joto la jiwe
JF-Expert Member
- Sep 4, 2017
- 26,117
- 46,617
Japo watu wengi husema mpira ni dakika 90, au mpira unadunda, lakini kuilinganisha Taifa stars na Senegal, ni ngumu sana kukubaliana na Maneno hayo.
Bahati mbaya sana, mashindano ya mpira sio kama ngumi, ambapo hawawezi kushindanisha bondia wenye uzito tofauti, kitendo cha kushindanisha Senegal ambayo ipo nafasi ya 22 duniani, na Tanzania nafasi ya 131 na kutegemea matokeo tofauti, ni lazima mtu awe na moyo wa mwendawazimu.
Yote kwa yote " Ukikubali kuolewa, pia ukubali kula bila nguo". Kila la kheri Taifa stars, tupo nyuma yenu, lolote litakalotokea, tumeshajiandaa kisaikolojia.
Bahati mbaya sana, mashindano ya mpira sio kama ngumi, ambapo hawawezi kushindanisha bondia wenye uzito tofauti, kitendo cha kushindanisha Senegal ambayo ipo nafasi ya 22 duniani, na Tanzania nafasi ya 131 na kutegemea matokeo tofauti, ni lazima mtu awe na moyo wa mwendawazimu.
Yote kwa yote " Ukikubali kuolewa, pia ukubali kula bila nguo". Kila la kheri Taifa stars, tupo nyuma yenu, lolote litakalotokea, tumeshajiandaa kisaikolojia.