Kilimanjaro: Amuua nduguye kwa kukataa kuchangia nyama ya 1,500 waliyokula

Kilimanjaro: Amuua nduguye kwa kukataa kuchangia nyama ya 1,500 waliyokula

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linamshikilia mkazi mmoja wa Kijiji cha Ndungi katika Wilaya ya Moshi kwa tuhuma za kumuua ndugu yake, William Shoo kwa madai ya kukataa kuchangia nyama ya Sh1, 500 waliyonunua.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 11, 2021 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amesema mauaji hayo yalitokea Oktoba 10, 2021 asubuhi baada ya marehemu kugoma kuchangia nyama hiyo waliyonunua.

Kwa mujibu wa Kamanda huyo, kabla ya mauaji hayo mtuhumiwa alinunua nyama kwa kushirikiana na marehemu ambapo walikula pamoja na walipomaliza kula marehemu alikataa kuchangia chochote ndipo ugomvi ukaanza.

Amesema katika ugomvi huo, mtuhumiwa alimkata ndugu yake na kitu chenye ncha kali kichwani na kusababisha kifo chake.

"Awali kabla ya tukio hilo, mtuhumiwa alinunua nyama kwa kushirikiana na mwenzake, ambayo ina thamani ya Sh1, 500 walipokula pamoja ndugu yake huyo alikataa kulipia, ndipo ugomvi ukaanza ambapo ilipelekea kuchukua maamuzi hayo ya kumkata na kitu chenye ncha kali"

Katika tukio lingine, Jeshi hilo linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kumuua John Nyaki kwa kumshambulia sehemu mbalimbali za mwili wake, wakimtuhumu kuiba mizani.

Kamanda Maigwa, amesema tukio hilo lilitokea Oktoba 6, 2021, asubuhi katika eneo la Kibosho Dakau Wilaya ya Moshi.
Nyama hapo imekua sababu ya mwisho.. huenda walikua na chuki chini.kwa chini au muuaji hayupo sawa kiakili.
 
Matukio ya mauaji kila siku. Mbaya zaidi sababu za mauaji mengine unashindwa hata kuelewa. Yaani mtu kala nyama anakataa kuchangia hela, anauawa.
 
Wazazi poleni..

Watoto wote wawili wanaondoka..mmoja

jela mwengine kaburini..!
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linamshikilia mkazi mmoja wa Kijiji cha Ndungi katika Wilaya ya Moshi kwa tuhuma za kumuua ndugu yake, William Shoo kwa madai ya kukataa kuchangia nyama ya Sh1, 500 waliyonunua.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 11, 2021 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amesema mauaji hayo yalitokea Oktoba 10, 2021 asubuhi baada ya marehemu kugoma kuchangia nyama hiyo waliyonunua.

Kwa mujibu wa Kamanda huyo, kabla ya mauaji hayo mtuhumiwa alinunua nyama kwa kushirikiana na marehemu ambapo walikula pamoja na walipomaliza kula marehemu alikataa kuchangia chochote ndipo ugomvi ukaanza.

Amesema katika ugomvi huo, mtuhumiwa alimkata ndugu yake na kitu chenye ncha kali kichwani na kusababisha kifo chake.

"Awali kabla ya tukio hilo, mtuhumiwa alinunua nyama kwa kushirikiana na mwenzake, ambayo ina thamani ya Sh1, 500 walipokula pamoja ndugu yake huyo alikataa kulipia, ndipo ugomvi ukaanza ambapo ilipelekea kuchukua maamuzi hayo ya kumkata na kitu chenye ncha kali"

Katika tukio lingine, Jeshi hilo linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kumuua John Nyaki kwa kumshambulia sehemu mbalimbali za mwili wake, wakimtuhumu kuiba mizani.

Kamanda Maigwa, amesema tukio hilo lilitokea Oktoba 6, 2021, asubuhi katika eneo la Kibosho Dakau Wilaya ya Moshi.
Kuna watu and then kuna Wachagga pia. Mchagga hata shillingi 500 tu anakuua kisha anajiua yeye mwenyewe....Yaani hawa ni watu wa hasara tu, zaidi ya Wahehe, wazee wa kujinyonga na kula mbwa.
 
Umaskini sio laana acha mambo ya ajabu. Kwaiyo tuliozaliwa katika familia za kimaskini tulizaliwa katika laana? Hiyo ni akili tu ya mtu na roho yake. Unatakiwa utumie akili uweze kucontrol hasira.
Umaskini ni laana Tena ya uhakika kama unaamini sio laana nenda kafunge na kuomba Mungu akupe umaskini
 
Marehemu nae kama walikubaliana na mwenzake wachange wanunue nyama wale, kwa nini ale kisha agome kulipa?

Marehemu ana mchango mkubwa sana kusababisha kifo chake.

700 tu imegharimu uhai wake.
Wangegawana kuwa tupe nyama ya 1500 kata katikati weka sahani mbili tofauti halafu kila mmoja mdai 750 wewe muuza nyama
 
Kibosho Dakau nyumbani kwetu huko watu misimamo mikali sana. Mbege nyama ndiyo habari kuu
 
Umaskini sio laana acha mambo ya ajabu. Kwaiyo tuliozaliwa katika familia za kimaskini tulizaliwa katika laana? Hiyo ni akili tu ya mtu na roho yake. Unatakiwa utumie akili uweze kucontrol hasira.

N

Nimeona upuuzi...haya Kuna Nini?

Kweli kabisa ni upuuzi m2pu na ushenzi m2pu,,,afrika inaongoza kwa ukatiri duniani+india=full kuuwana. 2nasafali ndefu sana
 
Ofa za bure zina shida, ukipewa ofa jitahidi ata uchangie kachumbari
 
Back
Top Bottom