Elections 2010 Kilichonishtua Juu Ya Dr Slaa Pale Mwembetogwa

Elections 2010 Kilichonishtua Juu Ya Dr Slaa Pale Mwembetogwa

Maggid,
Wewe una hakika gani hakupewa nafasi ya kusikilizwa? Mbona hujasema kwa nini alikuwa akipiga makofi pamoja na kushambuliwa? Yaani huu mjadala hakuwa na la maana ndio sababu umeshambuliwa na kila mmoja. Mbona hakuna mahali wewe kama mwandishi umesema ulikwenda kumuhoji Dr Slaa na yule bwana aliyeshambuliwa jukwaani ili uje na uhakika wa alichosema?

Mimi nimekuwa mmoja wa wasomaji wa makala zako kule Rai ya zamani (sio hii ya sasa), na kama unaendelea kuishi kwa matakwa ya Rai ya sasa hivi tutaendelea kukushambulia unapoleta mijadala isiyo na kichwa wala miguu eti kwa sababu wewe ni mwandishi. Hata hayo ya kulishitaki gazeti uliyoandika humu hayana sababu maana ukishaandika vitu vya hovyo bila kufikiri haya ndio matokeo yake. Pole.

Mchukia ufisadi, huyu si mwandishi hivyo hata zile A, B, C za uandishi hazifahamu. Alikurupuka tu kuandika bila hata ya kutafakari mantiki ya anachoandika. Ni bora tu akaendelea kuandika kuhusu Chai na Chapati nyumbani kwa michuzi badala ya kudandia field ambayo haijui hata kidogo.
 
Huyo mtu ambaye Majjid anasema hakutendewa haki ni kiongozi wa Chadema(Mkoa) na alikuwa anataka kugombea ubunge kwa hiyo tunajua kwamba anauwezo mkubwa kiakili. Kama anaona hajatendewa haki anajua njia ipi achukuwe.
 
Maggid,
nafikiri katika wakati huu mijadala kama hii ina umuhimu. Aliyetuhumiwa na kuhukumiwa pale Mwembetogwa ni mtu mdogo sana katika nchi hii. Amehukumiwa hadharani na mgombea urais bila kupewa nafasi ya kujitetea. Labda habari zake ndio kwanza mnazisoma humu.
Duh, labda nikuulize wewe, Hivi Hitler alipewa nafasi ya kujitetea na mbona anatuhukumiwa kwa yote aloyafanya..au tumseme mtu mdogo sana kama Osama naye vipi hutuwezi kuzungumza mabaya yake hadi afikishwe mahakamani? mbona viongozi wote duniani wanamzungumzia huyu mtu mdogo ktk majukwaa na sijakusikia hata siku moja ukiandika kusikitishwa na viongozi hao. Kama wewe unayo habari tofauti na Dr.Slaa alozungumza yasema wazi nasi tutapima makosa ya Dr.Slaa.

Mkuu wangu umechemsha hata kama unatafuta ligi basi haiendi hivi.. jaribu sana kutafuta mada yenye mvuto zaidi toka hotuba za Dr.Slaa kisha hapo weka staha kiasi kwamba hata mimi naweza fikiria kweli mpira umeahirishwa kuliko kuwaona vibaka wa kiboko msheri wakirudi, nitajua fika wahuni hao hawana uwezo wa kulipa kiingilio wanatafuta mnyonge.
 
Hapa ni kama yale ya Ilala enzi zile. Hii ya leo ni kama vile mtu unatembea kwa miguu peke yako kutoka viwanja vya Jangwani kupandisha kwenda Magomeni Mapipa. Juu mlimani unakutana na umati wa watu wanashuka kwa miguu kutoka Magomeni Mapipa kwenda Viwanja vya Jangwani. Ni lazima utasababisha majadiliano kwa wanaoshuka jangwani. Na hiii ndio staili ninayoitumia hapa katika kuamsha fikra.

