Kila mauaji hushuhudiwa na macho matano

Kila mauaji hushuhudiwa na macho matano

Upo Sahihi kabisa kaka mkuu kuna Channel moja naiangaliaga naipenda sana kwa ina jihusisha na mambo ya upelelezi yaan kusample zinachukuliwa hapo kwenye eneo la tukio mpk unajiuliza hiki ni nini sasa? Hata upigaji picha wanapiga kila details
Kwa wenzetu waliotutangulia kuona mbali macho yote matano kila moja huwa na wataalam wake rasmi tena wabobezi.. Mchanga/udongo kidogo tu usioendana na na ule wa eneo husika huwa ni break through kubwa sana
Leso iliyosahaulika, nyayo za viatu, kichungi cha sigara, alama za vidole nknk.. Ni clues muhimu sana kwenye kupata ukweli

Jr[emoji769]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huenda kukawa na uhusiano kati ya macho matano na ,,,,,,,,,, ya tano ya mamlaka
 
Ni jicho moja lililobeba macho yote hayo hivi ni kweli na huku kwetu tunatumia haya macho sidhani
Tunamaliza mwaka 2019 na taharuki za kutisha na kutosha. Kwa akili za wastani ni rahisi sana kuwanyooshea vidole wengine lakini kiroho tafsiri ni kubwa kuliko hilo.

Mojawapo ya 'case sensitive ' kwa binadamu ni kifo cha mauaji. Kifo cha dhamira. Hivi huacha fadhaa na maswali mengi yasiyo na majibu kwa wengi. Kifo cha mauaji ya dhamira huwa ni jambo la siri kubwa. Hivyo usipokuwa mahiri kwenye uchunguzi utaishia kufeli.

Wenzetu waliotutangulia kufikiri waliamua kuachana na dhana za kifo ni kazi ya Mungu... Wakiamini kabisa kila kifo cha mauaji ya dhamira hupangwa na kuna macho matano huona... Ni katika hayo macho matano utata wa mauaji husika hutatuliwa..

Ukiachana na macho ya BINADAMU, vitu navyo vina macho lakini yasiyoonekana
Majengo yana macho
Muda una macho/ mawasiliano
Silaha zina macho
Vyombo na mitambo na machine vina macho
Barabara zina macho
Mapori, maji milima mabonde misitu nknk... Kila kitu kina macho...

Vifo vya mauaji ya dhamira ya kupangwa huwa na macho muhimu matano
1. Macho ya eneo mauaji yalipofanyika.
2.silaha zilizotumika
3. Muda /mawasiliano
4.Muuaji/wauaji
5. Muuliwa/ Mhanga
Mipango mingi ya mauaji hupangwa na binadamu asiye mkamilifu... Hivyo kwa asilimia 95 ni lazima ataacha kiashiria onwa ambacho kikitumika vizuri.. Kitafumbua fumbo la mauaji husika...

1. Eneo la mauaji yalipofanyika.. Tambua kwanini huzunguushiwa uzio maramoja... Hapa ni kwa ajili ya kulinda ushahidi.. Hapa hukusanywa kila kitu kidogo ambacho kiasili hakikupaswa kuwepo pale

2.silaha zilizotumika /iliyotumika ukiachana na vitu kama bunduki na sumu (ambavyo ni traceable) kuna visu kamba mikono nk. Wataalam huweza kukwambia kwa hakika hiyo ni silaha ya aina gani iliyotumika na mtumiaji ni mahiri ama la...

3.Muda husema mengi. Muda roho ilipoacha mwili. Mawasiliano ya mhanga na wauaji nknk

4. Muuaji/wauaji... Hawa hukamatika kufuatilia clued za japo juu na hii moja ya mwisho hapa chini

5.Muuliwa... Unajua kwanini wengi huuliwa kwa nyuma? Macho ya Muuliwa huhifadhi picha za matukio ya mwisho kabla ya kukata roho na ndio sababu wengi kutobolewa macho..

