Chibu hebu Nipe namba za Lyna..katoroka na mimba yanguStori imejaa kujisifu na uzandiki.
1. Mwanzoni, Ulijivunia vitu badala ya UTU (upendo wa dhati). Ukaibuka na Mtoto wa mjini na genge lake
2. Mchumba/mke uliunganishiwa na ndugu (japo wa mbali) hukumchagua,
3. Mahusiano yako yamejaa washauri kibao (sister, jamaa wa kazini, mamaz, majirani) miluzi mingi humpoteza mbwa.
4. Mpaka mwanamke anakukimbia (na uwezo ulionao) ujue una tatizo.
**Ku-balance story ilipaswa tumsikie mwanamke nae maana wewe unajifagilia mwanzo -mwisho eg. Nilikuwa na kila kitu (nyumba ya kupanga?), Mark II, nilinunua bati 20,nikanunua shamba 1m
Nilishuhudia Mwanamke aliekwenda kuazima shoka kwa jirani kisha akapasua vyombo na thamani za nyumba nzima aliposikia mumewe ana mpango tu wa kuongeza mke wa pili. Jamaa alikuwa ni mfanyabiashara mkubwa sasa imagine thamani za ndani, kitu Sony Bravia 50 inch curve mpya kabisa ilipigwa shoka chali kifo cha mende...…..Pale ndio niliposema kweli mwanamke ni jalala.
Umeongea ukweli kabisa huyu hata akija kuoa tena bado atalipa tu huyo mke wake mpya anaweza mfanyia cha ajabu akaona heri yule wa kwanza ukishakaribisha shetani kwa maisha jua tu utacheza nae ngoma tu. Shetani kazi yake ni kuharibu na kuua tu hana jema kabisa na anafurahi sana ndoa zikisambaritika
Sawa mkuu, ila mkuu usiniombee/usinisemee mbaya kiasi hiki, hujui ni kwa jinsi gani hii kitu iliniumiza, nilifanya juhudi Zote kumrudisha mwenzangu ila ikashindikana, na kama umenisoma vzuri mwenzangu alikuwa hanipi nafasi ya kutosha kuongea naye baada ya kuwa ameondoka maana nikiongea naye kidogo tu akakata simu na mwishowe kuzima kabisa.
Mkuu zile pombe nilizokuwa nakunya nilikuwa sinywi kwa starehe mkuu, I bet you know what I mean.
Mkuu nilikosea hilo mpaka kesho nita-admit ila kwenye hii ishu ambaye huwa namlaumu mpaka kesho ni mama Mkwe, yule mama angevaa jukumu lake kama mama mambo yasingefika hapa yalipo, hata kama vitu baadhi vilishauzwa au hata vyote, yule mama angeamua Mtoto wake arudi na kuendelea na maisha angerudi. Mkuu naomba ujue tu kuwa I am not a monster, nina madhaifu yangu kama binadamu mwninge yoyote ila am not a monster boss
Asante
Sawa mkuu, ila mkuu usiniombee/usinisemee mbaya kiasi hiki, hujui ni kwa jinsi gani hii kitu iliniumiza, nilifanya juhudi Zote kumrudisha mwenzangu ila ikashindikana, na kama umenisoma vzuri mwenzangu alikuwa hanipi nafasi ya kutosha kuongea naye baada ya kuwa ameondoka maana nikiongea naye kidogo tu akakata simu na mwishowe kuzima kabisa.
Mkuu zile pombe nilizokuwa nakunya nilikuwa sinywi kwa starehe mkuu, I bet you know what I mean.
