Kigamboni Bridge Contract Signed

Serikali ya Tanzania imetiliana saini na kampuni moja ya uchina kujenga daraja la kigamboni.
Ujenzi unatarajiwa kuanza mapema mwezi huu ambapo katika harakati za ujenzi wake kutakuwa ajira 1000 kwa wakandarasi na ajira zingine 2000 kwa wafanyakazi wa kawaida.

My take.huu ni ukombozi wa wana wa kigamboni ambao juzi kati apa wamepandishiwa nauli.
 
Hongera NSSF na serikali kwa ujumla wake. Habari kama hii hauwezi ukapata wachangiaji wengi kwa vile wachangiaji wengi wameshazoea habari za ufisadi na zinazodhohofisha serikali. Tubadilike watz
 
Hongera NSSF na serikali kwa ujumla wake. Habari kama hii hauwezi ukapata wachangiaji wengi kwa vile wachangiaji wengi wameshazoea habari za ufisadi na zinazodhohofisha serikali. Tubadilike watz

Serikali ndiyo imeshazoea mambo ya ufisadi na ndiyo inazidi kujidhoofisha yenyewe ndiyo ibadilike
 
Design iliyochaguliwa siyo hiyo kwenye picha zilizotangulia. Design hii ilikuwa ni kama daraja lingekatisha pale magogoni. Huo mduara ni kwa ajili ya kupandisha magari urefu ambao daraja lingebidi liwe kama lingejengwa hapo kwenye lango la bandari.

Design iliyochaguliwa iko simple zaidi. Ni design isiyohitaji daraja lililo juu sana kwa sababu linajengwa kule mbele ya kurasini oil depot, sehemu ambao meli kubwa hazifiki.

Pamoja na yote hayo, mimi najiuliza bei hiyo ya 214 Billion Shs na muda wa Miaka 3 kulijenga. Ni gharama kubwa mno na ni muda mrefu sana wa kujenga daraja la kilometer 4. Mimi nina wasiwasi kuwa hapa kuna ufisadi uliojificha kama ule wa twin towers. Tena ukizingatia ni pesa za NSSF, pesa za SU, a.k.a sizizo na mwenyewe...🙁
 
kumbe daraja tu, nilifikiri wamesaini pia kutujengea mji wetu mpya.
 
Mkuu imetulia lkn hii ya kigamboni ni BOT[/QUOT

Offcourse at that magnitude! No doubt hata Kama sio kuiba Kama unaprofessional inayomatch na mradi itakulipa tu in 36months sio mchezo.
 
Maandalizi ya Bush kutwaa mradi wa Kigamboni Modern City,ngoja tuone kama kazi itafanyika
 
Halina. Hawajazingatia watembea miguu kwani muda wao kuthaminiwa haujafika.
,

Hii inaonesha kuwa MJI WA KIGAMBONI UTAKUWA NI WA KIBEPARI ZAIDI na kuwa watakaokaa maeneno hayo ni watu WENYE MAGARI TU ! au siyo ? Naomba Mr NSSf anijibu tafadhali ...haingii akilini kujenga daraja ambalo halina sehemu ya waenda kwa miguu wala baskeli , ni wazi huo ni mji mtarajiwa wa KIBEPARI ! Mr.NSSF tafadhali nijibu nina shauku!
 
Maandalizi ya Bush kutwaa mradi wa Kigamboni Modern City,ngoja tuone kama kazi itafanyika
,<br>
<br>
NA juzi tu alikuja kuona eneo lake na kukumbushia ile pesa yake alokwishalipa awali!
 
Interesting. . .
Ngoja sasa tuone kama kazi itafanyika au la.
na haya magari yetu yasiyo na break nzuri basi ajari lazima magari yatatumbukia baharini tu. daraja hili inaweza kuwa chinja chinja nyingine hasa kwenye hiyo duara
 
baskeli maguta na waenda kwa miguu watatumia vivuko. swali jingine?
 
Sisi tunataka kuona daraja kwani sas ni zaidi ya miaka mitano mnapiga porojo tu, Kusaini mkataba si kuanza kwa ujenzi.....Kinachotakiwa hapa ni daraja tu...Je huo mkataba na jamaa mmeusoma au mnatia tu sahihi?
Ndiyo ulikuwa wasiwasi wangu, halafu kuna mmoja wa waheshimiwa wetu alishawahi kusema kuwa wanasheria wetu hawana uzoefu wa mikataba ya kimataifa ndiyo maana tunaingia mikataba mibovu, kama haikuwa tu sababu isiyo na maana, sasa sijui kama hao waliosaini wameshakuwa na huo uwezo lakini kama haitoshi naogopa kile kipengele cha hata kama wakishindwa kujenga itabidi walipwe fidia ya kukatishiwa mkataba wao na zile charge za vifaa vya kuwapo nchini mwetu, Tunaomba mungu angalau hili daraja liishe iwe mfano mzuri na tupate angalau sehemu ya kupigia picha.
 
ukiumwa na nyoka hata ukiona kiunyasi unaruka..... ha ha ha. Mimi siko huko ila nafikiria tu ile 10% ya 214b, duh.... kufa kufaana.
 

Miaka 3 kutoka leo (2012) ni 2015.........na huhitaji kuambiwa kuna nini mwaka huo
 
it's politics kama kawaida yenu...huu mradi ulianza kupangwa tangu 1977 na mkandarasi alishapatikana tatizo mkasema ni ukosefu wa fedha, so mnataka kutuambia tangu 77 hadi leo 2012 ndio mmepata fedha?? kwa nini leo?? kwa nini uwe wa miaka 3 wakati fedha zipo na hao wachina wana uwezo wa kujenga kwa mwaka mmoja?? kila mtu anajua 2015 ni mwaka wa uchaguzi msituzuge.. matumizi ya kodi za wananchi ni pamoja na kujenga madaraja, barabara bora na kadhalika, toka mwaka 77 kodi za wananchi hazijatosha kufanya miradi kama hiyo?? acheni siasa.
 
inatakiwa tumnadi mgombea wetu wa 2015, na moja kati ya vivutio (performance yetu) litakuwa ni hili daraja la kisasa kabisa East Africa and Central, Pia tutakuwa ndiyo tumemalizia mradi mkubwa kabisa wa MegaWatt 3000 na umeshaingizwa kwenye grid ya taifa ili kutomomeza kabisa tatizo la umeme liwe ni ndoto.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…