Kikosi cha wachezaji 25 wa Simba SC kinachosafiri kuelekea Sudan kuwakabili Al Merreikh

Kikosi cha wachezaji 25 wa Simba SC kinachosafiri kuelekea Sudan kuwakabili Al Merreikh

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Kikosi cha wachezaji 25 cha Mabingwa wa Nchi na Wawakilishi wa TANZANIA Mnyama Mkali, Simba SC, ambao wanasafiri leo Jumatano saa 10:45 Alasiri Machi 3, 2021 kuelekea nchini Khartoum Sudan, kupitia Addis Ababa Ethiopia, kuwakabili Al Merreikh kwenye mchezo wa kundi A wa Klabu Bingwa Afrika ambao utapigwa siku ya Jumamosi ya Machi 6, 2021

Wachezaji wanne wa Simba SC ambao hawakujumuishwa kwenye msafara wa kikosi cha timu hiyo ni;

1.Bernard Morrison
2.Said Ndemla
3.Ibrahim Ame.
4.Junior Lokosa


FB_IMG_1614759876229.jpg


========

Kikosi cha Mabingwa wa Nchi Mnyama Simba SC, kimefika tayari uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya kwenda Khartoum Sudan kupitia Addis Ababa Ethiopia.
 
Msaada;
Hivi huyo uliyemuweka namba 22 mbona sijawahi kumuona akicheza hata kwenye benchi simuonagi ama ni mtunza vifaa wetu Na vipi mzee wa kuchetua mbona hayupo au umekosea mkuu
 
Msaada;
Hivi huyo uliyemuweka namba 22 mbona sijawahi kumuona akicheza hata kwenye benchi simuonagi ama ni mtunza vifaa wetu Na vipi mzee wa kuchetua mbona hayupo au umekosea mkuu
Kocha Gomes amesema;

"Peter Muduhwa ni mchezaji mzuri sana, anatupa kitu bora sana mazoezini, lakini bahati mbaya ana leseni ya kucheza Klabu Bingwa.

Huwa naongea naye ili kumsaidia kumpa kujiamini zaidi, tayari kama benchi la ufundi tunaamini juu ya uwezo wake, na tunaamini hazina kubwa na muhimu ndani ya klabu".


Kuhusu Morrison kwangu kama Ghazwat Kocha anangalia vitu vingi katika Selection yake, kubwa ni utimamu wa mwili kwa mchezaji
 
Hivi wachezaji wale ambao hawapo kwenye benchi siku husika ya match wanakuwaga wapi wakati wa mchezo?
Jukwaani??
Au wanakuwa kambini wakifatilia match kwenye ndani katika mwenye tv?
 
Hivi wachezaji wale ambao hawapo kwenye benchi siku husika ya match wanakuwaga wapi wakati wa mchezo?
Jukwaani??
Au wanakuwa kambini wakifatilia match kwenye ndani katika mwenye tv?
Naongezea swali pia, hivi jezi wanabadilisha mpya kila mechi? Na baada ya mechi zinaenda wapi?
 
Naongezea swali pia, hivi jezi wanabadilisha mpya kila mechi? Na baada ya mechi zinaenda wapi?
Na Mimi naongeza swali!
Baada ya pre match warm ups huwa wanaoga kabla ya kuvaa jersey na kuingia uwanjani?
 
waende na spirit ilele ile ya "teamwork", conference, wapambane kufa au kupona. lazima watatoka na ushindi wa zaidi ya goli 2.
 
Back
Top Bottom