Tetesi: Kikao cha siri cha CCM juu ya Jimbo la Singida Kaskazini

Tetesi: Kikao cha siri cha CCM juu ya Jimbo la Singida Kaskazini

Kuna tofauti ya kukata tamaa na kupuuza. Tungekata tamaa iwapo kuna ushindani kisha tunashindwa. Lakini tunapata ushindi kisha mnatangazwa nyie huku wafuasi wetu wakiwa wameachwa na vilema na wengine vifo hapo ni upuuzi tu. Tuna njia nyingine ya kuweza kupambana na tunaimudu lakini hata haya maendeleo duni tutayapoteza kwa kuwa si salama sana, na kwakuwa maisha yetu hayategemei siasa ni bora tuwapuuze nyie mnaotegemea siasa muendelee na huo upuuzi.
Ndugu acha jazba soma uzi vizuri uelewe halafu utoe maoni si kila mkosoaji upinzani ni mtawala kama ambavyo wengi mnaojiita wafuasi wa "ushabiki wa upinzani" mnavyodhani sasa kwenye hoja yako ya kupuuza na kusema waache tu wamtangaze hakuna mtu mwenye muda na uchaguzi tafsiri yake pana ni nini kama sio ukataji tamaaa? una mkakati gani unaonekana na kurudisha morali na mwamko wa wapiga kura wako inayoonekana na yenye mashiko apart from sympathy strategy ya kulaumu na kushutumu watawala kama ulivyoainisha hapo juu sijui anashinda huyu anatangazwa yule mara sijui watu wamepigwa hayo yana msaada gani kwa upinzani katika harakati za kushika dola? Isije mkawa mnacheza ngoma ya wajanja walio katika uongozi wa upinzani wanaojaribu kutoa lawama kila siku ili kuwaaminisha "washabiki wao" kuwa wanaonewa tu bila kutoa suluhu ya kweli juu ya hali halisi....mi napenda kubishana kwa hoja bila kuvaa joho la mtu yoyote sasa kama ndugu yangu utajibu huku ukiwa na joho flani hatutaweza kuelewana
 
Ndugu acha jazba soma uzi vizuri uelewe halafu utoe maoni si kila mkosoaji upinzani ni mtawala kama ambavyo wengi mnaojiita wafuasi wa "ushabiki wa upinzani" mnavyodhani sasa kwenye hoja yako ya kupuuza na kusema waache tu wamtangaze hakuna mtu mwenye muda na uchaguzi tafsiri yake pana ni nini kama sio ukataji tamaaa? una mkakati gani unaonekana na kurudisha morali na mwamko wa wapiga kura wako inayoonekana na yenye mashiko apart from sympathy strategy ya kulaumu na kushutumu watawala kama ulivyoainisha hapo juu sijui anashinda huyu anatangazwa yule mara sijui watu wamepigwa hayo yana msaada gani kwa upinzani katika harakati za kushika dola? Isije mkawa mnacheza ngoma ya wajanja walio katika uongozi wa upinzani wanaojaribu kutoa lawama kila siku ili kuwaaminisha "washabiki wao" kuwa wanaonewa tu bila kutoa suluhu ya kweli juu ya hali halisi....mi napenda kubishana kwa hoja bila kuvaa joho la mtu yoyote sasa kama ndugu yangu utajibu huku ukiwa na joho flani hatutaweza kuelewana

Sijui unaongea nini, toka mfumo wa vyama vingi umeingia hapa nchini wapinzani wenye nguvu wamekuwa wakifanyiwa vitimbwi vya kuumizwa na hata kuuwawa. Wamekuwa kila mara wakitaka tume huru ya uchaguzi na kanuni za uchaguzi kuheshimiwa. Hilo halijatekelezwa hadi sasa, kibaya zaidi kila mara wapinzani wa kweli wanabezwa kama mmekubali kushiriki ina maana mmeridhika na mwenendo wa uchaguzi. Sasa hivi unyama unazidi kuwa wazi huku wapinzani wakikutana na vipigo na ukatili mwingi sana. Imefikia mahali hata kura zinahesabiwa na kupigwa bila mawakala wa upinzani kuwepo. Haya yote yanatokea huku taifa zima likiwa kimya na kuonekana ni sawa na hata wasioridhika wameingiwa na woga na hawathubutu kukemea hali hiyo.

