Kifo cha Sokoine: Watoto wake wataka mwili uchunguzwe kubaini kama alikufa kwa ajali au la!

Kifo cha Sokoine: Watoto wake wataka mwili uchunguzwe kubaini kama alikufa kwa ajali au la!

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
sokoine.jpg

Picha: Gari lililosababisha kifo cha Hayati Sokoine​

Katika hali ya kushangaza, watoto na baadhi ya ndugu wa aliekuwa waziri mkuu wa Tanzania, Hayati Sokoine, wanataka uchunguzi ufanyike wa mwili wa marehemu ili kubaini kama ni kweli kifo chake kilitokana na ajali au laa.

Uamuzu huo ulofikiwa mara baada ya mwili wa Hayati Sokoine kuzikwa upya mwishoni mwa mwaka jana baada ya kabuli la awali kuharibiwa na tetemeko la ardhi katika milima ya Oldonyo Lengai.

Taarifa zinasema wanafamilia hao wanakusudia kuomba kibali serikalini ili wataalamu waufanyie uchunguzi mwili huo kubaini chanzo cha kifo chake.

Kulingana na taarifa za gazeti la Tanzanian Daima la tarehe 07/04/2013,ambapo habari hii imeelezwa kwa kirefu zinasema uamuzi huo ni kutokana na hofu kuwa huenda kifo chake kilitokana na hujuma za wale waliokuwa wakimpinga hayati Sokoine katika vita vyake vya kupambana na wahujumu uchumii wakati huo.

Imeelezwa mh.Lowassa ni miongoni mwa watu waliohudhuria mazishi hayo yalifanyika saa saba za usiku mwishoni mwa mwaka jana.

CHANZO:TANZANIA DAIMA ONLINE.
 
Hii habari inanichanganya. Nakiri kwamba sikuwahi kusikia kabisa habari za mazishi ya pili ya Ndugu Edward Moringe Sokoine hapo mwaka jana (sijui ni tarehe zip za mwezi upi?). N'nachokumbuka tu ni kwamba Moringe tulimzika katikati ya zizi la ng'ombe kijijini kwao Monduli na zizi likaendelea kutumika kusetiri ng'ombe kama ilivyo desturi yetu. Nakumbuka mengi yalisemwa baada ya kifo cha Moringe; ya kishirikina na ya kimafya kinyume kabisa na "post mortem report" ya madaktari. Leo ninapopata habari kama hii najiuliza maswali yafuatayo:

  1. tangu Sokoine afariki tarehe 12 Aprili 1984 hao watoto wake walikuwa wapi?
  2. Post mortem investigation hufainyika ili kubaini sababu za kifo cha marehemu si kwa malengo ya maelezo na kumbu kumbu tu bali pia ili kuchukua hatua kama kuna ushaidi wa kutosha kwamba kifo kimesababishwa na uzembe au makusudi ya mtu yeyote. uchunguzi huu ukifanyika sasa na ikagundulika kuna mazingira ya kuwa kifo kilisababishwa na makusudi au uzembe wa yeyote itasaida nini iwapo wasabishaji walishakufa miaka mingi?
  3. Mazingira mazuri zaidi ya kufanya post mortem investigation ni wakatimwili bado mbichi kikemikali. Kwa hali ya kifo hiki cha takribani miaka 29 tangu kitokee na mazingira aliyozikwa (na kuzikwa tena baada ya tetemeko) huo uchunguzi utatumia sayansi ipi?
  4. Uchunguzi huu unachochewa na nini sasa hivi na una maslahi gani kwa taifa na familia (kwa hao watoto wa marehemu?)
 
Miaka 29 ni mingi sana japo ilo linawezekana kama marehemu wanahisi alikufa kwa sumu
 
ama kwel magamba kkikulacho kinguoni kwako....ngoja tusubiri utasikiia tume imeundwa!
 
wamarekani walimfukua rais wao aliyekufa baada ya miaka 100 na kumfanyia uchunguzi km aliuwawa kwa sumu au la

Wapalestina kwa msaada wa Franch wakonjiani kumfanyia uchunguzi alie kuwa kiongozi wao
 
Washukuru Mungu na ubunge waliokumbukwa else watakuja humu watoto wa HORACE KOLIMBA;NA WENGINE WENGI TU EMBU OMBBEN BABAZENU WALALE PEMA PEPONI BASI MENGINE WAACHIEN MUNGU
 
