round kick
JF-Expert Member
- Feb 3, 2025
- 345
- 1,145
Kurogwa ni shambulio la kiroho kwa kutumia nguvu za giza, waweza kujilinda kwa njia kadhaa ikiwemo ya uhakika ulinzi wa Mwenyezi Mungu,
Vita ya Mababii na mitume dhidi ya shetani ilikuwa ya kiroho, Shetani hupendelea zaidi kutumia majaribu ya kuingiza tamaa na nguvu za giza kuroga, anaposhindwa vita ya kiroho huwa ni aibu sana kwake, anabaki kusubiri kwa aibu manabii na mitume washambuliwe kimwili aidha kwa kupigwa mpaka mauti, kufungwa jela, kusulubiwa, n.k.
Jinsi Mtume Mohammad alivyopigwa kipapai
Hadithi Maarufu katika Sahih al-Bukhari (5765) na Sahih Muslim (2189) inasimulia kuwa kuna mchawi aliweza kumpiga kipapai (kumroga) Mtume Muhammad kwa kutumia nywele zake na kitana, kisha akaviweka katika kisima, alimtupia uchawi wa kumvuruga akili. Muhammad alipitia kipindi kigumu sana.
Mtume alikuwa katika hali ya kufikiri kafanya mambo fulani lakini kwa hakika hakuwa amefanya, Alipata msongo wa mawazo na hali ya kuchanganyikiwa, Alikuwa na afya njema kimwili lakini alikuwa na mzigo wa kiakili. Ni mpaka baadae aliweza kupona kama ilivyo kwa watu wengine wanaorogwa wakifanya maombo na kupiga sala.
Kwa Upande wa kina Musa tumeshaona mengi sana, kundi la wachawi wakubwa kutoka Misiri walitaka kumjaribu lakini akawaonyesha yeye ni levels nyingine ana kipawa kikubwa zaidi kutoka kwa Mungu, fimbo yake ilipogeuka kuwa nyoka ilimeza wale nyoka wote wa wachawi.
Tukija kwa Yesu hizo ni levels nyingine kabisa, Shetani hakutumia wachawi alienda mwenyewe direc, Alimjaribu kwa kila kitu lakini hakufua dafu, vita ya kiroho dhidi ya Yesu ilimfedhehesha vibaya mno.
Nampa heshima zote Mtume Mohammad kwasababu anazistahili lakini apewe heshima kulingana na hali yake, sio sawa anavyotukuzwa kupitiliza