christeve88
JF-Expert Member
- Aug 11, 2018
- 2,841
- 4,531
Yeye alipokuwa namba 1 alichangia nini kuelekea huko anapopatamani! Huyu mzee naye mbona anatuingiza majaribuni! Hata kuitoa hiyo elimu ilipitwa na wakati bure alishindwa ati yakhe😜! Talking is cheap eeh😜!Rais mstaafu wa awamu ya nne Dk Jakaya Mrisho Kikwete ameonya tusipobadilika namna tunavyofundisha watoto wetu basi ajira zote zitatoweka ifikapo mwaka 2050.
My take.
Hii elimu yetu ya kuwafanya chadema washangilie kila baya linaloipata nchi yetu ikiwemo kukamatwa ndege, miradi kukwama , tutashitakiwa MIGA etc bora ifutwe kabisa tuanzishe elimu mpya itakayowafanya chadema wajitambue.
====
Dar es Salaam. Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete amesema kutokana na utoaji hafifu wa elimu nchini kuna hatari ya nusu ya ajira zilizopo kutoweka ifikapo mwaka 2050.
Ameyasema hayo leo Jumanne Mei 18, 2021 wakati akizindua kongamano la elimu linalojadili ufadhili wa elimu lililoandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (Tenmet) jijini Dar es Salaam.
Akieleza utafiti uliofanywa na tume ya kimataifa ya elimu ambayo yeye ni mjumbe, amesema elimu inayotolewa barani Afrika ilitolewa miaka 50 hadi 70 iliyopita kwa nchi zilizoendelea.
"Sisi bado tunatumia chaki, wakati wenzetu wanatumia tablets. Tuliona kuwa kuna watu zaidi ya milioni 263 waliotakiwa kuwa shule lakini hawapo, kati yao milioni 100 wapo Afrika. Kwa waliopo shule wengi hawamalizi shule. Wengi wanaishia njiani. Asilimia 67 wamemaliza shule, asilimia 33 ni idadi kubwa," amesema Kikwete.
Amesema kutokana na utoaji hafifu wa elimu na maendeleo ya teknolojia kuna janga la ukosefu wa ajira linakuja.
"Ifikapo 2050 asilimia 50 ya kazi zitafutika, kwa sababu ya matumizi ya mashine. Kutakuwa na magari yasiyotumia dereva. Unataka usafiri, unaita Uba, unatumia simu yako inakuja inakupeleka sehemu husika labda Ubungo Plaza au Millennium Tower," amesema.
Amesema mbali na ukosefu wa ajira, idadi ya watu barani Afrika itafikia watu bilioni mbili, “kama watu hao hawana ujuzi unafanya nini? Sijui itakuwaje. Kutakuwa na athari kubwa za kiuchumi na kijamii."
Akisisitiza matumizi ya teknolojia, Kikwete ameshauri kuwepo na uwekezaji katika elimu ili vijana wa Afrika wasiwe watazamaji, wawe washiriki wa uchumi.
"Kunatakiwa kuwepo na matumizi ya sayansi na teknolojia katika ufundishaji. Kila shule inatakiwa kuunganishwa na intaneti," amesema.
Huku akitoa mfano wa janga la corona, Kikwete amesema limethibitisha jinsi ukosefu wa teknolojia unavyoathiri ufundishaji.
"Tumeona wakati wa corona, moja hatua zilizochukuliwa ni kufunga shule. Wanafunzi wetu hawakusoma, wanacheza rede, lakini nchi zilizoendelea shule zilifungwa na watoto wakaendelea kusoma.”
"Nilipokuwa Rais tulianzisha matumizi ya intaneti katika ufundishaji, tuliwekeza sana kwenye mkongo wa Taifa. Lengo langu lilikuwa ni kuhakikisha kila shule, hospitali ziunganishwe na intaneti. Mwalimu mmoja wa hisabati afundishe nchi nzima,” amesema.
Kuhusu Elimu jumuishi ameitaka Serikali na wadau kuhakikisha hakuna mtoto anayebaki nyuma kwa kukosa elimu.
"Wengine wanadhani msichana ni wa kubaki jikoni. Wengine wameachwa nyuma kutokana sababu za kisiasa.
Tunatakiwa kuhusisha mashirika yasiyo ya kiserikali kuchangia elimu," amesema.
Awali akimkaribisha Kikwete mwenyekiti wa Tenmet, Dk John Kalage ambaye pia ni mkurugenzi wa taasisi ya HaliElimu amesema kongamano hilo litajadili kwa kina njia za ufadhili wa elimu nchini.
Chanzo: Mwananchi
Sina uhakika kama hoja yake ipo sawa. Ukienda Mlimani city japo kuna automated machines za car park bado utakuta kuna mtu ameajiriwa kubonyeza machine kutoa card na mwingine kutoa change kwenye machine ya kulipia. Huku Tanzania tunafanya vitu tofauti kidogo.Rais mstaafu wa awamu ya nne Dk Jakaya Mrisho Kikwete ameonya tusipobadilika namna tunavyofundisha watoto wetu basi ajira zote zitatoweka ifikapo mwaka 2050.
