Kila mtu kutaka kuwa Mwanasiasa ni dalili ya Taifa masikini lililokosa mwelekeo

Kila mtu kutaka kuwa Mwanasiasa ni dalili ya Taifa masikini lililokosa mwelekeo

Fumadilu Kalimanzila

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2016
Posts
1,770
Reaction score
5,423
Kwa muda mrefu nimekuwa nikijua kuwa dalili mojawapo ya Taifa masikini ni kuwa na wakulima wengi!
Tanzania ina wakulima kati ya 65% hadi 80% katika population ya watu milioni 60, hivyo hili ni Taifa masikini sana!
Marekani yenye watu zaidi ya milioni 300 ina wakulima wasiozidi asilimia 10%.

Kitu ambacho nimekigundua na ndo msingi wa mada yangu ni kwamba kiashiria kingine cha Umasikini wa Taifa ni pale kila mtu anapotaka kuwa mwanasiasa.

Leo katika Taifa letu kila mtu anataka kuwa mwanasiasa kuanzia matapeli, waganga wa kienyeji, wafanyabiashara,wasomi hadi maprofesa, vila.za na wengine wengi ambao hawana hata sifa za uongozi.

Ukichunguza kwa makini hata quality ya mijadala katika Bunge letu inadhihirisha kuwa wengi walioko Bungeni wako kimaslahi binafsi zaidi.

Hoja hazijengwi tena katika namna bora ya kupata majawabu ya changamoto mbalimbali za wananchi bali ni kuangalia mtoa hoja ni nani na zaidi afanyiwe " character assassination " basi!
( Rejea idadi ya waliojitokeza katika kura za maoni za CCM 2020 kuomba kuteuliwa kuwa wagombea ubunge katika majimbo mbalimbali).

Kinachowasukuma wengi ni maslahi ya kibunge ambayo hayazidi "in totality" milioni 15 kwa mwezi sawa na kama dola za marekani $6,452 kwa mwezi au dola za marekani $ 215 kwa siku ( Exchange rate: USDTZS = 2325).

Mtu mwenye hadhi ya Uprofesa kukimbilia mapato ya dola za marekani $ 215 kwa siku ni uwezo mdogo wa kufikiri na kwa mtazamo wangu watu wa model hiyo hawawezi kulikomboa Taifa hili!

Kingine ni kwamba maeneo mengine ya uzalishaji kama vile kilimo ,biashara yamevurugwa na watu hawa wenye maarifa na upeo mdogo lakini wapenda uongozi.

Unakuta Mkuu wa Mkoa anasema publicly kuwa hawezi kufuata sheria na taratibu katika manunuzi ya Serikali na anaagiza mtaalamu wa manunuzi akae pembeni mpaka ujenzi utakapokamilika.Sasa sijui nani atajibu hoja za ukaguzi pale ubadhirifu utakaponyika.

Mbunge wa Mtama Mhe.Nape Nnauye anapata wasiwasi na deni la Taifa na anataka ukaguzi tujue kiasi tulichokopa na kama zimeenda zote katika miradi iliyokusudiwa lakini Waziri wa Fedha Dr.Mwigulu Nchemba anatoa majibu kama vile deni la Taifa atalilipa yeye na familia yake!

Wabunge wengine wametoa macho kumzodoa mtoa hoja na kumhusisha na mambo ya ajabu ajabu kama vile chuki kwa uongozi wa awamu ya tano chini ya Rais Magufuli n.k.

Wabunge hawa watashtuka pale Serikali itakapowambia hakuna pesa za kulipa mishahara na marupurupu yao au wapunguziwe.

Ni dhahiri tuko hoi bin taabani kama Taifa, kama tunakusanya kwa mwezi 1.5 trillion na Bilioni 800 zinakwenda kila mwezi ku- service mikopo na tunabakiwa na bilioni 700 na ukitoa wage bill ( mishahara ya watumushi) kama bilioni 600 tunabakiwa na bilioni 100!!!!

Sisi ni masikini wa kutupwa! Taifa kubwa lenye rasilimali nyingi lakini halina uongozi wenye vision!

Umasikini wetu umejidhihirisha kwenye tu hela hutu Rais Samia amekopa kutoka IMF kukabili athari za COVID-19,kila kiongozi "amepagawa" ,huyu anasema hili ,huyu anasema lile!

Kama Taifa tunahitaji kuwa serious na kutafuta viongozi serious wenye maarifa wanaoweza kutukwamua hapa tulipo na si blah blah hizi!
 
Tatizo wenye uwezo wengi hawapati nafasi na wanaopata wengi hawana uwezo(vilaza)

Sheria zetu pia ni kikwazo(hapa umuhimu wa katiba mpya ndipo unapoonekana).

