Kila nikileta beki tatu mume wangu anatembea nao, nimechoka

Huna akili, hata nikikushauri utazidi kutoa boko tu, cha msingi endelea kuishi ivo ivo tu, kama ishu ni kutembea na hausigeli leta ndugu yake kutoka kijijini awasaidie kazi
 

Huyo jamaa ana roho chafu , anahitaji kufunguliwa ,
Ila huyo mpeleke ustawi wa jamii , amevuka mipaka , wala hiyo nyumba asikutishie maana ni ya kwako na watoto wako , haki yako ni kubwa , jiokoe nafsi yako ,maadamu yeye hajamaliza dunia , Mwache akili imkae , mpeleke ustawi wa jamii ,maana atatengeneza watoto wengi machokoraa ,ni ujinga ,
Pole sana !
 
kama kuna mtu atahamini kuwa hii story ni ya kweli basi ana matatizo
 
Mama nikuambie Kitu tunza risiti zako zote ulizokuwa unafanya manunuzi kipindi unafanya ujenzi wa nyumba Yako, na rekodi yote ya Mikopo ya Mabenki kwa ajili ya ujenzi, kuandikwa kwa jina la mmmeo kwenye Kiwanja siyo tija
Utakuja kunishukuru baadaye
kwa iyo na ww umeamini hii chai.
 
kama huna ushauri wa maana kwa uyu mwanamke usiongee chochote nimekuona hadi kwa idi makengo pole sana ...mpka nakukuta sehemu mbili mtandaoni unaomba msaada wa dhati natamani upate wataalamu wa mahusiano na ushauri wakusaidie swala lako.
ila nitakushauri uzingatie sana AFYA yako ya akili ndo ktu Cha muhmu ,ukipata nafasi burudisha moyo na nafasi yako Ili kuzuia msongo wa mawazo.
Pole na kaza mpo wengi na Kuna wengine wanaptia zaidi yako.haupo mwenyewe
 
Ajiri House Boy 😜
 
Trans-gender labda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…