Katika Uchaguzi wa mwaka 2005 niliandika makala kwenye Rai kuwakemea wale waliokuwa wakimbagua Dr Salim kutokana na rangi yake. Niliamini na bado naamini kuwa hawakumtendea haki. Dr Salim ni Mtanzania mwenzetu, hakukuwa na sababu za kuja na hoja za uhizbu na mengineyo.

Kuna mwandishi wa habari akaandika makala kwenye gazeti moja la kila wiki kunizushia mambo ya uongo yenye sura ya uchochezi. Aliandika mambo ya kunigombanisha mimi na wenyeji wa Iringa wa kabila la Wahehe. Ilikuwa ni stori ya uongo toka mwanzo hadi mwisho. Na kibaya zaidi mwandishi yule akafikia hata kutoa nukuu ya niliyoyaandika kwenye Rai. Nukuu kutoka kichwani mwake na si kile nilichoandika.

Nikamwandikia mhariri wa gazeti lile kumwomba kiungwana afanye mambo mawili; mosi, aniombe radhi kwa kuchapa taarifa ya kuniomba radhi ukurasa wa mbele wa gazeti lake katika matoleo matano mfululizo. Pili, achapishe makala halisi niliyoiandika katika Rai.

Kwamba asingefanya hivyo, basi, ningefikiria hatua zaidi za kuchukua. Mhariri alinielewa na akatekeleza ombi langu hilo.

Hoja hapa ni kwa nini tunatakiwa kuwa waangalifu katika kuandika na kutamka mambo ambayo kimsingi yanaweza kuwaletea wengine madhara, ya kijamii au hata kiuchumi. Pamoja na mimi kuombwa radhi mara tano na gazeti lile, bado naamini kuwa kuna Wahehe wa Iringa waliosoma makala ile potofu na hawakusoma kingine tena baada ya hapo. Kwao, mimi nabaki kuwa ni yule mchochezi na niliyewadharau Wahehe. Itabaki hivyo daima. Ni hasara kwangu.

Mi nafikiri katika wakati huu mijadala kama hii ina umuhimu. Aliyetuhumiwa na kuhukumiwa pale Mwembetogwa ni mtu mdogo sana katika nchi hii. Amehukumiwa hadharani na mgombea urais bila kupewa nafasi ya kujitetea. Labda habari zake ndio kwanza mnazisoma humu.

Nafikiri ni muhimu hata hao tunaokwenda kuwachagua nao wajue tunafikiri nini juu yao, maana wanakwenda kubeba dhamana kubwa. Kwa kufanya hivyo, tutawapa nafasi ya kutafakari yale ambayo huenda wasingeyatafakari kama si kuibuliwa mijadala kama hii. Mimi sitachoka kuanzisha mada na kuchokoza mijadala, kwa staili hii hii, na ni kuhusu mambo mbali mbali ninayoyatafakari ili tutafakari pamoja.

Kuchokoza mjadala au kuuthibitishia umma kuhusu ubabaishaji wako?Mjadala gani uko one-sided?

Wewe hutochoka au njaa yako ndio inakufanya usichoke?

Sio siri,Dkt Slaa akiingia Ikulu kilio hakitakuwa kwa akina Rostam na mafisadi wenzie pekee bali hata wababaishaji kama Mjengwa.Sijui ataandika nini tena!
 
Maggid hiki siyo kipindi cha kuoneana aibu wala nini!!!

huyo mwenyekiti hakufanya vibaya na hiyo iwe fundisho kwako na kwa jamii nyingine kuwa hiki siyo kipindi wala hakuna tena kipindi kitakuja wewe au mtu mwingine aonewe aibu kwa ujinga anaofanya..

huyo mwenyekiti ndiyo ameisha kisiasa na kamwe hakuwa mtu tena mwaminifu na wakutumainiwa katika jamii inayomzunguka....

ukiwa mwana mageuzi simama katika haki na tetea hoja hako..

People Power!!!!!!
 
Hivi huyu kijana alipomaliza shule yake tambaza alikwenda wapi...........alisomea chuo gani...........inaku/tupa picha gani...........if y'all know what i mean............
 
