Kifo hakipangwi na Mungu

Kifo hakipangwi na Mungu

Ahsante kwa kuniami

Ahlan wa sahlaan!

Kwa uelewa wangu,kuamini hakuhitaji factual knowledge

Ni kweli. Kwa sababu ukishakuwa na ukweli au uhakika wa kitu au jambo inakuwa siyo kuamini tena. Inakuwa ni kujua au kufahamu. Na ukishajua au ukishafahamu huwezi tena kuamini maana sasa unajua na/au unafahamu.

Lakini kuamini kwenyewe wala hakuna shida yoyote ile. Hakuna shida kwa sababu asilimia kubwa ya kuamini ni kufikiri na kujishawishi tu.

Hata mimi wakati mwingine huwa najishawishi kwamba mimi ni Superman, He-man, na Santa. Lakini kiukweli kweli mimi si Superman, He-man, Popeye the Sailor Man, wala Santa.

Mtu anaweza kuamini chochote anachotaka,lakini ili ujue lazima uwe direct perception pamoja na uelewa wa hicho kitu

Direct perception ndo nini?

Labda nikuulize wewe,

We niulize chochote tu....😉.

Unaamini kuwa Mungu hayupo au unajua kuwa Mungu hayupo?

Mimi kwa kweli sijui kama mungu hayupo.

Sina hakika kama hayupo na vilevile sina hakika kama yupo.

[utanisamehe kama wewe ni theist]

Kwa rejea za mijadala ya huko mbeleni, napenda kukufahamisha kuwa mimi ni agnostic.
 
Hujaelewa swali.

Naongelea pale mungu alipokuwa anapanga kuumba dunia.

Alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao uovu hauwezekaniki kabisa, hata mwanadamu ajitahidi vipi hawezi kufanya uovu.

Kama vile ambavyo mwanadamu hawezi kurudi nyuma katika muda kwa sasa, muda unaenda mbele tu.

Sasa kwa nini mungu hakuumba ulimwengu huo ambao uovu, mabaya, mateso, majanga etc haviwezekaniki kabisa?

Naongelea kabla mwanadamu hajatokea, mungu anaumba ulimwengu.Kwa hiyo usiniambie habari za uovu umeletwa na matendo ya binadamu.

That's logically impossible

Kama tukikubaliana kuwa sisi wanadamu tuna uwezo wa kuchagua
Basi kufanya maovu pia ni moja ya chaguo

Sasa dunia isiyo na maovu na mwanadamu mwenye uwezo wa kuchagua havichangamani[coexist]

Kwasababu kufanya maovu ni chaguo pia
Kuumba ulimwengu usio na maovu ni sawa na kumuondolea mwanadamu freewill
 
Nyani Ngabu said:
Direct perception ndo nini?
Nilisahau kuweka kiunganishi
Ili ujue lazima uwe na direct perception au cognition

Lazima uwe na uelewa mpana wa hicho kitu
That was my stance


Mimi kwa kweli sijui kama mungu hayupo.

Sina hakika kama hayupo na vilevile sina hakika kama yupo
Huwa napenda philosophical basis ya agonostics
Kwa sababu wapo tayari kwa matokeo yoyote
Aidha Mungu yupo au hayupo!

Kwa rejea za mijadala ya huko mbeleni, napenda kukufahamisha kuwa mimi ni agnostic.
Hahaa

Nashukuru kama wewe ni agnostic maana atheists ni wabishi kana kwamba wamesearch ulimwengu mzima na kupata uhakika kuwa Mungu

Japokuwa wao si omnipresents
 
Kama tukikubaliana kuwa sisi wanadamu tuna uwezo wa kuchagua
Basi kufanya maovu pia ni moja ya chaguo.


