Kila Mtanzania mwenye uchungu na elimu yetu aandamane Machi 25, 2013

mkuu mbona wewe mwenyewe unaonekana kama ulifeli?? maana hata kuandika neno feli hujajua hadi leo hii, hebu angalia neno argument wewe umeandika vipi? Rudi darasani maandamano hayatakusaidia

Huu ndo upofu na ukiziwi wa wakuu wenu wa serikali, badala ya kuangalia maudhui ya taarifa au maoni unaangalia spelling na matamshi kama ndivyo wamasai na wengi wengineo amabao matamshi kwa asili wengi hayaendi sawia na kiswahili au hiyo english, usingeelewana nao. Huu ni ukilaza tena wa hali ya juu. Unaonesha huna cha kujadili bali mzembe flani vile.

wale wazungu wako wanakuja pale UDsm kutoka Germany au Portugal na English fyongo huwa wamefeli eti? na hawana elimu? unaakili za ovyo kama kawambwa. nini hujaelewa?
 

we hujamuelewa. mie nimemsoma sana. kila mzazi anajijua kwa nini mtoto wake amefeli. na kila aliyefeli anajijua kuwa kwa nini amefeli. si issue ya kukaa na kuilaumu serikali
 
Safi sana Wamogori nimeipenda sana comment yako..fateni hii na sio kurumbana jamani humu tuna elimishana na sio kutupiana maneno.
 

mkuu na sisi tuliofeli kutokana na upumbavu wetu wa kuchora akina zombi na messi tuandamane?
 

Kiongozi

1. Hizi internet na mitandao, masimu nk vipo tanzania pekee kenya hakuna? kama kenya pia vipo tuambie kwanini hakuna 90% failure huko kwa wakenya?

2. Wakenya walizua mgogoro kati ya walimu na serikali kuhusu maslahi bora kwa walimu na serikali ilikaa na walimu wakatatua. Je serikali yako ya Tanzania imekaa na kutatua madai ya walimu kuhusu kuboresha maslahi yao? kama hapana unadhani walimu wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi? kama hapana kwanini watoto wasifeli?

Ni hayo tu kiongozi.
 
mkuu na sisi tuliofeli kutokana na upumbavu wetu wa kuchora akina zombi na messi tuandamane?

Ndiyo unatakiwa kuandama tena uwe mstari wa mbele.

Sababu ni kwamba usipofanya hivyo wadogo zako, ndugu zako, jirani zako na baadaye watoto wakuzaa wewe mwenyewe watafeli endapo hatutashinikiza mabadiliko ya sera ya elimu na uwajibikaji ili kuwandallia wanao mazingira mazuri wasijefedheheka kama wewe.
 
Mie nina uchungu lkn kuandamana mhhh?!Sidhani ni njia sahihi.Njia sahihi ni kupambana kumuondoa mkoloni anayekalia elimu yetu

me nadhani walioandaa maandamano hawakuwa na muda wa kujipanga na kuona ni nini na wapi tusimamie.kuna swali dogo tu mtu mwenye busara atajiuliza,tunaandamana waziri ajiuzulu,je akijiuzulu ndio wanafunzi watafaulu?jamani ni bora muda huu tunaotumia kuhamasisha fujo tungeutumia kutoa elimu kwa jamii itambue kuwa chanzo cha matatizo yote haya ni mifumo mibovu ya serikali ya ccm so solution ni kuiondoa madarakani.maandamano na fujo za kipuuzi vitawafanya wenye busara zao kuamini propaganda mbovu kuwa cdm ni chama cha vurugu na wanaharakati wasiokuwa na sifa ya kuongoza dola.
 
we hujamuelewa. mie nimemsoma sana. kila mzazi anajijua kwa nini mtoto wake amefeli. na kila aliyefeli anajijua kuwa kwa nini amefeli. si issue ya kukaa na kuilaumu serikali

Unafahamu kwanini elimu ni lazima kuliko chochote kile katika uhai wa mwanadamu?

Unafahamu kwanini Nyerere alibinafsisha mashule ya taasisi za dini?

Unafahamu ili taifa lisonge mbele linahitaji nini? na kwanini?

Unazifaha haki za msingi ambazo serikali lazima itekeleze kwa raia wake? unaweza kuzitaja?

Kama tutaendela na 70%.......kufelisha watoto madaktari, wahandisi wananga nk watatoka wapi? china eti?

Watanzania suala la elimu ni nyeti halihitaji majibu laini laini maana mwisho wa siku tutaliangamiza Taifa letu.
 
Wakati Mbowe anapata zero pia sera ya elimu ilikuwa mbovu?


wakati ni sasa. Ya mbowe hayatuhusu, ya kipindi icho ilikuwa ni kwa kizazi husika. Hiki ni kizazi kingne mkuu.

Kufeli kwa mbowe hakujustfy failure ya wizara na wasimamizi wake kwa wakati huu mkuu.
 


jamaa anataka kututoa kwenye mada. Analeta ushabiki
 
kama kawaida yao wameshatangaza kuwa maandamano hayaruhusiwi.
Hata kama watazuia maandamano, ila wajue mwakani watafeli kwa 80% endapo wataendelea kutoa sababu za kufeli za ajabu kama walizotoa juzi.
  • 2010 waliofeli ilikuwa 20% (Tume iliundwa na majibu yalitolewa)
  • 2011 waliofeli ilikuwa 40%
  • 2012 waliofeli ilikuwa 60%

Kulikuwa na haja ya kuwa na Tume tena.

Kwa aliyeona madodoso ya tume ya Pinda, anajua kuwa serikali haijadhamiria kutatua tatizo la wanafunzi kufanya vibaya kwa sababu madodoso yale yanalazimisha mtu akubaliane na sababu walizonazo wao na si sababu anazohisi mtu.

Kwan upungufu wa vitabu umeanza leo?Tangu zamani tatizo la vitabu lilikuwepo ila walimu ndio waliokuwa na moyo wa kufundisha na ndio waliotufanya tufanye vizuri.
 
Issue ni kufeli, ambapo na yeyd Mbowe yupo kwenye kundi la waliozunguka round about.

Hata ukieleweshwa mpaka mtondogoo hutaelewa maana umejiandaa kupinga tu. Pole maandamano 25th march
 



mkuu km huhusiki kuandamana, tuachie tunaohusika. Story zako peleka lumumba
 
NIPO MBEYA.
NITAKUWA MSTARI WA MBELE.
Hatuwezi kuwaruhusu wachina wawekeze, wakati tunazarisha mamburura mashuleni.
TUKOSE HATA KIBARUA CHA KUCHANGANYA KOKOTO?
Tutaandamana.
 
Yap ni zaidi ya zero. Naona mwenzangu ni chini ya zero.

Mimi nawashangaa wanajibizana na wewe kwa sababu hata username yako inajionyesha jinsi ulivyo.Wenzangu wa Iringa wanajua MABOSO ni nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…