Hii habari inanichanganya. Nakiri kwamba sikuwahi kusikia kabisa habari za mazishi ya pili ya Ndugu Edward Moringe Sokoine hapo mwaka jana (sijui ni tarehe zip za mwezi upi?). N'nachokumbuka tu ni kwamba Moringe tulimzika katikati ya zizi la ng'ombe kijijini kwao Monduli na zizi likaendelea kutumika kusetiri ng'ombe kama ilivyo desturi yetu. Nakumbuka mengi yalisemwa baada ya kifo cha Moringe; ya kishirikina na ya kimafya kinyume kabisa na "post mortem report" ya madaktari. Leo ninapopata habari kama hii najiuliza maswali yafuatayo:

  1. tangu Sokoine afariki tarehe 12 Aprili 1984 hao watoto wake walikuwa wapi?
  2. Post mortem investigation hufainyika ili kubaini sababu za kifo cha marehemu si kwa malengo ya maelezo na kumbu kumbu tu bali pia ili kuchukua hatua kama kuna ushaidi wa kutosha kwamba kifo kimesababishwa na uzembe au makusudi ya mtu yeyote. uchunguzi huu ukifanyika sasa na ikagundulika kuna mazingira ya kuwa kifo kilisababishwa na makusudi au uzembe wa yeyote itasaida nini iwapo wasabishaji walishakufa miaka mingi?
  3. Mazingira mazuri zaidi ya kufanya post mortem investigation ni wakatimwili bado mbichi kikemikali. Kwa hali ya kifo hiki cha takribani miaka 29 tangu kitokee na mazingira aliyozikwa (na kuzikwa tena baada ya tetemeko) huo uchunguzi utatumia sayansi ipi?
  4. Uchunguzi huu unachochewa na nini sasa hivi na una maslahi gani kwa taifa na familia (kwa hao watoto wa marehemu?)

Hapo kwenye red mkuu; uchunguzi unawezekana kwa sayansi hii hii tuliyonayo ila na mi nauliza kama ulivyouliza kwenye swali la nne.
 
Kazi ya Lowasa hiyo.

Natamani wangefanya vile wakati Marehemu Mzee Kawawa na Cleopa Msuya wote wakiwepo.
 
itafukuliwa miili mingi sana mi nataka hata kamanda kombe ufanyike uchunguzi kama risasi alipigwa kusudi au
 
wamarekani walimfukua rais wao aliyekufa baada ya miaka 100 na kumfanyia uchunguzi km aliuwawa kwa sumu au la

Wapalestina kwa msaada wa Franch wakonjiani kumfanyia uchunguzi alie kuwa kiongozi wao

  1. Tangu Sokoine afariki tarehe 12 Aprili 1984 hao watoto wake walikuwa wapi?
  2. Post mortem investigation hufainyika ili kubaini sababu za kifo cha marehemu si kwa malengo ya maelezo na kumbu kumbu tu bali pia ili kuchukua hatua kama kuna ushaidi wa kutosha kwamba kifo kimesababishwa na uzembe au makusudi ya mtu yeyote. uchunguzi huu ukifanyika sasa na ikagundulika kuna mazingira ya kuwa kifo kilisababishwa na makusudi au uzembe wa yeyote itasaida nini iwapo wasabishaji walishakufa miaka mingi?
  3. Mazingira mazuri zaidi ya kufanya post mortem investigation ni wakatimwili bado mbichi kikemikali. Kwa hali ya kifo hiki cha takribani miaka 29 tangu kitokee na mazingira aliyozikwa (na kuzikwa tena baada ya tetemeko) huo uchunguzi utatumia sayansi ipi?
  4. Uchunguzi huu unachochewa na nini sasa hivi na una maslahi gani kwa taifa na familia (kwa hao watoto wa marehemu?)

Hapo kwenye red mkuu; uchunguzi unawezekana kwa sayansi hii hii tuliyonayo ila na mi nauliza kama ulivyouliza kwenye swali la nne.

Inawezekana ndugu zangu MUSSOLIN, chipanga na Chum Chang ni motuary attendants na mnajua zaidi mambo ya maiti kuliko mimi. Lakini nina mashaka kama mmezingatia vizuri mazingira na namna ya wapalestina na wamarekani wanavyo"hifadhi" maiti (siyo kuzika kama sisi) na mazingira ya maiti ya Sokoine ilivyozikwa? Japokuwa ni kweli kwamba kama mifupa yake bado iko vizuri wanaweza (japo bila uhakika wa kutosha) kubaini kama ni risasi ilimuua, lakini hayo maswali yangu bado nayapa uzito,
 
Last edited by a moderator:
Miaka 29 ni mingi sana japo ilo linawezekana kama marehemu wanahisi alikufa kwa sumu

Yataibuka kwamba Edward Lowasa kuhusika na kifo cha Sokoine kama ilivyotokea Salim kuhusika Kumwua Karume Zanzibar. Ikumbukwe baada ya kifo cha Sokoine Edward Lowasa aliibuka ghafla, lakini kwangu naona ni tafsiri nyepesi.
 
Back
Top Bottom