Sasa dunia isiyo na maovu na mwanadamu mwenye uwezo wa kuchagua havichangamani[coexist]

Kwasababu kufanya maovu ni chaguo pia
Kuumba ulimwengu usio na maovu ni sawa na kumuondolea mwanadamu freewill

Vipi kuhusu wale watu wenye genetic predisposition to violent behavior?

Nao wana uwezo wa kuchagua kutofanya maovu?

 
You are employing sidetracking tactics.

Hapa tupo tunaongelea uwepo na uwezo wa mungu halafu wewe unaleta habari za Jupita.

Maswali umeulizwa toka jana. Ukaahidi utarudi kuyajibu ukishakunywa chai.

Nasadiki chai ushakunywa na pengine hata chakula cha mchana ushakula. Sitashangaa kama hadi supu ushakunywa.

Maswali yangu bado hujajibu lakini unaniuliza swali lako.

Nikikujibu hilo swali lako tutatoka kwenye maswali niliyokuuliza na kuanza kuhojiana kuhusu Jupita.

Hapana. Jibu kwanza maswali yangu. Tukimalizana na hayo ndo tutaenda huko kwenye Jupita na hata Mushtara kama utapenda.

Sawa?
Kwamba nikujibu kama naamini au najua kama Mungu yupo?

Niseme hivi...naamini kuwa Mungu yupo kupitia uzoefu wangu binafsi na kupitia kwa watu wengine.

Natamani niseme najua kuwa Mungu yupo lakini sitaki niseme hivyo kwa leo.
 
Kwamba nikujibu kama naamini au najua kama Mungu yupo?

Niseme hivi...naamini kuwa Mungu yupo kupitia uzoefu wangu binafsi na kupitia kwa watu wengine.

Natamani niseme najua kuwa Mungu yupo lakini sitaki niseme hivyo kwa leo.

Case closed!
 
Bado hujaelewa swali. Hiyo complexity imekuja bila mungu kuipanga? Au alipanga iwepo na baadaye ikaleta mabaya?

Kama imekuja bila mungu kuipanga, je ni kweli mungu anajua na kuweza yote? Mbona complexity imekuja bila kupangwa?

Kama aliipanga complexity iwepo na baadaye ikaleta mabaya, utasemaje kwamba hakuumba ulimwengu unaowezekana kuwa na mabaya?

In any case, ultimately your god is responsible for the world.Ukisema watu wamefanya dhambi ndiyo maana ulimwengu ukawa na mabaya, nitakuuliza, mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao watu hawawezi kufanya dhambi?



Mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao uchu wa madaraka hauwezekani?



Mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao uchangudoa hauwezekani?

Kama alishindwa, ni kweli ana uwezo wote?

Kama hakushindwa ila aliamua tu kutouumba, je, ni kweli ana upendo wote?

Mfano wako wa mzazi na mtoto ni mfano fyongo. Mzazi hana control juu ya maisha ya mtoto kama mnavyosema mungu ana control juu ya ulimwengu. Unapotoa mfano, toa mfano wa vitu vinavyofanana ama kulingana kwa namna Fulani.



Mfano wako una mawaa na mtu anayetumia mantiki hawezi hata kuutumia.

Zaidi ya hapo, kama unajua kwamba huwezi kumlaumu mzazi kwa makosa ya mtoto, wala mtoto kwa makosa ya mzazi, ungejua kwamba habari ya mungu kumhukumu mtoto kuzaliwa mfu kwa sababu mama yake alikuwa mlevi ni habari isiyoyumkinika kwa mtu yeyote anayetumia ubongo wake kufikiri.
Mungu katuumba na utashi (free will) tofauti na mimea na wanyama. Ile kuamua jema na baya. Unaweza kuamua kuishi au kufa.

Huwezi kumpangia Mungu. Hivyo ndivyo alivyoamua mfumo wa ulimwengu uwe. Kwamba kaumba dunia lakini katuachia jukumu sisi wanadamu tuamue jinsi gani dunia iwe....ama nzuri ama mbaya.