Suala la upinzani kushika dola inategemea kanuni za mchezo wa uchaguzi unafanyikaje, iwapo kanuni za mchezo zinakiukwa ili kukibeba chama tawala basi wapinzani nao inabidi waanze kukiuka kanuni za mchezo na hatimaye itakuwa ni mauaji na machafuko, hatuko tayari kufika huko maana sio wote ni wajinga ama wenye uchu wa madaraka. Wewe hapo ulipo mbali ya kujifanya unaona sisi wengine tumekata tamaa hatujakuona ukienda mahakamani kufungua kesi dhidi ya huu ukatili unaofanywa, unaishia kuleta porojo tu hapa. Watu wanaumizwa na kuachiwa vilema vya maisha na sio jukumu la chama kutibu wafuasi wake walioumizwa tena mara nyingine na vyombo vya dola. Tumeona wabunge wa upinzani juzi na wafuasi wao wakidhalilishwa kisa madaraka. Mbona hatukukuona ukienda kutoa msaada wa kisheria mahakamani?

Kibaya zaidi, narudia kibaya zaidi katika mazingira hatarishi ya hivyo mgombea wa upinzani anaweza kufanikiwa kushinda, kisha haipiti muda anajiuzulu eti anakwenda kumuunga mkono rais!! Kama una akili timamu kupiga kura kwenye mwenendo huu ni upuuzi uliopita kiasi. Kama mnataka watu wapige kura ili kuungopea umma na dunia kwamba kuna demokrasia ili kupatiwa misaada basi safari hii mmenoa. Ukitaka nenda na familia yako na wapambe wako, tena mpige picha mkiwa kituo cha kupigia kura mrushe kwenye facebook hakuna anayekuzuia. Sisi wengine maisha yetu hayategemei siasa bali tunapenda siasa safi sio huu ushenzi unaoendelea sasa.
 
Waambiwe wasihangaike hakuna anayeweza kishiriki huo upuuzi wa uchaguzi. Wamtangaze tu maana tumewapuuza.
Mbona mnaweka mpira kwapani mapema hvi.. Hamuoni kwamba mnapoteza ari na mwamko wa wanachama wenu.
 
Kuna tofauti ya kukata tamaa na kupuuza. Tungekata tamaa iwapo kuna ushindani kisha tunashindwa. Lakini tunapata ushindi kisha mnatangazwa nyie huku wafuasi wetu wakiwa wameachwa na vilema na wengine vifo hapo ni upuuzi tu. Tuna njia nyingine ya kuweza kupambana na tunaimudu lakini hata haya maendeleo duni tutayapoteza kwa kuwa si salama sana, na kwakuwa maisha yetu hayategemei siasa ni bora tuwapuuze nyie mnaotegemea siasa muendelee na huo upuuzi.
Kwa mtu yeyote anaeelewa kwa anayechaguliwa kwa Haki ni chaguo la Mungu na anayechaguliwa kinyume na hapo ni chaguo la Shetani. Tushiriki uchaguzi ili watakaopenda kwa na viongozi wa Kishetani wenye laana zote zisizosame
heka wafanye hivyo. Mungu hulinda wote bila ubaguzi wowote, lakini siku ya hukumu huhukumu kwa matendo yetu.

CCM bhana unaanzanje kumbembeleza uyo jamaa
 
Mbona mnaweka mpira kwapani mapema hvi.. Hamuoni kwamba mnapoteza ari na mwamko wa wanachama wenu.

