Kijana wangu ana mafindofindo (Tonsils). Tunashindwa kuelewa kama ni ugonjwa au ni maumbile yake.

Kijana wangu ana mafindofindo (Tonsils). Tunashindwa kuelewa kama ni ugonjwa au ni maumbile yake.

Engager

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2011
Posts
1,522
Reaction score
3,255
Kama kunamtu anauelewa au alishawahi kukutwa na hali hii naomba ushauri au experience yake.

Tuligundua mtoto ana mafindofindo yamevimba alipokuwa na umri wa miaka miwili. Tulijaribu kumtibu traditionally. Kuna dawa flani tuu ya kienyeji ya kuyachua kwa siku mbili yanakwisha yenyewe. Tumekuwa tukitumia njia hii tangu sisi tukiwa wadogo na tunapona. Ajabu kwa dogo iligonga mwamba. Hayakunyauka. Zoezi la kumchua tulilifanya kwa wiki kadhaa lakini hayakuisha..

Ilipita miezi kama sita, mafindofindo yamevimba vile vile. Tukaamua kumpeleka hospitali. Tukapewa dawa, tukaambiwa ikiisha bila kuonesha matokea, turudi tena. Dogo alitumia dozi ikaisha, yako vile vile. Tukarudi hospitali, tukabadilishiwa dawa bado hayakuisha. Tukashauriwa tumpeleke akafanyiwe upasuaji yaondolewe kwa njia hiyo. Huo ushauri sikuuafiki moja kwa moja.

Sasa hivi dogo anamiaka minne. Tumebadilisha dawa za kuchua mara kibao. Kila mwenye kudhani anaweza kusaidia, anatia utaalamu wake pale lakini mtoto kila ukimwangalia yapo tuu yamevimba vile vile. Kiasi nimeanza kuufikiria ushauri wa kumpeleka kufanyiwa upasuaji, lakini kunavitu vinanitatiza.

1. Tangu tumeyagundua, hakuwahi kuonesha dalili yoyote kwamba pengine yanamsumbua. Tunajua jinsi mafindofindo yakivimba yanavyouma, yanavyoumiza kichwa na kuleta vihoma homa, yanavyosumbua kumeza etc... lakini kwa huyu mtoto hatujawahi kuona mabadiliko hayo.

Mwanzo tulidhani labda anashindwa kuyatambua maumivu pengine sababu ni mdogo sana. Lakini sasa anamika mi4 walau anajua kuumwa kukoje na kuwa salama kukoje. Lakini ukimuuliza kama anaumia kumeza au makoo yanamuuma au kichwa anakataa, yaani hata kwa kumwangalia tuu unajua kabisa hapati taabu yoyote. Ila yapo. Yamevimba. Miaka miwili na sehemu sasa.

2. Muonekano wake. Hayaonekani kuwa na usaha au rangi ya kutatanisha. Yanaonekana kuwa na rangi sawasawa na ile ya kinywa chake tu ya kawaida. Ila yapo yamevimba. Kuna muda tunawaza au labda nae ni wa hivo hivo kimaumbile?!

Naona shida kubwa yanayo msababishia ni kwenye kupumua. Kunamuda akitulia, anapumua kwa sauti kama mtu aliye usingizini. Hii inatokea hasa usiku, sijawahi kumsikia mchana. Pia baadhi ya siku uwa anakoroma akisinzia.

Tatizo lingine ni kuugua mafua na kikohozi mara kwa mara. Mtoto hapitishi wiki mbili bila kuugua mafua, yakipona kikohozi kinapokea, kikipona anakuwa sawa chini ya wiki mbili anaugua tena.

Sina ushahidi wowote kama hayo matatizo yanahusiana moja kwa moja na mafindofindo aliyo nayo.

JF inawatu wengi, natarajia kupata chochote cha manufaa hapa kabla sijaamua kumpeleka kwenye upasuaji.
 
