kikombe atumiacho babu Alikiokota nyumbani kwake!!!!!!!

kikombe atumiacho babu Alikiokota nyumbani kwake!!!!!!!

Je, mmegundua sababu za babu kuzuiwa kutolea tiba zaka nje ya Samunge? Ni kwa sababu kuna wengine weengi wa aina yake wangefuata, hivyo kuwa confined kwenye maeneo yao tu. Waliopo mpaka sasa:

1. Loliondo
2. Mbeya
3. Tabora
4. Mtwara
5. Magu
6. Mwanza
7. Morogoro
8. Pwani
9. ..........

Still more to come. Just wait and see. Yule wa Tabora amekuwa endorsed na maaskofu kiaina kama mzee wa Samunge. Wa Morogoro kuna kila dalili maimamu wamemkubali kwani sehemu ya mapato yake yanapelekwa misikitini.

Mbeya nako kaibuka mchungaji mwingine ambaye ameoteshwa dawa na kwamba yeye ni tawi la babu. People open your eyes and see.

Mathew 7 : 13-14
"Enter by the narrow gate. For the gate is wide and the way is easy that leads to destruction, and those who enter by it are many.
For the gate is narrow and the way is hard that leads to life, and those who find it are few."

Hivi mbeya si yule kijana aliyeoteshwa na marehemu mama yake, ambaye alikuwa ni mganga?

SWALI LA KUJIULIZA KWAMBA HAO WATU WALIOIBUKAA MIKOA MINGINE WALIKUWA WAPI SIKU ZOTE? Kwangu mimi naona ni utapeli ambao unakuja kwa lengo la kutengeneza mazingira yatakayoonyesha hata babu wa loliondo ni tapeli. Japokuwa babu wa loliondo ameanza kutibu agosti mwaka jana, hawa wengine wote wameoteshwa ndani ya wiki 3 zilizopita. Ni vizuri serikali ikawa makini katika kuthibitisha uponaji wa hao wagonjwa wanaopata vikombe ili kupata ukweli.
 
mimi ningekuwa miss judith ningeachana na habari za babu kwasababu kama ambavyo watu hawawezi kunibadilisha imani yangu maana nina msimamo mkali na ninachoamini ni sahihi ndivyo hivyo hivyo ambavyo mimi siwezi kubadilisha imani za watu.

mpendwa, kwa nini tuachane nazo wakati watu wanaangamia kwa kukosa maarifa? huoni kuwa hata wasipobadilika, lakini mbegu ya neno itakuwa imepandwa na inasubiri kuota?

huu sio mchuano kama wa mpira wa ligi ya premier hadi tuache eti kwa kuwa tu hatupati ushindi. sisi ni watenda kazi tu na hatutafuti ushindi wetu wenyewe. ushindi wowote katika hili ni wa Bwana Yesu ambaye ndiye mwenye shamba na mchungaji mwema na mkuu wa kondoo

ubarikiwe sana
 
Hivi mbeya si yule kijana aliyeoteshwa na marehemu mama yake, ambaye alikuwa ni mganga?

SWALI LA KUJIULIZA KWAMBA HAO WATU WALIOIBUKAA MIKOA MINGINE WALIKUWA WAPI SIKU ZOTE? Kwangu mimi naona ni utapeli ambao unakuja kwa lengo la kutengeneza mazingira yatakayoonyesha hata babu wa loliondo ni tapeli. Japokuwa babu wa loliondo ameanza kutibu agosti mwaka jana, hawa wengine wote wameoteshwa ndani ya wiki 3 zilizopita. Ni vizuri serikali ikawa makini katika kuthibitisha uponaji wa hao wagonjwa wanaopata vikombe ili kupata ukweli.

Kwani babu alikuwa wapi siku zote? Au yeye ndio amekuwa nabii wenu wa mwisho hata muwakane wengine?