Bora hiyo ari ifutike kabisa kwani hao wanachama wetu watabaki wazima na viungo vyao ili watunze familia zao. CCM haiwezi tena siasa za ushindani bali ukatili na hatuko tayari kuwafundisha wafuasi wetu mbinu chafu za kuingia msituni kwani hakuna atakayebaki salama. Tungekuwa sisi ni masikini tungeona hatuna cha kupoteza hivyo tungeweza kujibu mapigo kwa kutumia mbinu za machafuko.Kwahiyo bakini wenyewe, mkiona ushindani haunogi fanyeni ushindani wa kikabila na kikanda maana sasa hivi hiyo ndio fashion mpya. Tunaweza kufanya siasa za kistaarabu kuliko kushiriki uchaguzi unaondeshwa kikatili kwa ushirikiano wa vyombo vya dola.
 
Kwa mtu yeyote anaeelewa kwa anayechaguliwa kwa Haki ni chaguo la Mungu na anayechaguliwa kinyume na hapo ni chaguo la Shetani. Tushiriki uchaguzi ili watakaopenda kwa na viongozi wa Kishetani wenye laana zote zisizosame
heka wafanye hivyo. Mungu hulinda wote bila ubaguzi wowote, lakini siku ya hukumu huhukumu kwa matendo yetu.

Sisi tusioamini kuna Mungu inakuwaje?
 
Mikakati muhimu..nyie juzi si mlikuwa na vikao vyenu mpaka mkaanza kuchapana ngumi kati ya mbunge na meya..? Mbona hatukuwaingilia tukawaacha mchapane vizuri
 
Kukata tamaa kwa kiwango hiki kwa wafuasi wa upinzani kunaonesha ni namna gani tunatakiwa turudi mfumo wa chama kimoja maana hakuna maana ya kusapoti watu ambao hawtashinda chaguzi au tuchague kuwa upinzani kwa ajili kuwa kioo cha serikali kuwa kazi ni moja tu kukosoa halafu serikali irekebishe basi.
Vipi mkuu wewe kwa hali ilivyo ya kisiasa unaona kuna haja ya vyama vya upinzani kushiriki hizo chaguzi? Rejea uchaguzi mdogo wa madiwani......
 
Taarifa zilizo nifikia muda huu kutoka chanzo cha kuaminika na mjumbe wa kikao inasema hivi:

Mpaka sasa kikao cha siri kinaendelea katika ukumbi wa juu wa KBH Hotel, agenda ni kumbebembeleza Kitila agombee ubunge Singida Kaskazini.

Pia Daftrari la wapiga kura lipo Tayari mezani kuongeza idadi ya wapiga kura na wanachama wa chama cha mapinduzi 4500 majina yao yapo kwenye kikao kuwekwa kuongeza nguvu.

Source: Informer Wetu
Utakappitwa kuthibitisha uombe wakuruhusu kuja humu ututaarifu pia
 
Ndugu acha jazba soma uzi vizuri uelewe halafu utoe maoni si kila mkosoaji upinzani ni mtawala kama ambavyo wengi mnaojiita wafuasi wa "ushabiki wa upinzani" mnavyodhani sasa kwenye hoja yako ya kupuuza na kusema waache tu wamtangaze hakuna mtu mwenye muda na uchaguzi tafsiri yake pana ni nini kama sio ukataji tamaaa? una mkakati gani unaonekana na kurudisha morali na mwamko wa wapiga kura wako inayoonekana na yenye mashiko apart from sympathy strategy ya kulaumu na kushutumu watawala kama ulivyoainisha hapo juu sijui anashinda huyu anatangazwa yule mara sijui watu wamepigwa hayo yana msaada gani kwa upinzani katika harakati za kushika dola? Isije mkawa mnacheza ngoma ya wajanja walio katika uongozi wa upinzani wanaojaribu kutoa lawama kila siku ili kuwaaminisha "washabiki wao" kuwa wanaonewa tu bila kutoa suluhu ya kweli juu ya hali halisi....mi napenda kubishana kwa hoja bila kuvaa joho la mtu yoyote sasa kama ndugu yangu utajibu huku ukiwa na joho flani hatutaweza kuelewana
Shutuma haziji bila matendo ambayo sio hulka ya Wanzania ndo maana sintofahamu imetamalaki kila mahali ktk hii nchi yenye upendo
 