Kaka ni wasiwasi wako usimcheleweshe mtoto kupata upasuaji hii ilimtokea mtoto wa kaka angu Alikua na umri wa miaka miwili na nusu nenda hospital ya Regency au cardinal rugambwa moja kwa moja kwa daktari wa koo hii hali ni ya kawaida hoso zote mbili wana huduma nzuri katika sector hiyo
Nakumbuka ilikua unamsumbua hivyo hivyo inakuja anapewa dozi inakauka unakuja tena ndo tukaenda kwa daktari bingwa wa hizi mambo na ikaonekana tumemchelewesha mpka kufikia hatua ya kutoa usaha hvyo alipewa sindano KUMI kwaajili ya kukausha usaha ili afanyiwe upasuaji
Na upasuaji sio kwamba wanachana koo au shavu lahasha anafungua kinywa wanamsafisha hii haichukui muda ni ndani ya dkk 15 mpka 20s tayari ammesha maliza
Hali ya dogo ipo vizuri nakushauri ukipata muda nenda hospital tajwa hapo zote mbili ukifika reception waambie unamtaka daktari wa kinywa na Koo
Afya ni muhimu afya ni utajiri
 
Kaka ni wasiwasi wako usimcheleweshe mtoto kupata upasuaji hii ilimtokea mtoto wa kaka angu Alikua na umri wa miaka miwili na nusu nenda hospital ya Regency au cardinal rugambwa moja kwa moja kwa daktari wa koo hii hali ni ya kawaida hoso zote mbili wana huduma nzuri katika sector hiyo
Nakumbuka ilikua unamsumbua hivyo hivyo inakuja anapewa dozi inakauka unakuja tena ndo tukaenda kwa daktari bingwa wa hizi mambo na ikaonekana tumemchelewesha mpka kufikia hatua ya kutoa usaha hvyo alipewa sindano KUMI kwaajili ya kukausha usaha ili afanyiwe upasuaji
Na upasuaji sio kwamba wanachana koo au shavu lahasha anafungua kinywa wanamsafisha hii haichukui muda ni ndani ya dkk 15 mpka 20s tayari ammesha maliza
Hali ya dogo ipo vizuri nakushauri ukipata muda nenda hospital tajwa hapo zote mbili ukifika reception waambie unamtaka daktari wa kinywa na Koo
Afya ni muhimu afya ni utajiri
Asante kwa ushauri kaka. Nitafanyia kazi hili.
 
Ulifanikiwa mkuu kupata Suluhu? Ndio leo hii naona huu uzi jaman
 
Mkuu mwanangu alikuwa hivyo ila kuna Dr aligundua tatizo baada ya kuhangaika kila hospital

Alituambia aache vitu vyote vitamu kama pipi, juice aina zote na alipoacha tu tataizo likakoma kabisa na sasa amepona kabisa

Ni jambo la kushukuru Mungu kwa kutuelekeza kwa huyo Dr kumbe ilikuwa ni bacteria tu

Hebu jaribu hata Ice cream usimpe bali Apple na Yogurt tu
Mpe matunda sana ila mapipi na juice hizi hata soda usimpe kata kabisa
 
Tonsils ni mojawapo ya Kinga za Mwili.

Usizitoe au kuzipasua muache akue zitapona tu.

Kuvimba ni kawaida tu labda inflammation au infection ndogo ndogo tu.

Hebu tuachane na huu ugonjwa wa kutaka kudunga watoto machanjo kwa kila tatizo.

Let the body function in its natural way. Tonsils kuvimba ni kawaida tu.

Cc: DR Mambo Jambo Dkt. Gwajima D
 
Mkuu mwanangu alikuwa hivyo ila kuna Dr aligundua tatizo baada ya kuhangaika kila hospital

Alituambia aache vitu vyote vitamu kama pipi, juice aina zote na alipoacha tu tataizo likakoma kabisa na sasa amepona kabisa

Ni jambo la kushukuru Mungu kwa kutuelekeza kwa huyo Dr kumbe ilikuwa ni allergy tu

Hebu jaribu hata Ice cream usimpe bali Apple na Yogurt tu
Mpe matunda sana ila mapipi na juice hizi hata soda usimpe kata kabisa
Sio allergy.

