Kila mauaji hushuhudiwa na macho matano

Kila mauaji hushuhudiwa na macho matano

Tunamaliza mwaka 2019 na taharuki za kutisha na kutosha. Kwa akili za wastani ni rahisi sana kuwanyooshea vidole wengine lakini kiroho tafsiri ni kubwa kuliko hilo.

Mojawapo ya 'case sensitive ' kwa binadamu ni kifo cha mauaji. Kifo cha dhamira. Hivi huacha fadhaa na maswali mengi yasiyo na majibu kwa wengi. Kifo cha mauaji ya dhamira huwa ni jambo la siri kubwa. Hivyo usipokuwa mahiri kwenye uchunguzi utaishia kufeli.

Wenzetu waliotutangulia kufikiri waliamua kuachana na dhana za kifo ni kazi ya Mungu... Wakiamini kabisa kila kifo cha mauaji ya dhamira hupangwa na kuna macho matano huona... Ni katika hayo macho matano utata wa mauaji husika hutatuliwa..

Ukiachana na macho ya BINADAMU, vitu navyo vina macho lakini yasiyoonekana
Majengo yana macho
Muda una macho/ mawasiliano
Silaha zina macho
Vyombo na mitambo na machine vina macho
Barabara zina macho
Mapori, maji milima mabonde misitu nknk... Kila kitu kina macho...

Vifo vya mauaji ya dhamira ya kupangwa huwa na macho muhimu matano
1. Macho ya eneo mauaji yalipofanyika.
2.silaha zilizotumika
3. Muda /mawasiliano
4.Muuaji/wauaji
5. Muuliwa/ Mhanga
Mipango mingi ya mauaji hupangwa na binadamu asiye mkamilifu... Hivyo kwa asilimia 95 ni lazima ataacha kiashiria onwa ambacho kikitumika vizuri.. Kitafumbua fumbo la mauaji husika...

1. Eneo la mauaji yalipofanyika.. Tambua kwanini huzunguushiwa uzio maramoja... Hapa ni kwa ajili ya kulinda ushahidi.. Hapa hukusanywa kila kitu kidogo ambacho kiasili hakikupaswa kuwepo pale

2.silaha zilizotumika /iliyotumika ukiachana na vitu kama bunduki na sumu (ambavyo ni traceable) kuna visu kamba mikono nk. Wataalam huweza kukwambia kwa hakika hiyo ni silaha ya aina gani iliyotumika na mtumiaji ni mahiri ama la...

3.Muda husema mengi. Muda roho ilipoacha mwili. Mawasiliano ya mhanga na wauaji nknk

4. Muuaji/wauaji... Hawa hukamatika kufuatilia clued za japo juu na hii moja ya mwisho hapa chini

5.Muuliwa... Unajua kwanini wengi huuliwa kwa nyuma? Macho ya Muuliwa huhifadhi picha za matukio ya mwisho kabla ya kukata roho na ndio sababu wengi kutobolewa macho..

Kwa wenzetu waliotutangulia kufikiri wameongeza macho mengine kurahisisha ufanisi... Camera za siri na tracking devices zilizofichwa sehemu mbalimbali mpaka hata mwilini...

Mkurugenzi wa taasisi moja ya kidini na mmiliki wa shule amekutwa ofisini kwake akiwa kauliwa.. Kuna maswali muhimu ya kujiuliza

. Ofisini yuko peke yake? Ama wauaji walitegea akiwa pekeyake?
. Hana mawasiliano ya kawaida na watu wengine? Maana mwili uligunduliwa baada ya siku tano kupita...
. Hana marafiki wa kumtafuta walau kwa siku ambazo alikuwa haonekani?
. Hana familia? Kwamba baba leo jajarudi au kama imesafiri hakukuwa na mawasiliano kwa siku 5 mfululizo?
. Dhamira ya mauaji huwa ni jambo la muhimu pia.. Lakini pia wauaji mahiri hutumia historia na mazoea ya mtu kufanisha mauaji salama na kadiri muda unavyopita ndio baadhi ya yale macho matano hupoteza uwezo wake

