Kikao gani kiliamua Nyerere awe 'Baba wa Taifa'?

Kikao gani kiliamua Nyerere awe 'Baba wa Taifa'?

Sina imani kama majibu yangu yatamridhisha mleta mada hapa kwa kuwa tayari ameonesha kupingana na uhalisia..
HATA HIVO NITAJARIBU.
Katika hali ya kawaida, Baba ni kiongozi na mwanzilishi wa familia. Hii inaapply hata kama baba huyu si mzazi wa kibiolojia wa mtoto.
Tukubali kitu kimoja cha msingi sana. Baada ya kupata uhuru wa Tanganyika, Tanganyika ilifanyika kuwa familia.. Raia wake walianza kushiriki kikamilifu kufanya maamuzi juu ya Taifa lao. Wote kwa pamoja tuliipata heshima iliyokosekana kwa zaidi ya miaka 120!! Tukaanza kujituma wenyewe kwa maslahi yetu na ya nchi yetu badala ya kutumikishwa na wazungu kwa maslahi yao na mataifa yao. HII ILIKUWA NA KILA ELEMENT YA FAMILIA. Baba wa Taifa, mwalimu J.K. Nyerere alilisimamia hili akishirikiana na mlolongo mrefu wa wapigania uhuru, wengine tunaowataja katika historia na hata wale ambao historia haiwataji, walio hai leo na wale waliotangulia. Mwalimu aliikamilisha kazi njema ambayo baba na babu zetu akina Kinjekitile, Mkwawa, Mirambo, Isike na wengine wengi waliifanya miaka mingi kabla. Historia na masimulizi yanazielezea juhudi za Baba wa Taifa katika kufanikisha mapinduzi ya Zanzibar na hata uhuru wa mataifa mengine ya Afrika. Baada ya mapinduzi ya Zanzibar, mwalimu pamoja na wapigania uhuru wa Zanzibar, hawakuona sababu ya kuwa na nchi mbili ilhali umoja ndiyo iliyokuwa falsafa yao. Zanzibar ikaungana na Tanganyika kuunda Tanzania. Muungano huu ulileta mtoto mpya, taifa la Tanzania. Hapa mchango wa Mwalimu ulikua mkubwa,wa kipekee na uliotukuka. Nyingi ya hotuba zake zinaonesha namna alivyopendezwa na umoja wa waafrika.
Wapigania uhuru wenzake, wengine bado tuko nao leo (Mwenyez Mungu awape heri ya maisha marefu zaidi) waliridhia Nyerere aitwe BABA, na walimwita hivyo tangu siku za awali za uhuru..
HUYU NI BABA!
HUYU NI MSINGI WA UANZISHWAJI WA TAIFA LA TANZANIA!
HUYU NI CHIMBUKO LA MAFANIKIO YA JUHUDI ZA KUJIKOMBOA!
R.I.P BABA WA TAIFA..
 
Sina imani kama majibu yangu yatamridhisha mleta mada hapa kwa kuwa tayari ameonesha kupingana na uhalisia..
HATA HIVO NITAJARIBU.
Katika hali ya kawaida, Baba ni kiongozi na mwanzilishi wa familia. Hii inaapply hata kama baba huyu si mzazi wa kibiolojia wa mtoto.
Tukubali kitu kimoja cha msingi sana. Baada ya kupata uhuru wa Tanganyika, Tanganyika ilifanyika kuwa familia.. Raia wake walianza kushiriki kikamilifu kufanya maamuzi juu ya Taifa lao. Wote kwa pamoja tuliipata heshima iliyokosekana kwa zaidi ya miaka 120!! Tukaanza kujituma wenyewe kwa maslahi yetu na ya nchi yetu badala ya kutumikishwa na wazungu kwa maslahi yao na mataifa yao. HII ILIKUWA NA KILA ELEMENT YA FAMILIA. Baba wa Taifa, mwalimu J.K. Nyerere alilisimamia hili akishirikiana na mlolongo mrefu wa wapigania uhuru, wengine tunaowataja katika historia na hata wale ambao historia haiwataji, walio hai leo na wale waliotangulia. Mwalimu aliikamilisha kazi njema ambayo baba na babu zetu akina Kinjekitile, Mkwawa, Mirambo, Isike na wengine wengi waliifanya miaka mingi kabla. Historia na masimulizi yanazielezea juhudi za Baba wa Taifa katika kufanikisha mapinduzi ya Zanzibar na hata uhuru wa mataifa mengine ya Afrika. Baada ya mapinduzi ya Zanzibar, mwalimu pamoja na wapigania uhuru wa Zanzibar, hawakuona sababu ya kuwa na nchi mbili ilhali umoja ndiyo iliyokuwa falsafa yao. Zanzibar ikaungana na Tanganyika kuunda Tanzania. Muungano huu ulileta mtoto mpya, taifa la Tanzania. Hapa mchango wa Mwalimu ulikua mkubwa,wa kipekee na uliotukuka. Nyingi ya hotuba zake zinaonesha namna alivyopendezwa na umoja wa waafrika.
Wapigania uhuru wenzake, wengine bado tuko nao leo (Mwenyez Mungu awape heri ya maisha marefu zaidi) waliridhia Nyerere aitwe BABA, na walimwita hivyo tangu siku za awali za uhuru..
HUYU NI BABA!
HUYU NI MSINGI WA UANZISHWAJI WA TAIFA LA TANZANIA!
HUYU NI CHIMBUKO LA MAFANIKIO YA JUHUDI ZA KUJIKOMBOA!
R.I.P BABA WA TAIFA..
 
