Kijana wangu miaka 11 kashaanza kutongoza na kujisifu handsome boy, kanistua sana, nichukue hatua zipi?

Kijana wangu miaka 11 kashaanza kutongoza na kujisifu handsome boy, kanistua sana, nichukue hatua zipi?

Mkuu Uncle bright ulimwengu ushaharibika, vitoto vingi vya miaka 7-10 vimeharibika sana kupitia maudhui ya kingono/kishoga toka kwenye movie/tamthilia.

Ulimwengu wa sasa, bila kufanya maagano ya kukilinda kizazi chako na ushenzi ni ngumu sana kupata kizazi bora.
 
Wataalam wa malezi naombeni msaada wenu

Na huwa nipo bize kumuwekea katuni na muvi za watoto kwenye flash, nimemnunulia game ya tv (playstation), kwenye tv nimembana aangalie zaidi mpira na mieleka tu. hakuna simu wala internet.

Jana nikiwa sebuleni nilikuwa nacheki tv, sikuiona rimoti ikabidi nianze kuitafuta kwenye masofa.

Nikaanza kufunua mito ya masofa nikakuta kuna bahasha ya karatasi za rim nyeupe imekunjwa kwa ustadi, kuichunguza nikaona maneno ya jina la mtoto kwa chini yake kaandika the handsome boy.

Nikafungua bahasha kulikuwa na kikaratasi nikaanza kuisoma, MH !!!!!

Sio kwa vocal / mtongozo ule, Mtu mzima nilikuwa naisoma huku nimesimama ila ilibidi nikae chini.

Kiufupi kamsifia halafu mwishoni kaandika mimi nakupenda, wewe unanipenda? Nijibu sitamwambia mtu yeyote ila mimi nakupenda.

Binafsi nimechukulia ni yale mapenzi ya kitoto kuwa karibu kama mabesti lakini siwezi jua, labda ni zaidi ya hapo mfano kukumbatiana na kubusiana ama vikubwa zaidi visivyowafaa watoto.

Niliirudisha barua, asubuhi sijaikuta, namchora tu huyu mvulana anavyojifanya katoto kumbe ana wachuchu.

Angekuwa ni kijana mwenye 15 ningeelewa ni balehe imekolea na ningekaa nae chini kumpa a,b,c,d... Ila kwa huyu mtoto sijafurahi kwasababu bado ni mtoto mdogo kajiingiza kwenye mambo mazito

Ni mvulana mdogo bado, sijui hata nichukue hatua ipi
  • Nimtie viboko vya kutosha kama ilivyozoeleka kwa tamaduni za kiafrika
  • Nimpe onyo
  • Nikae kimya
  • Nikae nae chini niongee nae nini?
  • n.k.
Mtafutie na kadi ya ccm ili asajiliwe rasmi kwenye chama cha mafirauni.
 
Unapaswa uzungumze na mwanao kila kitu nje na ndani, ngono ni nini na ushoga ni nini.. madhara gani anaweza kupata na kwann asubirie wakati wake ..
Kila kitu kiwe wazi wazi...

Ukiacha duniani imfundishe utampoteza
 
40411597d620d681c8455eefef2c0df7.jpg
 
Wataalam wa malezi naombeni msaada wenu

Na huwa nipo bize kumuwekea katuni na muvi za watoto kwenye flash, nimemnunulia game ya tv (playstation), kwenye tv nimembana aangalie zaidi mpira na mieleka tu. hakuna simu wala internet.

Jana nikiwa sebuleni nilikuwa nacheki tv, sikuiona rimoti ikabidi nianze kuitafuta kwenye masofa.

Nikaanza kufunua mito ya masofa nikakuta kuna bahasha ya karatasi za rim nyeupe imekunjwa kwa ustadi, kuichunguza nikaona maneno ya jina la mtoto kwa chini yake kaandika the handsome boy.

Nikafungua bahasha kulikuwa na kikaratasi nikaanza kuisoma, MH !!!!!

Sio kwa vocal / mtongozo ule, Mtu mzima nilikuwa naisoma huku nimesimama ila ilibidi nikae chini.

Kiufupi kamsifia halafu mwishoni kaandika mimi nakupenda, wewe unanipenda? Nijibu sitamwambia mtu yeyote ila mimi nakupenda.

Binafsi nimechukulia ni yale mapenzi ya kitoto kuwa karibu kama mabesti lakini siwezi jua, labda ni zaidi ya hapo mfano kukumbatiana na kubusiana ama vikubwa zaidi visivyowafaa watoto.

Niliirudisha barua, asubuhi sijaikuta, namchora tu huyu mvulana anavyojifanya katoto kumbe ana wachuchu.

Angekuwa ni kijana mwenye 15 ningeelewa ni balehe imekolea na ningekaa nae chini kumpa a,b,c,d... Ila kwa huyu mtoto sijafurahi kwasababu bado ni mtoto mdogo kajiingiza kwenye mambo mazito

Ni mvulana mdogo bado, sijui hata nichukue hatua ipi
  • Nimtie viboko vya kutosha kama ilivyozoeleka kwa tamaduni za kiafrika
  • Nimpe onyo
  • Nikae kimya
  • Nikae nae chini niongee nae nini?
  • n.k.
Kick hisass
 
Back
Top Bottom