Elections 2010 Kikwete kukutana na wanahabari

Bado Niponipo

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2008
Posts
680
Reaction score
168
JK anatarajiwa kukutana na waandishi wa habari, katika ukumbi wa Arnatoglo-ilala, siku ya ijumaa, waandishi hao watapata mwaliko maalumu na watakuwa waandishi wa digital media i.e radio and Tv.

NOTE: Waandishi kupata mwaliko maalumu.
 
Am sure watakuwa very selective yaani I can imagine aina ya maswali watakayomuuliza very pumbafull.
Kazi ipo
Sasa why digital media peke yake,JK mzee wa madesa naona atakuwa bize anaandaa majibu ya maswali ambayo yashaandaliwa
 
Akisahau majibu itakuwaje? Bora wafanye recorded na sio live
 
Habari za kuaminika ni kwamba walishapita kwenye vyombo hivyo kukusanya maswali, Tatizo vyombo vyetu vya habari vinafanyakazi kwa kujikomba hata pale vinapojaribu kuinukia vinaingiwa na woga hebu angalia swala la marudio ya mdahalo, ITV baada ya kufanya vizuri wakatishwa na wao badala ya kugangamala wakayumba sasa ndio wamejimaliza kabisa maana ile heshima waliyojizolea siku ile ya mdahalo wameiua wenyewew.
 
Nilimwona Kinana kuwa jeikei atayajibu maswali yatakayotoka kwa WALIOALIKWA.

Huu ndo uhuni wa kijinga kabisa. mnadhani kuna maswali yatatoka nje ya Kikwete campaign 2010???
mimi nitasoma magazeti kesho yake.

kwa nini tusifanye booking kwa slaa kupata naye airtime such day??? au na sisi tukate umeme???? I am on the way to see Kakobe anipe funguo ya kukata umeme

 
Mie bado nacheka na facebook ya kikwete ambayo ERNESTO SHEKA na wenzake wanaimonita. hebu cheki hapa
 
Naam hiyo ndo my comment of the day, I loved it
 
Kama hizi ndizo akili za wapambe, I can now understand why some people cannot see anything wrong with JK and CCM
 
JK anatarajiwa kukutana na waandishi wa habari, siku ya ijumaa, waandishi hao watapata mwaliko maalumu na watakuwa waandishi wa digital media i.e radio and Tv.

NOTE: Waandishi kupata mwaliko maalumu.

Hapa watakaokuwepo ni wafuatao: Mkumbwa, Maggid, Kibonde, Tido Mhando, Marini H Marini. Usitegemee kumuona Jenerali Ulimwengu, Saed Kubenea, Absaloum Kibanda, Rioba, na wengine wa namna hiyo.
 
jk lazima ataulizwa maswali magumu sana. Mojawapo yatakuwa haya yafuatayo:-

(i) Mhe. rais, serikali yako imejitahidi sana kupambana na mafisadi ikilinganishwa na serikali zingine zilizopita. wananchi tumeshuhudia serikali ikiwafikisha mahakamani watuhumiwa wazitowazito, jambo ambalo ni nadra sana. hongera sana mhe. rais. sasa watanzania wengi wangependa kujua, je, umejipangaje kuendeleza vita hii nzito dhidi ya mafisadi katika awamu yako ya pili ya uongozi.

(ii) Mhe. rais, katika eneo ambalo serikali imeliwekea mkazo ni ukuzaji wa uchumi. wananchi wengi wameshuhudia hali ya maisha ikiboreka japo siyo kwa kasi kubwa sana kutokana na kuyumba kwa uchumi duniani. Sasa, labda wananchi wangependa kupata maelezo yako namna utakavyoongeza kasi ya kukuza uchumi.

(iii) Mhe. rais, baadhi ya wananchi wanasifu sana uungwana wako wa kuwaruhusu watuhumiwa na fedha za EPA kurejesha fedha walizokwapua kwenye akaunti ya madeni ya nje. hongera sana mhe. sasa labda tungependa utufahamishe japo kwa ufupi, fedha hizo zimewanufaishije wakulima wetu.

(iv) Mhe. maeneo mengi uliyotembelea umekuwa ukitoa ahadi nyingi kwa wananchi na sisi kama waandishi wa habari kwa kuzingatia umakini wako tuna imani unaweza kutekeleza zote. lakini baadhi ya wananchi wana mashaka. je, unaweza kutoa maelezo mafupi tu namna utakavyohakikisha ahadi zote, ukiondoa sababu zilizo nje ya uwezo wako.

(v) Mhe. rais kwanza nikupongeze kwa juhudi na bidii zako za kusafiri mara kwa mara nje ya nchi kwenda kuhemea misaada kwa ajili ya wananchi. tunajua ni safari za kuchosha lakini unafanya kutokana na uchungu wa wananchi wako maskini. tungependa utufahamishe faida ulizopata kutokana na safari hizo.

(vi) Mhe. rais kumekuwa na tetesi na malalamiko ya chinichini kwamba wewe ni mdini. vyeo vingi serikalini umejaza waislamu wenzio bila kujali uwezo na inasemekana hata suala la mahakama ya kadhi na nchi yetu kujiunga na oic umeamua kunyamaza lakini umewaahidi waislam wenzio kwamba utaishughulikia kimya kimya. tetesi hizi zimewashtua sana viongozi wa dini zingine hususani wakristo. je, unasemaje kuhusu suala hili.

(vii) Mhe. rais utafiti umeonesha kuwa watanzania wengi bado wanakuunga mkono. lakini baadhi inaonekana wameanza kupata mashaka ya kukuunga mkono. je, hao walio na mashaka unapenda kuwaambia nini ili wasiwe na mashaka.

(viii) Mhe. rais una ujumbe gani unaotaka kuwaeleza watanzania waliojiandikisha kupiga kura
 
Hivi si walisema hana muda huyu????????????????///
 
JK anatarajiwa kukutana na waandishi wa habari, siku ya ijumaa, waandishi hao watapata mwaliko maalumu na watakuwa waandishi wa digital media i.e radio and Tv.

NOTE: Waandishi kupata mwaliko maalumu.

Kwa nini hawawataki wazee wa print media Raia Mwema, MwanaHalisi na Mwananchi Coroporations!!? Lakini hata hawa si digital - wako online!
 
chichiem ni kigeugeu. mwanzoni walisema wapo busy lakini wamepima upepo na kugundua haja ya kufanya kamdahalo ka uongo na ukwli ili kutibu majeraha aliyoacha Dr. Slaa. It is too late, waTZ wameamuza zamaaaaaaaaaaaaani.

Pipoooooooooooooooooooooooooooooooooz..............
 
Kati ya vitu vinaivyoitofautisha prind na digital media kwa hapa kwetu ni inquisitiveness, watu wa print baadhi wanajua kutafuta ukweli kwa kuhoji wakati watu watakaoongea na JK ni watu wanaopenda kupakatwa kama mwl, Ryioba alivyowahi kusema wakati akiwaelezea wanahabari na mfano wa mbwa. Ijumaa hiyo usitegemee kuwaona watu wanaofikiri sawasawa na utakaowana ni hawa Tido, Kibonde, Kulangwa tena wakiwa wamelishwa maswali yenye majibu yake tayari.

Kwangu mimi nahofu kwamba hawa watakaoalikwa hawatakuwa tofauti na wale wazee waliokuwa wakimpigia JK makofi wakati anazuia mgomo wa TUCTA
 
mwanamazingaombwe Shekhe yahaya alishasema kwamba tayari amedhiti hali ya jk kuanguka anguka. ama kweli nchi hii inaongozwa kiaina kwelikweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…