Kikao cha CCM: RA Atema Cheche "Nitajiuzulu...."

Kikao cha CCM: RA Atema Cheche "Nitajiuzulu...."

CCM wanabore sana hamna hata plan ya maendeleo, kila siku tume na kujitetea flani msafi huyu kaonewa.
 
Hawawezi kuubadili UONGOZI wa BUNGE angalau kwa sasa. Uzuri ni mmoja kwenye uongozi wa mhimili huu; SPIKA anachaguliwa, hateuliwi mbali na uteuzi ule wa awali wa chama chake ambao kwa sasa hauwezekani pia kufanyika.
Acheni CCM wanyukane kwanza. Wanayemharibia kwa sasa ni JK. Anaonekana Uraisi hauwezi na Uenyekiti wa chama chake pia umemshinda.

WildCard,

Unaijua katiba ya Tanzania? akiwasilisha mtu mmoja ndani ya Bunge hoja ya kutokuwa na Imani na Spika na kukafanyika kikao ambacho Spika hutoka nje, mchezo umekwisha!

Mkandara,

La nyongeza, tulishangilia kanyaboya la Mramba na Yona kufikishwa mahakamani, nikaandika https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/21106-paukwa-pakawa.html watu wakafikiri natania!

Leo hii Kiwira imerudishwa kwa Serikali, walionunua kwa bei chee wamerudishiwa pesa zao, hakuna atakayepelekwa mahakamani.

Hizo za EPA, waliopelekwa mahakamani wote ni wale waliojichongea binafsi pembeni ya mchoro orijino wa Saidia CCM Ishinde! Wataungua, mtashangilia lakini KAGODA kamwe hataguswa, Jeetu Patel kapewa tenda mpya ya Bilioni 50, je unaamini kuwa ataendelea kuwa na kesi Kisutu?
 
ccm bado ina viongozi wachache ambao ni wasafi crystal clear, na pia miongoni wa wapiganaji, wako baadhi ni wapiganaji wa kweli, wengine ni wapiganaji kutimiza malengo yao ya agenda zao, na wengine ni njaa zao tuu kazi yao kulishwa maneno na mfadhili wao mkuu na kuja kuyatapika bungeni.
mkuu tusaidie nani huyo mlishaji ?
 
Pale Dodoma wabunge wamemwambia mzee Ruksa na kamati yake kuwa amwambie muungwana kuwa ugomvi wote na mpasuko utaisha mara moja wakiondoka kwenye uongozi/ccm lile gruop of 4, RA, El, VjiCent na Mzee wa Tics. Na wameonyesha ni wakali kweli kwenye hilo, I hope hawatarudi nyuma, maana wakishindwa kwenye hilo, wamejimaliza.

EDO,

Hili ndilo nimekuwa nauliza siku zote, kwa nini ndani ya Chama hawawaondoi hawa jamaa? Ni miezi 18 tangu wamepewa tuhuma na hata wakaondoka madarakani kwa aibu, kwa nini bado wanalelewa na Chama na kuonewa haya na Mwenyekiti wa Chama?

Je mnataka tuanze kuhoji Uhalali wa Mwenyekiti na kumhoji Uzalendo wake uko kwa nani? Tukifika huko si mtatuita WAHAINI au?
 
Yaani tutumie mamillioni ya kodi kwa ajili ya kutafuta Rostam ajiuzuru! mbona hiki ni kichekesho. dah! Rostam ...

Huyu jamaa ni kama chizi kweli, ameshatuibia vya kutosha kisha tena tuendelee kutumia fedha, kisa yeye ajiuzulu.

Muda wenu umewadia, kilichobaki ni kwenda mbele na hapa CCM ni lazima ichanike
 
Mkandara,

Wakati wa Uchaguzi wa 2005, pesa chafu ya EPA ndio iliyoirudisha CCM Madarakani, ingawa wala hawakuhitaji kuchota.


Uchaguzi wa 2000, pesa za Meremeta na upuuzi mwingine zilitumika vizuri sana maana kulikuwa na kutokuaminiana ndani ya Chama na ngao ya CCM Mwalimu Nyerere alikuwa katutoka

Uchaguzi wa 1995, pamoja na pesa zote zilizokwisha chukuliwa kisanii na CCM, ilibidi wamkimbilie Nyerere ambaye single handedly aliwaangusha Mrema na wenzake wa Muungano na kutumia fimbo ya matakoni kumrudisha Salmin.