Jr[emoji769]

Hii kesi hapa chini huwa napenda kui-site. Inathibitisha ulichoandika hapa. Jani la mti lilidondoka kwenye cabin ya pick-up ya mtuhumiwa, na hilo ndiyo likawa mwanzo wa taarifa zote

 
Mkuu Mshana Jr kwanini wahangaike vyote hivyo si wangeteua tu kitengo maalum Cha watu wakaenda China ku_Open The Third Eye ingesaidia Sana katika mambo ya upelelezi maana hiyo nasikia mtu anaona na anasimulia tukio Kama alikuwepo vile. VP serikali haijaliona Hilo au haiamini haya mambo? Nazani ingesaidia zaidi
 
Mkuu Mshana Jr kwanini wahangaike vyote hivyo si wangeteua tu kitengo maalum Cha watu wakaenda China ku_Open The Third Eye ingesaidia Sana katika mambo ya upelelezi maana hiyo nasikia mtu anaona na anasimulia tukio Kama alikuwepo vile. VP serikali haijaliona Hilo au haiamini haya mambo? Nazani ingesaidia zaidi
Vitengo vyote ni muhimu sana na vingine ni kama backup...BTW kutrain 3rd eye kwa intelligence service ni gharama mno ndio maana wazungu wameamua kufanyya human cloning
 
Mahakamani Kuu Kanda ya Iringa ambayo imefanya kikao mkoani Njombe imemuhukumu kunyongwa hadi kufa aliyekuwa Katekista wa Kanisa katoliki jimbo la Makambako Daniel Philipo Mwelango mwenye umri wa miaka 43 kwa kosa la mauaji baada ya kukutwa na hatia.

Mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Februari 8, 2022 kwa kumuua Daniel Elias Myamba mwenye umri wa miaka 43 mkazi wa mtaa wa Kahawa Makambako kesi Na MC 74/2022 katika mtaa wa Bwawani mjini Makamabako.

Hukumu hiyo imetolewa mbele ya Jaji Mhe. Said Kalunde.

Akisoma hukumu hiyo Jaji wa Mahakama kuu Kanda ya Iringa amesema Mahakama imefikia uamuzi huo baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa pasipo shaka yoyote kwamba mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo.

Jaji Kalunde amesema siku ya tukio mshitakiwa alifanya maandalizi kwa kuandaa Panga,Chuma pamoja na mifuko minne ya Kinga njaa,mifuko miwili ilikuwa kwa ajili ya kuzuia damu isisambe na miwili mingine kwa ajili kuhifadhi mwili wa marehemu.

Baada ya hapo akampiga na chuma kwenye kisogo baada ya kuona ameanguka chini na kufariki alimkata vipande viwili na kuvipaki katika mifuko ya kinganjaa ili iwe rahisi kubeba mwili huo na kwenda kuutupa mbali,baada ya kuona mke wa marehemu anapiga simu mara kwa mara kwenye simu ya Maherehemu pamoja mwenyekiti wa kigango alishindwa kuubeba mwili huo na kuamua kuondoka huku akiwa amelibeba panga na kwenda kulitumbukiza katika shimo la choo cha shule ya msingi Makambako na chuma alichotumia kumpiga nacho alikificha kwenye gata karibu na duka na yeye kutorokea Dar es Saalam.
 
Tunamaliza mwaka 2019 na taharuki za kutisha na kutosha. Kwa akili za wastani ni rahisi sana kuwanyooshea vidole wengine lakini kiroho tafsiri ni kubwa kuliko hilo.

Mojawapo ya 'case sensitive ' kwa binadamu ni kifo cha mauaji. Kifo cha dhamira. Hivi huacha fadhaa na maswali mengi yasiyo na majibu kwa wengi. Kifo cha mauaji ya dhamira huwa ni jambo la siri kubwa. Hivyo usipokuwa mahiri kwenye uchunguzi utaishia kufeli.