Kuna shida gani hapo?
 
Huwa napenda philosophical basis ya agonostics
Kwa sababu wapo tayari kwa matokeo yoyote
Aidha Mungu yupo au hayupo!

Yup....we are open-minded, rational, and reasonable!

Nashukuru kama wewe ni agnostic maana atheists ni wabishi kana kwamba wamesearch ulimwengu mzima na kupata uhakika kuwa Mungu

Mimi naona atheists ni bora mara mia kuliko theists.

Walau atheists wanatumia akili/ mantiki katika kupinga uwepo wa mungu.

Theists wao ni mwendo wa hisia na mambo ya kufikirika tu. Matumizi yao ya akili ni kidogo sana. Wengine hata tofauti ya kujua na kuamini hawaijui.
 
Mungu katuumba na utashi (free will) tofauti na mimea na wanyama. Ile kuamua jema na baya. Unaweza kuamua kuishi au kufa.

Huwezi kumpangia Mungu. Hivyo ndivyo alivyoamua mfumo wa ulimwengu uwe. Kwamba kaumba dunia lakini katuachia jukumu sisi wanadamu tuamue jinsi gani dunia iwe....ama nzuri ama mbaya.

Kuna shida gani hapo?

Sijataka kumpangia mungu wako, nataka kujua kama unamuelewa na mimi kumuelewa pia. Kwa sababu kwa sasa hivi ha make sense.

Habari ya kwamba mungu katuumba na free will si kweli.

Mimi nataka kurudi 1982, siwezi kurudi. Free will iko wapi hapo?

Utaona kwamba ulimwengu hauna complete free will. Kuna mambo hatuwezi kufanya.

Sasa kama ulimwengu umeumbwa kuna mambo hatuwezi kufanya, kwa nini mungu hakuumba ulimwengu ambao mabaya, maovu, majanga, magonjwa etc hayawezekani?

Hujajibu hili swali.

Ukisema "huwezi kumpangia mungu, hivyo ndivyo alivyoamua", unachoniambia hapa ni kwamba huwezi kujibu swali langu.

Kama huwezi kujibu swali langu, huelewi unachokiamini.

Kama huelewi unachokiamini, inawezekana kabisa unachokiamini kama mungu hakipo.
 
Sijataka kumpangia mungu wako, nataka kujua kama unamuelewa na mimi kumuelewa pia. Kwa sababu kwa sasa hivi ha make sense.

Habari ya kwamba mungu katuumba na free will si kweli.

Mimi nataka kurudi 1982, siwezi kurudi. Free will iko wapi hapo?

Utaona kwamba ulimwengu hauna complete free will. Kuna mambo hatuwezi kufanya.

Sasa kama ulimwengu umeumbwa kuna mambo hatuwezi kufanya, kwa nini mungu hakuumba ulimwengu ambao mabaya, maovu, majanga, magonjwa etc hayawezekani?

Hujajibu hili swali.

Ukisema "huwezi kumpangia mungu, hivyo ndivyo alivyoamua", unachoniambia hapa ni kwamba huwezi kujibu swali langu.

Kama huwezi kujibu swali langu, huelewi unachokiamini.

Kama huelewi unachokiamini, inawezekana kabisa unachokiamini kama mungu hakipo.
Mkuu hakuna andiko Mungu linalotaka watu wamwelewe ila maandiko yanataka watu wamwamini na siyo kuelewa ukijua kutofautisha hayo maneno mawili basi hutakuwa na tatizo,, tena anataka uchague kumwamini au kutomwamini wala hakulazimishi
 
Mkuu hakuna andiko Mungu linalotaka watu wamwelewe ila maandiko yanataka watu wamwamini na siyo kuelewa ukijua kutofautisha hayo maneno mawili basi hutakuwa na tatizo,, tena anataka uchague kumwamini au kutomwamini wala hakulazimishi

Kwa nini wamuamini na si kumuelewa?
 
