Kikwete Alipata Wapi Madaraka ya Kuanzisha Mchakato wa Kuandika Katiba Mpya ya JMT?

Kikwete Alipata Wapi Madaraka ya Kuanzisha Mchakato wa Kuandika Katiba Mpya ya JMT?

Hautaki wewe ni nani kwani kuna mtu amekulazimisha kuukubali.

Ritz stop monopolizing other member! Ana haki ya kuandika anachoamini, acha kudharau maoni yake kwani amequalify kuwa na maamuzi.

Heshimu maoni ya wengine
 
Last edited by a moderator:
Yaani akiwa "Rais" basi ana madaraka ya kufanya lolote lile hata kama linakiuka Katiba aliyoapa kuilinda, kuitetea na kuihifadhi?

Ungeyasema haya wakati wa nyenyere!?

Kama hukukatwa maskio bila ganzi! Na huyu kikwete kawa mpole mno mpaka wakulima kama wewe wanajaribu kumkosoa kosoa kama mwanao!
Mtu kama wewe unatakiwa ucharazwe viboko hadharani kwa kumkosea adabu RAIS WA NCHI! ili iwe mfano kwa wale nyau wengine!
 
Ibara ya 98 inasemaje kuhusiana na kuandika upya Katiba? siyo kufanyia marekebisho vipengele tu vya katiba ya sasa bali kuifuta ya sasa na kuleta Katiba Mpya Ibara hiyo inasemaje?
Inazungumzia kuhusu kufanya "marekebisho" lakini pia kufanya "mabadiliko". Ibara ndogo ya pili inatoa ufafanuzi (definition) kuhusu mabadiliko:

Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa masharti ya ibara ndogo ya (1), kubadilisha masharti ya Katiba hii au masharti ya Sheria maana yake ifahamike kuwa ni pamoja na kurekebisha au kusahihisha masharti hayo au kufuta na kuweka masharti mengine badala yake au kusisitiza au kubadilisha matumizi ya masharti hayo.

Rais na bunge wanapata mamlaka yao chini ya ibara ndogo ya 1 (ya ibara hiyo ya 98) ambayo imetumika kupata "Sheria ya Mabadiliko ya Katiba" (Sura ya 83):

Bunge laweza kutunga Sheria kwa ajili ya kubadilisha masharti yoyote ya Katiba hii kwa kufuata Kanuni zifuatazo:-

Tafsiri yangu ni kuwa, ibara ya 98 haijaweka ukomo wa kiwango cha mabadiliko (maana inasema "yoyote"), hivyo masharti yote (au kwa kiwango kikubwa) ya katiba yanaweza kufanyiwa mabadiliko (ikiwa ni pamoja na kufuta masharti yote ya katiba ya sasa na kuweka masharti mengine badala yake) kwa mara moja na hivyo kimantiki kupata katiba "mpya".

Kwa hivyo kisheria, mchakato uliopo ni wa "mabadiliko ya katiba". Sasa kama mabadiliko hayo yatatuletea "katiba mpya" (kwa maana ya kufuta masharti mengi na kuweka mengine mapya) hilo ni suala la wenye nchi kuamua.

Nadhani kumekuwa na matarajio ya mchakato huu wa mabadiliko ya katiba kubadilisha masharti mengi ya katiba ya sasa kwa sababu moja ama nyingine. Naamini ni kutokana na matarajio hayo, ndio maana mchakato huu kwa haki kabisa unaonekana ni wa kupata "katiba mpya". Nadhani ndio sababu hata dira ya tume ni "kufanikisha kupata katiba mpya".

EMT , ningependa kusikia kutoka kwako kuhusu hoja ya mchakato wa katiba mpya/mabadiliko ya katiba kukosa uhalali wa kikatiba
 
Smu kama unaamini madaraka yao yanatoka ibara ya 98 je utaratibu wa kubadili kayiba uliopo kwenye ibara hii unefuatwa?
 