Kwa wenzetu waliotutangulia kufikiri wameongeza macho mengine kurahisisha ufanisi... Camera za siri na tracking devices zilizofichwa sehemu mbalimbali mpaka hata mwilini...

Mkurugenzi wa taasisi moja ya kidini na mmiliki wa shule amekutwa ofisini kwake akiwa kauliwa.. Kuna maswali muhimu ya kujiuliza

. Ofisini yuko peke yake? Ama wauaji walitegea akiwa pekeyake?
. Hana mawasiliano ya kawaida na watu wengine? Maana mwili uligunduliwa baada ya siku tano kupita...
. Hana marafiki wa kumtafuta walau kwa siku ambazo alikuwa haonekani?
. Hana familia? Kwamba baba leo jajarudi au kama imesafiri hakukuwa na mawasiliano kwa siku 5 mfululizo?
. Dhamira ya mauaji huwa ni jambo la muhimu pia.. Lakini pia wauaji mahiri hutumia historia na mazoea ya mtu kufanisha mauaji salama na kadiri muda unavyopita ndio baadhi ya yale macho matano hupoteza uwezo wake

Jr[emoji769]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mihimili mitano? [emoji848][emoji848][emoji144][emoji144][emoji144][emoji124][emoji124][emoji124]
Huenda kukawa na uhusiano kati ya macho matano na ,,,,,,,,,, ya tano ya mamlaka

Jr[emoji769]
 
Mihimili mitano? [emoji848][emoji848][emoji144][emoji144][emoji144][emoji124][emoji124][emoji124]

Hhhhhhhhhhhhaaaa,,,,,
Hhhhhhhhhhhaaaaaa,,,, sijasema Mimi.na si kwamba nafurahia Ila kuna payment time,uzuri dunia ni duara.
 
Mmmh [emoji848]
Uzuri ni kwamba, kwa maelezo ya mtoa mada, kuna macho mengi sana ambayo husaidia kufanikisha kukamatwa kwa muaji/wauaji, rpc muroto ametuambia jana kwamba eti marehemu alifariki baada ya moyo kushindwa kufanya kazi, anasahau kwamba mtu akikabwa koo moyo utakosa hewa na utasimama, kwa hiyo moyo kushindwa kufanya kazi haimaanishi kwamba mtu huyo amekufa mwenyewe kama ambavyo rpc alijaribu kutudanganya, kuna possibility kubwa kwamba aliuawa na wasiojulikana ambao sasa tumeanza kuwajua, maswali ya mtoa mada hapa juu ni ya muhimu sana kujibiwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yote umenena mkuu hapo kwenye kazi nyingine ndio patakuwa pamebeba yote japo hujasema.alamsiki....[emoji848]
Amani iwe ndugu zangu wa Jamii Forum.

Nimeisikiliza kwa Makini taarifa ya RPC wa Dodoma Ndugu Muroto juu ya Kifo cha Ndugu yetu Mpendwa Marehemu Sheikh Rashid Bura ambaye pia alikuwa Mkurugenzi wa The Dalai Islamic Centre.

Awali ya yote napenda Jamii ifahamu kuwa;

a/ Sheikh Rashid Bura alikuwa ni Rafiki yake na Kamanda Muroto.

b/ Sheikh Rashid Bura alikuwa ni Mmiliki wa ZAMZAM PRE & PRIMARY SCHOOL.

c/ Sheikh Rashid Bura alikuwa akijishughulisha na shughuli nyingine pia (Naiweka kapuni kwa Sasa) licha ya kuwa ni Mmiliki wa Shule.

Kamanda Muroto ameficha mengi juu ya Kifo cha Sheikh Rashid Bura. Hapa naomba nielezee utata uliopo juu ya Kifo chake.

UTATA.

