Kifo cha Mwalimu Nyerere 14/10/1999, ulikuwa wapi?

Nilikua std 6 Niko mwananyamala Mara nkaona Komba anaombolezaa eti Nyerere kafa...

Nakumbuka nilienda hadi taifa kuuona mwli wake!
 
Nilikuwa mwaka wa nne mwanzoni enzi hizo panaitwa FoE... Electrical Engineering..

Redio zote no kupiga ndombolo mwezi mzima. Ni nyimbo za maombolezo tu...

ILA HUMU KUNA WATOTO WENGI... ndo maana wengine tunavumiliaga matusi na kashfa nyingi humu
 
Mimi nilikuwa elephant and castle. Na kazi nilikuwa st. Thomas. Katikati ya London. Nilipofika job naambiwq your president is dead!! Wakati jana yake nilikuwa nao (mama Maria na mwl. Akiwa ICU) nilikuwa nategemea kitu kama hicho. But when sikujua.
 
Nilikuwa form two st. Francis Mbeya.. Masista wakatutangazia Nyerere kafariki. Kulipooza mnoo
 
Lazima niwe mkweli nilikuwa darasa la sita shule ya msingi Mbuyuni hapo njia ya kuelekea posta, tulirudishw home kisa nyerere kafa, nilipofika nyumbani nilimkuta mwenye nyumba analia mithili ya mtu aliyebakwa
Utakuwa classmate wangu
 
Form one, jana yake nilikuwa nimerudi home baada ya suspension shuleni. Ilikuwa bonge la ahueni coz masimango toka kwa mzee na mkewe yalikoma na muda wote wakiwa hawana kazi wakawa wanashinda kwenye TV kuangalia maombolezo.
 
Nilikua std 6 Niko mwananyamala Mara nkaona Komba anaombolezaa eti Nyerere kafa...

Nakumbuka nilienda hadi taifa kuuona mwli wake!
on a serious note,nilikuwa nimeuweka usingizi baada ya kutoka nightshift,nilikuwa nafanya tempo ya receptionist ktk hotel,nashituka saa tisa nan mchana nasikia watoto wa wenye nyumba,nilikua nimepanga wanaongea uwani ,nyerere kafa,nikaoga faster na kuwahi job ili nikaangalie ktk Tv,nilikua naingia saa tisa job,ndo nikakuta nyimbo za maombolezo,nakumbuka usiku yake tukiwa job,mi na wahudumu wa kike tulikuwa tuna alternate kutoka kutizama iTv na video kwani tulikuwa na mkanda wa x,ulikuwa unasaidia kutusahaulisha majonzi,ha ha ha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…