Mkuu nilikosea hilo mpaka kesho nita-admit ila kwenye hii ishu ambaye huwa namlaumu mpaka kesho ni mama Mkwe, yule mama angevaa jukumu lake kama mama mambo yasingefika hapa yalipo, hata kama vitu baadhi vilishauzwa au hata vyote, yule mama angeamua Mtoto wake arudi na kuendelea na maisha angerudi. Mkuu naomba ujue tu kuwa I am not a monster, nina madhaifu yangu kama binadamu mwninge yoyote ila am not a monster boss
Asante
Na pia ombea sana watoto wakija kuwa wakubwa wakagundua mama yao Ali react hivyo baada ya kujua ulicheat wata simama na mama yao tu. Mama ni mama na mara nyingi watoto huwa wanaegemea kwa mama hata kama alikuwaje
Hii point nimemuonesha mke wangu na kumsomesha kisa kizima kwa sababu anamsikiliza mama yake na anamuona ni dira ya dunia kama vile dochi veree na imefikia point wanajenga kisiri siri mama yake ndo mkandarasi ila mimi najenga mali za familia anyway ngoja jipu langu nami likitumbuka nitakuja na uzi mrefu kama huu.ASANTE MTOA MADA NATAMANI WANAWAKE WOTE WA JF WANGESOMA HII HADITHI YAKO.
Sawa mkuu.ila sio hadithi hiki ni kisa cha kweli kabisa.
COLE nilikuwa naona uvivu wa kutype ila umenipa motisha. Ujue wengi wetu huwa tunaangalia ni wapi tulipoangukia; na sio wapi tulipojikwaa. Kila kitu kilianza kubadilika baada ya mume kuchepuka. Na bado watu tunachanganya kuhusu kufanya kosa na kuvunja trust ya mtu. Mtoa mada alivunja trust ya mkewe; mkewe hakusamehe kosa lake na zaidi hakurudisha Imani kwa mumewe. Inawezekana kabisa alijenga uchungu juu ya mumewe. Tutamlaumu ooh si bora basi kama alichukia angemuacha tu huyo mwanaume: ila tunasahau kuwa ndoa ni investment ambayo mtu anaifanya; sio rahisi kuiacha investment yako ipotee; wengi wanagugumia ndani. Mke aliendelea kuishi na mume ila mambo yakiwa yameshabadilika; alikuwa na uchungu tayari. Usaliti unaweza ukasameheka; ila kuna baadhi ya mambo yanaweza yakabadilika completely; usaliti unaondoa ubora wa ndoa. Mke alijaza uchungu na hivyo akakosa hekima ya kukabili changamoto yake hiyo; mwishowe akapata kichaa cha ndoa.
Siku zote waliposema uchungu unakutafuna kwanza wewe mwenyewe kabla ya mwingine uliyembebea; hawakukosea. Upumbavu wote ambao mke ameufanya was just part ya yeye kutoa uchungu wake; thinking kwamba labda nikifanya hivi mume wangu na yeye ataumia. Na kuna wengine; yeye akiumizwa na mume; uchungu unaishia kwa watoto; usishangae mtu anakuwa katili kwa watoto aliowazaa mwenyewe; huyu uchungu wake uliishia kwa mume. Bahati mbaya sana wakati mke amejaa uchungu na kukosa hekima, alikutana na washauri wabaya; bora hata angekimbilia kanisani maana angeambiwa na kufundishwa kusamehe. (Binafsi hata nione mtu analala kanisani; i won't judge him/her kwa sababu siwezi jua amebeba nini moyoni mwake; na zaidi ya yote is there any safe place to run to if not to Jesus?).
Mke amefanya upumbavu sana; lakini ni kwa sababu ya kutokusamehe na kulimbikiza uchungu. Mtoa mada wakati unakaa na kujiaminisha kuwa wanawake ni watu wasioeleweka wakuishi nao kwa machale; usisahau kuwa hata ukimpata anayeeleweka kama hayupo stable emotionally; ukizingua tu; she will turn into a disaster. Funga zipu yako huko nje; usifikiri kuna mwanamke anayefurahia mumewe kuchepuka; wengine wanalia kimya kimya; wengine wanakuwa wanyama etc.