Nchi iliyoserious haiwezi kuokota mtu anayejua kusoma na kuandika tu akawe mbunge mkuu wa wilaya au mkoa.

Huyu bungeni ataweza kweli kuchambua sheria na mikataba mbalimbali ya taifa na kimataifa?

Mtu kama msukuma sijui lusinde babu tale hawakupaswa kuwapo bungeni kwa nchi iliyo serious.

Kibaya zaidi watu wengi wasio na uwezo wanaojua kujipendekeza vizuri na kulamba miguu ya wenye vyeo ndo wanaopata nafasi mbalimbali za uongozi.

Tuna safari ndefu sana.
 
Umeongea kwa uchungu Sana mkuu na umetoa facts tupu.

Hasa ulipogusia mijadala isiyo na afya kwa taifa ya bungeni. Nilidhanj ni Mimi tu ndiyo nakwazika. Inatia kinyaa kuwasikiliza mazuzu hawa walioko bungeni.
 
Natoa wito wasomi wote ingieni kwenye siasa..shida siasa ya nchi hii wasomi wachache vilaza ndio wengi..mwisho wasiku msomi huwezi kuwashinda man vilaza ndio wapiga kelele.

Kisha baada ya kujaa kila ngazi ya maamuzi kuanzia serikali za mitaa hadi bungeni..tuhakikishe tunabadili mfumo..

Vinginevyo vilaza wataimaliza hii nchi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kwa muda mrefu nimekuwa nikijua kuwa dalili mojawapo ya Taifa masikini ni kuwa na wakulima wengi!
Tanzania ina wakulima kati ya 65% hadi 80% katika population ya watu milioni 60, hivyo hili ni Taifa masikini sana!
Marekani yenye watu zaidi ya milioni 300 ina wakulima wasiozidi asilimia 10%.

Kitu ambacho nimekigundua na ndo msingi wa mada yangu ni kwamba kiashiria kingine cha Umasikini wa Taifa ni pale kila mtu anapotaka kuwa mwanasiasa.

Leo katika Taifa letu kila mtu anataka kuwa mwanasiasa kuanzia matapeli, waganga wa kienyeji, wafanyabiashara,wasomi hadi maprofesa, vila.za na wengine wengi ambao hawana hata sifa za uongozi.

Ukichunguza kwa makini hata quality ya mijadala katika Bunge letu inadhihirisha kuwa wengi walioko Bungeni wako kimaslahi binafsi zaidi.

Hoja hazijengwi tena katika namna bora ya kupata majawabu ya changamoto mbalimbali za wananchi bali ni kuangalia mtoa hoja ni nani na zaidi afanyiwe " character assassination " basi!
( Rejea idadi ya waliojitokeza katika kura za maoni za CCM 2020 kuomba kuteuliwa kuwa wagombea ubunge katika majimbo mbalimbali).

Kinachowasukuma wengi ni maslahi ya kibunge ambayo hayazidi "in totality" milioni 15 kwa mwezi sawa na kama dola za marekani $6,452 kwa mwezi au dola za marekani $ 215 kwa siku ( Exchange rate: USDTZS = 2325).

Mtu mwenye hadhi ya Uprofesa kukimbilia mapato ya dola za marekani $ 215 kwa siku ni uwezo mdogo wa kufikiri na kwa mtazamo wangu watu wa model hiyo hawawezi kulikomboa Taifa hili!

Kingine ni kwamba maeneo mengine ya uzalishaji kama vile kilimo ,biashara yamevurugwa na watu hawa wenye maarifa na upeo mdogo lakini wapenda uongozi.

Unakuta Mkuu wa Mkoa anasema publicly kuwa hawezi kufuata sheria na taratibu katika manunuzi ya Serikali na anaagiza mtaalamu wa manunuzi akae pembeni mpaka ujenzi utakapokamilika.Sasa sijui nani atajibu hoja za ukaguzi pale ubadhirifu utakaponyika.

Mbunge wa Mtama Mhe.Nape Nnauye anapata wasiwasi na deni la Taifa na anataka ukaguzi tujue kiasi tulichokopa na kama zimeenda zote katika miradi iliyokusudiwa lakini Waziri wa Fedha Dr.Mwigulu Nchemba anatoa majibu kama vile deni la Taifa atalilipa yeye na familia yake!

Wabunge wengine wametoa macho kumzodoa mtoa hoja na kumhusisha na mambo ya ajabu ajabu kama vile chuki kwa uongozi wa awamu ya tano chini ya Rais Magufuli n.k.

Wabunge hawa watashtuka pale Serikali itakapowambia hakuna pesa za kulipa mishahara na marupurupu yao au wapunguziwe.