Huyo mchungaji wa Mbeya ni mwingine kabisa. Gazeti la majira la leo limeripoti habari zake. Anaitwa mchungaji Kennedy Mwasomola wa kanisa la mitume wapya kusanyiko la Tukuyu mjini. Ameoteshwa na Mungu mti na majani yake yanayotibu magonjwa sugu baada ya kuchemsha na kunywa kikombe. Aliota yuko kwenye foleni ya babu Loliondo. Alipokaribia kufika kupata kikombe akagundua kuwa hana hela (500). Akatoka kwenye foleni na kusimama pembeni. Ndipo akaona umbo mithili ya malaika. Akamponya uvimbe mkononi. Akamchukua mpaka kwenye mti uitwao mpandapanda. Akamwambia, " kwa kuwa wewe ni mwenyeji mwombe mzee mwenye mti huo uitwao mpandapanda ili ukatwe kwa ajili ya dawa." Mzee huyo akakubali kutoa mti bila kinyongo. Ndipo mchungaji akaamka. Akautafuta mti huo na ameshaanza kugawa dozi ya kikombe. Zaidi ya watu 2000 tayari wamekunywa. Anasema ameonyeshwa kuwa ni tawi la babu wa Loliondo.

Mwingine ni John Agunda mkazi wa Ruvu Darajani. Kaoteshwa na malaika. Ameshatoa tiba kwa zaidi ya watu 100. Hatozi hata senti moja. Haulizi mtu anaumwa nini. Ukienda kwa imani tu utapona.
 
Unaweza na ufahamu mkubwa kuhusu biblia,ukaitafsiri kutokana na akili zako,lakini kuna uhitaji wa Roho mtakatifu akuongoze,wako wapi waliojawa na Roho wa Mungu ambao kila siku anawashukia? Watumbie anasemaje kuhusu tiba hiyo,au mengi ya makanisa ya kiroho ni ya uzushi?
 
Huwa sipendi mijadala inayohoji imani ya watu wengine.
 
Kwani babu alikuwa wapi siku zote? Au yeye ndio amekuwa nabii wenu wa mwisho hata muwakane wengine?

Huyo mchungaji wa Mbeya ni mwingine kabisa. Gazeti la majira la leo limeripoti habari zake. Anaitwa mchungaji Kennedy Mwasomola wa kanisa la mitume wapya kusanyiko la Tukuyu mjini. Ameoteshwa na Mungu mti na majani yake yanayotibu magonjwa sugu baada ya kuchemsha na kunywa kikombe. Aliota yuko kwenye foleni ya babu Loliondo. Alipokaribia kufika kupata kikombe akagundua kuwa hana hela (500). Akatoka kwenye foleni na kusimama pembeni. Ndipo akaona umbo mithili ya malaika. Akamponya uvimbe mkononi. Akamchukua mpaka kwenye mti uitwao mpandapanda. Akamwambia, " kwa kuwa wewe ni mwenyeji mwombe mzee mwenye mti huo uitwao mpandapanda ili ukatwe kwa ajili ya dawa." Mzee huyo akakubali kutoa mti bila kinyongo. Ndipo mchungaji akaamka. Akautafuta mti huo na ameshaanza kugawa dozi ya kikombe. Zaidi ya watu 2000 tayari wamekunywa. Anasema ameonyeshwa kuwa ni tawi la babu wa Loliondo.

Mwingine ni John Agunda mkazi wa Ruvu Darajani. Kaoteshwa na malaika. Ameshatoa tiba kwa zaidi ya watu 100. Hatozi hata senti moja. Haulizi mtu anaumwa nini. Ukienda kwa imani tu utapona.

NAshukuru kwa ufafanuzi
Naona sasa hawa wawili watakuwa wame amua kuondoa swali la kwa nini babu anatoza 500, tuendelee kufuatilia hizi habari, na mimi naamini cha muhimu ni watu kupona, na kutokwenda kinyume na matakwa ya Mungu. Kama ni mtindo mpya wa shetani kuwarubuni watu, sisi tuendelee na maombi, ili shetani ashindwe
 
Kwa wanafunzi makini wa Biblia:
Hu ni mwendelezo wa utimilivu wa kilicho andikwa na Johana, katika
Ufunuo 16:13,14 (13And I saw three unclean spirits like frogs come out of the mouth of the dragon, and out of the mouth of the beast, and out of the mouth of the false prophet.14For they are the spirits of devils, working miracles, which go forth unto the kings of the earth and of the whole world, to gather them to the battle of that great day of God Almighty. ).

Soon mtasikia mtakatifu fulani amefufuka/yupo semu fulani anasema hivi na hivi.
Yesu alisema katika Mathayo 24,' angalieni mtu asiwadanganye' tuwe makini tuchunguze maadiko, otherwise tutakwenda na maji

Ufunuo (14:12) Here is the patience of the saints: here are they that keep the commandments of God, and the faith of Jesus

What is right is not always popular and what's popular is not always right. God is not after the majority, He is after those who diligently seek Him.
 
