Kilichonikuta Mlimani City: Nimekula chakula na kupewa bili kubwa nisiyotarajia

Kilichonikuta Mlimani City: Nimekula chakula na kupewa bili kubwa nisiyotarajia

Shopping uliyofanya ulinunua nini? ulipigwa kiasi gani?
 
pesa ya nyanya hata haitoshi kwa hiyo yako,,,
ina onekana hata kushiba hukushiba coz ulikua una waza bill
 
ungekua hauna hela kabisa wangekupeleka jikoni kushainisha masufuria au kuchonga viazi... Hii tabia nmeiona kwa wakenya lakini...
 
Umetoka mkoa gani kwani....mbona 22.000/ ni nauli ya mwanafunzi hiyo + kula yake ya mchana
[emoji1] [emoji1] nimecheka sana.. wanafunzi apewe 22,000.wakati asubhi unakuta mtoto anatumwa dukani na mia tano akaombe chenji ili yeye achukue mia nne ya nauli na mia ibaki nyumbni ya maji wew unacheza na zama hizi nini ukisia vyuma nimekaza vimekaza kweli kweli..
 
Jana nilienda mlimani city, katika kufanya shopping, nilipomaliza wakati natoka nikaona kuna Restaurant, nikaagiza chakula wali kwa samaki "change"na juice ya ukwaju ila kosa nililofanya sikuulizia bei

Sasa nilipomaliza kula ikafikia wakati wakulipa hela nikamuuliza muhudumu nadaiwa sh. ngapi? yule muhudumu akaenda counter akarudi na bili inasoma 18,000/= na juice 4,000/= jumla 22,000/= kwakweli niliishiwa nguvu kabisa na nilijilaumu sana kwanini sikuuliza bei kabla hadi ninaondoka pale hadi muda huu bado akili haijakaa sawa

Yaani kama nimeibiwa mwenyewe nilishazoea uswahilini 3,000/= unapata msosi wamaana kabisa ila nimejifunza kitu kuulizia bei kabla yakuagiza kamajana ningekuwa sinahela sijui wangenifanya nini
Pole sana ndugu hata me imewai kunitokea saiv nimejifunza huwa nauliza kwanza bei..
 
[emoji1] [emoji1] nimecheka sana.. wanafunzi apewe 22,000.wakati asubhi unakuta mtoto anatumwa dukani na mia tano akaombe chenji ili yeye achukue mia nne ya nauli na mia ibaki nyumbni ya maji wew unacheza na zama hizi nini ukisia vyuma nimekaza vimekaza kweli kweli..
Mzee vyuma vimekaza kwetu sisi tu kuna watu wanafanya kufuru usipime......unajua kuna madent wanaenda shule na vyombo vya usafiri binafsi kwenda na kurudi shule + lunch na matumuzi mengine.....hapo 22.000/ ni nini kwake.
 
pole sana kaka ila nakushauri unapoingia hoteli yoyote uliza kwanza bei sio aibu nahata ukiingia hotel za mitaani jitahidi uwe unauliza kwanza na pili ukitaka kutengenezewa kitu chochote patana bei kwanza na asikuambie fundi usijali gatuwezi kushindana mimi na wewe wewe mteja wetu nooo usikubali patana kwanza haya ni mafundisho ya dini inavyotuambia
 
Mi nlikuwa naenda nchi flan kumbe vitu vya airport ni majanga, kwenye internationa lounge na domestic loung vitu vinauzwa bei tofauti, nliagiza bablish nikalipa elf10 nikarudishiwa elf6, sikujali sana coz nlikuwa naenda shule na nlikuwa na mshiko wa kutosha. Shida ikaja UAE mji unaitwa abudhabi, nlifika mida ya saa mbili usiku nikaka hadi saa nane hapa kati nikaanza kutafuta kishtua tumbo nlikuwa na dola km 1000 hivi mfukon nlizokuwa nimechenj DIA. nikalipa dola 100 nlichorudishiwa ni siri yangu. Mpaka sasa huwa nikiwa nasafiri huwa nahakikisha nimekula nikashiba kabla ndege haijatua. Airport labda maji ya kunywa tu nikisubiri kuunga ndege.

wewe sio kweli nimeishi abudhabi miaka 25 chakula nchi hiyo ni rahisi sana watu mpaka wanamwaga chakula mpaka wazungu wanashangaa
 
naona wachangiaji hamuwajui wasukuma mnaropoka tu kwanza msukuma huwa akija mjini ana pesa msukuma huwa wengi wao wanapesa akinunua kitu hangalii bei hutoa tu wala halalamiki na anapokula hupenda anayepita karibu yake amkaribishe wale pamoja hata kama hamjui
 
hao sio wasukuma
Huyo alie lala umemtambua...[emoji45] [emoji45]
Maana wenzie wakati wanasoma, yeye alikuaga analala tu...... alafu leo hii yeye ndie anakula good time kuliko wale waliokuaga wanasoma kwa bidii wakati yeye anauchapa...[emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12]
 
Jana nilienda mlimani city, katika kufanya shopping, nilipomaliza wakati natoka nikaona kuna Restaurant, nikaagiza chakula wali kwa samaki "change"na juice ya ukwaju ila kosa nililofanya sikuulizia bei

Sasa nilipomaliza kula ikafikia wakati wakulipa hela nikamuuliza muhudumu nadaiwa sh. ngapi? yule muhudumu akaenda counter akarudi na bili inasoma 18,000/= na juice 4,000/= jumla 22,000/= kwakweli niliishiwa nguvu kabisa na nilijilaumu sana kwanini sikuuliza bei kabla hadi ninaondoka pale hadi muda huu bado akili haijakaa sawa

Yaani kama nimeibiwa mwenyewe nilishazoea uswahilini 3,000/= unapata msosi wamaana kabisa ila nimejifunza kitu kuulizia bei kabla yakuagiza kamajana ningekuwa sinahela sijui wangenifanya nini

Pole na dhahama hiyo.

Kwani huo mgahawa hawana "menu" ionyeshayo bei ya vyakula na vinywaji?
 
Back
Top Bottom