Mtu anachagua kuwa aina ya mtu anayemtaka yeye; ila mpendwa umechangia sana kwa mkeo kuwa mpumbavu. Wewe ndo sababu ya yeye kuwa na uchungu. (Usishangae; ndo maana kuna wanaume out of bitterness anajiua au anafyeka mke au mke na watoto etc.). Kama mtu akiamua kuharibu maisha yake muache tu; ila usiruhusu kuwa sababu ya mtu mwingine kuharibikiwa. Wewe una % kubwa kwa kilichotokea kwa ndoa yenu leo. Kila mtu kati yenu anahitaji kujisamehe na kusamehe; na kwa kuwa mkeo ameshamove on na maisha yake; find a way ya kumsaidia hadi awe stable again amlee huyo mwanae na a-play part kwenye malezi ya watoto wenu pia. Hutokuwa umemsaidia tu yeye; bali utakuwa umeinvest kitu chema kwa watoto wako.
Kusema ukweli wewe ndiye chanzo cha matatizo na uone aibu kulalamika. "Unamla demu kiaina, sijui kipoozeo" shiiit. Ulitaka yeye afurahi kwa wewe kukosa uaminifu?.
Watu wengi hufanya makosa makubwa halafu wanataka wenza wao wayachukulie kawaida na wawapende kama mwanzo haifai.
Sawa mkuu hilo najua linaweza Kutokea na nilishajiandaa kwa ajili yake. Mkuu kuna mambo nilifikiria sana, je niwaache watoto na mama yao wapotee (hapa unaweza sema inawezekana wasingepotea au labda ningefanya juhudi za kuwasaidia wakiwa mikononi mwa mama yao, ila mkuu kila mtu anamjua mtu wake, nadhani unanielewa)au niwachukue nijaribu kuwaandalia maisha, nikamua kwenda na option ya pili.
Kwa hyo hapa nilipo nafanya jukumu langu kama baba, inawezekana watakapopevuka na kuujua ukweli wanaweza kunichukia au sijui itakuweje, nitaongea nao, wanaweza kunielewa au wasinielewe ila nitakuwa nimetimjza jukumu langu kama baba.
Nadhani hasira yao juu yangu haitakuwa Kubwa kama ambavyo labda ningeamua kuwaacha wapotee huku nikiwa na uwezo wa Kufanya kitu juu yao.
All in all tuombee mazuri
Asante.
Mkuu huu ujumbe Wako ni Mkubwa sana sana and I wish mwenzangu angekutana na mtu kama wewe baada ya ile ishu maana hii thread isingekuwa Kwenye server ya JF. Nimeelewa 100% ulichoandika na nakubaliana na wewe 110%
Mkuu Nina madhaifu yangu kama binadamu mwingine yoyote yule Ila Nina ubinadamu Wangu pia, mkuu unamsaidia mtu ambaye anahitaji msaada Wako au hata anaonyesha basi kuhitaji msaada Wako. Mwenzangu baada ya hii ishu Kutoka aliangukia Kwenye mikono mibaya na mpaka Sasa yupo Kwenye mikono mibaya sana.
Mwenzangu hajawai kujutia alichokifanya (inawezekana labda yeye anaona hana cha kujutia, sijui). Kwa hyo hata msamaha aliokuwa anaomba au wanaomba walikuwa wanaomba kwa sababu fulani, trust me I know what I am talking about. Sio kuwa nilikuwa tu na vile niliongelea Kwenye thread, nilikuwa na assets nyingine pia ambazo mwenzangu alikuwa anazijua ila alinikuta Nazo pia.
Baada ya kutokea yaliyotokea bado alikuwa Anataka na sehemu ya zile assets ila alipoenda polisi wakamwambia alifanya kosa kuuza vile vitu kwa hyo hata akifungua kesi haitakuwa na uzito wowote, na haya yote alikuwa anafanya chini ya muongozo wa watu fulani fulani. Kwa hyo she was determined to finish me for good. Hvi mkuu mtu amefanya haya yote (Sawa nilikuwa chanzo) mimi nimepata ajali nimeumia sana, nimelala ndani karibia miezi sita, huyu mtu ananiandikia sms "Nitaendelea kulia na Mungu yakukute zaidi ya hilo". Hivi mkuu hata kama mimi ni malaika huyu mtu nitamwelewa kweli? Ngoja ebu nikae kimya aisee.