Kijana aliyemaliza JKT na kurudi nyumbani akili yake inakuwa kama mtu anayehangaika na kutafuta Rupia ya Mkoloni

Kijana aliyemaliza JKT na kurudi nyumbani akili yake inakuwa kama mtu anayehangaika na kutafuta Rupia ya Mkoloni

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Nimefuatilia mazungumzo ya vijana kadhaa waliomaliza mikataba yao ya JKT miaka 2 na wengine kuongezewa miaka au miezi kisha kurudi nyumbani bila ajira. Wengi wao akili zao zinakuwa na walakini utadhani watu wanaotafuta Rupia ya Mjerumani mapangoni na milimani.

Unaweza ukamuuliza swali moja akakujibu na maswali usiyomuuliza. Anakaa anasubiri nafasi za jeshi anasahau kuwa makambini nako kuna vijana wenzake ambao ni wabichi zaidi yake. Nilimsikia mmoja leo ananiuliza kuna nafasi za polisi, uhamiaji, fire na zimamoto zimetoka umeziona?

Nikamjibu hakuna nafasi, anasema zipo zitatangazwa mUda wowote nazisubiri. Nilimuonea huruma sana.

Mwingine akisikia Mh. Rais anahutubia tu anasikiliza huenda Rais atatoa tamko Op. Magufuli wote waajiriwe.

Hebu serikali ibadili mfumo wa JKT, kwakweli vijana hawaendi kule kujitolea bali wanakwenda kusaka ajira ndio maana kule humkuti mtoto wa kigogo na ukimkuta huyo harudi nyumbani baada ya kujitolea.

Vijana wanaorudi wengi akili zinafyatuka kidogo na kimbilio lao ni kwenye makampuni ya ulinzi ikiwemo SUMA JKT GUARD ambako hawapati fedha ya kukidhi mahitaji yao.

Thanks.
 
Nimefuatilia mazungumzo ya vijana kadhaa waliomalima mikataba yao ya jkt miaka 2 na wengine kuongezewa miaka au miezi kisha kurudi nyumbani bila ajira. Wengi wao akili zao zinakuwa na walakini utadhani watu wanaotafuta Rupia ya Mjerumani mapangoni na milimani.

Unaweza ukamuuliza swali moja akakujibu na maswali usiyomuuliza. Anakaa anasubiri nafasi za jeshi anasahau kuwa makambini nako kuna vijana wenzake ambao ni wabichi zaidi yake. Nilimsikia mmoja leo ananiuliza kuna nafasi za polisi, uhamiaji, fire na zimamoto zimetoka umeziona?

Nikamjibu hakuna nafasi, anasema zipo zitatangazwa mda wowote nazisubiri. Nilimuonea huruma sana.

Mwingine akisikia Mh. Rais anahutubia tu anasikiliza huenda Rais atatoa tamko Op. Magufuli wote waajiriwe.

Hebu serikali ibadili mfumo wa jkt, kwakweli vijana hawaendi kule kujitolea bali wanakwenda kusaka ajira ndio maana kule humkuti mtoto wa kigogo na ukimkuta huyo harudi nyumbani baada ya kujitolea.

Vijana wanaorudi wengi akili zinafyatuka kidogo na kimbilio lao ni kwenye makampuni ya ulinzi ikiwemo SUMA JKT GUARD ambako hawapati fedha ya kukidhi mahitaji yao.

Thanks.
Wewe shukuru Mungu tu usiombee mambo mengine ni magumu sana hawapendi kuwa hivyo niishie hapo tu..
 
Rai yangu wasije jiingiza kwenye Makundi mabaya hasa misimamo mikali ya dini/ Imani. Maana nina uhakika wakipata mentor wa kuwapandikiza mabaya na njaa waliyonayo basi chochote chaweza tokea.

Serikali ifuatilie movement ya hawa watu. Isiishie tu kusema "walisaini fomu kujitolea sio ajira"

Hiki kizazi chaweza kuwa haramu baadae kama hakuna jambo litafanyika

Emaphakadeni
 
Suma jkt ipo mwambie apeleke maombi huko... Kifupi asitegemee ajira za serikali huku umri ukizidi kwenda...
 
Wasiishie kufuatilia nyendo zao tu kama gaidi aliyetoka kwa msamaha jela, iwape hata office attendance au ulinzi kwenye ofisi za serikali. Serikali ina taasisi takribani 450 nazo zina matawi. Kila ofisi wakimpeleka moja au 2 watakaribia kumaliza tatizo na kuleta morali kwa vijana
Rai yangu wasije jiingiza kwenye Makundi mabaya hasa misimamo mikali ya dini/ Imani. Maana nina uhakika wakipata mentor wa kuwapandikiza mabaya na njaa waliyonayo basi chochote chaweza tokea.

Serikali ifuatilie movement ya hawa watu. Isiishie tu kusema "walisaini fomu kujitolea sio ajira"

Hiki kizazi chaweza kuwa haramu baadae kama hakuna jambo litafanyika

Emaphakadeni
 
Hao vijana wanamsongo wa mawazo hatari na pia ndoto za kuwa wanajeshi haziwaishigi mie mpaka naona hii ya kujitolea itoke wanateseka Sana kwa kuaminishwa kupata ajira jeshini au police
Yaani wanakuwa labda 20000 wanachaguliwa 20000 alafu bado wanajaribu kuvumilia waliobaki na kila mwaka wanaongezwa wengine matokeo wanafanyishwa kazi tuu mwisho kurudi home alafu hawashauriki hao ata[emoji119]
Wakwangu alishaanza kuchanganyikiwa anabaati kajenga ukuta mwenzie alishaanza kunywa mapombe mtaani na kuokota dampo kinyamwezi Ila aliitwa akatiboa hoiii [emoji17] akuamini
Kwa kifupi nawaonea huruma Sana vijana[emoji24][emoji24]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila Taasisi ina ikama yake ya rasilimali watu. Serikali haiwezi force kuwapa ajira ki rahisi hivyo
Wasiishie kufuatilia nyendo zao tu kama gaidi aliyetoka kwa msamaha jela, iwape hata office attendance au ulinzi kwenye ofisi za serikali. Serikali ina taasisi takribani 450 nazo zina matawi. Kila ofisi wakimpeleka moja au 2 watakaribia kumaliza tatizo na kuleta molari kwa vijana

Emaphakadeni
 
Dah nilikuepo pande hizo miaka ya nyuma kidogo .yaani mpaka leo naona kama DISHI langu liliyumba kidogo .siokama nilivyokua kabla
 
Back
Top Bottom