Jamani nilichomuelewa mzee wetu Kikwete ni; creating brighter future kwa vizazi vyetu! Kwanza ukimsoma amezungumzia issue ya gender hasa kuondoa primitive nonsense kwamba watoto wa kike ni wa kufanya domestic roles (mapishi, mahunjumati na kulea wanaume na watoto). Katika hili anatambaa kwenye kuwezesha hadi watoto wa kike kujifunza ICT ambayo ni dunia inayokuja. Hata ITU wana siku maalum ya Girls in ICT. Kila April.
Kila mwanasiasa ukimpa nafasi ya kujadili jambo fulani hatakosa la kuongea, kwa sababu wanasiasa wengi huwa hawaishiwi maneno mdomoni.
Hivyo basi inapofika hatua ya wananchi kujadili jambo fulani kwa masilahi ya taifa, kila mwananchi atazungumza lake kulingana na nafasi aliyopo kwa wakati huo.
Lakini binafsi kama mwananchi wa kawaida na niliyesoma elimu ya TANZANIA, kuanzia chekechea hadi chuo kikuu, maoni yangu ni haya:
Kwanza kabisa, ingetupasa kama taifa la TANZANIA tuwe na sheria za wanafunzi wa shule za msingi yaani PRIMARIES ACTS na sheria za wanafunzi wa shule za sekondari yaani SECONDARIES ACTS kama muongozo na kanuni za wanafunzi wawapo shuleni.
Suala lingine, ni kuwepo na uwazi katika matokeo ya wanafunzi wa shule za msingi na shule za sekondari. Hii itasaidia kuondoa udanganyifu na upendeleo katika upangaji wa matokeo ya wanafunzi wote kwa ujumla.
Pili, kasema elimu yetu ya Afrika iendane na dunia ya sayansi na teknoloji. Anatoa mfano, utafika wakati unaita gari halihitaji 'mpigadebe wala suka' bali ni teknoloji. Hivyo tunahitaji kuandaa vizazi vyetu viweze kukabili hili.
Sote inatupasa tufahamu kuwa AFRIKA ni bara linalojumuisha mataifa zaidi ya hamsini [ 50 ]. Kwahiyo, Rais Mstaafu Mheshimiwa Mrisho Khalufani Kikwete anajapojaribu kujadili mataifa zaidi ya hamsini [ 50 ] kwa pamoja inakuwa haijakaa sawa kitaaluma.
Na kwa upande wa ubora wa elimu, huwa kuna taasisi ya kimataifa inayoshughulika na masuala ya ubora wa elimu, taasisi hii inaitwa UNESCO.
Kwa taarifa za UNESCO kwa miaka kadhaa iliyopita ni kuwa, ubora wa elimu ya TANZANIA umeshuka ukilinganisha na mataifa mengine.
Ubora wa elimu ya TANZANIA umeshuka kwa sababu gani? Sababu kubwa ni UDANGANYIFU WA MADARAJA YA UFAULU YA WANAFUNZI - kwa lugha ya kiingereza wanaita ni "REPLACEMENT OF PASSMARKS [ GRADES ]".
Wanafunzi wengi wanapewa madaraja tofauti na ufaulu wao. Pale Baraza la Mitihani [ NECTA ] huwa wanasema hivi - "UNAPEWA UNACHOSTAHILI, SIO KILE UNACHOPATA KWENYE KARATASI LAKO LA MITIHANI" na kwa lugha ya kiingereza huwa wanasema hivi - "YOU SCORE WHAT YOU DESERVE, NOT WHAT YOU GET ON YOUR ANSWER SHEETS".
Hii inatoka na kupika matokeo ya wanafunzi wa shule za msingi na shule za sekondari kwa pamoja. Madhara yake taifa linapata wahitimu wasiokuwa na sifa za kitaaluma na sifa za kuajiriwa au kujiajiri wenyewe.
Sababu nyingine iliyopelekea elimu ya TANZANIA kushuka ni "KUTOKUWA NA UWAZI KATIKA KUTANGAZA MATOKEO YA WANAFUNZI". Kwa lugha ya kiingereza huwa wanasema hivi - "LACK OF TRANSPARENCY ON ANNOUNCEMENT OF PUPILS AND STUDENTS ACADEMIC RESULTS".
Sote tunafahamu kuwa, matokeo ya wanafunzi wote wa shule za msingi na shule za sekondari yalianza kutangazwa rasmi kipindi cha HAYATI RAIS JOHN POMBE MAGUFULI, mwaka 2016.