CCM ni chama si cha kuaminiwa na wewe unalijua hilo. KInachotokea sasa hivi ni ugomvi wa nani ashike hatamu na kula utamu kwa kutumia CCM na wala si kuhusiana na maslahi ya Taifa.

Waziri wa Usalama wa Taifa anapota kauli kuwa kila mtu ni safi kuhusu RICHMOND na RADA, je unafikiri ni nani aliyetoa baraka kwa kauli kama hiyo kutolewa?

Lowassa, Rostam, Sitta, Mwakyembe na wengineo wana madhambi yao, na tatizo limekuja sasa hivi ni mapiku!

Kama kina Sitta na Wapiganaji wangesikiliza lile tulilowaambia la kutetea maslahi ya Taifa na kufanya kazi kwa manufaa ya Taifa, fedheha kama hii isingetokea na kina Lowassa, Rostam na Sophia wasingediriki kufanya wanalolifanya leo hii!

Kwa miaka mitatu tumekaa tukizungumzia tuhuma kuhusu Rostam na Lowassa, je wameshakalishwa kitako ndani ya Chama au Serikalini na wakachukuliwa hatua?

Je Chenge naye ambaye ni mkuu wa Maadili ndani ya Chama ni lini amekalishwa kitako akaambiwa ajieleze?

Juzi suala la Richmond limegeuzwa kuwa ZeComedy, kina Sitta wanabanwa Golori zao kuttokana na kupenda posho, kina Ngwiliza wanafunuliwa kwa kupata pensheni mbili mbili, huku Richmond, Kagoda, EPA, Rada na sasa Kilimo Kwanza wanapeta na tunadanganywa kuwa ni kukua kwa Demokrasia ndani ya Chama!

Huu ni uhaini wa hali ya juu, na Watanzania tunachezewa akili, tunafujiwa hazina yetu na tunafanywa wapumbavu!

Nilihoji kwa nini Wapiganaji hawajiondoi na UCCM na kupigania mambo ya Taifa? Kwa nini wanaendelea kuogopa panga na rungu la Chama kwa kuendelea kuimba CCM mbele, Tanzania nyuma kam Wakristo wanavyoimba Msalaba Mbele Dunia nyuma?

Kwao Wapiganaji wa CCM, wokovu wao(binafsi) ni kupitia CCM na si kupitia Taifa la Tanzania!

Ni upuuzi kuendelea kuwasikiliza! Kwanza afadhali na tunajua kuwa Lowassa, Rostam na Chenge ni Mafisadi na hilo kila Mtanzania analijua na usishangae kuwa mwakani, viti vyote vya Ubunge Dar vitakwenda CCM na zaidi CCM inaweza kupunguza nusu ya viti vya Upinzani hasa Bara.

Lakini kwa kuwa ni jadi ya kuoneana aibu ndani ya Chama, kina Sitta wamepoteza nafasi moja kubwa sana, walipoleta ripoti ya Richmond wakadai kuna mambo mengine hawatayazungumza ili kuifichia aibu Serikali, hapo ndipo walipouza utu wao na wakapoteza sifa ya kuwa wapiganaji na hata maana ya kuwa na tume.

Kuondoka kwa Lowassa hakukutosha, ilipaswa ripoti ilete mabadiliko ya kweli si ya watu kujiuzulu tuu!

Kama wasingeficha baadhi ya mambo eti kuionea aibu Serikali, leo hii kila lililoovu lingeanza kuweweseka na kuogopa. Lakini midhali waliamua kufukia maovu na uzembe mwingine kwa kuonea huruma na aibu Chama na Serikali, basi ni vigumu sana kwa mabadiliko na vita dhhidi ya uhujumu, uzembe na kutofuata kanuni kufanikiwa.

Lakini swali langu na lile la Mwanakijiji linarudi, Wapiganaji wanapigania nini na wanampigania nani?

Ukiona Sophia na Rostam wanatamba kama walivyofanya sasa hivi, jiulize Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yupo wapi na yupo upande gani?


Umekasirika?

Juzi uwanja wa ndege ya JK Nyerere nilikutana na kale ka Rais ka Madagascar Bw. Rajoelina
 
Haya maneno gani lakini jamani.. Huyu RA na Wabunge wote Mafisadi hawafahamu kwamba Spika Sitta is third in line ktk uongozi wa nchi?..

Third in line maana yake nini?
 
Huyu jamaa ni kama chizi kweli, ameshatuibia vya kutosha kisha tena tuendelee kutumia fedha, kisa yeye ajiuzulu.

Muda wenu umewadia, kilichobaki ni kwenda mbele na hapa CCM ni lazima ichanike

mtachanika nyie lakini CCM itaendelea kudumu daima
 
WildCard,

Unaijua katiba ya Tanzania? akiwasilisha mtu mmoja ndani ya Bunge hoja ya kutokuwa na Imani na Spika na kukafanyika kikao ambacho Spika hutoka nje, mchezo umekwisha!

Mkandara,

La nyongeza, tulishangilia kanyaboya la Mramba na Yona kufikishwa mahakamani, nikaandika https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/21106-paukwa-pakawa.html watu wakafikiri natania!

Leo hii Kiwira imerudishwa kwa Serikali, walionunua kwa bei chee wamerudishiwa pesa zao, hakuna atakayepelekwa mahakamani.

Hizo za EPA, waliopelekwa mahakamani wote ni wale waliojichongea binafsi pembeni ya mchoro orijino wa Saidia CCM Ishinde! Wataungua, mtashangilia lakini KAGODA kamwe hataguswa, Jeetu Patel kapewa tenda mpya ya Bilioni 50, je unaamini kuwa ataendelea kuwa na kesi Kisutu?


Unahitaji wabunge 20 tu kusaini petition na kuweka hoja ya kumwondoa Spika. Anaondolewa kwa simple majority.

Njia nyingine ni chama chake kuondoa udhamini wake na hivyo kuondoka uspika. Hawatafika huko! Wanasema hawataki kutengeneza hero!
 
The next step wataleta hoja ya ya kupiga kura ya kutokuwa na imani na Spika; Sitta ataondoshwa (kwani wabunge kadhaa watapangiwa visema kule nje na kura itapigwa). Akiondoshwa atawekwa Spika wao (jina tunalo) ambaye ataridhia maombi ya kina RA na Sofia. Ndipo tume wataiunda wao na kina RA na EL watasafishwa rasmi kwa kutumia utaratibu wa kibunge na hivyo maamuzi kuwa legally binding.

Tayari kwa karibu wiki kadhaa sasa pesa imetembea Dodoma kwa ajili ya jambo hili na kwa ajili ya kupata support ya wabunge. Novemba 7 ni siku muhimu kwa ajili ya hili.

Mzee Mwkjj,

Suala la kumuengua six likifanikiwa, basi huo utakuwa mwanzo wa Demokrasia mpya, natabiri kuanzishwa chama chenye nguvu zaidi na kitakachoweza kukibwaga chama cha mafisadi na maneno ya Mwl. yatakuwa yametimia "upinzani wa kweli wa CCM utatoka ndani ya CCM"

Siku hiyo naomba wanajamvi wote tukachukue kadi pamoja na familia zetu.
 
Sina cha kuongeza, MTOTO nakuunga mkono asilimia 200%. Huo ndio ukweli hakuna mpiganaji kila mtu ana intrest zake!!!!!!! 😕
 
WildCard,

Unaijua katiba ya Tanzania? akiwasilisha mtu mmoja ndani ya Bunge hoja ya kutokuwa na Imani na Spika na kukafanyika kikao ambacho Spika hutoka nje, mchezo umekwisha!

Mkandara,

La nyongeza, tulishangilia kanyaboya la Mramba na Yona kufikishwa mahakamani, nikaandika https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/21106-paukwa-pakawa.html watu wakafikiri natania!

Leo hii Kiwira imerudishwa kwa Serikali, walionunua kwa bei chee wamerudishiwa pesa zao, hakuna atakayepelekwa mahakamani.

Hizo za EPA, waliopelekwa mahakamani wote ni wale waliojichongea binafsi pembeni ya mchoro orijino wa Saidia CCM Ishinde! Wataungua, mtashangilia lakini KAGODA kamwe hataguswa, Jeetu Patel kapewa tenda mpya ya Bilioni 50, je unaamini kuwa ataendelea kuwa na kesi Kisutu?
Rev.
Azimio la Bunge la kumwondoa Spika Madarakani linahitaji theluthi mbili ya Wabunge kuliunga mkono (84.7.d). Kwa mazingira ya sasa hiyo ni ngumu sana. CCM pia wanaelewa madhara yake na ndio maana ile njia rahisi zaidi na ya mkato kupitia NEC yao ilishindikana.
 
Hawawezi kuubadili UONGOZI wa BUNGE angalau kwa sasa. Uzuri ni mmoja kwenye uongozi wa mhimili huu; SPIKA anachaguliwa, hateuliwi mbali na uteuzi ule wa awali wa chama chake ambao kwa sasa hauwezekani pia kufanyika.
Acheni CCM wanyukane kwanza. Wanayemharibia kwa sasa ni JK. Anaonekana Uraisi hauwezi na Uenyekiti wa chama chake pia umemshinda.

Wanamharibia JK?.

No, hawamharibii, bali wanathibitisha kuwa JK is indeed weak, 'dhaifu'. Yaani nasema bila kujiuma uma ulimi, JK ni DHAIFU!.

Niliwahi kukaa na Kinana mahali over gahawa, nikamwambia my honest opinion kuwa JK ni dhaifa, na kama kweli sio dhaifu, basi anaonekana dhaifu. Nilimtolea mifano miwili tuu kuhusu udhaifu wa JK, moja jinsi alivyoyumbishwa kwenye issue ya muafaka, huu ni udhaifu mkubwa sana mbele ya jamii ya kitaifa na kimataifa.

Tatizo hakuna watu wa karibu wa kumweleza. Mbona Nyerere alikuwa na msimamo. Udhaifu wa pili nilioteta na Kinana ni jinsi anavyowakumbatia watuhumiwa wa ufisadi, hata kama hakuna uthibitisho, hili linamchafua na litamuangusha. Mhe. Kinana alimtetea sana JK kuwa sio weak, alikiri kuwa hili la Zanzibar hata JK hafurahishwi na hali ilivyo, bali alizidiwa nguvu ndani ya vikao naye hakutaka kufanya udikteta, kwangu huu ni udhaifu.

Kama hili la kumng'oa spika Six ni la kweli, CCM itampasukia mkononi and this is healthy for opposition, we will at least get serious opposition ili litimie lile neno "Upinzani wa kweli utatoka CCM" - Mwl. J.K Nyerere.
 
Hii kamati ya mzee Ruksa imegeuka kuwa uwanja wa vijembe na mipasho, na mkuu amekaa kimya...
 
Rev.
Azimio la Bunge la kumwondoa Spika Madarakani linahitaji theluthi mbili ya Wabunge kuliunga mkono (84.7.d). Kwa mazingira ya sasa hiyo ni ngumu sana. CCM pia wanaelewa madhara yake na ndio maana ile njia rahisi zaidi na ya mkato kupitia NEC yao ilishindikana.

wabunge walioko Bungeni.. siyo wabunge wote!
 
Rev.
Azimio la Bunge la kumwondoa Spika Madarakani linahitaji theluthi mbili ya Wabunge kuliunga mkono (84.7.d). Kwa mazingira ya sasa hiyo ni ngumu sana. CCM pia wanaelewa madhara yake na ndio maana ile njia rahisi zaidi na ya mkato kupitia NEC yao ilishindikana.

Katiba?

Then kuna mgongano mkubwa na kanuni ambazo zimeweka taratibu za kumwondoa Spika. Hata hivyo Katiba prevails. Thanks
 
Umekasirika?

Juzi uwanja wa ndege ya JK Nyerere nilikutana na kale ka Rais ka Madagascar Bw. Rajoelina

Zitto,

Taifa linapoteza muda na kodi kubembeleza upuuzi!

Leo hii pesa zote tulizopoteza katika miaka 10 iliyopita tungekuwa na Reli moja kabambe mpaka jimbo la Kalemi. Tungekuwa na hospitali za Rufaa za kisasa kila mkoa, tungekuwa na vyuo vikuu vya kutosha, barabara zetu zingeunganisha nchi vizuri kabisa, GDP yetu ingekuwa si chini ya $5000 kwa kila mtu, ajira zingekuwapo za kutosha na tungekuwa na suluhisho la kudumu la umeme na nishati!

Nisipokasirika mimi kama ninavyoruhusiwa na Katiba, nimwachie nani jukumu hilo? nilisukume kuwa ni la Zitto pekee? nope ni letu sote!
 
Back
Top Bottom