Mkuu hakuna andiko Mungu linalotaka watu wamwelewe ila maandiko yanataka watu wamwamini na siyo kuelewa ukijua kutofautisha hayo maneno mawili basi hutakuwa na tatizo,, tena anataka uchague kumwamini au kutomwamini wala hakulazimishi
Nani kasema nafuata andiko la mungu?

Mimi hata sikubali uwepo wa mungu, nitafuata vipi andiko la mungu?

Ukiamini bila kuelewa una tofauti gani na msukule?
 
Sasa kama hutaki kusoma maandiko yanayomhusu Mungu utaelew vp mkuu,, nimekwmbia hakuna lazma ni uamzi wwe kama hukubali basi fanya shuguli zingine tuachie Mungu wetu
 
Sijataka kumpangia mungu wako, nataka kujua kama unamuelewa na mimi kumuelewa pia. Kwa sababu kwa sasa hivi ha make sense.

Habari ya kwamba mungu katuumba na free will si kweli.

Mimi nataka kurudi 1982, siwezi kurudi. Free will iko wapi hapo?

Utaona kwamba ulimwengu hauna complete free will. Kuna mambo hatuwezi kufanya.

Sasa kama ulimwengu umeumbwa kuna mambo hatuwezi kufanya, kwa nini mungu hakuumba ulimwengu ambao mabaya, maovu, majanga, magonjwa etc hayawezekani?

Hujajibu hili swali.

Ukisema "huwezi kumpangia mungu, hivyo ndivyo alivyoamua", unachoniambia hapa ni kwamba huwezi kujibu swali langu.

Kama huwezi kujibu swali langu, huelewi unachokiamini.

Kama huelewi unachokiamini, inawezekana kabisa unachokiamini kama mungu hakipo.
Honestly....sina majibu. Hata mimi wakati mwingine huwa najiuliza hivyo hivyo.
But in the end, I choose to (cautiously) believe.
 
Sasa kama hutaki kusoma maandiko yanayomhusu Mungu utaelew vp mkuu,, nimekwmbia hakuna lazma ni uamzi wwe kama hukubali basi fanya shuguli zingine tuachie Mungu wetu
Nani kasema hataki kusoma maandiko yanayomhusu mungu?

Wewe umesoma vitabu gani vinavyomhusu mungu?
 
Kwa imani yangu nasoma biblia ndiyo guide yangu ya kuimarisha imani yangu, nakuombea kiranga upate pia muda wa kumwamini Mungu kabla hujaondoka duniani,, narudia kusema 'swali kuhusu Mungu halina jibu' unapaswa kumwamini basi
 
Sijataka kumpangia mungu wako, nataka kujua kama unamuelewa na mimi kumuelewa pia. Kwa sababu kwa sasa hivi ha make sense.

Habari ya kwamba mungu katuumba na free will si kweli.

Mimi nataka kurudi 1982, siwezi kurudi. Free will iko wapi hapo?

Utaona kwamba ulimwengu hauna complete free will. Kuna mambo hatuwezi kufanya.

Sasa kama ulimwengu umeumbwa kuna mambo hatuwezi kufanya, kwa nini mungu hakuumba ulimwengu ambao mabaya, maovu, majanga, magonjwa etc hayawezekani?

Hujajibu hili swali.

Ukisema "huwezi kumpangia mungu, hivyo ndivyo alivyoamua", unachoniambia hapa ni kwamba huwezi kujibu swali langu.

Kama huwezi kujibu swali langu, huelewi unachokiamini.

Kama huelewi unachokiamini, inawezekana kabisa unachokiamini kama mungu hakipo.
Siku zote nilikuwa nadhani naongea na Mtu mzima kumbe toto la mwaka 1982?

Ndio maaana nilikuwa nashindwa kuelewa Kosa lako ni nini.
Kumbe toto dogo bado.
 
Back
Top Bottom