1. SAFARI,
a/ Marehemu Sheikh Rashid Bura alisafiri kutoka Dodoma kwenda Dar es salaam siku ya Ijumaa Tarehe 20/12/2019 na siyo Tarehe 21/12/2019 kama alivyosema Kamanda Muroto. Tarehe 21/12/2019 ilikuwa ndiyo siku ya Kongamano / Mkutano huo wa Kidini. Katika Safari hiyo waliondoka watu wawili katika chombo kimoja cha usafiri.

b/ Tarehe 22 Marehemu alirudi Dodoma lakini akiwa amemuacha aliyeenda naye Safari huko Dar es salaam. Alipofika Dodoma alienda Kuswali katika MSIKITI wa NUNGE na baadae kuelekea Ofisini kwake.

NB: KWENYE TAREHE YA SAFARI KUNA JAMBO HALIPO SAWA.

2. MAWASILIANO,
Marehemu Sheikh Bura, aliwasiliana na Ndugu zake kwa njia ya Maongezi kwa mara ya Mwisho Jumamosi Usiku akiwa Dar es salaam. Baada ya hapo Simu za Ndugu zake hazikupokelewa tena na Meseji hazikujibiwa pia. Siku ya Jumapili Mawasiliano yaliyopatikana Pekee ni UJUMBE wa WHATSAPP ambao uliwapa taarifa Ndugu kuwa Amewasili Dodoma. Baada ya hapo hakukuwa na Mawasiliano tena.

NB: SHEIKH BURA HAKUWAHI KUTOPOKEA SIMU AU KUKOSEKANA HEWANI SIKU ZOTE AMBAZO AMEKUWA AKISAFIRI. KUTOPOKEA SIMU NA KUKOSEKANA KWAKE HEWANI KUMELETA MKANGANYIKO MKUBWA.

3. MAZINGIRA YA KUPATIKANA KWAKE,
Mazingira ya kupatikana kwa Sheikh Bura yana utata mwingi Sana,

a/ Sheikh Bura alipatikana Ofisini kwake siku ya tatu baada ya Mauti yake tena Mwili ukiwa umeanza kuharibika. Maswali ya kujiuliza,

i/ Je Ofisi yake haina Msaidizi wa Kazi ambaye angeweza kugundua kifo chake?

ii/ Je Ofisi za Jirani hawakuweza kusikia hata harufu ya kitu kinachotoa harufu kutoka Ofisini kwake?

b/ Polisi na Ndugu walipofika Ofisini kwake walikuta Mlango umefungwa na walipo uvunja na kuingia ndani walikuta mwili wa Marehemu LAKINI UFUNGUO HAUKUWEPO MLANGONI NA HATA NDANI PIA. Swali la kujiuliza, NI NANI ALIMFUNGIA SHEIKH BURA KWA NJE?

c/ Mwili wa Marehemu Sheikh Bura ulikutwa na Vazi lake la Kanzu lakini likiwa na Damu. Swali la kujiuliza, JE DAMU HII KWENYE KANZU YA MAREHEMU ILITOKA WAPI?

4. SIKU YA MAZISHI,
Siku ya Mazishi 26/12/2019 Mwili wa Marehemu Sheikh Bura ulitolewa Mochwari na kupelekwa Nyumbani kwake na Gari la Polisi na hata kutoka Nyumbani kwenda eneo la Mazishi (MAKABURI YA CHAMWINO / CHINANGALI) Mwili wake ulipelekwa na Gari la Polisi. Polisi pia walitoa basi lao kwa ajili ya kubeba wafiwa. Basi hili lilikwama Kwenye eneo karibu kabisa Ofisi ya Serikali ya Mtaa. Maswali ya Kujiuliza,

i/ Je ni utaratibu wa kawaida kwa Magari ya Jeshi la Polisi kubeba Mwili wa Marehemu mpaka Nyumbani na Eneo la Maziko?

ii/ Je ni utaratibu wa kawaida kwa Basi la Jeshi la Polisi kubeba wafiwa?

iii/ Uwepo wa Jeshi la Polisi kwenye eneo la tukio kulimaanisha nini?

Nawasilisha.

Sent using Jamii Forums mobile app

Jr[emoji769]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
.
DOCvbNnVAAAnje6.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom