Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa faida ya afya yakokwanini
sawa kwanza nimeshaacha!.
wewe je, unakunywa..?
[/QUOTE
Sinywi na wala sijui inaladha gani
Hata ungeandika kitabu kizima Bado hujanishawishiMarcy
si mbaya ukinywa ki afya, uliza hata ma daktari watakuambia ukweli labda kama unashida za kiafya ndio itakuwa mbaya kwako!.
ipo hivi..
kuna aina nyingi za pombe, na moja ya pombe hizo ni pombe kali hizi naweza sema si nzuri maana ni kali na zinawahi kumchukua mtu, inategemea na kiasi utakachokunywa ila ni nzuri kunywa hii kwa kiasi kidogo sana kwaajili ya kupata hamu ya kula tu!, narudia kwa kiasi kidogo.
kuna wine hizi nashauri watu wanywe kwasababu zimethibitika kuwa na manufaa pia ki afya, ni nzuri sana kunywa wakati wa kula ama baada ya kula!.
pia kuna liqueur hizi zinafaa kunywa baada ya kula ni zinarahisisha mmeng'enyo wa chakula!.
shida ya pombe ni kuizidisha na unakunywa nini kwa wakati gani!.
pombe hutakiwi kunywa mpk ukalelengeta,ukakera watu,kupiga kelele na kero nyengine na ndio maana huwa tunasema sio kwaajili ya kila mtu!, maana si wote wanaiweza pombe kwani wengine wanakunywa kulewa!.
kitu chochote ukikifanya kwa kupitiliza lazima kitaleta tafrani.
hapo vipi marcy..?
🤣🤣🤣🤣🤣usinge nitag kama ndivyomi sikushawishi unywe mi nimeandika maoni tu!..
kwahiyo mimi kusimulia matukio yangu ya kweli ndo kunafanya mimi nionekane nina kipaji cha komedi..?We jamaa una kipaji cha uchekeshaji kabisa, kama bado haujaanza comedy show rasmi nakushauli tu anza sasa utapiga hela huko ndio kipaji chako kilipo
Hii ni kweli na nisababu miss ku fallkwahiyo mimi kusimulia matukio yangu ya kweli ndo kunafanya mimi nionekane nina kipaji cha komedi..?
aisee!
mkuu kunywa mwenyewe dawa yako ya unga.kama sio kahawa tea
mkuu,walikukosea sana dawa yakuachisha mtu pombe sio kwanjia hiyo,Mimi ninayo ya unga
sharti namba Moja,hutakiwi kujua Leo unawekewa au kesho
Pili,usimjue katu anayekuwekea mana atakuja kuja kuwa adui mkubwa
TATU ,hapa ndosiku yenyewe mkeo anaweza tafuta mtu wakaribu au hata mama Ako mzazi ukashangaa unaambiwa wikend hii tunaenda wote bar ukatununulie soda ,kimsingi utafurahia
nakufundisha ,hata kama ni mama Ako hakikisha sikuhizo huachi pombe mezani pale kila uendapo chooni hakikisha imeisha yote ,ukizingua tu uache unawekewa huo unga nitakao kuwa nimewapa(Mimi nimganga watiba mbadala)
ukiwekewa ,ukanywa baada ya MUDA utaanza kutapika tapika sana hii dawa ilivyo inakubadilisha kila kilicholadha ya pombe ..itakuwa pona yako ...kwa mawasiliano zaidi karibu gharama ni burekabisa mwenye nia mlevi wako akiacha pombe ndipo unaweza leta asante/takrima
Hama hapo nyumbani la sivyo watakuadabisha tuIlikuwa mida fulani hivi ya saa mbili usiku ile naingia nyumbani kabla sijafika sebuleni nikasikia ndugu zangu wanajadili "Tumemletea tiba leoleo lazima aache hizo pombe zake!"
hapo walikuwa hawajashitukia kama nimeingia na siku hiyo mpk narudi sikua nimeweka vyombo!, wakati nimeendelea kujibanza wakawa wanakazia!, mi nikafikiri kidogo nikaona ngoja nirudi kwanza mtaani nikapige vyombo halafu nirudi niwachane kuwa niliwasikia na hawaniwezi!.
taratibu nikachomoka pasipo wao kujua nikazama kiwanja kimoja chapchap!, bapa kubwa ya kwanza ikaisha nikaisindikiza na bapa nyengine ndogo nilipojiona sasa nipo tayari huyo nikaanza kurudi nyumbani!
ile nafika palikuwa kimya sana mpk nikahisi kama hakuna watu!, wakati nafika sebuleni ghafla nikasikia mtu akisema "huyo hapo mkamateni!!"
wakati nataamaki nikahisi nimebanwa kwa nyuma, ndugu yangu mwengine akaja kwa mbele!. hapo bado bumbuwazi limenikamata mlevi wa watu sijui natekwa ama vipi, halafu natekwaje nyumbani tena na ndugu zangu!.
