Kigezo gani unatumia kuchagua mavazi yako dada?

Kigezo gani unatumia kuchagua mavazi yako dada?

The Analyst

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2011
Posts
464
Reaction score
246
Mitindo ya mavazi ni mingi mno kwa wanawake, na wanapeyapenda haswaaaa! Ninachoomba kuwauliza wana MMU hapa JF ni je wanatumia kigezo gani kuchagua mavazi? Mfano ni viatu virefu sana kwa madada wafupi kwa madai ya kuongeza height kidogo ili kupendeza zaidi kwenye mavazi kama suruali au kumatch na urefu wa partner wake kama wanatoka nk. Hii kwangu....
icon14.png
maana huona wanapendeza zaidi.

>>>Nimekuwa napata wakati mgumu sana ninapomkuta mdada (mjanja sana tu) maeneo kama vyuo vikuu kavaa suruali inayombana sana wakati umbo lake linaelekea kuwa "7 au 9" Mtazamo wangu dada kama huyu angependeza zaidi kwa mavazi yanayombana juu na kumpwaya chini ya kiuno ili kuleta zile shape zinazozimikiwa na wengi. Madada wa Figure "8 au 6" wanapojibana na kuonesha figure zao halisi naona...
icon14.png
. To say the truth sichoki kuwa around.

>>>Swali langu halitakuwa na maana kama sitasema kila mtu kwa maumbile yake anapendeza katika mavazi ya aina fulani. Inapotokea mdada akavaa nguo ambayo ipo chati kama vipedo nk lakini haviendani na umbo lake (mtazamo wangu na wa enthusiasts wengi) anakuwa anatumia kigezo gani?

>>>Nimewahi kumshauri mdada mmoja kutovaa nguo za kubana sana hasa kiunoni kwenda chini kwa kuwa zinapunguza ass yake na kuonekana kama hana figure nzuri wakati Mungu kamjaaalia, akakubali siku ya kwanza na tulipotoka watu wengi wakawa wanageukageuka na kufanya tucheke lakini cha ajabu siku si nyingi nikamkuta na ki-jeans kimemshika halafu juu blauz gani sijui lina pwaya yaani kimsingi hajapendeza kabisa nikashangaa hawa wapendwa wetu vipi?

>>>Madada wengine mkivaa kanga (pasipokujali ni moja au mia) mnasababisha watu tusiende nje ya nyumba zetu lakini cha ajabu madada kama hawa utawakuta hata doti mbili hawana na kama zipo basi ndiyo zitakuwa zimejificha zaidi ktk makabati yao..........Why?....
 
Watu wengi tunashindwa kujielewa maumbo yetu ni ya aina gani natuvae nini, utamkuta msichana mwembamba kavaa guo kubwaaaa, hata hapendezi lakini ndio aina yake ya mavazi na huwezi mbadili mawazo
 
Hahaha Gaga umenichekesha..... Well mie naangalia umbo lol huwa naukumbuka ule wimbo wa uzuri wa Tausi .... Uzuri wangu wa tausi, kila vazi linakubali...lol ili mradi tu ni refu la kuficha hizi pingili zangu za miguu na kuficha makalio yangu ya 'embu' bila kusahau majaaliwa ya kifua changu.... Nsipojipenda mie na kujisifia nani atansifia?

Sijui kuvaa sarawili wala mnaita nini zile sijui leggings! Ntachekesha, mkanda sivai kwani kiuno nehhi! Lol tite sivai ntachekesha wenye matatizo yao kichwani.
 
kigezo ni umbo langu nipendeze na niwe huru,vigezo vingine ni inategemea naenda wapi,wakati gani na kwasababu gani na kumuona nani!!
 
Hahaha Gaga umenichekesha..... Well mie naangalia umbo lol huwa naukumbuka ule wimbo wa uzuri wa Tausi .... Uzuri wangu wa tausi, kila vazi linakubali...lol ili mradi tu ni refu la kuficha hizi pingili zangu za miguu na kuficha makalio yangu ya 'embu' bila kusahau majaaliwa ya kifua changu.... Nsipojipenda mie na kujisifia nani atansifia?

Sijui kuvaa sarawili wala mnaita nini zile sijui leggings! Ntachekesha, mkanda sivai kwani kiuno nehhi! Lol tite sivai ntachekesha wenye matatizo yao kichwani.
Hahahahaha umenichekesha sana mwali, tujisifie mwenzangu nani atakusifia? mie napenda shorts tu iwe skirts au pensi au kigauni mguu sawa na paja loooooooo???hahahahahaha kiuno ninacho wallah vile acha nipige umini tu.....na wewe pia ukisubiri miguu ikue itakua lini? we piga tu mpaka watazoea kama mange au halle berry
 
Hahaha Gaga umenichekesha..... Well mie naangalia umbo lol huwa naukumbuka ule wimbo wa uzuri wa Tausi .... Uzuri wangu wa tausi, kila vazi linakubali...lol ili mradi tu ni refu la kuficha hizi pingili zangu za miguu na kuficha makalio yangu ya 'embu' bila kusahau majaaliwa ya kifua changu.... Nsipojipenda mie na kujisifia nani atansifia?Sijui kuvaa sarawili wala mnaita nini zile sijui leggings! Ntachekesha, mkanda sivai kwani kiuno nehhi! Lol tite sivai ntachekesha wenye matatizo yao kichwani.
teh teh teh! We mrembo umenichekesha mno,sasa hii "embu" inakuwaje vile? Na pingili zisikuzuie kuvaa min unless kama ni tuthpik
 
Kama hamna umeme navaa jeans na ka t-shirt kakubana.
 