  • Thanks
Reactions: SMU
EMT , ningependa kusikia kutoka kwako kuhusu hoja ya mchakato wa katiba mpya/mabadiliko ya katiba kukosa uhalali wa kikatiba

Katiba nyingine ni ngumu kuzibadilisha au kuzifuta kabisa kwa kutengeneza katiba mpya. Katiba nyingi hazisemi chochote kuhusiana na mchakato wa kutengeneza katiba nyingine. Nyingi zinaghusia tuu kufanya marekebisho ya hapa na pale. Kwenye katiba nyingine mazingira yanaweza ku-dictate kufanyanika kwa marekebisho ya lazima au kutengenezwa kwa katiba mpya kabisa.

Baadhi ya mifano ambayo inaleta ugumu kubadilisha katiba ni Australia ambapo katiba ya sasa inataka kuwepo kwa referendum ambapo zaidi ya nusu ya Waustralia katika kila jimbo lazima wapige kura ya ndiyo ili kubadilisha katiba. Pili, bado kuna doubts kama mamlaka iliyopewa bunge na katiba kufanya mabadiliko kwenye katiba yanajumuisha pia kufanya mabadiliko ambayo ni radical au kutengeneza katiba na kufuta iliyopo. Mfano, ni hiyo Ibara ya 98 ya katiba ya sasa.

Tatu, mwaka 1990, Bunge chini ya serikali ya kibaguzi ya Afrika ya Kusini ilikuwa na mamlaka ya kubadilisha katiba, lakini weusi walikuwa hawaruhusiwi kupiga kura au hakuwa na wawakilishi kwenye bunge hilo. Nne, Nepal huwa inatumika sana kama mfano wa kutengeneza katiba mpya. Katiba yao ya mwaka 1990 ingeweza kubadilishwa tuu na sehemu mbili za bunge na kutiwa saini na King. Hata hivyo baada ya mwaka 2006 hakuna aliyetaka kumhusisha King katika kubadilisha katiba.

Kwa hapo kwetu, mchakato wa katiba mpya umekuja from nowhere. Katiba mpya haikuwa hata kwenye ilani ya chama tawala. Hata hivyo, kubwa zaidi hapa ni kuhusu hiyo Ibara ya 98 ya katiba na suala ni kama kweli ndiyo legal basis ya mchakato wa katiba mpya unaondelea hivi sasa. Umetumia version ya Kiswahili. Nitatumia version ya Kiingereza, with emphasis kwenye bold.

Heading ya kifungu hicho inasema "Procedure for altering the Constitution and certain laws."

98.-(1) Parliament may enact law for altering any provision of this Constitution in accordance with the following principles:

(a) a Bill for an Act to alter any provisions of this Constitution, other than those relating to paragraph (b) of this sub-article or any provisions of any law specified in List One of the Second Schedule to this Constitution shall be supported by the votes of not less than two thirds of all the Members of Parliament; and

(b) a Bill for an Act to alter any provisions of this Constitution or any provisions of any law relating to any of the matters specified in List 56 Two of the Second Schedule to this Constitution shall be passed only if it is supported by the votes of not less than two-thirds of all Members of Parliament from Mainland Tanzania and not less than two-thirds of all Members of Parliament from Tanzania Zanzibar.

(2) For the purpose of construing the provisions of sub-article (1), alteration of provisions of this Constitution or the provisions of a law shall be understood to include modification, or correction of those provisions or repeal and replacement of those provisions or the re-enactment or modification of the application of the provisions.

Ibara hiyo inaongelea zaidi kwenye alteration ya kifungu chochote cha katiba hiyo. Ibara haingelei juu ya ku-repeal katiba hiyo au kutengeneza katiba mpya kabisa. Katiba haijasema lolote kuhusiana na mchakato wa katiba mpya. Naweza kusema kuwa it is silient on this issue. Pia sidhani kama the Constitutional Review Act imefanya reference kwenye Ibaya 98. Hivyo, nafikiri kuna tofauti kati ya ku-alter vifungu vya katiba hiyo na ku-replace au ku-repeal katiba yote kwa ujumla.

