Kikwete: Sera zinazowanyima watu uhuru ni hatari kwa usalama wa nchi

Kikwete: Sera zinazowanyima watu uhuru ni hatari kwa usalama wa nchi

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Akizungumza kwenye hafla ya Miaka 10 ya Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC), Rais Mstaafu amesema ni muhimu kuhakikisha kunakuwa na sera nzuri zisizobagua na kuwanyima watu uhuru wao kwasababu hiyo ni njia nyingine kuu ya kulinda usalama wa nchi.

Amefafanua kuwa usalama wa nchi unahusisha mambo mengi, na kutolea mfano majukumu ya JWTZ kulinda mipaka, Idara ya Usalama wa Taifa kufanya upelelezi na kupekua mambo yanayotokea duniani kote lakini kipengele kikubwa ni nchi kuwa sera nzuri za ndani.

Kikwete amesema "Nchi ikiwa na sera nzuri za ndani na mahusiano mazuri na nchi nyingine haitalazimika hata kununua vifaru vya jeshi kwa sababu hakutakuwa na matishio ya usalama na hivyo hakutakua na wa kupigana naye".
 
C kwamba Mambo ya kijinga yanayoendelea ndani ya nchi wakati mwingine hatuyaoni, la hasha, Kila nyanja wamekaba( iwe media, jeshi, mahakama, vyama vya wafanyakazi, polisi, tume ya uchaguzi nk nk) lakini hata hao wenye kuwatumikia na kulinda maslahi yao kunasiku Huwa wananchoka na hali hubadilika. Hakuna lisilo na mwisho.
 
Mstaafu anasahau kuwa amani inakuja wananchi wakiwa na uhakika wa maisha yao.

Yaani ile basic need inapatikana.

Ni hatari kwa usalama wa nchi kuwa na kikundi cha watu wachache waliohodhi mamlaka ya nchi na njia za kiuchumi.

Gap kubwa kati ya maskini na matajiri linaweza pelekea amani ya nchi kuondoka haraka mno.
 
Kalynda njoo tupige pesa na KALYNDA gusa Link sign up/register utapata buku kweny account yako

Nicheki nikupe maelekezo zaidi watsap 0719537104
Hii ndo the best app ever kwa sasa KALYNDA
 
Kuwa na uhusiano mzuri na majirani na sera nzuri za ndani sio sababu za nchi kutokuwa na silaha kwa ajili ya kujilinda, Iddi Amin alituletea ujinga bila kumchokoza, kama tusingekuwa na silaha angetutandika na ardhi yetu angeichukua.
Ila inasemekana jk aliloacha jeshi lipo vizuri, Sasa sijui aliemfuata
 
Back
Top Bottom