Kujitambua kiasi hicho kuzuri. Pia nashauri msikilize jamaa (kama ana tabia ya kupenda uonekane maridadi) Wakati mwingine unaweza kuwa tishio zaidi kwa vazi fulani na yeye akagundua mapema kabla wewe hujatambua.
Hahahahaha umenichekesha sana mwali, tujisifie mwenzangu nani atakusifia? mie napenda shorts tu iwe skirts au pensi au kigauni mguu sawa na paja loooooooo???hahahahahaha kiuno ninacho wallah vile acha nipige umini tu.....na wewe pia ukisubiri miguu ikue itakua lini? we piga tu mpaka watazoea kama mange au halle berry
 
Kujitambua kiasi hicho kuzuri. Pia nashauri msikilize jamaa (kama ana tabia ya kupenda uonekane maridadi) Wakati mwingine unaweza kuwa tishio zaidi kwa vazi fulani na yeye akagundua mapema kabla wewe hujatambua.
Infact yeye ndio anayependa na aliyenifanya niwe navaa navyovaa, na nikivaa tofauti ataniambia kwamba leo umechemka
 
1. Umbo....siwezi kuvaa nguo itakayonifanya nisione raha barabarani.Jeans too low kila saa kupandisha....kitop kifupi sana kila saa kushusha...suruale too tight hatua kupiga shida and so so...

2.Mood....nikiwa down napenda nguo ambazo ni loose au hata kama inabana nisiisikie ilivyoshika mwili.Tofauti kati ya jeans navitambaa laini.

3.Mazingira....niko wapi..nafanya nini na kwa wakati gani.

4.Company...niko nani!Siwezi kutembea na mama...bibi..shangazi au mjomba huku nimevaa nguo za kisichana sana.

Nadhani ni hayo tu kwa upande wangu....ila hua naboreka sana kumwona mtu kavaa nguo utadhani ya mdogo wake wa mwisho.Tumbo kuleee...nyuma pasi alafu anavaa nguo za kubana utadhani hataki kupumua sana.Bora mdogo avae loose kuliko bonge anaevaa tight isiyoendana na mwili wake.
 
Ninachoona siku hizi wanawake wengi wanavaa ovyo sana. Yaani nadhani watu hatutaki kupitwa na fashion regardless tutapendeza au la. Kuna watu wanavaa nguo mpaka unatamani kucheka. Mimi nadhani inabidi ujue ni nguo gani zinakupendeza na ndiyo iwe staili yako. Nguo nzuri ni ile inayo kufanya uwe na confidence regardless umesifiwa au la. Sipendi mtu avae nguo afu unamuona kabisa amekosa amani. Kwa mfano kama unaenda kwenye official meeting ukipiga suti ya suruali (au sketi) ni poa sana. It is better to over dress kuliko kwenda mahali casual afu uje ujione mdogo.
 
Nimeikubali! Ila kuna umuhimu wa kuwashauri mashost wenzenu pia. Si kila mdada lazima avae tight jeans au mibano mingine ya kuminya nyama. Wengine magauni yanawatoa mchicha kuliko mnavyodhania sasa kwa nini ujitese wakati wa ku-pee kwa kitu ambacho hata hakikupendezi?
1. Umbo....siwezi kuvaa nguo itakayonifanya nisione raha barabarani.Jeans too low kila saa kupandisha....kitop kifupi sana kila saa kushusha...suruale too tight hatua kupiga shida and so so...

2.Mood....nikiwa down napenda nguo ambazo ni loose au hata kama inabana nisiisikie ilivyoshika mwili.Tofauti kati ya jeans navitambaa laini.

3.Mazingira....niko wapi..nafanya nini na kwa wakati gani.

4.Company...niko nani!Siwezi kutembea na mama...bibi..shangazi au mjomba huku nimevaa nguo za kisichana sana.

Nadhani ni hayo tu kwa upande wangu....ila hua naboreka sana kumwona mtu kavaa nguo utadhani ya mdogo wake wa mwisho.Tumbo kuleee...nyuma pasi alafu anavaa nguo za kubana utadhani hataki kupumua sana.Bora mdogo avae loose kuliko bonge anaevaa tight isiyoendana na mwili wake.
 
Nimeikubali! Ila kuna umuhimu wa kuwashauri mashost wenzenu pia. Si kila mdada lazima avae tight jeans au mibano mingine ya kuminya nyama. Wengine magauni yanawatoa mchicha kuliko mnavyodhania sasa kwa nini ujitese wakati wa ku-pee kwa kitu ambacho hata hakikupendezi?
Kuna watu hawashauriki kabisaaaa....zaidi wataona unawaonea wivu.Ila nashukuru watu wangu wa karibu wanajua mapungufu yao kwa hiyo wanavaa kuendana na miili yao!
 
Mi huwa navaa nguo kuendana na mazingira,sehem huska pamoja na umbo langu
 
kigezo changu kikubwa ni Nguo safi,hua sijalishi nguo yoyote safi navaa,iwe jeans,kadeti au kitambaa.
 
Back
Top Bottom