Kikwete: Kutokana na utoaji hafifu wa Elimu nchini, kuna hatari ya nusu ya ajira zilizopo kutoweka ifikapo mwaka 2050

Kikwete: Kutokana na utoaji hafifu wa Elimu nchini, kuna hatari ya nusu ya ajira zilizopo kutoweka ifikapo mwaka 2050

Jamani nilichomuelewa mzee wetu Kikwete ni; creating brighter future kwa vizazi vyetu! Kwanza ukimsoma amezungumzia issue ya gender hasa kuondoa primitive nonsense kwamba watoto wa kike ni wa kufanya domestic roles (mapishi, mahunjumati na kulea wanaume na watoto). Katika hili anatambaa kwenye kuwezesha hadi watoto wa kike kujifunza ICT ambayo ni dunia inayokuja. Hata ITU wana siku maalum ya Girls in ICT. Kila April.

Pili, kasema elimu yetu ya Afrika iendane na dunia ya sayansi na teknoloji. Anatoa mfano, utafika wakati unaita gari halihitaji 'mpigadebe wala suka' bali ni teknoloji. Hivyo tunahitaji kuandaa vizazi vyetu viweze kukabili hili.

Tatu, kuhusu kuunganisha shule na maeneo mengine ya kijamii kweli Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa ulikuwa ndiyo moja ha malengo yake. I do remember! Sasa tusibeze kutumia tablets ndiko kujenga kizazi cha digital.
Na hili ni azimio la WSIS.

Nne, wanaodrop kwenye elimu. Huwezi kuingia kwenye dunia kijiji halafu bado ukawa na watu asilimia zaidi ya asilimia 30 hawamalizi shule. Ndiyo maana hata UN ina Azimio la Education For All ambalo ni la Dakar, Senegal (2000). Lilianzia Jomtie, Thailand.

Kimsingi, hii presentation ya JK siyo ya level ya kufikiri kwa kukurupuka. Inahitaji utulivu wa akili ujue kwanza hoja. Ni mada kubwa!😀😀😀
 
Rais mstaafu wa awamu ya nne Dk Jakaya Mrisho Kikwete ameonya tusipobadilika namna tunavyofundisha watoto wetu basi ajira zote zitatoweka ifikapo mwaka 2050.

My take.
Hii elimu yetu ya kuwafanya chadema washangilie kila baya linaloipata nchi yetu ikiwemo kukamatwa ndege, miradi kukwama , tutashitakiwa MIGA etc bora ifutwe kabisa tuanzishe elimu mpya itakayowafanya chadema wajitambue.

====

Dar es Salaam. Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete amesema kutokana na utoaji hafifu wa elimu nchini kuna hatari ya nusu ya ajira zilizopo kutoweka ifikapo mwaka 2050.

Ameyasema hayo leo Jumanne Mei 18, 2021 wakati akizindua kongamano la elimu linalojadili ufadhili wa elimu lililoandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (Tenmet) jijini Dar es Salaam.

Akieleza utafiti uliofanywa na tume ya kimataifa ya elimu ambayo yeye ni mjumbe, amesema elimu inayotolewa barani Afrika ilitolewa miaka 50 hadi 70 iliyopita kwa nchi zilizoendelea.

"Sisi bado tunatumia chaki, wakati wenzetu wanatumia tablets. Tuliona kuwa kuna watu zaidi ya milioni 263 waliotakiwa kuwa shule lakini hawapo, kati yao milioni 100 wapo Afrika. Kwa waliopo shule wengi hawamalizi shule. Wengi wanaishia njiani. Asilimia 67 wamemaliza shule, asilimia 33 ni idadi kubwa," amesema Kikwete.

Amesema kutokana na utoaji hafifu wa elimu na maendeleo ya teknolojia kuna janga la ukosefu wa ajira linakuja.