Mr Mjengwa, in the past you were attention-seeker activist blogger openly supporting CUF. I don't know what has happened to your relationship with CUF. I see you are indirectly trying to infiltrate CCM by bashing Dr Slaa. No way!
CCM supporters do not like your dumb tricks and we condone your low class behavior.
You better stick with what you write and believe in your nonesense and useless blog. All you write and post in your cheap blog is telling people "ooh I was in Sweden, ooh This morning I was in Moro, Oooh I was in KLM flight etc"...who cares or give a sh-it!
Unlike your cheap blog, this is JF where everybody is allowed to express his/her thoughts.
My advice to you: Do keep taking those funny street photos about things or events that make no sense and continue to write those dumb poems of yours.
This is not a blog for small minded and dumb folks like you or your stupid followers. JF is open for everybody.
Please do not come here. Don't even come to Dar. Stay with your dumb issues in Iringa. Stay with CUF or TLP!
Vote CCM
 
Mr Mjengwa, in the past you were attention-seeker activist blogger openly supporting CUF. I don't know what has happened to your relationship with CUF. I see you are indirectly trying to infiltrate CCM by bashing Dr Slaa. No way!
CCM supporters do not like your dumb tricks and we condone your low class behavior.
You better stick with what you write and believe in your nonesense and useless blog. All you write and post in your cheap blog is telling people "ooh I was in Sweden, ooh This morning I was in Moro, Oooh I was in KLM flight etc"...who cares or give a sh-it!
Unlike your cheap blog, this is JF where everybody is allowed to express his/her thoughts.
My advice to you: Do keep taking those funny street photos about things or events that make no sense and continue to write those dumb poems of yours.
This is not a blog for small minded and dumb folks like you or your stupid followers. JF is open for everybody.
Please do not come here. Don't even come to Dar. Stay with your dumb issues in Iringa. Stay with CUF or TLP!
Vote CCM
na wewe unafanya nini hapa?
 
Ndugu Zangu,

Nimeona mada niliyoianzisha kwenye mjengwablog imeingizwa humu na wengi wameshiriki kuichangia, na mimi pia. Mada inasema " Nilichokiona Jana pale Mwembetogwa". Lakini ziada ya pale Mwembetogwa ni ukweli kuwa mwanzoni kabisa mwa hotuba yake, Dr Slaa alitoa kauli mbele ya umati ule. Kauli ambayo binafsi niliisikia na ilinishtua sana. Dr Slaa alisikika akitamka kuwa kuna kiongozi wa mkoa ( CHADEMA) ( Alimtaja jina) ambaye amehongwa na mgombea ubunge wa CCM jimbo lingine la Iringa ( naye alimtaja jina) ili asirudishe fomu zake. Dr Slaa akataka kiongozi huyo wa zamani wa CHADEMA apuuzwe na akitaka aende mahakamani.

Nadhani katika wakati huu kuna umuhimu wa kuwafahamu zaidi wagombea wetu. Na kumtakia mema Dr Slaa ni pamoja na kumwambia yale tunayoyaona ni mapungufu. Si kummwagia sifa tu. Maana, kwa kitendo kile, Dr Slaa kwa mtazamo wangu alimdhalilisha kiongozi yule wa CHADEMA mbele ya umati ule. Na bahati mbaya au nzuri kiongozi huyo wa CHADEMA alikuwapo. Kwa macho yangu nilimwona kiongozi huyo wa CHADEMA akishiriki kupiga makofi kuungana na umati uliokuwa ukishangilia kauli ya Dr Slaa. Masikini, kiongozi yule wa CHADEMA, bila shaka alipigwa na butwaa na hakuwa na la kufanya bali naye kupiga makofi!