My take.
Hii elimu yetu ya kuwafanya chadema washangilie kila baya linaloipata nchi yetu ikiwemo kukamatwa ndege, miradi kukwama , tutashitakiwa MIGA etc bora ifutwe kabisa tuanzishe elimu mpya itakayowafanya chadema wajitambue.
====
Dar es Salaam. Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete amesema kutokana na utoaji hafifu wa elimu nchini kuna hatari ya nusu ya ajira zilizopo kutoweka ifikapo mwaka 2050.
Ameyasema hayo leo Jumanne Mei 18, 2021 wakati akizindua kongamano la elimu linalojadili ufadhili wa elimu lililoandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (Tenmet) jijini Dar es Salaam.
Akieleza utafiti uliofanywa na tume ya kimataifa ya elimu ambayo yeye ni mjumbe, amesema elimu inayotolewa barani Afrika ilitolewa miaka 50 hadi 70 iliyopita kwa nchi zilizoendelea.
"Sisi bado tunatumia chaki, wakati wenzetu wanatumia tablets. Tuliona kuwa kuna watu zaidi ya milioni 263 waliotakiwa kuwa shule lakini hawapo, kati yao milioni 100 wapo Afrika. Kwa waliopo shule wengi hawamalizi shule. Wengi wanaishia njiani. Asilimia 67 wamemaliza shule, asilimia 33 ni idadi kubwa," amesema Kikwete.
Amesema kutokana na utoaji hafifu wa elimu na maendeleo ya teknolojia kuna janga la ukosefu wa ajira linakuja.
"Ifikapo 2050 asilimia 50 ya kazi zitafutika, kwa sababu ya matumizi ya mashine. Kutakuwa na magari yasiyotumia dereva. Unataka usafiri, unaita Uba, unatumia simu yako inakuja inakupeleka sehemu husika labda Ubungo Plaza au Millennium Tower," amesema.
Amesema mbali na ukosefu wa ajira, idadi ya watu barani Afrika itafikia watu bilioni mbili, “kama watu hao hawana ujuzi unafanya nini? Sijui itakuwaje. Kutakuwa na athari kubwa za kiuchumi na kijamii."
Akisisitiza matumizi ya teknolojia, Kikwete ameshauri kuwepo na uwekezaji katika elimu ili vijana wa Afrika wasiwe watazamaji, wawe washiriki wa uchumi.
"Kunatakiwa kuwepo na matumizi ya sayansi na teknolojia katika ufundishaji. Kila shule inatakiwa kuunganishwa na intaneti," amesema.
Huku akitoa mfano wa janga la corona, Kikwete amesema limethibitisha jinsi ukosefu wa teknolojia unavyoathiri ufundishaji.
"Tumeona wakati wa corona, moja hatua zilizochukuliwa ni kufunga shule. Wanafunzi wetu hawakusoma, wanacheza rede, lakini nchi zilizoendelea shule zilifungwa na watoto wakaendelea kusoma.”
"Nilipokuwa Rais tulianzisha matumizi ya intaneti katika ufundishaji, tuliwekeza sana kwenye mkongo wa Taifa. Lengo langu lilikuwa ni kuhakikisha kila shule, hospitali ziunganishwe na intaneti. Mwalimu mmoja wa hisabati afundishe nchi nzima,” amesema.
Kuhusu Elimu jumuishi ameitaka Serikali na wadau kuhakikisha hakuna mtoto anayebaki nyuma kwa kukosa elimu.
"Wengine wanadhani msichana ni wa kubaki jikoni. Wengine wameachwa nyuma kutokana sababu za kisiasa.
Tunatakiwa kuhusisha mashirika yasiyo ya kiserikali kuchangia elimu," amesema.
Awali akimkaribisha Kikwete mwenyekiti wa Tenmet, Dk John Kalage ambaye pia ni mkurugenzi wa taasisi ya HaliElimu amesema kongamano hilo litajadili kwa kina njia za ufadhili wa elimu nchini.
Chanzo: Mwananchi
DuhMhhh! Hii ni hatari ssna. Mwanafunzi anamaliza form six hajui Microsoft Word. Power points, au excel. Huyu anaenda kuajiriwa na nani. Hajui hata kutengeza CV ya kuombea kazi. Atakuwa mgeni wa nani huyu?
Binafsi nimeshindwa kumuelewa Kikwete; anataka ajira ziongezeke au zipungue? Kwanini anahimiza matumizi ya teknolojia ambayo anafahamu matokeo yake ni kupunguza ajira?Ukweli mchungu by 2050 kila kitu kitabaki kwenye technology
Hivyo wanaitajika watu ambao wapo tayari kujiajiri, Machine na operators wa machine
Maroobot vile vile yatakuwa yakifanya kazi sehemu kama shelli na super market
So kazi zitakuwa chache au kutokuwepo kabisa
Kikwete ana hoja tuchukue hatua.