"Ifikapo 2050 asilimia 50 ya kazi zitafutika, kwa sababu ya matumizi ya mashine. Kutakuwa na magari yasiyotumia dereva. Unataka usafiri, unaita Uba, unatumia simu yako inakuja inakupeleka sehemu husika labda Ubungo Plaza au Millennium Tower," amesema.

Amesema mbali na ukosefu wa ajira, idadi ya watu barani Afrika itafikia watu bilioni mbili, “kama watu hao hawana ujuzi unafanya nini? Sijui itakuwaje. Kutakuwa na athari kubwa za kiuchumi na kijamii."

Akisisitiza matumizi ya teknolojia, Kikwete ameshauri kuwepo na uwekezaji katika elimu ili vijana wa Afrika wasiwe watazamaji, wawe washiriki wa uchumi.

"Kunatakiwa kuwepo na matumizi ya sayansi na teknolojia katika ufundishaji. Kila shule inatakiwa kuunganishwa na intaneti," amesema.

Huku akitoa mfano wa janga la corona, Kikwete amesema limethibitisha jinsi ukosefu wa teknolojia unavyoathiri ufundishaji.

"Tumeona wakati wa corona, moja hatua zilizochukuliwa ni kufunga shule. Wanafunzi wetu hawakusoma, wanacheza rede, lakini nchi zilizoendelea shule zilifungwa na watoto wakaendelea kusoma.”

"Nilipokuwa Rais tulianzisha matumizi ya intaneti katika ufundishaji, tuliwekeza sana kwenye mkongo wa Taifa. Lengo langu lilikuwa ni kuhakikisha kila shule, hospitali ziunganishwe na intaneti. Mwalimu mmoja wa hisabati afundishe nchi nzima,” amesema.

Kuhusu Elimu jumuishi ameitaka Serikali na wadau kuhakikisha hakuna mtoto anayebaki nyuma kwa kukosa elimu.

"Wengine wanadhani msichana ni wa kubaki jikoni. Wengine wameachwa nyuma kutokana sababu za kisiasa.

Tunatakiwa kuhusisha mashirika yasiyo ya kiserikali kuchangia elimu," amesema.

Awali akimkaribisha Kikwete mwenyekiti wa Tenmet, Dk John Kalage ambaye pia ni mkurugenzi wa taasisi ya HaliElimu amesema kongamano hilo litajadili kwa kina njia za ufadhili wa elimu nchini.

Chanzo: Mwananchi
Vipi na yale mazombie kule mjengoni yanayoshangilia mambo ya kipuuzi hakuna Chadema kule wamejaa nyumbu wa kijani toka mitaa ya Lumumba. Kinuju bila kuitajataja Chadema kigololi chako hakitulii
 
Ajira zitatoweka vipi means panakuwa hamna Serikali, aache uongo Serikali hela ipo ya kutosha na tunataka kuona raia mnajenga nchi msiwe na wasiwasi.
soma vizuri umuelewe JK mfumo wa elimu yetu leo unatuandaa kuwa watazamaji wa mapinduzi ya kiteknolojia baadaye.
 
Hapa tunapaswa kumlaumu mzungu kwa ushetani aloufanya wa kutumezesha dini badala ya kutumezesha elimu anachokizungumza JK ni kitu cha kweli kabisa ukiangalia provision ya elimu waliyoipata karne ya 15-16 imeanza mwanzoni mwa miaka ya 1910 na hiyo effect imeanza kuonekana miaka ya 60.
 