Wenzetu waliotutangulia kufikiri waliamua kuachana na dhana za kifo ni kazi ya Mungu... Wakiamini kabisa kila kifo cha mauaji ya dhamira hupangwa na kuna macho matano huona... Ni katika hayo macho matano utata wa mauaji husika hutatuliwa..

Ukiachana na macho ya BINADAMU, vitu navyo vina macho lakini yasiyoonekana
Majengo yana macho
Muda una macho/ mawasiliano
Silaha zina macho
Vyombo na mitambo na machine vina macho
Barabara zina macho
Mapori, maji milima mabonde misitu nknk... Kila kitu kina macho...

Vifo vya mauaji ya dhamira ya kupangwa huwa na macho muhimu matano
1. Macho ya eneo mauaji yalipofanyika.
2.silaha zilizotumika
3. Muda /mawasiliano
4.Muuaji/wauaji
5. Muuliwa/ Mhanga
Mipango mingi ya mauaji hupangwa na binadamu asiye mkamilifu... Hivyo kwa asilimia 95 ni lazima ataacha kiashiria onwa ambacho kikitumika vizuri.. Kitafumbua fumbo la mauaji husika...

1. Eneo la mauaji yalipofanyika.. Tambua kwanini huzunguushiwa uzio maramoja... Hapa ni kwa ajili ya kulinda ushahidi.. Hapa hukusanywa kila kitu kidogo ambacho kiasili hakikupaswa kuwepo pale

2.silaha zilizotumika /iliyotumika ukiachana na vitu kama bunduki na sumu (ambavyo ni traceable) kuna visu kamba mikono nk. Wataalam huweza kukwambia kwa hakika hiyo ni silaha ya aina gani iliyotumika na mtumiaji ni mahiri ama la...

3.Muda husema mengi. Muda roho ilipoacha mwili. Mawasiliano ya mhanga na wauaji nknk

4. Muuaji/wauaji... Hawa hukamatika kufuatilia clued za japo juu na hii moja ya mwisho hapa chini

5.Muuliwa... Unajua kwanini wengi huuliwa kwa nyuma? Macho ya Muuliwa huhifadhi picha za matukio ya mwisho kabla ya kukata roho na ndio sababu wengi kutobolewa macho..

Kwa wenzetu waliotutangulia kufikiri wameongeza macho mengine kurahisisha ufanisi... Camera za siri na tracking devices zilizofichwa sehemu mbalimbali mpaka hata mwilini...

Mkurugenzi wa taasisi moja ya kidini na mmiliki wa shule amekutwa ofisini kwake akiwa kauliwa.. Kuna maswali muhimu ya kujiuliza

. Ofisini yuko peke yake? Ama wauaji walitegea akiwa pekeyake?
. Hana mawasiliano ya kawaida na watu wengine? Maana mwili uligunduliwa baada ya siku tano kupita...
. Hana marafiki wa kumtafuta walau kwa siku ambazo alikuwa haonekani?
. Hana familia? Kwamba baba leo jajarudi au kama imesafiri hakukuwa na mawasiliano kwa siku 5 mfululizo?
. Dhamira ya mauaji huwa ni jambo la muhimu pia.. Lakini pia wauaji mahiri hutumia historia na mazoea ya mtu kufanisha mauaji salama na kadiri muda unavyopita ndio baadhi ya yale macho matano hupoteza uwezo wake

Jr[emoji769]
ASANTE KWA SOMO NAAMINI KAMA BEN SAANANE ALIUAWA IPO SIKU MACHO 5 YALIYOSHUHUDIA YATAONYESHA WAUAJI WAKE

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
 
mbaya zaidi ukute haina hatia. Inanuka kama ya habili.

Damu ya mtu hunuka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom