Kila nikirejea kuangalia Mechi za AS Vita Club dhidi ya Al Ahly kule Misri na Kwao Congo DR napatwa na uwoga kwa Mkapa Jumamosi

Kama kawaida yake kila baada ya mechi ya simba huyu utopolo eti all rounder huwa anazikimbia nyuzi zake maana si kwa aibu zile!!
Hata jumamosi hii hutamwona All Rounder baada ya mechi!!
Si nilisema? Mtoa uzi keshatoroks tayari na kutelekeza uzi wake!! Kina All-Rounder, Senzo, na utopolo et Al huwezi kuwaona tena jukwaani!! Kina Generalist hata ukiwaitia pesa hawawezi kusogea hapa, si kwa aibu hiyo!!
 
Asante mkuu kwa kua mzalendo sio wana yanga wabishi wasio kubali ukweli
 
Umesha andikanombi lako la public holiday ?
 
Simba haitabiriki tukubali tu wenzetu wako Bora Sana unaweza shangaa vitaa anakula. Tano tukaanza kuona aibu bure Bora uwe mpole
Mdau ulichungulia mechi ktk birauri lako la uganga nn maana kama sio yule mwana hizaya Mugalu bac Ibenge ange pata AIBU Dsm
 
Sioni Mikia wakiingia robo fainali maana mechi zote mbili atapoteza
Hivi huchoki?Chuki hudhuru moyo.Heri ujinga wa kuuza kuliko ubaradhuli wa kununua. Haisaidii kupinga mafanikio kwa kulalamika Dawa ni kuiga mafanikio na kuongeza juhudi.
 
Maombolezo ya nani vile? Kama ni yule yesu wa kangi imekula kwako.Tumeshamsahau na tunaendelea na yetu.Kwanza katuchelewesha saaana! SSC nguvu moja.
 
Umesoma bila kuelewa kumbuka 2017 -2018 Vita club walikuwa finalist wa kombe la shirikisho wakafungwa na Rajer Casablanca.

Msimu uliofuata wa 2018 -2019 walikuwa na kikosi bora sana japo walishindwa kuingia hatua ya mtoano kwa kutolewa na Simba hapa Dar.

Msimu uliofuata waliondokewa na wachezaji wao wengi muhimu akiwemo Mshambuliaji wai Mundele Makusu na nahodha wao Fabrice Muamba Ngoma na wengineo akiwemo Kisinda aliyeporomoka kiwango na kutolewa kwa mkopo kwenye vilabu vingine.

Kikosi walichonacho sasa ukiondoa Djuma Shaban, Emanuel Luzolo Sita, Jaques Mangoba ni kikosi ambacho ni ingizo jipya hata golikipa wao Omosola hakuwa regular starter kikosini.

Hata uchezaji wao hawana uelewano kama msimu wa 2018-2019.

Ni ngumu kuelewa mambo ya mpira kama unafuatilia matokeo tu.
 
Ila mkuu naona kama "ambao hatuna uelewa wa mpira" na "tunaofuatilia matokeo tu" kama vile kila wakati huwa tunakuwa sahihi kuhusu Simba kushinda licha ya vigezo vyote kuwa vinatuelemea.
Ilianza sijui Pyramids wana fowards yenye magoli 120 ndani ya nusu msimu.... Tukaamini tutashinda wenye uelewa wa mpira na takwimu mkawa chali...
Wakaja Platnums walivyotufunga kule kwao mkatuambia yale ya UD Songo yanatukabili.... Mnajua wenyewe sisi tusio na uelewa wa Mpira tulienda uwanjani kwa nguvu zote.
Makundi yalivyopangwa basi mnaojua mpira mkatuambia kuwa rekodi zinaonesha kuwa Simba atakuwa wa mwisho kwenye kundi na atapigwa bao nyingi...
Tusiojua mpira tuliamini Simba atashinda na Tukampiga Vita kwake.... Tulipompiga Al Ahly mnaojua mpira mkasema tumechokoza nyuki tutaumia...
Al Merrikh tulipotoa sare wenye uelewa wa Mpira mkasema wachezaji wao 5 walikuwa na COVID-19 ndio maana na mechi ya marudiano Simba atapigwa nyumbani... Hata hivyo Al Merrikh alikula 3 na mkasema Simba alifanya fitna wachezaji wao 8 wakazuiwa kwa kukutwa na COVID-19.
Sasa kazi ikaja kwenye mechi ya As Vita wenye uelewa wa mpira kama wewe hapo, All-rounder na CARFONIA mkaja na takwimu za As Vita alivyompelekesha Al Ahly huko kwa Farao mkidai kuwa Simba atakufa kipindi cha kwanza tu mapema tena sio chini ya goli 3. Tusio na uelewa wa mpira tukawa na imani Vita anakufa kwa Mkapa tena kwa goli nyingi.... Mnaojua mpira nadhani sasa mnajua kama sio "HILA" za Mugalu basi Ibenge ingebidi aombe uraia wa Tanzania maana angeenda kunyongwa kwa aibu ambayo ingetokea.
Kwa kifupi tu ni kuwa nyie wenye "UELEWA" wa Mpira kila mara linapokuja suala la Simba mmekuwa mkipoteza tu kila wakati.... Au mtuambie labda uelewa wenu wa mpira ni wa FIFA PES games.
 
Kuna sehemu umeona nimesema Simba hawezi kushinda against hizo teams ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…