Kikosi bora cha timu ya Mpira wa Miguu cha England kuwahi kutokea

England ya 90, itabakia kua bora kuliko zote. Ila Nakubali Shearer na Sheringham na Mcmanaman vipaji vao vikubwa.
Sheringham alikua Class ya aina yake very joyful kumtizama. Best England No 10.
90 ipi unazungumzia? 1990 au 1996? Kwangu mimi three lions ya 1990 ndio bora ingawa haikubeba taji lolote.

Baadhi ya wachezaji walikuwa

Peter Shilton, Poul Parker, Terry Butcher,Garry Liniker aliyeendesha juzi draw ya kombe la dunia mwakani kule Russia. Peter Berdslay, Chriss Waddle, John Burnes, David Platt Poul Gascogne na wengine.

Kwenye makundi walikuwa hivi

England
Holland
Ireland
Egpty.
Baada ya makundi walikutana kwenye mtoano na Cameroon ya Rodger Milla. Nusu fainali wakatandikwa na iliyokuwa Ujerumani Magharibi na kutupwa nje ya mashindano ambapo walikuja kuchapwa na wenyeji italia kwenye kumtafuta mshindi wa 3 na 4.

Hiko ndio kikosi bora kwangu.

Nakumbuka hizi game nilikuwa nikiangalia pale ccp nikiwa bado mtoto nikiongozana na baba yangu R.I.P Ndani ya land rover 109.
 
Afadhali wewe ulishuhudia live.
Naomba unifahamishe hivi ni kweli kuwa Cameroon walionewa na mwamuzi mpaka kutolewa na England?
Ni kweli kulikuwa na figisu. Mwamuzi alitoa penalt 3. 1 kwa cameroon na mbili kwa england. Kumbuka england walianza kufunga , cameron wakasawazisha na kuongeza. Mpaka dk ya 80 waingereza walikuwa nyuma kwa 2-1. Dk 1o za mwisho england wakapewa penalt mbili tena dhahiri shahiri zikiwa soft sana. Lineker akafunga zote na mpira kwisha kwa 3-2. England akisonga mbele
 
Hayupo hapo kilele chake mwaka wa 90 na Cameroon hata mwaka wa 92 penye euro umri ulikuwa umesogea alikuwa na 31 waqt wa mashindano ya ulaya.Umemjibu vyema kabisa mzee mwenzangu.
Gary Lineker nae ana rekodi za upekee, Ni miongoni mwa wachezaji wachache sana ambao hawajawahi kupewa Kadi ya njano wala Nyekundu.

Alikuwa na nidhamu ya aina yake sana!
 
Wakongwe kama wewe mnahitajika sana hapa jukwaani kuwapa darsa hawa vijana walioanza kufatilia mpira Euro 2008
 
Dhuluma siku zote haifai, England ikaenda kukutana na Germany kwenye semi final, Gazza akamwaga chozi baada ya kupata kadi ya njano ambayo ingemfanya akose Fainali kama England wangeshinda. Wakatolewa na Mjerumani...
 
Acheni mambo yenu ya kiafrica ayo. Wapi Cameroon walionewa? Au kwakua zimotolewa penalti ndo wameonewa? Waafrica mtihani kweli.
Katafute mechi utizame au japo highlight kwenye youtube uhakikishe. Mtu kalamba buti kafyeka asa ndani ya boksi alafu kaonewa?
 
Ya 1990 iliokua inafundishwa na Sir Bobby Robson, Peter Berdslay, Chriss Waddle, Poul Gascogne walikua wanaburudisha asa. Garry Liniker nae striker ya ukweli alikua.
 
K
Yaah king Kenny alikuwa mkufunzi pale khalafu nadhani pana mchezaji alikuja pale Darren peack baadae 1998 alikuwa anafunga kishungi kama Petit. Pia mjumuishe David batty


Yes King Kevin Daglish was great coach at that time. he is actually of one of top 10 greatest player to come from Britain.
 
Kumbe ndiyo maana na wao England 2010 South Africa kwa Madiba goli la Lampard lilikataliwa Kumbe ilikuwa inajilipa.
 
Hivi walifanya nini cha maana?ungeweka cha 1966 ningekuelewa,baada ya hapo waingereza ni wale wale,toka Allan Shearer,Michael Owen,Berkham,Wilshear,Walcot,Andy Caro na hata Rashford.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…