Nikiwa na mke wa aina ya Miss Judith ni mwanzo wa kukesha bar tu!....
 
Huwa sipendi mijadala inayohoji imani ya watu wengine.

kaka yangu hujitendei haki kwa kuwa na hulka ya namna hii!

imani za watu wengine zinahusu na kuwaathiri watu wengine tena wengi zaidi. kama imani yako haimuathiri mtu mwingine basi labda twaweza kusema tukuache, lakini kwa kuwa nawe tunakupenda, hatutakuacha upotee! sasa angalia imani ya mtu kama babu inazoa maelfu kwa maelfu ya ndugu zetu na kuwapeleka kusikojulikan, kwa nini sisi kama wapendwa wao tusione kuwa tunahusika kuziponya roho zote hizo za wapendwa zinazoangamia kwa kukosa maarifa?

Yesu alisema tupeleke neno lake na tuwafundishe watu kulishika hata miisho ya dunia na ukamilifu wa dahari. na ndio maana tunapeleka. imetupasa kumtii Mungu zaidi ya wanadamu hivyo hatutanyamaza mpendwa

enendeni duniani kote mkawafanye watu wote kuwa wanafunzi wangu
mkiwafundisha yote niliyowaamuru nilipokuwa ningali pamoja nanyi
na tazama niko pamoja nanyi siku zote hata ukamilifu wa dahari
 
How? Anayerudisha sifa ni yule aliyepona, aliyeponywa au wote?

Babu anasema tiba imetoka kwa Mungu na sifa irudi kwake. Yeye hataki chochote kile. Wewe nenda Youtube andika Loliondo Wonders au Maajabu ya Loliondo. Kwenye hiyo video anasema kabisa haya maneno. Sasa watu kama Miss Judith wanakwepa hayo na kuangalia machache. Sijui sasa tuwaonaje.
 
haya mambo ya babu haya kuna familia jana imezika mama yao mzazi,alikuwa siku zote anaumwa sukari na alikuwa mzima wa afya ni il tu kuna kipindi inashuka,fuata mkumbo kaenda kunywa kikombe kama wiki 2 zilizopita na juzi usiku kafa ghafla chumbani kwake nafikiri mpaka yakishakukuta ndio utaamini babu ni upuuzio tu wa shetani


kipi kilianishwa kuwa ni cause of death ya huyo mama?

Lakini hata ivo nina swali hili: wale wote walioponywa kwa miujiza ya Yesu ktk biblia waliishi milele ama hatimae nao walikufa?

Ukijibu hilo utakua ktk nafasi ya kuelewa pia kwa nini mama huyo alifariki
 
Mungu wetu ni mwema, hawezi kufanya maovu kwa binadamu, au kumpa kikombe babu ni uovu?
Kwani kitu gani katika dunia hii Mungu hawezi kufanya. Tusaidie kutafakari vizuri hili

Judy unalo lako jambo

you wanna walk high above God

unazidi mpaka hata chembe ya nia yako njema inapotea

Ata Yesu alitumia vitu vilivyotengenezwa na binadamu kufanya miujiza.Mungu daima anafanya kinyume cha akili zetu.You can not connect the dot easy with matendo ya Mungu.Yesu aliongeza samaki na mikate iliyonunuliawa na mtu aliyekuja ktk mahubiri.Kule kana Altumia mkasiki ya. Watu na ata maji yalichotwa na watu pia. With God no scientific way to under stand him.
If God can be defined his power and his hollyness at the laboratory or in a test tube ,Then is not so big cause he can stay in the lab testtube

"Mafarisayo wkamuuliza Yesu kati ya huyu kipofu na wazazi wake nani aliyekuwa na dhambi hata akazaliwa kipofu! Akwaambia hakuna ambaye alikuwa na dhambi ila ilikuwa mipango ya Mungu ili jina lake liinuliwa. Yesu akatema mate chini akafinyanga tope na tazama akampaka machoni kisha akamwambia nenda kanawe kwenye lile bwawa. Baada ya yule kipofu kunawa na tazama alipata kuona. Watu walipomwona wakasema huyu si yule kipofu ombaomba? Wengine walikubali na wengine walikataa! Wakuu wa sinagogi walimwita na kumuuliza yule aliyekuwa kipofu naye akawaambia kuwa yule mtu aitwaye Yesu ndiye aliyemtendea haya. Wakasema hakika huyu siyo mtu wa Mungu maana anatenda dhambi".

