Kila nikijaribu kumsamehe/kuwasamehe nashindwa

Mkuu David Harley

Unaonaje ukiianzishia uzi wake baada ya kuipa nyama ya kutosha?

Bazazi
 
naona mkuu alikuwa sawa maana alipenda mkewe asome tena elimu ya chuo ila mkuu "umesahau mke hasomeshwi"?
hongera kwa kupata rafiki mzuri ambaye amekuonyesha njia nzuri mpaka ukapata watoto wako, ulijitahidi sana ili mkeo aishi maisha mazuri ila ameshindwa mwenywe kuna wanaume wanazaa nje na mtu bado anabaki ili kulinda ndoa yae yaani sms tu ndo kuamua kuondoka mwishowe kakosa bara na pwani...........
 
Hii thread ni ndefu But it worth reading, Kila mtu anakosa lake hapo ili yametofautiana uzito.
1) Kosa lako ni kuchepuka,na alilijua hili sijuibkama ulimwomba msamaha na kuhakikisha yaliishi bila kuwa na doubt nyingine

2) Kosa lake ni kuleta ushetani na wizi.

Ila hii story tumeiskilizia in one sided,lakin inaonekana ina ukweli kwa sababu kwanza yule kaka wa bar alikuelewa,polisi alikuelewa na mpka yule wa ustawi.Kusamehe msamehe kwa ajili ya amri ya kusamehe mara sabini,lakini kamwe usianze wewe kuwasiliana naye,usikutane naye na usiruhusu akutane na wanao kama vile ulivyoapa.

Inaelekea huyo mwanamke Alikuwa na tatizo la kisaikolojia linalompelekea yeye kuchukua maamuzi magum yasiyo na huruma,tija na pia ana roho ya kikatili, mshukuru Mungu Huyo mwanamke hakukudhuru Afya yako, Kwa kukuumiza au kwa Kemikali.
 
Tuhadithie nasi kidoog, halafu unitag ukisimulia
 
Hauna jipya ndio wale wale tu
 
COLE nilikuwa naona uvivu wa kutype ila umenipa motisha. Ujue wengi wetu huwa tunaangalia ni wapi tulipoangukia; na sio wapi tulipojikwaa. Kila kitu kilianza kubadilika baada ya mume kuchepuka. Na bado watu tunachanganya kuhusu kufanya kosa na kuvunja trust ya mtu. Mtoa mada alivunja trust ya mkewe; mkewe hakusamehe kosa lake na zaidi hakurudisha Imani kwa mumewe. Inawezekana kabisa alijenga uchungu juu ya mumewe. Tutamlaumu ooh si bora basi kama alichukia angemuacha tu huyo mwanaume: ila tunasahau kuwa ndoa ni investment ambayo mtu anaifanya; sio rahisi kuiacha investment yako ipotee; wengi wanagugumia ndani. Mke aliendelea kuishi na mume ila mambo yakiwa yameshabadilika; alikuwa na uchungu tayari. Usaliti unaweza ukasameheka; ila kuna baadhi ya mambo yanaweza yakabadilika completely; usaliti unaondoa ubora wa ndoa. Mke alijaza uchungu na hivyo akakosa hekima ya kukabili changamoto yake hiyo; mwishowe akapata kichaa cha ndoa.

Siku zote waliposema uchungu unakutafuna kwanza wewe mwenyewe kabla ya mwingine uliyembebea; hawakukosea. Upumbavu wote ambao mke ameufanya was just part ya yeye kutoa uchungu wake; thinking kwamba labda nikifanya hivi mume wangu na yeye ataumia. Na kuna wengine; yeye akiumizwa na mume; uchungu unaishia kwa watoto; usishangae mtu anakuwa katili kwa watoto aliowazaa mwenyewe; huyu uchungu wake uliishia kwa mume. Bahati mbaya sana wakati mke amejaa uchungu na kukosa hekima, alikutana na washauri wabaya; bora hata angekimbilia kanisani maana angeambiwa na kufundishwa kusamehe. (Binafsi hata nione mtu analala kanisani; i won't judge him/her kwa sababu siwezi jua amebeba nini moyoni mwake; na zaidi ya yote is there any safe place to run to if not to Jesus?).

Mke amefanya upumbavu sana; lakini ni kwa sababu ya kutokusamehe na kulimbikiza uchungu. Mtoa mada wakati unakaa na kujiaminisha kuwa wanawake ni watu wasioeleweka wakuishi nao kwa machale; usisahau kuwa hata ukimpata anayeeleweka kama hayupo stable emotionally; ukizingua tu; she will turn into a disaster. Funga zipu yako huko nje; usifikiri kuna mwanamke anayefurahia mumewe kuchepuka; wengine wanalia kimya kimya; wengine wanakuwa wanyama etc.

