Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kikiwa ndani ya ndege maalumu ya kukodi kuelekea nchi ya Cape Verde kusaka tiketi ya kufuzu michuano ya mataifa ya Afrika AFCON 2019.
Awali Taifa stars ilikuwa wasafiri na ndege ya Air Tanzania Boeing 787-8 Dreamliner, lakini imeshindikana baada ya kubaini kuwa uwanja wa ndege wa Cape Verde hupokei ndege kubwa kama Dreamliner.
Kiwanja cha ndege Praia ni kidogo njia yake ina urefu wa KM 2.1 Dreamliner inahitaji kiwanja chenye urefu si chini ya KM 3 iweze kutua na kuruka.
Kipo kisiwa cha Sal Cape Verde ndio chenye kiwanja kirefu ambapo Dreamliner ingetua, kutoka Sal kwenda Praia ni mwendo wa dakika 45 ambazo zingeweza kuathiri performance ya timu ya Taifa na usumbufu.
Katika michuano hiyo ya mataifa ya Afrika, Taifa Stars inakwaruza na Cape Verde siku ya Ijumaa Oktoba 12, 2018 na itarudiana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Oktoba 16, siku nne baadaye.
Awali Taifa stars ilikuwa wasafiri na ndege ya Air Tanzania Boeing 787-8 Dreamliner, lakini imeshindikana baada ya kubaini kuwa uwanja wa ndege wa Cape Verde hupokei ndege kubwa kama Dreamliner.
Kiwanja cha ndege Praia ni kidogo njia yake ina urefu wa KM 2.1 Dreamliner inahitaji kiwanja chenye urefu si chini ya KM 3 iweze kutua na kuruka.
Kipo kisiwa cha Sal Cape Verde ndio chenye kiwanja kirefu ambapo Dreamliner ingetua, kutoka Sal kwenda Praia ni mwendo wa dakika 45 ambazo zingeweza kuathiri performance ya timu ya Taifa na usumbufu.
Katika michuano hiyo ya mataifa ya Afrika, Taifa Stars inakwaruza na Cape Verde siku ya Ijumaa Oktoba 12, 2018 na itarudiana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Oktoba 16, siku nne baadaye.