Kumbe kweli humuJFkuna wapumbavu kwelikweli.Hivi kwanini udini wawakristo hauwenekani ila wawaislamu tu?Au hiyo yenu sio dini ya kweli hivyo haistahili kuitwa udini bali ukafiri?Mtoa uzi kauliza vizuri tu,Baba wataifa ni heshima tu kwamchangowake ktk Taifa,Lakini maaskofu wanataka kumsimika mwenyeheri kalifanyia nini kanisa na kuwaacha waislam nyuma haliyakua yeye si MDINI?.Hapo ndo tunaamini Nyerere ndiye mwasisi wa UDINI tanzania.Baada ya kulegalega ktk utawala wa kikwete maaskofu wanataka kuurudishia nguvu kupitia DR SLAA.

Nyerere alikua mkatoliki kwa dini. Yeye alijitambulisha hivyo. Yeye alizijua, alizishika na kuziheshimu taratibu za dini yake. Alipobatizwa kikatoliki, NANI ALIHOJI?
Alipopata komunyo na kipaimara, NANI ALIHOJI?
Alipofunga ndoa ya kikatoliki, NANI ALIHOJI?
Alipokua anahudhuria ibada za kikatoliki, NANI ALIHOJI?
Alipokua anakula na kunywa vinavyoruhusiwa na viongozi wake wa dini, NANI ALIHOJI?
Alipokua anaenda hija, kutoa zaka au mavuno, NANI ALIHOJI?
Alipovaa rozari, kutembea na biblia au kufunga kwaresma, NANI ALIHOJI?
Alipofanyiwa ibada ya mazishi ya kikatoliki, NANI ALIHOJI?
Anapoendelea kufanyiwa Ibada za kumbukumbu na wakatoliki, NANI ANAHOJI?
Anapoandaliwa kuwa mtakatifu na wakatoliki wenzake, WANAOHOJI WANATOKA WAPI??
Mwalimu alikua na maisha yake binafsi ya kidini,
Waacheni wakatoliki waheshimu taratibu na tamaduni zao!!
 
Kikao gani cha serikali na chama walikaa na kuamua kumwita Mwl.Nyerere kuwa aitwe baba wa taifa? Kikao hicho kilifanyika wapi na tarehe ngapi? Tangazo la jina hilo lilitolewa na nani na katika chombo kipi halali cha serikali?
Kuna wakati mbunge mmoja simkumbuki jina alisema"kwakuwa Nyerere anaingia kwenye mchakato wa utakatifu basi heshima ya ubaba wa taifa apewe mh.Mkapa!" akaongeza "kwakuwa utawala wa Mkapa ulikuwa mzuri basi napendekeza bunge liridhie tubadili katiba ili mkapa agombee tena ili aweze kutawala kwa miaka 10 mingine?".

Mytake:
Huu ni mlolongo wa sintofahamu ndani ya Tanzania ambazo zimepaliliwa tangu enzi! Kwani Nyerere alilifanyia nini kanisa katoliki hadi limpe hadhi ya utakatifu wakati yeye mwenyewe alidai ni haramu/dhambi kuchanganya dini na siasa?

Naomba tujadili hoja hii nyeti kwa ueledi nasio matusi na kejeli.