Je, tukiuliza orodha ya wanafunzi bora waliofanya vizuri kitaifa kwa mwaka wa 2015, iwe kwa darasa la saba, kidato cha nne na kidato cha sita tutazipata? Jibu ni hakuna?
Je, tukiuliza orodha ya wanafunzi bora waliofanya vizuri kitaifa kwa mwaka wa 2007, iwe kwa darasa la saba, kidato cha nne na kidato cha sita tutazipata? Jibu ni hakuna?
Kwahiyo, taifa la TANZANIA lilikuwa linazalisha wahitimu wasiokuwa na ufahamu wa sifa zao za kitaaluma mpaka mwaka 2016, ambapo HAYATI RAIS JOHN POMBE MAGUFULI alipoamua kuweka wazi kila kitu hadharani. MWENYEZI MUNGU amrehemu huko alipo!!
Kwahiyo suala la KUTOKUWA NA UWAZI KATIKA SEKTA YA ELIMU lilichangia ubora wa elimu ya TANZANIA kushuka ukilinganisha na ubora wa elimu ya mataifa mengine. Na madhara yake ni makubwa sana kwa wahitimu waliosoma elimu ya TANZANIA.
Kwa wale Watanzania waliobahatika kufanya kazi nje ya nchi au kwenye makampuni ya kimataifa watakubaliana na mimi kuwa - WATAALAMU KUTOKA TANZANIA HUWA HAWAAMINIKI KWA MATAIFA YA NJE. Na hii iko wazi kabisa, watalaamu kutoka TANZANIA huwa wanaitwa ni INCONSISTENCY PERSONEL, kwa lugha ya kiswahili sijui imekaaje hii.
Na kwa upande wa WAHANDISI yaani ENGINEERS huwa wanaanzia hatua ya TECHNICAL OPERATION kwa kipindi cha miaka miwili [ 2 ] hadi miaka mitatu [ 3 ] hata muhitimu awe na Shahada ya Uzamili au Shahada ya Uzamivu. Na hii ipo hata kwa upande wa MADAKTARI WA AFYA yaani DOCTORS OF MEDICINE, huwa wanaanzia kuwa CLINICAL OFFICIAL kwa kipindi cha miaka miwili [ 2 ] hadi miaka mitano [ 5 ].
Na haya ndio madhara ya mfumo wa elimu ya TANZANIA. Baraza la Mitihani la TANZANIA yaani NECTA ni taasisi ya HOVYO sana, kuna uchafu mwingi sana pale. Imefikia hatua hata mataifa mengine yanaita TANZANIA ni "GARBAGE FROM PUERTO RICO" yaani "TANZANIA IS NO LONGER A BANANA REPUBLIC, IT'S A GARBAGE FROM PUERTO RICO".
Tatu, kuhusu kuunganisha shule na maeneo mengine ya kijamii kweli Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa ulikuwa ndiyo moja ha malengo yake. I do remember! Sasa tusibeze kutumia tablets ndiko kujenga kizazi cha digital.
Na hili ni azimio la WSIS.
Ndio! Hapa nakubali, kuwa ni muhimu kwa wanafunzi wa shule za sekondari kuanza kujifunza masomo ya kompyuta na kuna baadhi ya shule za sekondari ziliisha anza kutumia na kusoma masomo ya kompyuta kama somo.
Nne, wanaodrop kwenye elimu. Huwezi kuingia kwenye dunia kijiji halafu bado ukawa na watu asilimia zaidi ya asilimia 30 hawamalizi shule. Ndiyo maana hata UN ina Azimio la Education For All ambalo ni la Dakar, Senegal (2000). Lilianzia Jomtie, Thailand.
Huu mradi wa EDUCATION FOR ALL upo na upatikana sana kwa nchi za KENYA, UGANDA na RWANDA. Sijafahamu vizuri kwa upande wa TANZANIA hali ni ikoje.
Lakini huu mradi wa EDUCATION FOR ALL una malengo wezeshi kwa wanafunzi kuweza kusoma katika mazingira mazuri na rafiki ili kupata elimu iliyo bora.
Malengo ya EDUCATION FOR ALL yanaweza kabisa kufanana na malengo ya MMEM na MMES kwa upande wa TANZANIA.
Kimsingi, hii presentation ya JK siyo ya level ya kufikiri kwa kukurupuka. Inahitaji utulivu wa akili ujue kwanza hoja. Ni mada kubwa!πππ
Ni mada nzuri kwa wakati uliopita. Ilimpasa awe na mada hii kipindi yeye ni mtendaji mkuu na ni kiongozi wa serikali ya TANZANIA.