Sijui unaongea nini, toka mfumo wa vyama vingi umeingia hapa nchini wapinzani wenye nguvu wamekuwa wakifanyiwa vitimbwi vya kuumizwa na hata kuuwawa. Wamekuwa kila mara wakitaka tume huru ya uchaguzi na kanuni za uchaguzi kuheshimiwa. Hilo halijatekelezwa hadi sasa, kibaya zaidi kila mara wapinzani wa kweli wanabezwa kama mmekubali kushiriki ina maana mmeridhika na mwenendo wa uchaguzi. Sasa hivi unyama unazidi kuwa wazi huku wapinzani wakikutana na vipigo na ukatili mwingi sana. Imefikia mahali hata kura zinahesabiwa na kupigwa bila mawakala wa upinzani kuwepo. Haya yote yanatokea huku taifa zima likiwa kimya na kuonekana ni sawa na hata wasioridhika wameingiwa na woga na hawathubutu kukemea hali hiyo.

Suala la upinzani kushika dola inategemea kanuni za mchezo wa uchaguzi unafanyikaje, iwapo kanuni za mchezo zinakiukwa ili kukibeba chama tawala basi wapinzani nao inabidi waanze kukiuka kanuni za mchezo na hatimaye itakuwa ni mauaji na machafuko, hatuko tayari kufika huko maana sio wote ni wajinga ama wenye uchu wa madaraka. Wewe hapo ulipo mbali ya kujifanya unaona sisi wengine tumekata tamaa hatujakuona ukienda mahakamani kufungua kesi dhidi ya huu ukatili unaofanywa, unaishia kuleta porojo tu hapa. Watu wanaumizwa na kuachiwa vilema vya maisha na sio jukumu la chama kutibu wafuasi wake walioumizwa tena mara nyingine na vyombo vya dola. Tumeona wabunge wa upinzani juzi na wafuasi wao wakidhalilishwa kisa madaraka. Mbona hatukukuona ukienda kutoa msaada wa kisheria mahakamani?