Mtu anachagua kuwa aina ya mtu anayemtaka yeye; ila mpendwa umechangia sana kwa mkeo kuwa mpumbavu. Wewe ndo sababu ya yeye kuwa na uchungu. (Usishangae; ndo maana kuna wanaume out of bitterness anajiua au anafyeka mke au mke na watoto etc.). Kama mtu akiamua kuharibu maisha yake muache tu; ila usiruhusu kuwa sababu ya mtu mwingine kuharibikiwa. Wewe una % kubwa kwa kilichotokea kwa ndoa yenu leo. Kila mtu kati yenu anahitaji kujisamehe na kusamehe; na kwa kuwa mkeo ameshamove on na maisha yake; find a way ya kumsaidia hadi awe stable again amlee huyo mwanae na a-play part kwenye malezi ya watoto wenu pia. Hutokuwa umemsaidia tu yeye; bali utakuwa umeinvest kitu chema kwa watoto wako.
 
Hiyo nchi 32 kumbuka inaongelewa mwaka gani sio saizi
Vitu vyenyewe vitu gani bro ? Vitanda na TV ya inch 32?
Kuna watu wanaacha magari na nyumba na hawalalamiki.
Kama una hela kweli hivyo vitu si unareplace tu.
Kwanza mlitaka asepe bila kitu kabisa ?
 
Hahaha bro punguza uvivu, inaonekana unastory nzuri sana tena ilio sheheni elimu kubwa naomba tusaidie
 
sijui wewe una matatizo gani!!? Mbona umekomaa saana na TV ya 32''
Ndio imekwezwa kwa kuwa yeye kwake ni kitu cha thamani kubwa saaaana!! Tambua unapopima jambo unalinganisha na uwezo na mfuko wako si na mifuko ya wengine!!!!


Hizo mali ni za mshkaji na hata watoto ni wakwake na mke pia ni wake ndio maana alimlipia mahari!!!!vyote ni vyake!!!
 
dadaangu suala la kuchepuka kwa mwanaume ni jambo la kawaida saana!!!

Yaani about 80% ya wanaume tunachepuka!!! Ni jambo la ninyi kukubali tu,

Nakumbuka tukiwa wadogo kijijini wazee wetu walikuwa wanaleta watoto nyumbani from no where!! Na kutuambia hawa wadogo zenu!! Anachinjiwa mbuzi tunakula
 
Huyo mwanamke ana mchango gani wakati kakuta kila kitu, na mwana alikuwa na mipango ya kumwendelea juu ila demu akawa fala. Wewe hayo maisha anayoelezea mwana umeishi miaka 5 nyuma, yeye kaishi miaka 10 Nyumba, unadhani 32" flat Sumsung mwaka 2009 ulikuwa inauzwa 300,000 kama Sasa hivi mnavonunua hzo za Kichina. Mkuu ni wivu tu unakusumbua huna lolote.
 
Poa poa bro, I rest my case. Ngoja nifanye mambo mengine.
Ila wabongo tujifunze kuheshimu wanawake, kuchepuka ni kosa kubwa sana.
Jeff Bezos alichepuka wamegawana mali na mke wake, sasa hivi mke wake ni third richest woman.
 
Poa poa bro, I rest my case. Ngoja nifanye mambo mengine.
Ila wabongo tujifunze kuheshimu wanawake, kuchepuka ni kosa kubwa sana.
Jeff Bezos alichepuka wamegawana mali na mke wake, sasa hivi mke wake ni third richest woman.
Mkuu samahani kama hautajali naomba kujua umri wako!??
 
Bro hujui maisha yangu kabisa. Na wala sina haja ya kufanya comparison. Na huwa sina dharau, nimelelewa kuheshimu kazi na watu.

Hata hilo la kumwendeleza inaonyesha kabisa jamaa alikuwa anaona huyo mwanamke hawezi kufanya maamuzi yoyote ya maana. Leo hii hata watoto wetu huwa tunawasikiliza wanachokitaka.

Na vipi kuhusu swala la kuchepuka mbona hajaliongelea, aliendelea na yule mwanamke au aliacha? Na ameongea katika namna ya kwamba ilikuwa lazima kwa yule mwanamke amsamehe.

Bro, kuna sintofahamu nyingi sana kuhusu hadithi ya ndugu yetu. The way anavyoelezea msaada aliuotoa kwa mama mkwe, it was like he was counting everything. Najua wewe hujafika hapo kwa msaada wako mwenyewe, vipi unajisikia ukikorofishana na mtu halafu aanze kuelezea misaada aliyokupatia nyuma.

Mimi naona kosa la huyo mwanamke ni ignorance, exposure, na umaskini. Na ndio maana hata watoto kashindwa kulea vizuri.

Mkuu I rest my case, ngoja nifanye mambo mengine. Ila na wewe next time ongea kwa heshima bro, mimi mwenyewe mtoto wa mjini, matusi nayajua, nimechagua tu kutotukana.
 

Uzinzi huwa haulalishwi na adhabu yake si ndogo kama wewe hutaki mwenza wako achepuke jua na yeye ni hivyo hivyo unless hakupendi wanawake wengi mnawaona ni mashetani kwa sababu mioyo yao imejeruhiwa yaani moyo uko vipande vipande. Jitahidi sana kuheshimu moyo wa mke ili uishi maisha marefu na ya furaha. Hata Mungu hapendi uzinzi unless uwe mfuasi wa shetani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…