Masukari sukari yanaleta bakteria mdomoni wanaovamia mifuko ya tonsils na kusababisha infections hence uvimbe na inflammation.

Cc: DR Mambo Jambo
 
Asante.

Sukari ni mbaya.

Unaweza kuhangaika na jambo dogo kwa gharama kubwa sana kumbe CHANZO NI SUKARI.
Tuko pamoja mkuu,
Halafu kuna waganga wengi wanajaribu badala ya kutibu pia vifaa adimu
Sukari mbaya sana na watoto wanakufa sana kwa kupewa madawa ya kila aina ambayo hayasaidii
Kumbe tatizo ni masukari na baba anamshindilia pipi na
Juice tu
 
Mkuu mwanangu alikuwa hivyo ila kuna Dr aligundua tatizo baada ya kuhangaika kila hospital

Alituambia aache vitu vyote vitamu kama pipi, juice aina zote na alipoacha tu tataizo likakoma kabisa na sasa amepona kabisa

Ni jambo la kushukuru Mungu kwa kutuelekeza kwa huyo Dr kumbe ilikuwa ni bacteria tu

Hebu jaribu hata Ice cream usimpe bali Apple na Yogurt tu
Mpe matunda sana ila mapipi na juice hizi hata soda usimpe kata kabisa
Mwanzisha thread kasema mtoto hana homa. Nijuavyo mimi tonsils huwa zikipata uambukizo hivimba na kuleta homa. Zinakuwa na usaha wakati mwingine. Kwa kesi yake inaweza isiwe kuna shida yoyote bali ni maumbile tu kwa sababu zingekuwa na uambukizo, mtoto ni lazima angeugua na kupata homa.
 
Mwanzisha thread kasema mtoto hana homa. Nijuavyo mimi tonsils huwa zikipata uambukizo hivimba na kuleta homa. Zinakuwa na usaha wakati mwingine. Kwa kesi yake inaweza isiwe kuna shida yoyote bali ni maumbile tu kwa sababu zingekuwa na uambukizo, mtoto ni lazima angeugua na kupata homa.
Hilo linawezekana pia
Mwanangu alikuwa hana Homa kabisa
Ila tonsils na pia uvimbe chini ya masikio yote

Labda huyo ana tatizo lingine ila ni bora kuangalia alternative zote
Haitamgharimu akiacha kumpa sukari
 
Tonsils ni mojawapo ya Kinga za Mwili.

Usizitoe au kuzipasua muache akue zitapona tu.

Kuvimba ni kawaida tu labda inflammation au infection ndogo ndogo tu.

Hebu tuachane na huu ugonjwa wa kutaka kudunga watoto machanjo kwa kila tatizo.

Let the body function in its natural way. Tonsils kuvimba ni kawaida tu.

Cc: DR Mambo Jambo Dkt. Gwajima D
Good Sana I see now Y've Become a Good Doctor..
I am proud of You..

Umeona sasa ukielewa tu Haya mambo hayakusumbui
 
Hapana mkuu. Nimeamua nimuangalie tuu kwanza.
Kuna majani unatakiwa umfukize nayo, mimi ñilikuwa sikai wiki sijaumwa, sinywi kitu cha bard usk lazma nijifunike shingo, hata kama ni dar, pia nisilale dirsha waz hata wakat wa joto ila nilipofukiza kwisha, au

kuna ness aliniambia alikuwa nàyo akiumwa mpk yanayoka usaha hajiwez unakuta anakimbizwa maututi, akawekewa canyula na kuchombwa cristapen dozi 6 hapo anavyoniambia anakunywa peps bard baraf anakula na haumwi. Mie nilijifukiza hayo majani ni mwaka wa pili sijawah kuvimba wala kuumwa.
 
Back
Top Bottom