Wakati hayo yanaendelea nikawa nimewekwa mtu kati, yule aliembele yangu akabwatuka "Mganga njoo haraka mtu wako tayari!!"
sasa hapo ndo nikaelewa hawa binadamu wanataka kunimaliza,wameniletea mganga wakunitibu niache pombe! nikawatikisa kidogo walivyokuwa wamenibana lkn hata hawakutikisika!, nikajisemea moyoni "kwisha habari yangu!"
punde hiyohiyo nikaona mtu anatokeza, huyo ndo alikuwa mganga mwenyewe sasa muonekano wake tu ulitosha kujua leo kazi ipo!
alikuwa amevalia ile kiganga kabisa yani juu kaniki nyekundu chini kaniki nyeusi, huku kichwani akivalia kilemba cheupe!. mkono wake wakushoto akawa ameshika usinga!, kuliponitisha zaidi ni mkono wake wa kushoto akawa na kidude fulani kama chaduara kidogo kikawa kinarukaruka chenyewe hata hakirushi! hapo ndo kijasho mshenzi kikaanza kunitoka!.
Nikajitikisa tena mara hii walionishikiria wakatikisika!, mganga akawa mkabala na mimi akanipiga na ule usinga kwanza hakuna kilichotokea hapo mimi mapigo yanaenda mbio tu!, mara mganga akasema "sasa mbaneni vyema nimshike mdomo amezee hii!" yani kile kidubwasha kinachorukaruka natakiwa nikimeze!.
Kusikia hivyo just from no where nikajirusha kwa nyuma!, kumbe yule wa nyuma akawa hana balansi akanishinda akaniachia si nikaanguka! yule wa mbele akawa anakuja mkuku kunidhibiti pale chini nikamkwatua mguu akaanguka!, ile mi nataka kuinuka yule ndugu mwengine akawa ananivizia anikabe nikamuona akija kama kifaru nikaachia kifuti cha nyumanyuma! akaachia ukelele mzito!.
sasa walivyoona zoezi limeingia ndimu mmoja akawahi switch ya taa akazima!, mchezo ukawa wa gizagiza sasa!.. ghafla nikapigwa mtama kwa jinsi nilivyopigwa ule mtama nikahisi kabisa huyu alienipiga huu mtama alifanya mazoezi kabla!.. hapohapo nikapigwa kabari nyengine nzito ile natapatapa nikasikia "mganga njoo sasa!"
mganga akawa anahangaika kutafuta mdomo ile anaukaribia kaleta vidole nikamuuma! akapiga welelo mkubwa sana!, hawa wengine wakawa wameduwaa nini kimempata mganga!, hapohapo nikatupa kichwa kama mara mbili hivi ya tatu nikasikia mtu anakema nikajua tayari nishacheza na pua ya mtu!!.
hapohapo watesi wangu hawakunilazia damu nikasikia napapaswa zinatafutwa malighafi taifa (vinyanya mshenzi ama mapera ya adamu) zibinywe ili niachie ubingwa mapema!, nikaona hii haiwezekani!..
Nilizunguka kwa nguvu bila kuangalia nitakutana na nini, sikugusa kitu nikaona kabisa sekunde tano zijazo hawa mazwazwa wataniweza nikaamua kubetuka kwa nyuma nikasikia mtu anapiga kelele!, nikarusha na teke kwa mbele nikahisi limempata mtu!!.
si wakajichanganya wakawasha taa!, kuangalia hivi nipo karibu na mlango!! bila kuangalia nikatokomea kwa spidi ya sgr wakabaki wameduwaa!.
sikwenda mbali nikawa nasikia mtu analia huko ndani, kumbe lile teke lilimpata mganga sehemu mbaya hivyo maumivu yakawa makali, si akapandisha mizimu yake ikaanza kulalamika ati kiti wao ameumizwa!, msala ukahamia kwao wakashindwa kuelewana na mizimu nikiwa nimejibanza nikasikia vishindo watu wakikimbizwa, kumbe ni wale ndugu wawili walikuwa wakikimbizwa na mganga mi kuona hivyo nikazama ndani nikafunga milango nikalala!..
kesho asubuhi wananipigia simu wapo polisi nikawatoe wamekamatwa wote watatu kwa kesi ya uzururaji usiku!.. na shughuli ya kuniachisha pombe ndo ikawa imefia hapo!.😅
Ahsante sana nikaribie wapi rafikiKaribu!
Kwa nia njema kabisa una kipaji kikubwa cha uchekeshaji unaweza kupata pesa kwenye fani hiikwahiyo mimi kusimulia matukio yangu ya kweli ndo kunafanya mimi nionekane nina kipaji cha komedi..?
aisee!