Tuna wengi nao wanabisha kazi ya Mungu kama Mafarisayo ambavyo hawakuamini kazi ya Yesu. Sitoshangaa Kwa baadhi ya watu kutoitambua kazi ya Mungu kupitia kwa watumishi wake. Hata Yesu angerudi leo bado kuna ambao hawataamini pia. Uzao wa Tomaso bado upo.

Kikombe cha babu ni kitendea kazi tu Judy wala usihofu hata kama kiliokotwa au kilidondoshwa kutoka juu, cha msingi babu anakitumia kama measuring tool yake ndo mana hakiachi kisije kikapotea, kutembea nacho ni aina tu ya utunzaji na haimaanishi vinginevyo... Usiitetereshe imani yako kwa kutafuta uhalali wa kikombe cha babu kwamba ni made in where!

Miss Judith Kwanza nakupa pole kila unacho dadisi kuhusu Babu kila mtu anakupinga na kukuona MJINGA Tuliokunywa tumepona Kama wewe huumwi shida yako nini?

...Judith, Wewe huna imani na anayofanya Babu basi baki na werevu wako kwa Amani.
Uache ule umati unamiminika kwa Babu kupata kikombe waendelee na Ujinga wao Kwa Amani.
It is Simple as That.
Why do you get so worked Over about Babu and his Kikombe? Why??? :noidea:


Namuliza Miss Judith kama ana uelewa ni wapi maandiko yanaonyesha kuwa Mungu ni careless? So why does she expect watumishi wawe kuwa careless.

Dada yangu Judith...

Kwa busara za kawaida na hekima ya kiwango cha kati........ hebu soma posts hizi na uzitafakari....Mimi pia sina uhakika wala imani juu ya tiba ya babu, lakini sauti ya watu ni sauti ya Mungu.........kama umeshindwa kabisa kuamini, basi tafadhali nakusihi, kaa kimya kuliko kuwakwaza watu.

What if hii huduma ya babu ikawa ni kweli ina baraka za Mungu, utapata muda wa kutubu dhambi ya kumwekea Mungu mashaka?
 
mpendwa, kwa nini tuachane nazo wakati watu wanaangamia kwa kukosa maarifa? huoni kuwa hata wasipobadilika, lakini mbegu ya neno itakuwa imepandwa na inasubiri kuota?

huu sio mchuano kama wa mpira wa ligi ya premier hadi tuache eti kwa kuwa tu hatupati ushindi. sisi ni watenda kazi tu na hatutafuti ushindi wetu wenyewe. ushindi wowote katika hili ni wa Bwana Yesu ambaye ndiye mwenye shamba na mchungaji mwema na mkuu wa kondoo

ubarikiwe sana

Miss Juddy..... kuangamia unamaanisha nini? Hao wanaopona wameangamia?

Miss Juddy....kikosa maarifa mana yake nini? Unahisi wewe una maarifa kuliko watu wote wale wanaopiga foleni kwenda kwa babu na hawa unaobishana nao kwa hoja hapa JF?

Miss Juddy.............mshukuru Mungu kwa kuwa una afya njema na wala huna ndugu unayemuuguza kwa magonjwa haya anayoyatibu babu.......tema mate chini yasikutokee kwa sababu utajikuta uko kwenye foleni Loliondo, bila kujua umefikaje pale.....Mungu apitishe mbali.
 
mkuu!! Shetani amepata kuponya! amepata kufufua! amepata kutenda miujiza mingi sana! Tazama wakati wa Mussa na Firauni pata picha...

Well, I guess you are not trying to prove kwamba shetani ana nguvu kushinda Mungu! Labda twende na hypothesis kwamba babu ametumwa na shetani (kama unavyoashiria hapa), je, motive ya huyo shetani kuwaponya (kama kweli wanaponna) ni nini?

... (nami simhukumu babu) ila kuna mambo mengi ya kujiuliza hapo! Je ni Mungu huyuhuyu Muumba au ni ile miungu ya mababu zetu? kwa sababu Samunge!? miundo mbinu mibaya, watu wanapata shida... unakwenda kupona kisukari unakufa kwa homa ya matumbo na kipindupindu au Mungu huyo anahitaji WAHANGA?

