Kigoma: Mbaroni kwa kumuua mama yake mzazi

Kigoma: Mbaroni kwa kumuua mama yake mzazi

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Jeshi la Polisi mkoani Kigoma linamshikilia kijana Helman Jonh (23) kwa tuhuma za kumuua mama yake mzazi Selina William (63).

Akizungumza leo Jumanne Februari Mosi 2022 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, James Manyama amesema kuwa kijana huyo alikuwa akimdai mama yake Sh300, 000.

Amesema tukio hilo limetokea Januari 05 katika kijiji cha Kinonko wilayani Kakonko ambapo kabla ya mama huyo kufariki dunia alijeruhiwa kwa kupigwa na mpini wa jembe na kijana huyo.

Amesema kuwa tukio hilo la mauaji ya Selina ni moja kati ya watu 10 ambao walipoteza maisha katika mkoa huo kwa mwezi Januari kutokana na matukio mbalimbali.

Kamanda Manyama amesema watu wengine tisa walifariki dunia kutokana na matukio tofauti ambayo yamesababishwa na wivu wa mapenzi, ulevi pamoja na watu watatu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi kuuawa na Jeshi hilo katika majibizano ya risasi baada ya kuvamia soko la kijiji cha Nyarugusu kwa lengo la kupora mali.

"Katika hatua za kuzuia uhalifu tumekamata silaha zilizo kuwa zikitumiwa na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi katika kufanya uhalifu pamoja na kuwashikilia watu sita akiwemo mwenyekiti wa kijiji cha Kabulazwili kutokana na kumiliki silaha aina ya gobole zilizokuwa zikitumika katika uhalifu," amesema Kamanda Manyama.

Chanzo: Mwananchi
 
Laki 3 pesa ya kula masaa machache tu wikiendi unamuondoa Mama yako mzazi kweli? Narejea kusema kwa mara nyingine vijana wa sasa wana msongo wa mawazo na tamaa za maisha haiwezekani kijana bado una nguvu kabisa tena kijana wa miaka 23 tu ambaye ukipambana kwa mwezi hiyo laki tatu unaipata uishie kutoa uhai wa mwezako inafikirisha sana?

Bora ukutane na simba utasalimika ila si kwenye kumi na nane ya vijana wa sasa maana asilimia kubwa wamechanganyikiwa.
 
Laki 3 pesa ya kula masaa machache tu wikiendi unamuondoa Mama yako mzazi kweli? Narejea kusema kwa mara nyingine vijana wa sasa wana msongo wa mawazo na tamaa za maisha haiwezekani kijana bado una nguvu kabisa tena kijana wa miaka 23 tu ambaye ukipambana kwa mwezi hiyo laki tatu unaipata.

Bora ukutane na simba utasalimika ila si kwenye kumi na nane ya vijana wa sasa maana asilimia kubwa yao wamechanganyikiwa.
Lak 3 ndogo kwako wee sio wengine, maisha magumu na mambo hayaeleweki. Japo haitoi uhalali wa kuua.
 
Duh! Mwaka huu umeanza kwa ardhi kunywa damu za watu
 
Lak 3 ndogo kwako wee sio wengine, maisha magumu na mambo hayaeleweki. Japo haitoi uhalali wa kuua.
Ndiyo auueee

Sema mijitu mingine ni zaidi ya wanyama

Ova
 
tamaa za maisha
Ndo jibu sahihi zaidi

Vijana wametanguliza tamaa sana. Nina mdogo wangu alizingua fiv akapata almost zero. Kakimbilia mjini huko kapata kazi maajabu anataka nimlipie kodi ya nyumba. Sasa najiuliza mshahara anaopata anafanyia nn ili hali baba na mama nawahudumia mimi akijitahidi sana ni elf 5 ya vocha kwa mama!!
 
Vijana tunamuhitaji Mungu sana yaani ukifatilia range ya umri wa hawa wauwaji ni vijana wadogo nguvu kazi ya taifa inaishia jela so sad
 
Jeshi la Polisi mkoani Kigoma linamshikilia kijana Helman Jonh (23) kwa tuhuma za kumuua mama yake mzazi Selina William (63).

Akizungumza leo Jumanne Februari Mosi 2022 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, James Manyama amesema kuwa kijana huyo alikuwa akimdai mama yake Sh300, 000.
Duh mauaji yamezidi sana wakati huu
 
Laki 3 pesa ya kula masaa machache tu wikiendi unamuondoa Mama yako mzazi kweli? Narejea kusema kwa mara nyingine vijana wa sasa wana msongo wa mawazo na tamaa za maisha haiwezekani kijana bado una nguvu kabisa tena kijana wa miaka 23 tu ambaye ukipambana kwa mwezi hiyo laki tatu unaipata.

Bora ukutane na simba utasalimika ila si kwenye kumi na nane ya vijana wa sasa maana asilimia kubwa wamechanganyikiwa.
Ni kweli vijana wanechanganyikiwa ila kukutana na simba hapana aisee. Labda simba wa pale msimbazi.

Ila simba mbarara wa Tsavo big no. Usithubutu
 
Kuua mzazi kwa sababu yeyote haikubaliki. Hata kama angejuwa anamdai billions
 
... wachaga (kabila la wauwaji) wako hadi Kigoma? Mkiambiwa haya mambo hayana cha ukabila iwe inaeleweka!
 
Duh! mwaka huu umeanza kwa ardhi kunywa damu za watu
Mpaka Januari hivi ndivyo mkeka unavyosoma..
20220202_122952.jpg


Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
 
Hii inaashiria matokeo mabaya ya kukithiri kwa hali duni ya vipato kutokana na kusinyaa kwa shughuli zinazoweza kuzalisha vipato kwa watu. Serikali ina wajibu mkubwa wa kutekeleza sera za uchumi zitakazoweza kuchochea uzalishaji na ajira kwenye sekta binafsi na serikalini, kuratibu mzunguko wa pesa ili uchochee shughuli za kiuchumi. Kuweka jitihada za makusudi kwenye kuchochea uzalishaji kwenye sekta za kilimo, mifugo na uvuvi kama kichocheo cha ajira na kipato kwa watu wengi......​
 
Back
Top Bottom