Kikokotoo: Wafanyakazi ambao wamebakiza muda mfupi kustaafu ni kilio kila kona ya nchi

Kikokotoo: Wafanyakazi ambao wamebakiza muda mfupi kustaafu ni kilio kila kona ya nchi

RWANDES

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2019
Posts
1,788
Reaction score
4,401
Ndugu zangu nimekutana na wazee wenye heshima zao na wamo ndani ya CCM wakilaumu mpango mzima wa Serikali wakutaka kupora hela zao za kustaafu eti kwa kigezo cha kuwapa kidogo kidogo kustaafu kitendo hicho wanakilaani kwa maneno ya chini kwa chini bila kujitokeza hadharani.

Nimewambia wapeleke malalamiko yao kwenye chama kwa katibu mkuu wa chama mheshimiwa Chongolo maana wanadai kwa upande wa Serikali wanaona hayupo mtu yeyote kuanzia waziri mwenye dhamana hadi katibu mkuu utumishi hawezi kuwasemehe.

Cha ajabu bado wanasema viongozi wao wanaupiga mwingi katika kuwaletea maendeleo wananchi, kahawa wamekunywa imeisha wananiambia kijana wetu tuachie hata hela ya chupa moja mimi sikuwa na kinyongo nao nimewapa tsh 1000/= wachukue chupa moja ya kahawa kwa muuzaji nikaondoka zangu maana kuna mambo yalitaka kunitokea yakutaka kuwatukana.

Ndugu zangu siyo raia wakawaida ambao hawana uelewa wa nchi inavyoendeshwa tu hata wafanyakazi wa serikali miongoni mwao hakuna walijualo, nilijaribu kugusia katiba mpya walinipuuza na kuanza kuniambia wewe ni mpinzani, nikawajibu katiba mpya haina upinzani bali ni yetu sote wananchi lakini hawakunielewa.
 
Ndugu zangu nimekutana na wazee wenyeheshima zao na wamo ndani ya CCM wakilaumu mpango mzima wa serikali wakutaka kupora hela zao za kustaafu eti kwa kigezo cha kuwapa kidogo kidogo kustaafu kitendo hicho wanakilaani kwa maneno ya chini kwa chini bila kujitokeza hadharani.

Nimewambia wapeleke malalamiko yao kwenye chama kwa katibu mkuu wa chama mheshimiwa Chongolo maana wanadai kwa upande wa serikali wanaona hayupo mtu yeyote kuanzia waziri mwenye dhamana hadi katibu mkuu utumishi hawezi kuwasemehe.

Cha ajabu bado wanasema viongozi wao wanaupiga mwingi katika kuwaletea maendeleo wananchi, kahawa wamekunywa imeisha wananiambia kijana wetu tuachie hata hela ya chupa moja mimi sikuwa na kinyongo nao nimewapa tsh 1000/= wachukue chupa moja ya kahawa kwa muuzaji nikaondoka zangu maana kuna mambo yalitaka kunitokea yakutaka kuwatukana.

Ndugu zangu siyo raia wakawaida ambao hawana uelewa wa nchi inavyoendeshwa tu hata wafanyakazi wa serikali miongoni mwao hakuna walijualo, nilijaribu kugusia katiba mpya walinipuuza na kuanza kuniambia wewe ni mpinzani, nikawajibu katiba mpya haina upinzani bali ni yetu sote wananchi lakini hawakunielewa.
Mbona hueleweki, unataka kusema nini tukusaidie kukupa ufafanuzi.
 
Hicho kikokotoo hakiwakokotoi wanasihasa na viongozi wakubwa wote wakiwemo wagonga meza, pm, chupika, vp na rahisi, kwa hiyo ule wimbo wa watajibeba unawahusu wengineo wote........walamba asali wengine wataponea kwenye kamba zao.
 
mkuu kama uko njema hebu tuwekee data za vikokotoo kwa nchi nyingine tulinganishe tupate pa kuanzia
Namaanisha wale wote waliopendekeza kuwepo kwa hicho kikokotoo kwa kuchagua makundi ya watumishi wa umma, wote hawana akili.

Haiwezekani hicho kikokotoo kisiwahusu Wabunge, Maspika, Majaji wakuu, Marais, nk! Badala yake kiwahusu watumishi wa ngazi za chini pekee.

Mbunge ndani ya miaka mitano tu, anapewa mafao yake yote! Mfanyakazi wa hali ya chini aliyefanya kazi kwa miaka zaidi ya 30, anapewa 33%!! Huu ni uwendawazimu.

Kwa nini sheria isitoe uhuru kwa hao wafanyakazi kuchagua aina ya kikokotoo wakipendacho? Kwa nini serikali ijimilikishe fedha ambazo siyo za kwao?
 
Mollel Wala hakuna sehemu kakosea ila tu ni kutopenda kwetu kuusikia ukweli.
 
Wapo wanatengeneza kivuko inchi ya hovyo sana hii

USSR
Wewe hueleweki,ni mkosoaji ama msifiaji wa serikali iliyopo madarakani. Kila mara unajicontradict wewe mwenyewe kwenye mada tofaut.
 
Namaanisha wale wote waliopendekeza kuwepo kwa hicho kikokotoo kwa kuchagua makundi ya watumishi wa umma, wote hawana akili.

Haiwezekani hicho kikokotoo kisiwahusu Wabunge, Maspika, Majaji wakuu, Marais, nk! Badala yake kiwahusu watumishi wa ngazi za chini pekee.

Mbunge ndani ya miaka mitano tu, anapewa mafao yake yote! Mfanyakazi wa hali ya chini aliyefanya kazi kwa miaka zaidi ya 30, anapewa 33%!! Huu ni uwendawazimu.

Kwa nini sheria isitoe uhuru kwa hao wafanyakazi kuchagua aina ya kikokotoo wakipendacho? Kwa nini serikali ijimilikishe fedha ambazo siyo za kwao?
Atakuja mtu atarekebisha haya...
 
Back
Top Bottom