Alicho
2050 dunia itakua ktk elimwengu mwengine Wa sayansi, elimu ya "sikuile akaenda, shambani kutembelea, akayaona matunda, mtini yamejaa" haitokuwa na matumizi tena miaka hiyo! Tubadilishe mitaala!
sahau ni kuwa wengi tutakuwa tushakufa so tutakuwa tumeepukana na kadhia hio
 
JK ameongea ukweli mtupu !angeshauri tu kwamba , kwakuwa tunakoenda dunia inakuwa ni finest digital , kila kitu dogital , tungeanza kuwekeza kwa watoto wa shule zetu , mfano hata kilimo chenyewe miaka. Ijayo kitakuwa digital tu , kila. Kitu ni digital , tusipobadilika tutaajiri wataalaumu watufanyie haya mambo
 
Kuzungumzia teknolojia leo wakati upatikanaji wa umeme tu bado ni shida ni mapema mno, mabadiliko ya teknolojia yatakuja pale ambapo tutajitosheleza kwa vitu vingine kama umeme, na wataalamu wa kutosha kufundisha.

Teknolojia itakapokuwa ndio itakuja kuathiri ajira za watu kama viwandani na kwingineko, lakini hapa kwetu bado wakati huo haujafika na sidhani kama tutafika 2050.
Tutaletewa vitendea kazi kwa gharama nafuu kutoka kwa hao waliotumia muda huu kubadilika na hizo kazi zitapungua kwa mtindo huo na zile zitakahitaji maarifa zaidi watakuja kuzifanya wao sisi tukiwa tumepigwa doro.
 
Ajira zitatoweka vipi means panakuwa hamna Serikali, aache uongo Serikali hela ipo ya kutosha na tunataka kuona raia mnajenga nchi msiwe na wasiwasi.
Kati ya vijana zaidi million ishirini Serikali inajiri watu wangapi ?
JK amesahau matumizi ya teknolojia hayabadilishi mitaala, usome kwa kutumia tablet au mwenzio aende kayumba at the end of the day wote watafanya mtihani mmoja.

Labda yule wa tablet atamzidi mwenzie topic alizo-cover in case ikitokea issue kama ya Corona, ila pasipokuwepo na Corona tofauti yao itakuwa ndogo sana.

Kitakachomyima mtoto wa masikini ajira hata akiwa na ufaulu mzuri bado ni kujuana (nafasi kutolewa kwa upendeleo) lakini sio kwasababu ya teknolojia, na ajira bado zitakuwepo pale pale haziwezi kuondoka.
Hizo Ni fikra za kiongozi mwenye maono ya mbali,
Tusipobadili elimu yetu ,tukubali kutawaliwa kiteknojia,
Swala halitakuwa kujuana isipokuwa mwenye maarifa sahihi ya wakati huo,
 
Wastaafu wana washwawashwa (in Mwendazake's Voice).

Hajatoa suluhisho zaidi ya kubwabwaja tu.

By the way yeye hatokuwepo duniani by 2050...aache kiherehere.
 
Teknolojia ikifanya kazi hakutakuwa na mambo ya wizi na rushwa. Roboti litaiba pesa lipeleke wapi. Kwenye vituo vya mafuta hakutakuwa na wizi wa mafuta kwakuwa roboti atafanya kazi otomatikali. Watakaokuwepo watafurahia maisha sana. Imajini saiv kakibwengo kanakuambia unanijua mi nani? Sa ngapi roboti litakuambia hayo. What a soft life that will be!
 
Rais mstaafu wa awamu ya nne Dk Jakaya Mrisho Kikwete ameonya tusipobadilika namna tunavyofundisha watoto wetu basi ajira zote zitatoweka ifikapo mwaka 2050.

My take.
Hii elimu yetu ya kuwafanya chadema washangilie kila baya linaloipata nchi yetu ikiwemo kukamatwa ndege, miradi kukwama , tutashitakiwa MIGA etc bora ifutwe kabisa tuanzishe elimu mpya itakayowafanya chadema wajitambue.

====

Dar es Salaam. Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete amesema kutokana na utoaji hafifu wa elimu nchini kuna hatari ya nusu ya ajira zilizopo kutoweka ifikapo mwaka 2050.

Ameyasema hayo leo Jumanne Mei 18, 2021 wakati akizindua kongamano la elimu linalojadili ufadhili wa elimu lililoandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (Tenmet) jijini Dar es Salaam.