Ni dhahiri tuko hoi bin taabani kama Taifa, kama tunakusanya kwa mwezi 1.5 trillion na Bilioni 800 zinakwenda kila mwezi ku- service mikopo na tunabakiwa na bilioni 700 na ukitoa wage bill ( mishahara ya watumushi) kama bilioni 600 tunabakiwa na bilioni 100!!!!

Sisi ni masikini wa kutupwa! Taifa kubwa lenye rasilimali nyingi lakini halina uongozi wenye vision!

Umasikini wetu umejidhihirisha kwenye tu hela hutu Rais Samia amekopa kutoka IMF kukabili athari za COVID-19,kila kiongozi "amepagawa" ,huyu anasema hili ,huyu anasema lile!

Kama Taifa tunahitaji kuwa serious na kutafuta viongozi serious wenye maarifa wanaoweza kutukwamua hapa tulipo na si blah blah hizi!
Mkuu hoja zako hazina mashiko hata kidogo.....nasema hivyo kwani kiashiria Moja wapo Cha Nchi kuwa na Amani na mshikamano ni UJAMAA .

Kilimo ni kiashiria Cha umoja Hivyo asilimia 80% ya watanzania wanadumisha umoja na mshikamano Kupitia Kilimo,Nchi yetu ina Amani na Mshikamano ndo maana Watanzania Mimi na wewe na wazee wetu Nchi nzima tumelelewa na kukuwa Kupitia Kilimo hata Nchi kama China,Vyetinamu,ufilipino zimeendelea kwa watu wake kuwekeza katika Kilimo

Kuhusu watu kuwa wanasiasa ni sahihi Kwa sababu maisha ni siasa na mie nawaunga mkono kwani wasipofanya wao watafànyiwa na kuamuliwa mstakabari wa Maisha yào...kwa hoja yako naijumuisha kwa kusema Watanzania wanadumisha MAISHA NA UJAMAA yaani SIASA NA KILIMO.

USIWALAZIMISHE WATANZANIA WAFUATE MIFUMO WASIYOIJUA YÀ KIGENI ITASUMBUA WATU WETU...... AHSANTE
 
Mkuu hoja zako hazina mashiko hata kidogo.....nasema hivyo kwani kiashiria Moja wapo Cha Nchi kuwa na Amani na mshikamano ni UJAMAA .

Kilimo ni kiashiria Cha umoja Hivyo asilimia 80% ya watanzania wanadumisha umoja na mshikamano Kupitia Kilimo,Nchi yetu ina Amani na Mshikamano ndo maana Watanzania Mimi na wewe na wazee wetu Nchi nzima tumelelewa na kukuwa Kupitia Kilimo hata Nchi kama China,Vyetinamu,ufilipino zimeendelea kwa watu wake kuwekeza katika Kilimo

Kuhusu watu kuwa wanasiasa ni sahihi Kwa sababu maisha ni siasa na mie nawaunga mkono kwani wasipofanya wao watafànyiwa na kuamuliwa mstakabari wa Maisha yào...kwa hoja yako naijumuisha kwa kusema Watanzania wanadumisha MAISHA NA UJAMAA yaani SIASA NA KILIMO.

USIWALAZIMISHE WATANZANIA WAFUATE MIFUMO WASIYOIJUA YÀ KIGENI ITASUMBUA WATU WETU...... AHSANTE
pumba
 
Mkuu hoja zako hazina mashiko hata kidogo.....nasema hivyo kwani kiashiria Moja wapo Cha Nchi kuwa na Amani na mshikamano ni UJAMAA .

Kilimo ni kiashiria Cha umoja Hivyo asilimia 80% ya watanzania wanadumisha umoja na mshikamano Kupitia Kilimo,Nchi yetu ina Amani na Mshikamano ndo maana Watanzania Mimi na wewe na wazee wetu Nchi nzima tumelelewa na kukuwa Kupitia Kilimo hata Nchi kama China,Vyetinamu,ufilipino zimeendelea kwa watu wake kuwekeza katika Kilimo

Kuhusu watu kuwa wanasiasa ni sahihi Kwa sababu maisha ni siasa na mie nawaunga mkono kwani wasipofanya wao watafànyiwa na kuamuliwa mstakabari wa Maisha yào...kwa hoja yako naijumuisha kwa kusema Watanzania wanadumisha MAISHA NA UJAMAA yaani SIASA NA KILIMO.

USIWALAZIMISHE WATANZANIA WAFUATE MIFUMO WASIYOIJUA YÀ KIGENI ITASUMBUA WATU WETU...... AHSANTE
Upuuzi wa kiwango cha SGR
 
Back
Top Bottom