Kwangu nilishtushwa na kusikitishwa sana. Bado naamini Dr Slaa hakumtendea haki kiongozi yule wa CHADEMA. Kama Dr Slaa alikuwa na ushahidi wa alichokisema, basi, hakuwa na haja ya kumtuhumu na kumtolea hukumu kiongozi yule pale hadharani. Kiongozi yule wa CHADEMA aliyehukumiwa hadharani ni mwanajamii hapa Iringa. Ameshapigwa mhuri mbaya bila hata kupewa fursa ya kujitetea. Kwa mzazi kama mimi naelewa jinsi kiongozi yule atakavyojisikia vibaya mbele ya familia yake, mke na watoto wake. Kwamba ametoka kwenye mkutano wa mgombea urais huku yeye akitajwa hadharani kuwa amehongwa asirudishe fomu.

CHADEMA wana vikao vyao, kwa kutanguliza busara wangeyamaliza ya kwao kwenye vikao vyao vya ndani, si hadharani. Na kama mgombea Urais, Dr Slaa anapaswa awe mfano wa kuheshimu utawala wa sheria. Hili ningelisema kama nilivyolisema hata kama lingefanywa na Kikwete wa CCM, Lipumba wa CUF au mgombea ye yote yule. Nisingelisikia nikalinyamazia. Kuandika ni kushauri pia. Tusingependa Dr Slaa apitishwe njia ya Mrema, ina miba na matope. Anayesoma na kuhusika na kilichoandikwa ana uhuru wa kupokea ushauri na kuufanyia kazi au kuachana nao. Nimechokoza mjadala....

Maggid,
Iringa.

Kadhalilishwa au kajidhalilisha mwenyewe? Mbali na hivyo yeye kadhalilisha watanzania wote wenye mapenzi mema,...., ila kweli watu huwa tuna fikra na upeo tofauti, vinginevyo hiyo statement hata mtu ambaye hajasoma kabisa hawezi kuitaja katika mazingira kama haya. Mshauri aende mahakamani!
 
Mi nafikiri katika wakati huu mijadala kama hii ina umuhimu. Aliyetuhumiwa na kuhukumiwa pale Mwembetogwa ni mtu mdogo sana katika nchi hii. Amehukumiwa hadharani na mgombea urais bila kupewa nafasi ya kujitetea. Labda habari zake ndio kwanza mnazisoma humu.

Nafikiri ni muhimu hata hao tunaokwenda kuwachagua nao wajue tunafikiri nini juu yao, maana wanakwenda kubeba dhamana kubwa. Kwa kufanya hivyo, tutawapa nafasi ya kutafakari yale ambayo huenda wasingeyatafakari kama si kuibuliwa mijadala kama hii. Mimi sitachoka kuanzisha mada na kuchokoza mijadala, kwa staili hii hii, na ni kuhusu mambo mbali mbali ninayoyatafakari ili tutafakari pamoja.

