Jumatatu machi 25, 2013,
lazima tuionyeshe serikali ya chama cha mapinduzi kuwa imeshindwa
kusimamia elimu yetu na sisi kama wananchi hatuko tayari kuona kizazi
cha waliokosa elimu bora kinazalishwa.
Watoto wetu zaidi ya asilimia 90 wamefeli. Elimu inayotolewa madarasani
ni mbovu, mitaala mibovu au hakuna kabisa. Hakuna mipango yeyote ya
kuimarisha elimu.
Waalimu wamesahauliwa na kuachwa kwenye mazingira magumu na
kuwasababisha msongo wa mawazo hivyo kukosa mori na ari ya kufundisha.
Waalimu wanadaharaulika na serikali kuwaona kama hawana kazi muhimu
kwenye taifa letu.
Fedha za vitabu zinaliwa na wajanja wachache na hakuna wa kuwajibika.
Madahara ya watoto kufeli yameanza miaka mingi na wengi tayari wako
mitaani wakiwa hawana la kufanya.
Tuandamane kwa amani, lazima tujue umuhimu wa kuandamana , serikali zote
za kidikteta duniani huongoza kwa nguvu na huwajibishwa kwa nguvu,
mazungumzo ya amani kwao ni kama kumsemesha chizi. Kilio cha wananchi
kwao ni maji ya kisima hawaoni matatizo yao. Kwao kila mwenye manufaa
nao ndio wakwao.
Wananchi wote wenye kuelewa na kuona madhara ya elimu yetu, kina mama na
baba ambao watoto wetu wamefeli baada ya kujitoa kwa miaka zaidi 10
ttwendeni barabarani kuonyesha serikali hatukubali kuona na wadogo za
hawa hawafeli tena.
Tunao watoto sasa mashuleni, kuanzia darasa la kwanza je tupo tayari
kuwaona nao wanafeli???
Jumatatu Nguvu ya umma lazima iongee, sisi ni wengi kuliko majeshi sisi
tunasauti kubwa kwani wananchi ndio wamiliki wa nchi yao.
Kila kanda lazima watoke kwa wingi, kila mwananchi lazima aone umuhimu
wa kuilazimisha serikali kutoa kipaumbele kwenye elimu.
Tukiwa na mitaala bora na elimu bora, tutakuwa na wataalamu wetu,
wabunifu, wajasiriamali wasomi, wagunduzi, nk.
Haya sime tushikamane kwa hili, mpigia baba, mama, dada, binamu nk simu
mwambie ukombozi wa elimu yetu upo mikononi mwetu. Bila kujali itikadi,
elimu inatuadhiri wote.
Chief Mkwawa
Elimu ni bora kuliko siasa.