Kifo kinatisha kwa sababu hatujui kule tuendako

Kifo kinatisha kwa sababu hatujui kule tuendako

Kifo ni hitimisho ya maisha yako hapa duniani,na hakuna anayekipenda.Na kikimfika mtu,haimaanishi kwamba ameenda mbinguni wala wapi,bali kila kitu kinakuwa kimeishia pale pale.Kutokana na hofu ya kifo,inatufanya kujipa matumaini ya kuwa tunaenda mbinguni n.k ili kujifariji.Ila ukweli hakuna cha mbingu wala nini.Ni sawasa na mende amekufa akaliwa na sisimizi,hata binadamu ni hivyo hivyo.Chamuhimu tu tuishi kwa wema tukijua tunapita
 
Sheikh wewe ni AHMADIYYA? Moto ni wa milele au ni muda (temporary) kwa fiqh za kisunni?



Common sense tu inahitaji kuona Mungu akiwa muadilifu,mwenye huruma, mrehemevu,mkarimu nk, zaidi kuliko binadamu, iweje mtu atende makosa, mfano wizi nk, mahakama za duniani zimuhukumu kifungo cha miaka kadhaa na akishamaliza kifungo anakuwa huru, lakini eti Mungu amuingize mkosefu motoni MILELE kwa makosa aliyotenda kwa muda fulani kipindi alipoishi hapa duniani !!??. Where is the absolute justice??!!

Hiyo "adhabu" ya moto ni kutokana na mapenzi na huruma yake, mfano ni kama vile mzazi kumpatia Quinine au muarubaini mtoto wake anayeugua malaria.

Qur'an na hadithi zinaunga mkono kuwa jehanamu siyo ya milele ila itakuwa "Abadan" yaani ya muda mrefu sana.
 
Kifo ni starehe , subiri kama unavyosubiri x- mas au mwaka mpya . Unaachana na haya maujanjajanja ya duniani . Tulitishwa na wamisionary kuwa kuna motoni na mbinguni hivyo hofu ni moto .
 
Hii mada ni nzito na sintofahamu yakutosha
Kwa uelewa wangu kifo ni kama ganzi ya ufamu isio eleweka na kuishia hapo ki dunia ndivyo navyo fahamu kiroho haina record kamili japo akili tunazo kwanini tusifanye kityu.
 
hv JF hakuna aliyekufa aje atupe updated kuhusu kifo ?



Usingizi ni nusu ya kifo, huna haja ya kumtafuta aliyekufa na kufufuka ili aje akusimulie kifo ninini!

Weka fikra zako unapolala usingizi na usiamke tena ukiwa katika hali hiyo, tofauti ni hii kwamba usingizi ni "kifo chepesi" ambapo mtu huamka baada ya kulala na akaendelea na shughuli zake na kifo ni usingizi mzito (too deep sleep) ambapo mtu hawezi tena kuamka hadi siku ya Akhera.

Kwa hiyo unapotafakari kuhusu usingizi hapo utapata kujua angalau kifo kinafananaje (resemblance).
 
Kifo kimebaki kuwa siri nzito kati ya yule aliyepata umauti na mola wake kwa sababu moja tu kwenye kifo hakuna uhai unaoweza kumfanya yule aliye mfu kusema yale anayoyaona mara tu baada ya kifo chake,

Kuna elimu nyingi zinazoelezea Kifo ziko zile ambazo ukizisoma zinakuongezea maarifa na nini kinatokea baada ya kifo chako,

Refer;

Sanaa ya kifo - JamiiForums

Licha ya Elimu hizo Adimu lakini bado hakuna ithibati ya moja kwa moja hivyo Kumeweza kukifanya Kifo bado kuwa ni siri kati ya yule marehemu na mola wake,

Kuna mengi ya kujiuliza na yakuogopesha kwa kweli kwa mfano
Ukiingia kwenye upande wa imani tunaambiwa Lazaro alifufuka katika wafu kwa maana hiyo lazaro ni mmoja kati ya wale wachache walioonja chungu ya mauti na kurudishiwa uhai wake tena,

Kama ni kweli kwanini lazaro hakuwahi kusema kile alichokumbana nacho baada ya kifo chake na badala yake ametuachia maswali na indication nyingi kuhusu kifo naweza kusema lazaro alikuwa mbinafsi kwa nini hakutaka wengine tujue.?

Upande wa pili pia wanasema ukifa unaenda kukutana na starehe ambayo hujawahi pata tangu uingie duniani ,hakuna magonjwa ,misosi ya kila aina ,bila kusahau mademu wakali ambao ni bikra ,

Ukija pia kuangalia huyo anaekuelezea ilo somo na kukuhubiria kuhusu raha na starehe zinazopatikana baada ya kifo Maisha yake ni ya kugongea na tabu tupu,unabaki kujiuliza kama ni kweli kuna hizo starehe kwa nini Asife yeye akazipate hizo Raha?

Wakuu nisiwachoshe sana ila kuna indication nyingi sana kuhusu kifo,hakuna namna yeyote ya kuelezea kuhusu kifo,kifo kinatisha kwa sababu kila mmoja wetu anajua ni lazima atakufa lakini hakuna anaejua ni nini kitamtokea baada ya kifo chake,

Na ndio maana kifo kinaogopeka.
Kinachitisha kwenye swala la kifo siyo kifo chenyewe, ni namna au manner ya namna kifo chenyewe ambavyo huwa kinakuja kwamba lazima upitie taabu na /au maumivu makali. Ingekuwa watu wanafariki pasipo maumivu yoyote let's say wakiwa hata usingizini, wachache sana wangeogopa kifo!
 
Common sense tu inahitaji kuona Mungu akiwa muadilifu,mwenye huruma, mrehemevu,mkarimu nk, zaidi kuliko binadamu, iweje mtu atende makosa, mfano wizi nk, mahakama za duniani zimuhukumu kifungo cha miaka kadhaa na akishamaliza kifungo anakuwa huru, lakini eti Mungu amuingize mkosefu motoni MILELE kwa makosa aliyotenda kwa muda fulani kipindi alipoishi hapa duniani !!??. Where is the absolute justice??!!

Hiyo "adhabu" ya moto ni kutokana na mapenzi na huruma yake, mfano ni kama vile mzazi kumpatia Quinine au muarubaini mtoto wake anayeugua malaria.

Qur'an na hadithi zinaunga mkono kuwa jehanamu siyo ya milele ila itakuwa "Abadan" yaani ya muda mrefu sana.
Uislamu ni dini ya mapokeo hususan ktk mambo ya ghaibu, yaani tunaamini kuran yote na Hadith sahihi zote tena si kwa uewelewa wetu bali kama walivyoelewa Maswahaba Allah awaridhie wote. Huu ni msingi muhimu sana ktk dini ya uislamu. Kwahivyo basi kwa mujibu wa Quran na Sunnah kama walivyofahamu Maswahaba Allah awaridhie wapo watu watakao kaa motoni MILELE na wapo watu watakaa motoni kwa muda fulani kisha watatolewa humo na kupelekwa motoni.
 
Sioni haja ya kuogopa kifo mkuu Zero IQ , uliwahi kujiuliza ulipokua upo tumboni kwa mamayo ama kama umepitia (IVF) in-vitro fertilisation ulikua unajua unaenda wapi, ama uko wapi? Kama ulikua hujui don't bother yourself about death experience! Je, kama uta transcend na kuingia kwenye another womb?
je, kama kabla ya kuwa hapo ulipo uliwahi kuishi sema tu upo clouded na conscious mind na hujawahi enda beyond ujue kuna nini?
Mfano, budha kabla ya kuzaliwa anasema alikuwa ni tembo.. vipi kuhusu wewe?
Btw,
Maisha mazuri sio jumla ya miaka uloishi hapa duniani bali ni kwa kiasi gani ume serve the humanity, universe.. sio unaishi kama methusela wa kwenye biblia ya wakristo and yet hakufanya chochote kwa mungu wake.
within u all answers to ur questions resides. .
Start ur journey home brother.
Mkuu umetisha sana
 
Mama yangu ni nurse muhimbili zaidi ya miaka 30 , aliwahi kuniambia Kwa experience yake ya kuwaona wagonjwa wakifariki aliniambia Kwa mtu anayekufa taratibu anajua wapi anaenda.
Aliniambia amewahi kushuhudia zaidi ya Mara kumi wagonjwa wanatoa tabasamu wakifurahia malaika wakija kuwachukua huku wakisifia mji wanaokwenda ni mzuri sana, akazidi kuniambia utashangaa mgonjwa alikuwa Amalia maumivu makali ya ugonjwa Mara anabadilika anaanza kutabasamu na anakuwa kama anataka kupaa huku akiwasihi malaika wamchukue.
Na upande wa pili wanaokwenda sehemu mbaya ndio balaa bora niishie hapa
Mkuu naomba umalizie wanaokwenda upande wa pili please.
 
mbona umesema ulikua haupo kisha ukawepo ,thena utakua haupo milele,kwanini baada ya kutokuwepo isitokee uwepo tena kisha uwe haupo then uwepo tena,kwanini baada ya kutokewepo hii mara ya pili iwe ndio forever wakati hata mwazo ulikua haupo kisha ukawepo
Ha ha haa

JF raha sana yaan nimejikuta nimecheka kwa Nguvu afu katikati ya watu
 
Back
Top Bottom