Hata vitu alivyofanya vilikuwa vinaonekana kuliko nyie mmejaza wapigaji wanajitafunia nchi kwa urefu wa kamba zao.
Kuna fry over ya ubungo. Wengine watakuja lile daraja. Mmeshindwa nini nyie kutengeneza madaraja kama hayo manne tu mbeya mawili mafiat na uyole,kwanza,morogoro. Wanaosema madaraja wamefeli pia ona ilivyoipendezesha dar.
2. Barabara ile ya kimara. Kumbuka foleni ilivyokuwa kabla hajaitanua hiyo barabara.
3. Barabara kufungua mkoa kwa mkoa kuingilika kwa barabara.
4. Alirudisha uwajibikaji ofisi za Umma. (Ona sasa unaingia ofisi ya Umma kama huna mkono mrefu hawana habari kipindi chako kulikuwa na hofu.
5. Alidhibiti utafunaji mali za Umma. Lakini siku hizi wale kwa urefu wa kamba zao.
6. Umeme ulishaanza kuwa historia kukatikatika mpaka wengi waliuza magerator yao ksbb yalikosa kazi. (Ona sasa umeme umetia fora ukatikaji toka Tz ipate Uhuru.
7. Alipunguza gharama za ulipaji huduma za umeme kwa kwa kiwango kikubwa ili kila mmoja mpaka masikini awe na hiyo nishati. (Ona alivyoondoka tu kuingiza umeme bei juu sana,imekuwa ni anasa,imebaki kwa matajiri.
Ni mengi mazuri yake kuliko mapungufu. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni kwa kuoanisha Kwanza mazuri ndipo muunganishe na mabaya,na mlinganishe na yanayoendelea sasa .
=}mapungufu yake ni machache kama kuminya democracy. Lakini vinginevyo mwamba angetusogeza sana sana kwa Tanzania hii ilimhitaji sana sana kiongozi wa namna ile.
MWISHO ALISEMA IMEKWISHA MTANIKUMBUKA.