Kwanza kabisa nakataa hoja ya bwana mkapa kuruhusiwa kugombea tena kwa awamu nyingine 7bu naamini kuna waTz wengi tena wenye uwezo zaidi yake na ujue wote sisi ni binadamu na ipo siku tutarudi kwa muumba wetu, sasa je siku ambayo hatakuwepo hakutakuwa na mtu wa kuiongoza Tz? Suala la Nyerere kupewa utakatifu ni jambo ambalo linafanywa na waromani pasipokujali ni mwana ndoa ama mtawa bali uwe muumini wao ambaye atakuwa amekidhi vigezo vilivyowekwa
 
Nyerere alikua mkatoliki kwa dini. Yeye alijitambulisha hivyo. Yeye alizijua, alizishika na kuziheshimu taratibu za dini yake. Alipobatizwa kikatoliki, NANI ALIHOJI?
Alipopata komunyo na kipaimara, NANI ALIHOJI?
Alipofunga ndoa ya kikatoliki, NANI ALIHOJI?
Alipokua anahudhuria ibada za kikatoliki, NANI ALIHOJI?
Alipokua anakula na kunywa vinavyoruhusiwa na viongozi wake wa dini, NANI ALIHOJI?
Alipokua anaenda hija, kutoa zaka au mavuno, NANI ALIHOJI?
Alipovaa rozari, kutembea na biblia au kufunga kwaresma, NANI ALIHOJI?
Alipofanyiwa ibada ya mazishi ya kikatoliki, NANI ALIHOJI?
Anapoendelea kufanyiwa Ibada za kumbukumbu na wakatoliki, NANI ANAHOJI?
Anapoandaliwa kuwa mtakatifu na wakatoliki wenzake, WANAOHOJI WANATOKA WAPI??
Mwalimu alikua na maisha yake binafsi ya kidini,
Waacheni wakatoliki waheshimu taratibu na tamaduni zao!!

Mpaka sasa ni viongozi wangapi wakatoliki serikalini wamepewa cheo hicho? Wa sasa na wa zamani.
 
Mila na taratbu za kila dini zinapaswa kuheshimiwa.. Uvumilivu ni jambo la msingi sana katika hili jamani.. Yapo mambo mema wanayofanya wakristo, hali kadhalika yapo mambo mema wanayofanya waislam.. Tujishughulishe zaidi na haya, tuhangaikie zaidi yanayotuunganisha. Pia mambo ya kitaifa tusiyachanganye na dini zetu, yanapelekea kuanza kutukanana, kurushiana vijembe na kututoa katika mstari..
 
Kwanini kanisa linataka kumpa cheo kalifanyia nini kanisa?

Sijajua kama kuitwa Mwenye Heri au Mtakatifu ni cheo katika kanisa, hilo ntawaomba viongozi wao watalitolea majibu kwa kuwa wapo humu.. Pamoja na hilo, jamani, WAKATOLIKI WANAJENGA KANISA LAO, INATUHUSU NINI SISI??
Wakatoliki wanataka kutumia taratibu zao, kumwomba Mungu wanayemwabudu, kwa kutumia taratibu zao, amkubali Nyerere, alie mkatoliki mwenzao, kuwa mwenyeheri na baadae mtakatifu kwa mujibu wa imani yao.. Tunajadili nini sasa??
Mbona wametangazwa wengi sana hatujahoji jamani?
YA WAKATOLIKI KUFANYA UKATOLIKI TUWAACHIE WAKATOLIKI WENYEWE!!
 
Mpaka sasa ni viongozi wangapi wakatoliki serikalini wamepewa cheo hicho? Wa sasa na wa zamani.

Kuwa kiongozi wa Serikali sio mojawapo ya kigezo cha mtu kutangazwa mtakatifu au mwenyeheri.. Hii inagusa zaidi maisha ya mtu peke peke katika dini yake, haiwi influenced na title aliyo nayo ktk serikali, chama wala jamii yake kisiasa..
 
Mkuu, leo sihitaji sana mjadala nimechoka, labda tusaidie na msaidie mtoa hoja kutuelimisha, tuwe kama wenye akili

timamu hivi.
Ilikukanusha jambo flani lazima ulijuwe vema undani wake, vinginevyo ni ushabiki usio na mizania katika kubisha.

Labda tukuulize unafahamu sifa za kiongozi wa taifa kuitwa baba wa taifa?

a) Kama jibu ni ndiyo zitaje, kisha fafanua kwanini?

b) kama jibu ni hapana, kwanini aiweke hii hoja hapa na hajui unachokiwakilisha.

