasa hana basi hata moja baada ya kukaidi amri ya chama
 
Mi najikumbukia Chai maharage, sijui zilipotelea wapi:A S cry::A S cry:?
 
Back
Top Bottom