Why do we doubt God? Hivi kifo ni kazi ya Mungu ama ya shetani? Kama watu wanakufa in maana Mungu ameshindwa kazi yake au hayupo fair au uwepo wake is simply a myth?

Kwa uzoefuu wangu watu tangia enzi hizo wanakufa, hata sasa wanakufa na wataendelea kufa whether kuna tiba ya ukimwi/kisukari ama la pamoja na kuwepo kwa Mungu kwa kipindi chote hicho. Lakini hili halina maana Mungu hatendi kazi yake.
 
Unataka na yeye aseme AMEOTESHWA NA MUNGU!?

Tumepewa AKILI, ili TUFIKIRI na KUAMUA...

Tumepewa MACHO ili KUONA....

Tumeumbiwa JUA ili LIMULIKE...

Tumepewa MAAMUZI, ili TUCHAGUE...

KUMSHUKURU MUUMBA ama KUMKUFURU.. basi!

Unataka na yeye aseme AMEOTESHWA NA MUNGU! = Kwa nini anadhani yeye (Judith) ni wa kuaminika zaidi kuliko wengine??

Tumepewa AKILI, ili TUFIKIRI na KUAMUA...= Waendao Loliondo wamefikiri na kuamua, shida iko wapii??

Tumepewa MACHO ili KUONA....= Kizuri kwako haimaanishi kitakuwa kizuri kwangu na kinyume chake ni sahihi, ingawa wote tuna macho.

Tumeumbiwa JUA ili LIMULIKE...= Na nyota ziangaze usiku, kwa hiyo hata ktk giza (shida, maradhi, uovu n.k) Mungu hutupa nuru.

Tumepewa MAAMUZI, ili TUCHAGUE...= Iweje mwenzio akiamua wewe uone kakosea wakati power ya maamuzi na kuchagua ni yake na matunda ya maamuzi/uchaguzi iwe mazuri/mabaya ni yake pia??

KUMSHUKURU MUUMBA ama KUMKUFURU...= Angalau mpaka sasa hakuna (kwa walioenda Loliondo) aliyesikika hadharani akimkufuru Mungu
 
Miss Juddy..... kuangamia unamaanisha nini? Hao wanaopona wameangamia?

Miss Juddy....kikosa maarifa mana yake nini? Unahisi wewe una maarifa kuliko watu wote wale wanaopiga foleni kwenda kwa babu na hawa unaobishana nao kwa hoja hapa JF?

Miss Juddy.............mshukuru Mungu kwa kuwa una afya njema na wala huna ndugu unayemuuguza kwa magonjwa haya anayoyatibu babu.......tema mate chini yasikutokee kwa sababu utajikuta uko kwenye foleni Loliondo, bila kujua umefikaje pale.....Mungu apitishe mbali.
Hommie na wewe umeingia kwenye mtego wa huyu Miss? wala usijisumbue kutoa busara zako maana yeye amaeshakiamua kile akitakacho kwa hiyo useme usemavyo hata kusikia kamwe na atandelea kupiga kelele as if yeye ndo nabii wa kweli. lol
 
Unataka na yeye aseme AMEOTESHWA NA MUNGU! = Kwa nini anadhani yeye (Judith) ni wa kuaminika zaidi kuliko wengine??

Tumepewa AKILI, ili TUFIKIRI na KUAMUA...= Waendao Loliondo wamefikiri na kuamua, shida iko wapii??

Tumepewa MACHO ili KUONA....= Kizuri kwako haimaanishi kitakuwa kizuri kwangu na kinyume chake ni sahihi, ingawa wote tuna macho.

Tumeumbiwa JUA ili LIMULIKE...= Na nyota ziangaze usiku, kwa hiyo hata ktk giza (shida, maradhi, uovu n.k) Mungu hutupa nuru.

Tumepewa MAAMUZI, ili TUCHAGUE...= Iweje mwenzio akiamua wewe uone kakosea wakati power ya maamuzi na kuchagua ni yake na matunda ya maamuzi/uchaguzi iwe mazuri/mabaya ni yake pia??

KUMSHUKURU MUUMBA ama KUMKUFURU...= Angalau mpaka sasa hakuna (kwa walioenda Loliondo) aliyesikika hadharani akimkufuru Mungu
hahahaha you have nailed it down. Kudos!!
 
Back
Top Bottom