Na kwa taarifa yako anaishi IKULU ya Dar. Kwa kisingizio cha hali yake ya usalama🤫Jamaa ndo Raisi right now
Hao unaowaita masikini na wenyewe wabadilike wawe matajiriJK amesahau matumizi ya teknolojia hayabadilishi mitaala, usome kwa kutumia tablet au mwenzio aende kayumba at the end of the day wote watafanya mtihani mmoja.
Labda yule wa tablet atamzidi mwenzie topic alizo-cover in case ikitokea issue kama ya Corona, ila pasipokuwepo na Corona tofauti yao itakuwa ndogo sana.
Kitakachomyima mtoto wa masikini ajira hata akiwa na ufaulu mzuri bado ni kujuana (nafasi kutolewa kwa upendeleo) lakini sio kwasababu ya teknolojia, na ajira bado zitakuwepo pale pale haziwezi kuondoka.
JK amesahau matumizi ya teknolojia hayabadilishi mitaala, usome kwa kutumia tablet au mwenzio aende kayumba at the end of the day wote watafanya mtihani mmoja.
Labda yule wa tablet atamzidi mwenzie topic alizo-cover in case ikitokea issue kama ya Corona, ila pasipokuwepo na Corona tofauti yao itakuwa ndogo sana.
Kitakachomyima mtoto wa masikini ajira hata akiwa na ufaulu mzuri bado ni kujuana (nafasi kutolewa kwa upendeleo) lakini sio kwasababu ya teknolojia, na ajira bado zitakuwepo pale pale haziwezi kuondoka.
Aher JK aliyezeeka mwili kuliko wewe uliyezeeka akili.Kuzeeka kuna mengi keshaanza kupoteza kumbukumbu
Kwa hiyo ikifika hiyo miaka serikalini na mahakamani tutaajiri wazungu kufanya kila kazi ya ajira iliyoko serikalini na kwenye mahakama zetu?
Tatizo ni kwamba akilini na uwezo wenu wa kufikiri unaishia mita 2.Kwa hiyo ikifika huo mwaka majeshi yetyu yote iwe polisi au JWTZ watakuwa wanaajiriwa wazungu wenye elimu bora?
Uwezo wako wa kufikiri ni mdogo sana.Kwa hiyo mahakimu na majaji watakuwa ni hayo maroboti ,mapolisi watakuwa ni hayo maroboti,Leseni za biashara zitakuwa zinatolewa na hayo maroboti,madaktari na manesi watakuwa ni hayo maroboti,WAtoto mashuleni na vyuoni watafundishwa na hayo maroboti au?
Umeshawahi kufanya interview kwenye taasisi za kimataifa kupitia electronic systems? Huyo anayetumia tablet ana nafasi kubwa ya kupita kuliko wa chaki. Tuwekeze kwenye elimu ya kisasa. Mambo ya A+ za makaratasi tuachane nayo yaani.JK amesahau matumizi ya teknolojia hayabadilishi mitaala, usome kwa kutumia tablet au mwenzio aende kayumba at the end of the day wote watafanya mtihani mmoja.
Labda yule wa tablet atamzidi mwenzie topic alizo-cover in case ikitokea issue kama ya Corona, ila pasipokuwepo na Corona tofauti yao itakuwa ndogo sana.
Kitakachomyima mtoto wa masikini ajira hata akiwa na ufaulu mzuri bado ni kujuana (nafasi kutolewa kwa upendeleo) lakini sio kwasababu ya teknolojia, na ajira bado zitakuwepo pale pale haziwezi kuondoka.
Mawazo finyu sana.Population itakuwaje mwaka huo? Population ikiongezeka ajira zinaongezeka pia haziwezi kushuka zaweza shuka eneo moja zikaongezeka eneo lingine mfano population ikiwa itaongezeka ajira za madaktari na manesi lazima ziongezeke,pia za walimu,Maaskari na watendaji wengine.Huwezi tu kusema tu kwa sababu kiwandani zitashuka haina maana sekta nyingine kuwa nako zitashuka
Kuongelea kushuka au kutoweka kwa ajira unatakiwa kuangalia vitu vingi kimojawapo ni population je itakuwaje kipindi hicho na itahitaji nini kutoka soko la ajira wa kuwahudumia?
Uongo hayo ni yale ya kukariri ,ni kwa masomo ya arts ambayo Kikwete mwenyewe ndio aliyasoma nafikiri hayo ya kukariri aliyosoma yeye ndiyo anaongelea yeye alisoma digrii ya kukariri ya uchumiElimu yetu haitoi kipaumbele kwa wanafunzi kuwa creative. Ina heshimu wanaoweza kukariri.