Kila la kheri Taifa stars "dhahifu", dhidi ya timu bora kabisa ya Senegal

Kila la kheri Taifa stars "dhahifu", dhidi ya timu bora kabisa ya Senegal

joto la jiwe

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2017
Posts
26,117
Reaction score
46,617
Japo watu wengi husema mpira ni dakika 90, au mpira unadunda, lakini kuilinganisha Taifa stars na Senegal, ni ngumu sana kukubaliana na Maneno hayo.

Bahati mbaya sana, mashindano ya mpira sio kama ngumi, ambapo hawawezi kushindanisha bondia wenye uzito tofauti, kitendo cha kushindanisha Senegal ambayo ipo nafasi ya 22 duniani, na Tanzania nafasi ya 131 na kutegemea matokeo tofauti, ni lazima mtu awe na moyo wa mwendawazimu.

Yote kwa yote " Ukikubali kuolewa, pia ukubali kula bila nguo". Kila la kheri Taifa stars, tupo nyuma yenu, lolote litakalotokea, tumeshajiandaa kisaikolojia.
 
Japo watu wengi husema mpira ni dakika 90, au mpira unadunda, lakini kuilinganisha Taifa stars na Senegal, ni ngumu sana kukubaliana na Maneno hayo.

Bahati mbaya sana, mashindano ya mpira sio kama ngumi, ambapo hawawezi kushindanisha bondia wenye uzito tofauti, kitendo cha kushindanisha Senegal ambayo ipo nafasi ya 22 duniani, na Tanzania nafasi ya 131 na kutegemea matokeo tofauti, ni lazima mtu awe na moyo wa mwendawazimu.

Yote kwa yote " Ukikubali kuolewa, pia ukubali kula bila nguo". Kila la kheri Taifa stars, tupo nyuma yenu, lolote litakalotokea, tumeshajiandaa kisaikolojia.
"Any thing is possible in soccer" Burundi nusura itoke sare na Nigeria ......taifa tar 1 Senegal 0.......it can happen
 
Soka ni maandalizi, nidhamu, selection bora ya Kocha kwa wachezaji, kujituma, talent, motivation kwa wachezaji na team work. Kama yote yametekelezwa andika ushindi, vinginevyo andika maumivu.
 
"Any thing is possible in soccer" Burundi nusura itoke sare na Nigeria ......taifa tar 1 Senegal 0.......it can happen
Hahahahaha, wewe ni miongoni mwa wale wenye MOYO wa mwendawazimu, ila hongera kwa kututia nguvu.
 
Kama tuliweza kupiga Ug cranes 3 .....any thing is possible
So far kwa kiwango kilichooneshwa na Burundi pamoja na Uganda.

Taifa stars sina hofu nayo sana, majina makubwa si tishio kihivo, ladha ya AFCON ni tofauti na uchezaji wa Europe
 
Kwa kweli tuombe tu Mungu hawajama squad yao nimeiangalia kwa kweli wametuacha mbali sana
Screenshot_20190622-191744.jpeg
 
Acha unafiki, tangu lini mkenya akaitakia mema Tanzania?
Ni Tanzania tu ndipo unapokuta raia wanafiki Kama wewe.hii timu ingekuwa ya Somalia pamoja na changamoto zote za kimaisha wanazopitia wangeungana kushangilia timu yao sio Kama hapa tz yaani watu ni wanafiki sijapata kuona!!!yaani wenzetu huko nje wanatushangaa Sana wanashindwa kuelewa sisi ni binadamu wa aina gani.
 
Ni Tanzania tu ndipo unapokuta raia wanafiki Kama wewe.hii timu ingekuwa ya Somalia pamoja na changamoto zote za kimaisha wanazopitia wangeungana kushangilia timu yao sio Kama hapa tz yaani watu ni wanafiki sijapata kuona!!!yaani wenzetu huko nje wanatushangaa Sana wanashindwa kuelewa sisi ni binadamu wa aina gani.

Mkuu kwa hili nakubaliana na wewe. Kulikuwako na vikosi zaidi ya hiki cha Senegal, Nani alidhani Zambia wangeshinda dhidi ya Kikosi kile cha Ivory Coast na Kuchukua Ubingwa?
 
Back
Top Bottom