Akieleza utafiti uliofanywa na tume ya kimataifa ya elimu ambayo yeye ni mjumbe, amesema elimu inayotolewa barani Afrika ilitolewa miaka 50 hadi 70 iliyopita kwa nchi zilizoendelea.

"Sisi bado tunatumia chaki, wakati wenzetu wanatumia tablets. Tuliona kuwa kuna watu zaidi ya milioni 263 waliotakiwa kuwa shule lakini hawapo, kati yao milioni 100 wapo Afrika. Kwa waliopo shule wengi hawamalizi shule. Wengi wanaishia njiani. Asilimia 67 wamemaliza shule, asilimia 33 ni idadi kubwa," amesema Kikwete.

Amesema kutokana na utoaji hafifu wa elimu na maendeleo ya teknolojia kuna janga la ukosefu wa ajira linakuja.

"Ifikapo 2050 asilimia 50 ya kazi zitafutika, kwa sababu ya matumizi ya mashine. Kutakuwa na magari yasiyotumia dereva. Unataka usafiri, unaita Uba, unatumia simu yako inakuja inakupeleka sehemu husika labda Ubungo Plaza au Millennium Tower," amesema.

Amesema mbali na ukosefu wa ajira, idadi ya watu barani Afrika itafikia watu bilioni mbili, “kama watu hao hawana ujuzi unafanya nini? Sijui itakuwaje. Kutakuwa na athari kubwa za kiuchumi na kijamii."

Akisisitiza matumizi ya teknolojia, Kikwete ameshauri kuwepo na uwekezaji katika elimu ili vijana wa Afrika wasiwe watazamaji, wawe washiriki wa uchumi.

"Kunatakiwa kuwepo na matumizi ya sayansi na teknolojia katika ufundishaji. Kila shule inatakiwa kuunganishwa na intaneti," amesema.

Huku akitoa mfano wa janga la corona, Kikwete amesema limethibitisha jinsi ukosefu wa teknolojia unavyoathiri ufundishaji.

"Tumeona wakati wa corona, moja hatua zilizochukuliwa ni kufunga shule. Wanafunzi wetu hawakusoma, wanacheza rede, lakini nchi zilizoendelea shule zilifungwa na watoto wakaendelea kusoma.”

"Nilipokuwa Rais tulianzisha matumizi ya intaneti katika ufundishaji, tuliwekeza sana kwenye mkongo wa Taifa. Lengo langu lilikuwa ni kuhakikisha kila shule, hospitali ziunganishwe na intaneti. Mwalimu mmoja wa hisabati afundishe nchi nzima,” amesema.

Kuhusu Elimu jumuishi ameitaka Serikali na wadau kuhakikisha hakuna mtoto anayebaki nyuma kwa kukosa elimu.

"Wengine wanadhani msichana ni wa kubaki jikoni. Wengine wameachwa nyuma kutokana sababu za kisiasa.

Tunatakiwa kuhusisha mashirika yasiyo ya kiserikali kuchangia elimu," amesema.

Awali akimkaribisha Kikwete mwenyekiti wa Tenmet, Dk John Kalage ambaye pia ni mkurugenzi wa taasisi ya HaliElimu amesema kongamano hilo litajadili kwa kina njia za ufadhili wa elimu nchini.

Chanzo: Mwananchi
Vikao vya kulipana posho tu hamna concrete measure yeyote hapo.

Maswahibu yatakayowakuta watanzania watakaokuwa wanaishi miaka hiyo kwa kiasi kikubwa yatakuwa yamechangiwa na ufisadi tu.

Wewe unasema kutakuwa hamna kazi lakini mmekazana kuwanyang'anya ardhi wakulima wadogo vijijini halafu eti unashangaa kuwa 2050 hawatakuwa na ajira!