Maggid,unaposema mtu mdogo sana una maana gani. Huyu bwana alitarajia kuwa mbunge,na uwezekano wa kuwa waziri kama mbunge ungekuwepo. La sivyo huyu bwana angeingia katika kamati za bunge. Kama amerubuniwa kwa vijisenti na kuwasaliti Chadema,usaliti huo ungeendelea kwa wakati akiwa kiongozi. Mbunge ni mtunga sheria,ndio wanaojadili masuala ya kiuchumi,kijamii na kiusalama, unaposema ni mtu mdogo sijui ni kwa misingi gani. Hebu tufahamishe yaweza kuwa una hoja muungwana.
Mimi ni msomaji wa makala zako ndani ya raia mwema,ni mtembeleaji mzuri wa blog yako ambayo imejikita kuonyesha uhalisia wa maisha ya mtanzania kule kijijini,hili nakupongeza sana. Kinachonishangaza ni wewe unayeyajua maisha ya kule nyeregete yanavyowakamaua wananchi,bado unadiriki kumtetea kiongozi ambaye ameonyesha wazi kujali kula na si masilahi ya taifa, kwa maana kuwa mbunge bila kujali anatoka chama gani ni kiongozi wa taifa tayari. Nasema kumtetea kwasababu hujatuthibitishia kuwa Dr Slaa hana taarifa za uhakika za huyu bwana,kana kwamba amehukumiwa bila kusikilizwa. Umetoa hukumu bila kumhoji Dr Slaa au kutueleza mahojiano na huyo bwana. Dr amempa uhuru aende mahakamani kama alivyowahi kuwaambia mafisadi wa mwembe yanga waende mahakamani, kielelezo cha uhakika wa yale anayoyasema.
Maggid, sisi ni masikini sana,lakini umasikini wetu si wa rasilimali, ni uzembe wa kulindana na kuoneana haya. Leo waliofuja mabilioni ya walala hoi wakiwemo wa Nyeregete eti wanapigiwa debe ni watu safi,ni mapanga ya zamani yenye makali. Vikao vya Chama vitajadili nini zaidi kama mwenyekiti amesema ni watu safi. Hatuwezi kuendelea na utaratibu huu wa kijinga wa kulindana, tuwataje wasaliti wote wa maendeleo yetu hadharani ili ifike wakati mtu akiwa na tuhuma anajinyonga kama kule Japan wanavyofanya ili kuepuka fedheha ya taifa. Ndio maana japan wapo hapo walipo.
Kule China kiongozi aliyesababisha uzembe wa maziwa alitajwa hadharani, akahukumiwa TV zikionyeshwa,hakuna vikao vya ndani wakati wa kupigania maendeleo. Labda nikuulize vikao vya ndani vya Chadema vingebaini kuwa ni msaliti 'So what''! yaishie uvunguni eti tumsitiri ana mke ana watoto,kama anajua hivyo asingefanya alichokifanya.
Naomba kutoa hoja
 
Majid alitaka Slaa aunde tume ya kumchunguza huyo jamaa. No chance for that in CHADEMA. I have been dreaming for a president like Slaa for long time. Mungu tusaidie tumpate huyu mtu atuongoze... Amen.
 
Kama ni kweli hakuhongwa, si arudishe hiyo fomu? Vikao hivyo vya siri wanavyoendekeza CCM ndivyo vinavyotumaliza kwa kufukia maovu! Muovu awekwe hadharani, na kama si muovu basi adhibitishe....!
 
ahahahaaahhahahhahha
maaaagid!!

jamaa anataka kuwa mwamndishi wa habari wa ikuru!!!
 
Me nadhani ni sawa tu, its calling a spade a spade and not a big spoon, Slaa ana data na mara nyingi haropoki ovyo vinginevyo angesha shitakiwa!
 
Bado napata shida kidogo kuelewa, huyu jamaa alihongwa asirudishe fomu je alirudisha au haukurudisha? na je Slaa alitaka kiongozi yupi apuuzwe? nahisi labda Maggid kwa makusudi kabisa anataka kupotosha ukweli au la hakuelewa. Maana haiingii akilini huyu jamaa alihongwa na CCM asirudishe fomu halafu ( na hakurudisha??) iweje hadi sasa bado awe kiongozi wa Chadema na hata baada ya kuwasaliti?. Nahisi huyu kiongozi yeye mwenyewe ndio alimwambia Slaa kuhusu kutakwa kuhongwa ( maana nijuavyo Chadema wamesimamisha mgombea Iringa mjini), so Slaa alitaka Kiongozi wa CCM aliyetaka kuhongwa ndio apuuzwe, na ndio sababu hata huyo Kiongozi "aliyedhalilishwa" alikuwa akipiga makofi. Sio kuwa alipiga makofi eti sababu hakuwa na jinsi, no alipiga makofi sababu Slaa alikuwa anampa makavu Monica Mbega. Tafadhali walioko Iringa na waliofanikiwa kuhudhulia mkutano huo hebu mtujuze zaidi, mimi sina imani na habari hii ya Mjengwa!
 
What if wapenzi wa Dr Slaa wangemvaa na kumrarua mtuhumiwa huyo.....bado tungeendelea ndoto za Utawala bora kutoka kwake???? ust thinking loudly........As a duty for critical citizenry..
 
Back
Top Bottom