Naomb angalia sifa za haw viongoz wamefanyia mataifa yao makubw lakin hakutukuzwa .hindira gandh wa india.mau wa china.muhamed wa malysia.na mandela
 
Heshma aliyoipata Nyerere haikutokana na vikao .Nyerere alijijengea Heshma kwa yale aliyo yafanya katika Jamii ya Tanzania na Kimataifa kwa Kadri ya uwezo wake ambao Mungu alimjali. Kumbuka kuna wengine walijaribu hapo katikati kutoa majina mbalimbali kwa Viongozi walifuatia lakini yalikosa mshiko kwani hayaku husiana kiuhalisia na yale waliyoyafanya katika Uongozi wao.

Kuhusu suala la Utakatifu halihusiani na nafasi yake kama Rais au Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wala si haki kufikiri kuwa Utakatifu unapatikana kwa lile ulilolitenda kwa Kanisa.Utakatifu kwa Maoni yangu siyo ofa au zawadi kwa Mtu ni mchakato maalum kabisa ambao unahusiana na maisha Binafsi ya Muumini na kwanamna alivyo ishi kwa unyenyekevu na kutekeleza maagizo ya Mungu .

nakubaliana na ww!jinsi alivyoonea raia anastahili kuitwa baba wa taifa
 
Anastahil kuitwa baba wa taifa kwani alikuwa hataki ushaur wala nini!na ukimzingua kidogo tu utaliona balaa lake!alikuwa mbabe hadi kwa watu wake wa karibu kabisa kama akina kambona
 
Omba kwanza kujua ni sifa gani za kanisa katoliki zinazomfanya mtu kutangazwa mtakatifu au mwenyeheri. Pili yaangalie kwa karibu maisha ya mwalimu Nyerere na Binadanu wenzake duniani wakati wa uhai wake.
Baada ya hapo uliza swali lako.
 
NI kazi sana kuongoza mtu wa aina yako, acha basi kuangalia hizo CD za kina sheikh nanihii, hazina la maana zaidi ya kukuchafua ubongo na kuipaka matope kama si kuiweka mfukoni elimu yako. Sikiliza maudhui ya masheikh wako msikitini yana tija na yatakufanya raia mwema
 
Umetoa hoja nzuri lakini ulipoingiza ukatoliki nikajua ni mfanyakazi wa redio imani morogoro!!!!!!!!!!!!!!
 
Hebu nijaribu kujibu swala la mleta mada kama ifuatavyo.

Suala la Mwl. Nyerere kupewa hadhi ya Ubaba wa Taifa halikuja hivi hivi bali lilikuwa Azimio la Bunge la Jamuhuri ya Muungano wakati Mwl. anastaafu kutoka kiti cha Raisi mwaka 1985. Hoja ya Azimio hili ilipelekwa Bungeni na Hayati Mzee Thabiti Kombo, wakati huo akiwa Mbunge toka Zanzbar, Hoja hii ilisomwa kwa niaba yake na Ndg. E.D Maokola Majogo, Mbunge wa Nachingwea tarehe 29.07.1985.

Bunge liliridhia hoja hii na hivyo kuazimia Mwl. Nyerere atambulike kama Baba wa Taifa, na picha zenye sura yake ziendelee kubaki kwenye Ofisi za chama/vyama na serikali, sarafu na mojawapo ya noti za fedha za Tanzania.

Azimio hili lilizingatia mchango wa dhati wa Mwl. Nyerere katika mambo mengi, nitaandika machache kati ya mengi:
1.Kuanzisha Tanu 1954, 2. Kuacha kazi ya Ualimu 1955 ili kuongoza harakati za kudai uhuru. 3.Kushiriki kuunda PAFMECA 1958. 4.Aliweka msimamo ktk jumuia ya Madola kuhusu Ubaguzi wa Rangi, msimamo huo uliitoa Afrika ya Kusini nje ya Jumuia ya Madola hadi mwanzoni mwa myaka ya 90. 5.Kuongoza Tanganyika kupata uhuru 1961. 6.Kujiuzuru Uwaziri Mkuu ili kuimarisha TANU, 1962.Kushiriki kuunda OAU 1963. 7. Kushirikiana na Karume kuunganisha Tanganyika na Zanzbar 1964. 8.Mwaka 1965 alivunja uhusiano na Uingereza kufuatia mgogoro wa Uhuru wa Rhodesia.

Kwa kweli mlolongo wa matukio muhimu kabisa na ya kihistoria, yanambainisha Mwl. kama mtu wa pekee kwa Tanzania, mtu mwenye msimamo usoyumba, mtetezi wa haki na zaidi ya yote mtu mwenye kipaji cha kushawishi kwa hoja. Viongozi wa mataifa makubwa walimuheshimu Mwl. kwa busara na hekima zake bila kujali itikadi yake ya Ujamaa mfano Jimmy Carter nk nk. Kung'atuka ktk Uraisi, ikumbukwe Mwl aliacha kazi ya Uraisi kabla ya muda wake kwisha. Azma hii alikuwa nayo muda mrefu na alikuwa amenuia kung'atuka mwaka 1980 kama isingetokea watu kumshauri aendelee kuongoza, lakini hili zaidi lilitokana na madhara ya vita ya Amini 1978-1979. Mwl, aling'atuka kwenye uongozi wa CCM mwaka 1992 lakini kabla ya hapo alikuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha mfumo wa vyama vingi unaanzishwa. Wakati ule hoja ya kuruhusu mfumo wa vyama vingi ilipingwa vikali na viongozi wa CCM na hata watanzania wenyewe.

Bila shaka, sifa hizi za kipekee ndizo zilizo fanya Bunge likaazimia aitwe "BABA WA TAIFA". Kuhusu kanisa katoliki kuanzisha mchakato wa kutafiti endapo aliishi maisha ya mfano wa utakatifu, hili pia linatokana na maisha yake binafsi. Nielezee kidogo.

Mwl. alibatizwa mwaka 1942 huko Nyegina Musoma, Alifunga ndoa mwaka 1953 na mama Maria Nyerere. Mwaka 1955 alipoacha kazi ya ualimu huko Pugu-Dsm, alirejea musoma alipofanya kazi na shirika la wamisionari wa Merynoll. Baadhi ya kazi alizozifanya ni pamoja na kutafsiri maandiko matakatifu ya biblia na Katekesmu Katoliki kwenda lugha ya Kizanaki. Kadhalika, alikuwa muumini mzingativu (Practising Christian) ktk masuala ya kiimani. Katika hili, yapo mambo mengi yaliyojificha ambayo si tu wakatoliki hawayajui bali pia watanzania na ulimwengu hauyafahamu kuhusu Mwl. Nyerere. Mimi pia siyajui kiivyo.

Mfano, wakati flani Mwl. Nyerere aliwahi kusema "Mimi katika handbag yangu daima siachi vitu viwili, Biblia na Kijitabu cha Azimio la Arusha......................' Kwa mantiki hii, huenda kanisa Katoliki limeona elements za maisha ya upekee ya kiroho ya mzee huyu. Mchakato hata ivyo, ni mrefu na wakati mwingine huchukua hata karne nzima kutafiti maisha ya utakatifu wa mtu ili hatimaye kumtangaza mtakatifu. Huko Ulaya, Marekani zote, Asia, Mashariki za mbali hata Afrika watakatifu wapo. Uganda wapo, Sudani yupo nk nk. Kwa hivi, hili lisitusumbue mana vizazi vyetu pengine ndio watakao shuhudia UTAKATIFU WA MWL JULIUS KAMBARAGE NYERERE (1922-1999).

Ikumbukwe pia, Mwl Nyerere pammoja na kuongoza nchi kwa zaidi ya miaka 20, alistaafu akiwa hajajilimbikizia mali yoyote, aliishi maisha ya kawaida, alipenda kukosoa hadharari maamuzi mabovu ya serikali na wakati wote, nasema wakati wote, Viongozi wa Chama cha CCM na serikali yake hawakumpenda Mwl kwa sababu ya msimamo wake dhidi ya ubinafsi, kiburi, rushwa, fitina na unafiki.

Wakati mwingine si rahisi kutoa majibu ya kuweza kumridhisha kila mtu, lakini ni vizuri kujitahidi kutoa maelezo mazuri kwa upole bila jazba. "Watu wengine wameshindwa kumtambua Mungu ktk maisha yao kwa sababu Waalimu wa dini hawajitahidi kutoa maelezo mazuri kuhusu Mungu, na zaidi ya yote.....wanashindwa kuishi kwa vitendo mafundisho wanayo wafundisha waumini wao". ............................. Huenda hizi sababu chache zinatosha kumfanya Mwl. kuwa BABA WA TAIFA? Hapana, zipo nyingi, Hata tukiacha kumuita Baba wa Taifa, tutamuita Mwalimu km yeye mwenyewe alivyopendelea kuitwa, na pengine jina Mwl. linamstahili zaidi? Sijui!
 
Back
Top Bottom