Kwa mfano, tofautisha na katiba ya Kenya ambapo Ibara ya 155(1)(a) inasema kuwa "A proposed amendment to this Constitution shall be enacted in accordance with Article 256 or 257, and approved in accordance with clause (2) by a referendum, if the amendment relates to... (a) the supremacy of this Constitution. Tofauti na Ibara ya 98, Ibara hii ya 155(1)(a) inaongelea mabadiliko juu ya supremacy ya katiba nzima kwa ujumla.

Hata hivyo, kwanza kabisa basis ya mchakato wa katiba mpya inaweza kuwepo siyo tuu kwenye kwenye katiba, bali pia kwenye vifungu vingine vya sheria. Hivyo katika kutafuta legal basis ya mchakato unaondelea wa katiba mpya ni vizuri zaidi kuangalia vifungu vingi vya sheria kama ilivyofanyika Nepal.

In deed, katiba yetu huwa inatumika, subject to other provisions of the law. Pia "Ifahamike kwamba masharti yaliyomo katika Sehemu hii ya Katiba hii, yanayofafanua misingi ya haki, uhuru na wajibu wa binadamu, hayaharamishi sheria yoyote iliyotungwa wala kuzuia sheria yoyote kutungwa au jambo lolote halali kufanywa kwa mujibu wa sheria hiyo, kwa ajili ya kuwezesha jambo jingine lolote kufanyika ambalo linastawisha au kuhifadhi maslahi ya taifa kwa jumla." Mchakato wa katiba mpya hauwezi kuwa jambo lolote ambalo linastawisha au kuhifadhi maslahi ya taifa kwa jumla?

Pili, machakato wa katiba mpya unaweza kuwepo kwa kutumia njia nyingine zilizopo hata kama zitakuwa kinyume na maslahi ya wanaotakiwa kuchukua hatua muafaka inayotetea maslahi ya wananchi wote kama ilivyokuwa Afrika Kusini. Suala la katiba mpya halikuletwa na serikali iliyo madarakani bali kupitia vyama vya upinzani. Tatu ni kukubali kuwa katiba yetu ya sasa ni mbovu sana kiasi kwamba haisemi hata jinsi ya kuifuta kwa kutengeneza katiba mpya.

Nne, ni kuendesha mchakato wa katiba mpya nje ya katiba ya sasa. Provided that the people have decided to make a new constitution, it is in itself a basis for a new constitution. If the will of the people is to have a new constitution, then that will be the basis for the new constitution. Maana katiba ingeweza kusema wazi kuwa hakuna mtu yoyote mwenye mamlaka ya kuifuta na kutengeneza katiba mpya, na hapo kusingekuwa na legal basis ya kuifuta, even if the will of the people demands so.

Baada ya kusema hayo yote, nadhani sehemu muhimu sana kwenye utengenezaji wa katiba mpya siyo kwenye application ya mchakato bali jinsi mchakato mzima unavyokuwa designed. Rais Kikwete alipotangaza mchakato wa katiba mpya watu wengi walifurahi sana. Kwa wengi it was the moment of greatest optimism. Vyama vya upinzani vilikubali kufanya concessions nyingi tuu. Watu waliipa jukumu Tume iliyoteuliwa na Rais kuendesha mchakato huo. Lakini wengi hawakuangalia kabisa design ya mchakato mzima. Ndiyo maana mpaka sasa kuna malalamiko mengi kutoka pande mabalimbali.

Tokea mwanzo nimepinga design ya mchakato mzima wa katiba mpya. We, the people of the United Republic of Tanzania, had two options in the making of the new Constitution. The first option, which is already in the pipeline, was that at the non-democratic extreme of the spectrum, we could have a sovereign lawgiver or intermediaries laying down the new constitution for all future generations. The second option, which many Tanzanians have never thought of it, was that at the democratic extreme, we could have a Constituent Assembly elected by universal suffrage for the sole task of writing the new constitution.
 
EMT , asante kwa mchango wako. Sina uhakika ni kwa nini umeamua kutumia version ya kiingereza badala ya ile ya kiswahili (naamini katiba imeandikwa kwa kiswahili na hiyo version ya kiingereza ni translation tu na hivyo ukitokea utata, tafsiri ya version ya kiswahili ina prevail).

