Kila la heri timu ya Taifa, Taifa Stars

Huyu Amunike aishie hukohuko asije na timu....Nitaenda airport na rungu akishuka tu nampa kibano kama tunavyoua mbwa vikongwe huku kwetu...
 
Misri na Ghana ni vinara wa kufika hatua ya Fainali AFCON tangu hii michuano iasisiwe. Lakini Misri ni kinara wa kutwaa ubingwa wa AFCON(mara 7), Ghana ipo nafasi ya 3 kutwaa ubingwa(mara 4).

Misri

Imeshinda taji ×7 (1957, 1959, 1986, 1988, 2006, 2008, 2010)
Imekuwa mshindi wa pili x2.

Kwa hiyo imefika hatua ya fainali mara 9.

Ghana


Imeshinda taji ×4 (1963, 1965, 1978, 1982)
Imekuwa mshindi wa pili x5.

Kwa hiyo imefika fainali mara 9.

Ni miaka 37 imepita tangu Timu ya Taifa ya Ghana(Black Stars) ilipotwaa taji lake la 4(1982), imekuwa ikilisaka taji la 5 bila mafanikio huku ikiwa kinara wa kuwa mshindi wa pili, ambapo mara ya mwisho kuwa mshindi wa pili ilikuwa mwaka 2015 ilipomenyana na Ivory Coast(The Elephants) na Ivory Coast kubeba taji lao la pili chini ya nyota zake(Gerivinho, Solomon Kalou, Yaya Toure).

Sambamba na hapo, Cameroon na Nigeria zinafuatia kufika hatua ya fainali AFCON baada ya Misri na Ghana, zimecheza fainali mara 7.

Cameroon

Imeshinda taji ×5 (1984,1988, 2000, 2002, 2017)
Imekuwa mshindi wa pili x2.

Nigeria

Imeshinda taji ×3 (1980, 1994, 2013)
Imekuwa mshindi wa pili x4.

DR Congo ni timu pekee ambayo haijawahi kupoteza nafasi ya fainali iliyowahi kucheza. Imecheza fainali mara 2(1968, 1974).

Timu zilizowahi kushinda taji mara moja ni Zambia (2012), Tunisia (2004) na Sudan (1970), na pia zimewahi kushika nafasi ya pili mara moja moja.

Timu zilizowahi kufika fainali mara moja na kushinda nafasi hiyo ni Afrika kusini (1996), Algeria (1990), Ethiopia (1962), Morocco (1976), na Congo (1972)

Je Misri ataweza kuendelea kuwa kinara wa mataji ya AFCON? (Ndio ataendelea kuwa kinara).

Je Misri na Ghana wataendelea kuwa vinara wa kufika hatua ya Fainali? Stay tuned!.

Je Ghana ataweza kuongeza taji lake la 5 la AFCON na kuwa katika nafasi ya pili kwa ushindi wa mataji sambamba na Cameroon? Stay tuned!

Je Cameroon na Nigeria wataendelea kuwa vinara namba 2 kufika hatua ya Fainali? Stay tuned!

Je Cameroon ataweza kutetea nafasi yake ya pili ya kutwaa taji la AFCON? Stay tuned!

Je Nigeria itaweza kunyakua taji lake namba 4 na kuwa sawa na Ghana katika nafasi ya 3 kwa ushindi wa mataji ya AFCON? Stay tuned!.

Je Cameroon ataweza kunyakua taji lake 3 la AFCON? Stay tuned!

Je DR Congo itaweza kuongeza taji lake la 3? Stay tuned!

"Avumaye baharini ni papa kumbe na wengine wapo" Tunisia, Afrika kusini, Morocco na Algeria zitafurukuta kusaka na kunyakua mataji yao ya 2 ? Stay tuned!

Taifa Stars je.....
 
Wale wamekaribiana na binadamu,
 
Watanzania wengi wana IQ ndogo sana ! Hivyo wana michezo ,wanasiasa hawana uwezo wa kufanya maamuzi sahihi na kwa haraka!
Tunachoweza na ambacho hatuna mshindani duniani ni unafiki na urongo tu!
Mpira ni hesabu. Kama huwezi faulu hesabu huwezi faulu chochote ksbbu kila kitu kinaanza na hesabu, alafu kinachotutesa ss tunapenda maisha ya kukatiza sana, mitoko yetu ni ya short cut kuanzia siasa tunashinda kwa kuibiana kura, darasani mpaka chuo kikuu nimeshudia watu wanaingia na viboot, a.k.a makaratasi ya kutazamia kwenye mitihani, kila kitu ujanjaujanja mpaka budget zetu zinapitishwa kwa ujanja ujanja ona pamaka soka letu tunafuzu kwenda misri kwa ujanjaujanja Nina wasiwasi na Mipango yetu ni ya ujanja tu, kwakweli inanikela mno, tunazidiwa na Burundi ? Tuko wajinga sana
 
Huyu Amunike aishie hukohuko asije na timu....Nitaenda airport na rungu akishuka tu nampa kibano kama tunavyoua mbwa vikongwe huku kwetu...
Kwa hiyo Unahisi hii timu akipewa Guadiola itaweza kumfunga Senegal?! Mkuu Senegal unawachukuliaje?!
 
Kuna ishu ya physique na body fitness....

Sijui wenzangu mnaonaje.

Na sielewi sijui ni namna ya kuchagua wachezaji....

Sijui ni "dieting" ndiyo tatizo, kwamba hawalishwi chakula vizuri pamoja na kutoingia "gym" kufanya mazoezi Ku - build body physique....

sijui ndivyo tulivyo kiasili kwa maumbo yetu kuwa madogo dogo...

Nilikuwa nawaona wachezaji wetu wanajipamia tu kwa jamaa na kuanguka anguka kurahisi rahisi tu...

Sijui siku tukikutana na Wa Ivory Coast itakuja kuwaje tu maana majamaa na mapandikizi ya mimutu hao!!
 
Kwa hiyo Unahisi hii timu akipewa Guadiola itaweza kumfunga Senegal?! Mkuu Senegal unawachukuliaje?!
Kwan nan kasema nafanya hv kwa ajili ya Senegal ... Kwan yy ni mara ya kwanza kufanya upumbav...hukumbuki mechi za kufuzu??....huyu kocha ashafukuzwa mara nyingi tu huko sijui tff walimpendea kitu gan...
 
But BLACK is the best color on earth.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…