Itakapifikia hali hiyo nchi haitakalika kwa ujambazi na kila aina ya uhalifu maana lazima watu wale, sasa watakula vipi ndio issue.
 
Ukweli utabaki kuwa ukweli tu. Tanzania inabidi tuamke. Swala la ajira bado ni tatizo na hatiwezi kubaki kuendelea kulijadilitu mitandaoni na kwenye mijadala mbalimbali...tunatumia gharama kubwa sana kuandaa mijadala ya kujadili kuhusu tatizo la ajira. Lkn tunasahau kuwa maneno matupu hayavunji mfupa.

1. Inabidi serikali iingie kwenye utekelezaji wa maadhimio yote yenye tija kuhusu tatizo la ajira.

2. Mtaala wa elimu yetu inabidi ibadilike mara moja ili kwendana na mabadiliko ya dunia. Masomo kama ya ujasiria mali, na uwekezaji, yafundishwe mashuleni kuanzia ngazi ya shule ya msingi hadi chuo kikuu ili kutoa uelewa mpana kwa wasomi wetu na kupunguza struggle kubwa iliyopo kwenye soko la ajira nchini.

3. Serikali iongeze uwanda mpana wa utengenezaji ajira kwamaana ya kwamba, itengeneze sera madhubuti ambazo zitajikita kwenye uwekezaji kwenye viwanda zaidi na kutengeneza room kubwa ya ajira kwa wananchi wake.

4. Uadilifu katika taifa letu umepungua sana....watu siku hizi wanapewa ajira kwa kujuana( technical know who) na sio kwa kuangalia mtu anajua nn ( technical know how). Heria zetu bado ni butu sana na sekretarieti yetu ya ajira bado haijafanya kazi kama inavyo takiwa.

Watu wengi walio officen hawana proffesional bali wanaujuzi ambao pia wameupata kwa kupitia ndugu zao
 
Kuzeeka kuna mengi keshaanza kupoteza kumbukumbu

Kwa hiyo ikifika hiyo miaka serikalini na mahakamani tutaajiri wazungu kufanya kila kazi ya ajira iliyoko serikalini na kwenye mahakama zetu?
Pamoja na kuzeeka lakini ana fikra na maona yanayopaswa kuwa ya vijana,
Tusipoendana na teknolojia ya wakati ,itafika mahali ajira zitatukataa kutokana na maarifa yanayotokiwa kwenye ajira husika,
Hata usimamizi itabidi tutafute wasimamizi wa nje wenye teknolojia husika,
Hiyo miradi mikubwa kwanini tunawapa wazungu, ina maana hutuna mafundi wa kujenga miaka 50 ya uhuru ?
Kwanini tusichimbe migodi sisi wenyewe ?
Tubadili fikra zetu kiukweli tutakwama pakabwaa
 
JK amesahau matumizi ya teknolojia hayabadilishi mitaala, usome kwa kutumia tablet au mwenzio aende kayumba at the end of the day wote watafanya mtihani mmoja.

Labda yule wa tablet atamzidi mwenzie topic alizo-cover in case ikitokea issue kama ya Corona, ila pasipokuwepo na Corona tofauti yao itakuwa ndogo sana.

Kitakachomyima mtoto wa masikini ajira hata akiwa na ufaulu mzuri bado ni kujuana (nafasi kutolewa kwa upendeleo) lakini sio kwasababu ya teknolojia, na ajira bado zitakuwepo pale pale haziwezi kuondoka.
Nakubali jambo kubwa si tablet wala ubao ukutani, ni
1) idadi ya wanafunzi darasani
2) elimu ya walimu wenyewe
3) mbinu wa elimu usiolenga kukariri lakini kutafakari
4) shule isiyotaka mwanafunzi aitikie bali awe tayari kupinga akiwa na sababu zake
5) mazingira inayoheshimu watoto badala ya kuvumilia kiboko...

nani ataongeza?
 
Back
Top Bottom