Mimi naamini ilikuwa sawa kwa katiba ya sasa kutokuweka detailed process ya kupata katiba mpya (au kubadili) na badala yake kuacha mchakato huo uamuliwe na kizazi/wakati husika kwa kuweka mwanya kutunga sheria ya mabadiliko inyokidhi mahitaji ya kizazi na wakati husika. Kama nilivyosema hapo juu ibara ndogo ya pili haijaweka ukomo wa kiwango cha mabadiliko hivyo vifungu (masharti) vyote vya katiba vinaweza kufutwa na kuwekwa vingine badala yake.

Nimependa wazo la kuwa uhalali wa mabadliko ya katiba unatokana na wananchi....kama wananchi wameamua (kupitia bunge??) kufanya mabadiliko ili kupata katiba mya yenyewe peke yake inatosha kuwa msingi wa mabadiliko hayo.
Mzee Mwanakijiji , so far naamini utaratibu umefuatwa kwa maana ya kwanza kutunga sheria ya mabadiliko ya katiba (ibara ndogo ya kwanza ya ibara ya 98) na chini ya sheria hiyo mambo mengine yote yanaendelea.

EMT hapo juu ametoa hoja kuwa "Provided that the people have decided to make a new constitution, it is in itself a basis for a new constitution. If the will of the people is to have a new constitution, then that will be the basis for the new constitution." Unaionaje hoja hii?
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: EMT
SMU unaposema "Utaratibu umefuatwa" una maana gani? Sijasikia Bungeni umeletwa mswada wa kubadilisha kipengele chochote cha Katiba hii. Mara ya mwisho Katoba kubadilishwa kwa "utaratibu" wa ibara ya 98 ilikuwa ni 2005. Ni lini bunge limepiga kura ya 2/3 kubadilisha Katiba?
 
Hili ni swali ambalo jibu lake liko wazi; kuwa Rais Kikwete hakuwa na madaraka hayo. Hata hivyo, wapo wanaoamini kuwa kwa vile Rais kaamua kufanya kitu basi kitu hicho ni halali.

Mimi na baadhi yetu tumekataa kuutambua mchakato huu wa Katiba Mpya kwa sababu ni haramu; haukuanzishwa na chommbo halali na hata hivi sasa matatizo tunayoyaona na yatakayotokea mbeleni (kwenye Bunge la Katiba na Kura ya Maoni) itakuwa ni mwendelezo tu wa kosa hili kubwa.

HUU NI MCHAKATO HARAMU. Sikiliza HOJA MARIDHAWA

[JFMP3]https://www.jamiiforums.com/attachment.php?attachmentid=115504&stc=1&d=1381127129[/JFMP3]



hivi wee unaishi nchi gani duh kweli umekosa cha kuandika.ulikuwa wapi mpaka mchakato umefikia hapa ulipo.ujui yaliyotokea mpaka mchakato ukaanza .mzee umekurupuka wajiabisha bure.
 
hivi wee unaishi nchi gani duh kweli umekosa cha kuandika.ulikuwa wapi mpaka mchakato umefikia hapa ulipo.ujui yaliyotokea mpaka mchakato ukaanza .mzee umekurupuka wajiabisha bure.

sasa kwenye kichwa chako unaamini kitu kikikosewa basi kimekosewa watu wasijisahihishe?
 
sasa kwenye kichwa chako unaamini kitu kikikosewa basi kimekosewa watu wasijisahihishe?

Uko sawa kabisa! Ingawa sijuwi maoni yako, tufanyeje?!!

Binafsi napenda katiba mpya, japokuwa hadi sasa ilipofikia ina mapungufu na nina hofu ya kuwa na katiba mpya mbovu... CCM wabunge wanaharibu...
 
Ulikuwa ni mchakato haramu ule wa mwanzo; tutarudia makosa yale yale?
 
Ritz stop monopolizing other member! Ana haki ya kuandika anachoamini, acha kudharau maoni yake kwani amequalify kuwa na maamuzi.

Heshimu maoni ya wengine
Sijadharau nimetumia pia uhuru wangu kueleza nilichokiona.
 
Back
Top Bottom