Kigugumizi cha CHADEMA juu ya akina Halima Mdee kinatokana na nini? Sikilizeni Rufaa na mtoe uamuzi wa mwisho

Mdee na wenzie hawawezi kufukuzwa Bungeni hata kamati kuu ya chama ikikaa na kutupilia mbali rufaa zao.
 
Baraza kuu linakaa muda gani, hivi kukaa na kusema haliwatambui wabunge wa viti maalumu chadema itapungukiwa na nn.
Kuna kitu nyuma ya pazia chadema hawakisemi na hilo swali limeulizwa muda mrefu.
 
UKIONA HAWATAKI KUKAA UJUWE KUNAMAHALA WANAENDA KUSHINDWA NA HAO KINA DADA WANAOGOPA KUMALIZANA NAO
 
Mtu akihukumiwa kifungo ataishi gerezani huku rufaa yake ikisikilizwa. matokeo ya rufaa ndo ama yamtoe hatiani au aendelee kuwa hatiani. Hukumu Cc ya cdm bado imesimama.
 
CCM manawaza uji pekee, katiba ya CHADEMA unaijua wewe kuliko viongozi wa CHADEMA? SHAME ON YOU
 
Kwahiyo kwa upeo wako chama kikifukuza mwanachama bunge linasubiri rufaa ikatwe ndio limsimamishe/mbunge?

is it a special case for CHADEMA au ni vyama vyote? Je katiba inasemaje kuhusu Hilo, je aliyeacha chama kama Mwambe, Lijualikali na wengine bunge lilikuwa sahihi kuwarudisha watu waliojitoa kwenye chama? Au ni special case kwa CHADEMA?

Je wao CCM wakimfukuza Mtu au CUF wakati ule nao Wanasheria tofauti kwenye katiba hiihii?

 
Usijishushie heahima yako Petro..

Hukumu ya Kamati Kuu ya Chadema ilishatolewa kwamba hawa wamevuliwa uanachama na Bunge lina taarifa yote na ushahidi wa Bunge kupokea taarifa hii ya Kamati Kuu upo..

Hawa hawapaswi kuwa Bungeni na hili unalifahamu vema Petro..

Kama walikata rufaa hilo haliwahalalishii kuwemo Bungeni kwani Hukumu ya Kamati Kuu ipo palepale kwamba hawa sio wanachama tena wa CDM, na kwanza waliokata rufai sio wote 19, vipi hao wengine ambao hawajakata rufau mbona wapo bungeni??..

Linda heshima yako ndg yangu.
 
Wenzako Chama kinachukua Ruzuku kama kawaida. Wale bado ni wanachama wa Chadema.
 
Nadhani kwasasa CHADEMA ina more serious issues kuliko hiyo rufaa ya covid 19.. Na usidhani CHADEMA ni ma layman kiasi cha kutojua wanafanya nini..!
Nani pale ana akili sasa, tunapenda tuwe na upinzani ila si wa aina ya CHADEMA. Hawako organized ata kidogo. Chama kisichojijenga kiuchumi ni chama au kikundi cha wahuni tu.
 
[emoji871]Na
Endapo watafukuzwa bungeni kweli.

[emoji871]Je! Mke wako atakuwa mmojawapo wa wabunge wapya halali kutoka Bawacha?
kutoka mamlaka halali za chadema?

[emoji871]Mnaacha kupambana na hali zenu kwa wakati na pia manufaa kwa familia zenu.
Mnabaki kuongoza kamati za Roho Mbaya Duniani.
 
 
waliwapeleka wenyewe wanaogopa wanawatoaje watu ambao tayari wana lamba asali
 
Majibu umepata sasa
 
waliwapeleka wenyewe wanaogopa wanawatoaje watu ambao tayari wana lamba asali
JF niliyoifahamu zaidi ya miaka 15 iliyopita, watu wa aina yako waliiogopa kama ukoma kwa sababu waliojiunga walikuwa na hoja, hekima na busara.

JF ya 2015 na kuendelea huhitaji hoja unahitaji tu kuwa na vidole (hata kama vimelemaa) na macho (hata kama yana makengeza) swaga tu...tayari wewe ni JF-expert member!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…