Kihasibu; Simba watapata bilioni 1 za CAF, Ni yanga pekee ndie ana nafasi ya kulipwa bilioni 2 au zaidi

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Kiasi unachopokea kihasibu tunahesabia ni baada ya kutoa matumizi.

Kwa kila safari ya kwenda kucheza mechi za nje, gharama inaweza kuwa milioni 40 kuanzia tiketi za ndege, gharama za malazi, vyakula na vinywaji, n.k.

Simba hadi wanafika robo fainali washakwenda nje mara 6 (mechi 2 za awali, mechi 3 za makundi na 1 ya robo), hivyo ni takribani milioni 240 imewatoka. Pesa atayolipwa simba ni dola laki 9 ambazo ukizidisha kwa 2,353 kiwango cha exchange kwa sasa ni 2,117,700,000 . baada ya kutoa matumizi ya milioni 240 inakuwa ni bilioni moja

Yanga hadi wamefikfa nusu fainali wameenda nje mara 8 hivyo ni takribani milioni 320 imewatoka. Pesa atayolipwa Yanga kwa uhakika hadi sasa ni dola milioni 1 ambazo ukizidisha kwa 2,353 kiwango cha exchange kwa sasa ni 2,353,000,000 . baada ya kutoa matumizi ya milioni 320 inakuwa bado inasoma bilioni 2. mechi ya fainali serikali itagaharamia.



 
Mpira una pesa. Ngoja niinunue Abajalo niipandishe ligi kuu tukiwashe. Wahuni wote wa mjini ni wetu.
Si mbaya hata ikiingia ligi kuu, Azam anacheua milioni 50 kwa kila timu za ligi kuu kila mwezi. sikuhizi huwezi sikia timu imekwama mishahara, usafiri ama hotel / lodge labda kuwe na udokozi uliokithiri.
 
Hizi Hesabu hazipo sawa, umesahau Yanga Alicheza Caf Champions league, mbona hujahesabu? Ama huko walisafiri Bure?
 
wakipewa hizo na hela za kuendesha timu msimu ujao watatoa wapi?
Nijuavyo mimi mkataba wa mchezaji na timu ni kulipwa mshahara hayo mengine ni bonus ( maelewano tu)
Bonus lazima iwepo, wachezaji wa Kisasa wanalipwa kwa mafanikio ya Timu, bila hivyo why wachezaji wapambane?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…