Kikuyus, Kalenjins to be barred from presidency for 30 years in proposed Bill

Kikuyus, Kalenjins to be barred from presidency for 30 years in proposed Bill

Tatizo eliakeem umekaririshwa mambo ya vijiweni hadi unaimba kama wimbo wa taifa, safiri utoke nje ya hicho kitaa cha uswazi uweze kuelewa na kuijua dunia.
Binafsi nimesafiri sana, ukienda kwa makabila yote, ya hapa Kenya na hata ya huko Bongo, humo ndani ya kila kabila kuna aina ya hao watu wawili, walionacho na walalahoi. Ukienda Ukikuyuni kule ndani, utakuta kuna maskini na pia utakuta wenye hela, vile vile hata kule kwa Wajaluo. Na hata hapo Bongo, tumeaminishwa kwamba Wachagga ndio wenye mali Tanzania, lakini utakuta kuna baadhi yao maskini pia.

Hakuna kabila ambalo linaweza kumiliki serikali, mimi binafsi ni Mkikuyu lakini kila siku nahangaika kwenye mishe zangu, hamna siku imetokea tangazo kwamba Wakikuyu wote tuweke foleni kwa mabenki tupate mgao wa serikali. Nimekutana na Wakikuyu na Wakisii huko Bongo wananiwiri kibiashara, wameenda hadi Malawi na Msumbiji, Rwanda, Burundi, wamevuka hadi Botswana na wanakwepa mabomu Somalia, sasa huko ina maana serikali za hizo nchi zinawasaidia ama vipi.

Ukikaa kama mjinga unawaza eti wenzio wanafaulu maana kuna usaidizi wa kiaina, utakufa ukiwa maskini hadi kuzimu. Nimeona mnafungua humu JF mada kadhaa kwamba waislamu Bongo huwa wanaonewa, kwamba hawapewi nafasi sawa na Watanzania wa dini nyingine. Huo ni uvivu na umbumbumbu wa kiaina, nyanyuka hapo ulipo, piga kazi hadi kieleweke.

Rais Uhuru leo akitaka kuteua, watapigiana simu huko juu kama wanavyojuana wenyewe, hatokuja kunitafuta kitaa kisa mimi ni Mkikuyu. Juzi rais Museveni ameteua mkewe kuwa waziri, tayari amemweka mwanaye katika mkao wa kumrithi.

Huko huko rais wenu Magufuli amewaita vila.za nyie msiokua na elimu, lakini akasahau kwamba na mwanaye Jesi yuko humo kati yenu kwenye level yenu ya elimu, niliona mumeweka bandiko na kumuanika huyo Jesi na kuhoji alifika vipi chuo kikuu. Lakini mwisho wa siku mtaishia kupiga makelele hatimaye mlale maana huyo Jesi yupo kwa kabila la walionacho wakati nyie vila.za wa kawaida mpo kwenye kabila la walalahoi na mtatukanwa kuwa malo.fa na wapumbavu siku zote.

Mkuu umeongea sahihi kabisa,Dunia hii ina makabila 2 tu,walionacho na walalahoi,,hayo makabila mengine ni majina tu!
 
Soma nilichokisema mara kumi halafu uje upya.
Haina haja ya kusoma those empty words of yours,
Nimesoma comments zako nimeona jinsi mkikuyu umetokwa povu..
and that's nothing but a naked truth!
Halafu huwa unanifurahisha vile ukibanwa unakimbilia kwenye mambo ya Tz,
 
Back
Top Bottom