Kibaya zaidi, narudia kibaya zaidi katika mazingira hatarishi ya hivyo mgombea wa upinzani anaweza kufanikiwa kushinda, kisha haipiti muda anajiuzulu eti anakwenda kumuunga mkono rais!! Kama una akili timamu kupiga kura kwenye mwenendo huu ni upuuzi uliopita kiasi. Kama mnataka watu wapige kura ili kuungopea umma na dunia kwamba kuna demokrasia ili kupatiwa misaada basi safari hii mmenoa. Ukitaka nenda na familia yako na wapambe wako, tena mpige picha mkiwa kituo cha kupigia kura mrushe kwenye facebook hakuna anayekuzuia. Sisi wengine maisha yetu hayategemei siasa bali tunapenda siasa safi sio huu ushenzi unaoendelea sasa.
Mkuu umeongea saana lakini bado unabaki kule kule katika ushabiki na hisia kuliko uhalisia! hayo unayosema yoote ni katika kutafuta huruma kwa wanananchi bila ya kuleta suluhu! Suluhu ni wapinzani kuacha maneno kufanya kazi kwa vitendo ionekane dhahiri kwa wananchi sijui kama kuna tawala itaweza kuzuia nguvu ya umma inayokubalika kwa wananchi wote bila kujali tofauti zao mfano kwa utendaji wa mbunge joseph haule jimboni kwake sioni kama kuna mtu anaewaza kuwa atatoka leo au kesho jamaa anakubalika kwa asilimia nyingi hata na hao wanaccm japo bado wenye uchu wa madaraka wanampinga kimtindo kwa kuwa jamaa yupo karibu na wananchi wake na anafanya kazi zao kwa kadri ya uwezo wake kama alivyokuwa yule late filikunjombe na ludewa hii ni miongoni mwa suluhu kwa upinzani kushika dola ila kama wapinzani wataendelea na siasa za kiharakati za kina lijualikali,lema kelele yingi majungu na kutia hamasa za fujo na chuki hakika vipigo kwa wafuasi wa upinzani havitawaacha salama sababu tz ukiwa mbwatukaji watu watajaa kukusikiliza kwa kuwa ni nchi yenye raia wanaopenda kusikia umbea, majungu, fulani kamsema fulani, but hawako tayari kukussuport katika mambo ya hovyo japo kuna watakaonaswa kutokana na sababu mbalimbali mfano kutokuwa na umri wa busara na mob psychology! Ukiangalia nchi za kiafrika ambazo upinzani umeweza kuwaondoa watawala mostly watu hao walijenga imani kwa wananchi kupitia kazi zilizonekana na sio maneno ya kelele mfano mfuatilie late michael satta wa zambia mfuatilie macky sally wa senegal ambae ni mkristo anaetawala taifa lenye 90% ya waislamu,adama barrow gambia kupitia Majum Real Estate aliweza kutoa ajira nyingi kwa vijana wa kigambia mwisho wa siku kaja kumng"oa kigogo yahya jameh. Wapinzani wa nchi hii kama wana dhamira ya kushika dola na si kula ruzuku kwa vyama vya familia zao, lazima waache usanii kwa kuwapumbaza watu na kutafuta huruma kwa wananchi wafanye kazi kweli kwani na wawe karibu na wananchi sidhani kama kuna mtu atakubali kupewa t shirt na kanga sijui na chumvi aunge mkono watu wasio karibu nao wala kuwajali. Nina hakika kupitia tume hiyo hiyo ndio iliyowaptia hao wabunge na madiwani sasa iweje sehemu upinzani ukishindwa tume hiyo iwe mbaya?? Mzee lowasa alitoa wosia mzuri sana kwa mameya walipoenda kumtembelea ofisini kwake pale mikocheni KUWA NENDENI MKAFANYE KAZI WATU WAONE TOFAUTI YA SISI NA WAO nadhani hii ndio silaha pekee ya upinzani kuwin the situation pia akongeza kule arusha katika mkutano wa madiwani wa Ukawa TUACHE SIASA ZA KIHANAHARAKATI TUJENGE CHAMA TOKEA KATIKA MASHINA YA CHINI KABISA nadhani wewe pia unaweza kuwa shahidi wanazi na mashabiki wa Ukawa walivyomponda mzee huyu. Mdau hamna shortcut katika maisha upinzani lazima ufanye kazi kubwa na si kubwata bwata, kuzungusha mikono,kumsema rais vibaya,kushadadia nyufa za hostel, kupaka watu rangi na kusema wamepigwa mapanga,(ushawahi kujiuliza hali zao zinaendeleaje baada ya uchaguzi) kuandaa vijana kuzuia kina mama kwenda kupiga kura,kuzungumzia sana mambo ya chama tawala kuliko ya chama chao,Kuhamisha magoli kuwa mtu akihama kanunuliwa basi kama ni hivyo hamna mtu mwenye akili timamu atakepigia kura mtu ambae baadae atanunuliwa.Upinzani Lazima ufanye kazi na uache usanii wa kihanaharakati
 
Vipi mkuu wewe kwa hali ilivyo ya kisiasa unaona kuna haja ya vyama vya upinzani kushiriki hizo chaguzi? Rejea uchaguzi mdogo wa madiwani......
Mkuu haja ipo tena sana kwa kuwa ni haki ya kikatiba ila lazima upinzani ufahamu eneo husika wanakubalika kiasi gani na hata kama hawakubaliki kiivyo je kuna changamoto gani katika eneo hilo wanazoweza kuzianisha kwa wananchi na namna ya kuzitatua kwa mifano iliyo dhahiri kuacha kuhubiri majungu kwa muda mrefu katika kampeni!! kuhusu uchaguzi mdogo wa madiwani kuna shutuma nyingi za ukiukwaji wa haki za kibinadamu zinazotolewa na upinzani lakini mkuu mbona hata wapinzani pia wanashutumiwa kuwafanyia fujo watawala katika uchaguzi huo huo!! ila kwa kuwa matokeo hayakuwa mazuri kwa upande wa upinzani Hilo la fujo ndio ikatumika kama sababu kuu ya wao kushindwa chaguzi!
 
Back
Top Bottom